Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Mwandishi ameelezea utofauti kati ya Baba na Rais bora wa Taifa,kila mtu ameelewa,labda kama mtu hakubali. Halafu ameonyesha kuwa asili ya ubaba wa taifa ama jina hilo haikutokea kanisa katoliki wala si Roma wanaotoa jina hilo kwa viongozi wa nchi hapa duniani,iwe za kiislamu au kikristo. Hata hatukuwahi kusikia aliyetoa jina hilo alikuwa kardinali Rugambwa au Pengo! Mi nadhani imechukuliwa kifamilia zaidi kwamba...kiongozi wa familia huwa ni mwanamume. Na kwa bahati ni kwamba wanaharakati wengi katika ukombozi na mapinduzi ya nchi zao,walikuwa wanaume... Kifamilia kuna mambo ambayo hayakamiliki hadi baba aje.. Heshima ya ubaba,ni kuonesha uongozi,msimamo,ujasiri,vision,na maamuzi ambayo hata kama yatapingwa na watoto au wake zake,ya baba yanakuwa ya mwisho.. Someone can correct me ila huo ndiyo ufahamu wangu.
and this?
 
Kabla ya mjadala huu na mingine iliyotangulia na inayoendelea kuibuka juu ya Mwalimu sikuwa nafahamu kwamba Mzee huyu bado yumo mioyoni na akilini mwa watu kwa kiwango hiki. Hatutakuwa na Nyerere mwingine nchi hii miaka mingi ijayo.

Sio kwa miaka mingi ijayo bali daima hatuwezi kuwa nae tena.Ninaomba tusiwe na mtu kama yeye ambae wengi waliumia juu yake.Mapinduzi ya umwagaji damu Zanzibar yana mkono wake,vifo vya watu walioliwa na simba wakati wa vijiji vya ujamaa,to mention but few
 
YAH: HOJA YA FOLENI WAKATI WA UJAMAA NA MWALIMU KUOMBA MSAMAHA
ATTENTION: MR.RIGHT, FAIZA FOXY NA WENZENU KATIKA HOJA

Kwanza na awali ya yote, Mr. Right, naomba tuelewane kwamba hapa hatubishani, or at least on my part, tunachofanya ni kujadiliana kwa hoja. kwahiyo hoja kwamba huu ni ubishi baina yangu na wewe naomba uiondoe akili mwako.

Ø Tulijadili hili la Nyerere Versus Free Market – Kwa hoja, sio Malumbano.

Pia hili linamhusu Dada yangu Mpendwa, FAIZA, maana hata kwake, suala la foleni wakati wa Mwalimu limekuwa wimbo wa taifa sasa.

Mr Right, Kwanza, nilishaeleza kwa kirefu jinsi gani umaskini Tanzania, Kenya, Nigeria, etc, haujalishi nchi zetu zinafuata Ujamaa au Soko Huru (SOKO HOLELA). Nikauliza, je, Kwa wale wanaosema Ujamaa ulitupotezea muda, kwanini nchi zilizoendelea na soko huru moja kwa moja baada ya uhuru wao, leo wote wapo na sisi kwenye lowest level ya Maendeleo kwa vipimo vya UNDP – HDI? According to the UNDP, kuna levels nne za development: (1) Very High; (2) High; (3) Middle; and (4) Low Level. Katika Africa, only one country is in High level (Libya), Middle level zipo nchi kama 7, the rest of the countries in Africa i.e 85% of the continent zipo kwenye LOW LEVEL pamoja na sisi Tanzania. Isitoshe, hata Nigeria, Taifa lililojikita kwenye soko huru tangia uhuru, na la saba duniani kwa uzalishaji wa mafuta, limepitwa na Tanzania in terms of vigezo hivyo vya HDI vinavyoangalia impact of uchumi kupaa (kama wanavyotuimbia wanasiasa wetu) i.e. GDP Growth katika kuboresha maisha ya wananchi – literacy levels, educational outcomes, life expectancy, and improved standard of living (quality of life);

Nikauliza, je, haitoshi kutuamsha watanzania wanaomdhihaki Nyerere kwamba mdudu anayetutafuna wote ni mmoja bila ya kujali mfumo wetu ni upi kiuchumi?

Mwalimu aliwahi kusema, uhuru wa kisiasa tumeupata, kazi kubwa iliyopo mbele yenu nayowaachia ni ya kujikomboa kiuchumi. Pia alitamka haya alipoenda USA kwa mwaliko maalum by JFK, White House 1963 (video clip ipo Youtube), aliposema huu ni uhuru wa kisiasa tu, mapambani ndio kwanza yameanza. Ndugu zangu, kinachotumaliza baada ya miaka 50 baada ya uhuru wa Kisiasa,sio kingine bali the unfair integration of our societies into the global capitalist system. Suala la uongozi na sera zetu za nyumbani ni suala secondary. The global current capitalist system – ni mfumo ambao unatupokonya uhuru wa kufanya maamuzi yetu ya kiuchumi from the MACRO PERSPECTIVE – decisions on where and how to invest, what to produce, how to mobilize savings, exchange rates, employment/unemployment levels, trade movements, inflationary targets etc; jukumu hili wamelipokonya wakubwa – World Bank, IMF na WTO ambao wapo kwa ajili ya maslahi ya Nchi Tajiri (G8). Uhuru tulionao kiuchumi sisi ni ule wa MICRO LEVEL – households zetu, kwamba leo tule chai na nyanya, ugali na kachumbari, etc. Muundo wa uchumi unaowapa wananchi control ya household decisions (MICRO), huku MACRO ikiwa sio tu nje yao, bali hata serikali yao, ni uchumi Uchwara. Kwa mfumo huo, Maendeleo ya mwananchi yatatokea wapi? Watapenya penya wachache tu kama wewe Mr Right, Faiza na wengineo. Wengi wanaopenya wanapata uwezo wa maisha ambao ni very artificial, sio kutokana na mishahara yao.

Sijui kwanini wengi wetu tunaendeshwa na ushabiki, huku wakubwa wa nje wakitucheka kwani nia yao ni Tanzania na other parts of Africa zibakie kuwa a rural Yard for Europe and North America. Rural Yard kwa maana ya supply of raw materials, minerals…; Wanaofaidi katika mfumo huu ni wachache sana. Kwa kweli hoja kwamba Bora Afrika ije tu kutawaliwa tena na Mkoloni ina mantiki kama watu wa namna yenu ndio walio wengi. Nyerere alijitahidi sana kuzuia huu upuuzi.

Ø Tulitazame suala lako juu ya Nyerere Kukiri kushindwa na Ujamaa
Kama una busara na uelewa wa hali halisi, haitakiwi ubeze Mwalimu kuomba msamaha, bali kumuona shujaa na kuhimiza awe mfano wa kuigwa na viongozi waliomfuatia. Nyerere alikuwa na ujasiri wa ajabu kuthubutu kuwaambia wakubwa wa nje we are a self- determined nation, but ofcourse wakamzidi nguvu; Sasa msamah wa kwamba we wanted to be self determined but we failed ni wa kukejeli jamani? Pia Mwalimu alituacha na warning kuhusu yatakayojiri mbeleni. Ndio haya haya ya GDP growth kuwa na wastani wa 7% kwa miaka zaidi ya kumi sasa, huku Human Development Index inayopima matokeo ya GDP Growth kuboresha maisha ya watanzania kiafya, kielimu etc, ikituweka permanently nafasi ya 150-152 kati ya nchi 187 duniani. Na wanasiasa mnaowashabikia kwamba ndio wamefanya mema chini ya soko huru (SOKO HOLELA) wanapita majukwaani kuisifia hali hiyo, huku nyinyi mkipiga makofi.

Mr Right, ebu tuambie Whats Right:

· JE, unajua ni watanzanai wangapi katika Tanzania ya leo ISIYOKUWA NA FOLENI, wanalala njaa i.e. hawawezi kupata mlo zaidi ya mmoja kwa siku chini ya hilo soko huria, lisilo na foleni?

· JE, ni kiongozi gani chni ya soko huria amewahi kuomba msamaha kwamba sera za soko huria zinawanyima maisha bora wananchi walio wengi pamoja na familia zao?

· JE, ni kiongozi gani wa soko huru amewahi waomba radhi ndugu zetu kule Mwanza na Musoma kwa jinsi gani kemikali za wawekezaji kwenye migodi zinazomwagwa ovyo in the name of soko huria zinawamaliza ndugu zetu?

· JE, ni kiongozi gani wa soko huria amewahi kuomba radhi jinsi gani wananchi wa kanda ya ziwa (Mwanza), ambao walijaliwa na mwenyezi mungu Ziwa Victoria ili liwapatie vitoeo vya samaki, leo hii wanaambulia mapanki?

· JE, nani ambae amewaomba radhi wananchi kwamba, walipigania uhuru kwa ajili ya kurudisha hali ya haki na usawa, only kupigwa virungu na polisi wakidai haki zile walizoahidiwa?

Mr. Right, mambo ya kuombewa radhi ni mengi, lakini hakika, hakuna aliyeombea radhi kwa lolote chini ya soko huruhilo, na sidhani kama yupo atakayethubutu kwani, aliyewajali kwa dhati hatunae tena.

Mr. Right, let us see what is right and what is wrong hapa. Ebu tutazame takwimu zifuatazo ambazo kwa maoni yangu, nazo zinahitaji viongozi waliokuja baada ya Mwalimu, kuwaomba wananchi wa vijijini kwa kuachia soko huru (HOLELA) limalize kabisa matumani yao.

Mmezungumza suala la foleni wakati wa Mwalimu, Mr.Right, Faiza, Je, Tanzania ya Leo ipo nafuu gani bila ya foleni?
· 68% of Tanzanians (milioni kama 30 kati ya jumla ya watu milioni 45) wanaishi chini ya $1.25 a day, hii ni sawa na just about T.sh 2,000 kwa siku. Mr. Right, Fauza, given the current exchange rate (compared na enzi za Mwalimu), unajua mlo mmoja kwa MAMA NTILIE ni shilling ngapi, hata kama mama ntilie wamejaa mitaani na hivyo kutohitaji mtu upange foleni?

· Wangapi wanaweza afford kila ya nyama, unga, sukari kwenye maduka ya kumwaga, ambayo hayahitaji tena foleni?

· Je, mnajua nauli ya basi ya siku nzima ni shillingi ngapi, pamoja na utitiri wa mabasi ambayo hayahitaji watu kupanga tena foleni? Wakati wa Mwalimu kulikuwa na foleni, tena katika kipindi fulani tu, lakini ilitokana na juhudi za Mwalimu kupunguza tatizo la inequity; soko huria limesaidia kina nani sasa compared to Mwalimu?

· Je, mnajua gharama ya umme ni shilling ngapi, umeme ambao hauhitaji foleni kwani unaweza lipia hata kwa M-PESA, TIGO PESA au AIRTEL MONEY?

Ujamaa ulizaa mambo kadhaa ambayo mmeyaweka bayana. Fine, Je, soko huria mbali na kuondoa hizo foleni kama tulivyokwisha ona hapo juu, limezaa nini?

Leo hii, ni mengi ikiwa ni pamoja na yafuatayo:
· Income share held by the highest 10% of the population is 30%;
· Income share held by the highest 20% of the population is 45%;
· Hapa ina maana, 30% of the population wanahodhi 75% of wealth in Tanzania.

· Income share held by the lowest 10% is 7%;
· Income held by the lowest 20% is 3%;
· Hapa ina maana, 30% of the population (wale maskini wa kutupwa), kwa umoja wao wanahodhi only 10% of wealth in Tanzania.

This means the remaining bit, 15% ndio middle Class in Tanzania;
Now, 75% hapo juu PLUS 15% hapo juu, leaves us with 15% to make it 100%; Hii 15% remaining ndio middle class ya Tanzania.

Je, Mr. Right, Dada Faiza, katika Tanzania ya leo isiyokuwa na foleni, mpo kwenye kundi lipi?

Ndugu zangu, with intense concentration of power, wealth and knowledge in the few hands hapa Tanzania, hata mtoto mdogo wa shule might be able to tell kwamba katika mazingira haya hakuna kitu kinatwa free market (let alone demokrasia); kumbukeni: Free Market assumes and requires more or less equal actors in the game, not a few GIANTS living among many DWARFS or MIDGETS. Ndugu zangu, Free Market doesn’t count heads, it counts dollars. It favors the rich and powerful, not the miserable many because of their numbers (70% of wanavijiji). Sasa hawa ndio watakuja weka mambo sawa. Nyerere alishawaonyesha njia, lakini safari yao iliyojaa matumaini, ik
akatishwa ghafla.
 
Takashi, just out of curiosity, hayo madai ya nyerere na maisha ya watu, ni Nyerere Per Se meaning it was a direct order ya watu kuuwawa au ni kwa hoja kwamba mauaji yalitokea chini ya utawala wake? Ni mauaji gani hayo if you dont mind to share info?
Bw, Mchambuzi, Madikteta wote duniani, iwe Africa ,South America na hata Ulaya wilitumia system ya uuaji ili kuhakikisha wanaendelea kukaa madarakani mpaka watosheke. Kuna units za ziri ndani ya serikali hua zinatumika kufanya kazi hiyo. Mambo hayo bado yanaendelea Zimbabwe na sehemu nyengine.
Mauaji yalifanyika kisiri siri. Hayakuandikwa kwenye vyombo vya habari .Watu walikua wanafutwa majumbani mwao usiku wa manane na askari kanzu. Baada ya hapo ni kimya , wapo walioachiwa baada ya mateso na wengine hawajulikani mpake leo hii wako wapi. Sio Nyerere aliwafata watu usiku wa manane bali ni units zake zilifanya kazi hiyo kwa amri na baraka zake.

List ya watu walio uwawa wakati wa Nyerere inaweza kupatika labda baada ya mabadiliko ya kiutawala kwa miaka ijayo. Kwasababu ,serikali ya CCM bado inalazimishwa kulinda na kutukuza jina la "Nyerere".
 
Bw, Mchambuzi, Madikteta wote duniani, iwe Africa ,South America na hata Ulaya wilitumia system ya uuaji ili kuhakikisha wanaendelea kukaa madarakani mpaka watosheke. Kuna units za ziri ndani ya serikali hua zinatumika kufanya kazi hiyo. Mambo hayo bado yanaendelea Zimbabwe na sehemu nyengine.
Mauaji yalifanyika kisiri siri. Hayakuandikwa kwenye vyombo vya habari .Watu walikua wanafutwa majumbani mwao usiku wa manane na askari kanzu. Baada ya hapo ni kimya , wapo walioachiwa baada ya mateso na wengine hawajulikani mpake leo hii wako wapi. Sio Nyerere aliwafata watu usiku wa manane bali ni units zake zilifanya kazi hiyo kwa amri na baraka zake.

List ya watu walio uwawa wakati wa Nyerere inaweza kupatika labda baada ya mabadiliko ya kiutawala kwa miaka ijayo. Kwasababu ,serikali ya CCM bado inalazimishwa kulinda na kutukuza jina la "Nyerere".

Until then, I consider this to be a conspiracy;
 
Mchambuzi, darasa lako ni zuri sana. Halihitaji mashairi kujibu, kupinga bali linahitaji data. Huo ndio ukweli unao tusukuma kumuenzi yule mzee. Mimi natamani mtu afanye research ili kujuwa hasa watu wanaomlalamikia Nyerere ni watu wa aina gani? Sidhani kama ni wa-Islam wa kweli. Tunatoka familia za wa-Islam wazuri tu lakini sijawahi kushuhudia chuki iliyopindukia dhidi ya Mwalimu kama ninavyoshuhudia kutoka baadhi ya watu hapa. Sidhani kama ni wa-Zanzibar kama Takashi, kuna wa-Zanzibar wanamsifu na kumuheshimu sana Mwalimu nawafahamu mimi. Je kuna uwezekano wa hao wanaolaani sana Mwalimu ni wahamiaji waliotoka mataifa ya nje au wale walionunua uraia... hili linahitaji research, na kama ni kweli basi nchi yetu bado iko mashakani huko tunakokwenda.


Asante sana ndugu Mchunguzi kwa analysis yako hii..
 
Kabla ya hapo mbona husemi? 1961 - 1967 alivyopewa madaraka na alipotaifisha? na 1985 alipoondoka.
Bibie kwanza sielewi unachotaka kuelewa kama ni kutazama jinsi tulivyoshindwa ama kudadisi uzalishaji uloshuka. Lakini najua wewe msomi mzuri unaweza kutafuta data hizo kirahisi sana na nakuhakikishia utaona kwamba Wakati wa Nyerere tuli double production ya Kahawa baada ya serikali kutoa mikopo kwa wakulima, unfortunately we failed kutokana na hali ya uchumi duniani ambayo ilikwenda hadi 1982...Lakini utaona kwamba uzalishaji ulikuwa mkubwa na tukitumia ardhi ndogo zaidi, lakini leo hii ili kupata magunia sawa na miaka ile tunatumia ardhi mara mbili na nusu kuvuna kile kile tulichoweza miaka ya 70s.

Kwa hiyo unaposoma leo kwamba agricultural GDP imeongezeka kwa asilimia 3 ama 5 toka mwaka 1985 ama ongezeko la main food crops na export ni muhimu zaidi kutazama imetugharimu kiasi gani kwa kupanda huko..na ndio nilichoweka hapo juu. Imeonyesha wazi kwanza inahitajika ardhi kubwa zaidi, matumizi ya mbegu, mbolea maji yote haya yanamgharimu mkulima na tunakosa matumizi ya technologia. At the end of the day mkulima anabaki hana kitu na ndio maana umaskini unazidi kupanda kila siku kukicha..

Nachotaka wewe uitazame picha hii kwa mapana zaidi na sii kumlaumu tu mwalimu wakati shida zipo mbele yetu. Foleni ya mwaka 1982 hata Marekani walikuwa wakiweka foleni during great depression..au umesahahu..Na kiuchumi toka mwaka 1973 hadi 1975 GDP ya Marekani ilikuwa negative up to - 4% by 1975.. Mwaka 1980 hadi 1982 GDP ya Marekani ilikuwa negative ktk kipindi hicho pia tena kwa asilimia -7, lakini ndio hatuwezi kulinganisha mapafu ya Marekani na Tz wao walikuwa mbele yetu miaka 200 kimaendeleo.
 
Wewe Mchambuzi unapoteza muda wako bure kujibizana na huyo Taka shi... hao wanajulikana dunia nzima katika JF kuwa wapo kinyume na Nyerere kwa sababu alitetea wanyonge na kuwaadabisha wezi na waporaji wa wakati huo.

Kitu cha ajabu ni kuwa, shutuma zingine haziwezi hata kuthibitika isipokuwa isipokuwa kuthibitisha chuki zao wenye vijiba na hududa. Wanamrushia taka taka zao Nyerere na kuwahifadhi wauwaji wanaojulikana mchana kweupe. Ipo siku kila mtu atatowa hesabu ya maneno yake, chuki zake, ukosefu wa nidham, matukano yake ... na siku hiyo hakutakuwepo na mabishano ya JF.

Nakumbuka hata mimi binafsi nilishawishiwa sana kumchukia Mwalimu na kwa kweli kichwa changu kilijazwa ujinga mwingi sana juu ya jinsi gani Mwalimu ameharibu hii nchi n.k; Hakika wenye kazi hiyo maalum wanatumia mikakati mikubwa sana yenye elements za kutongoza; Baada ya muda nikasema, ebu ngoja niangalie upande wa pili wa hoja, kwa kufanya utafiti wangu mwenyewe from an objective stand point, not subjectively, ili nione historia inatuambia nini kuhusu mtu huyu; ilinichukua kama Mwaka mzima (2007 - 2008) kumsoma Mwalimu kwa undani sana, ndipo nikaja nikaja elewa tatizo lipo wapi; tatizo ni kwamba kuna mkakati maalum wa kumfuta mwalimu katika historia ya nchi hii ili abakie kama watu kama kina kinjeketile na na mkwawa; mpango uliopo ni kuwapotosha watoto na vijana wenye umri mdogo; ni rahisi sana kwa mtu kufuata mkumbo huu, haswa haswa ukiwa mrahisi kudanganyika na material life; ni rahisi sana kushawishika uwe mvivu wa kutumia akili yako huru; hali hiyo ndiyo inayowakumba wengi kwa sasa; lakini nina imani kubwa sana hata kama tupo wachache, tutapigana hadi umauti wetu utufike kulinda heshima ya Kiongozi huyu ambae amenifanyia mengi sana - nina pride kubwa sana ya kuwa mtanzania, ndani a nje ya nchi; muhimu zaidi, kuweza kuishi na wenzangu bila kwanza ya kuuliza kama jina lake ni Peter, Juma, Khadija au Stella; au kama jirani yangu ni Mrangi, Mmasai, mchaga au mfipa; bila ya kuwa na hali hiyo, maendeleo mengine kama yale ya kiuchumi hayawezi kuwa sustainable; Mwenyezi mungu amrehemu;
 
nyerere day and "ubaba" wa taifa are two different things- remember nyerere had been called "baba" wa taifa long before nyerere day ever existed!, so what do you want to say, wasn't he a "baba" wa taifa until when nyerere day was set up?.

By the way, we have "karume" day as well- i think that infer the legacy of karume as a "baba" wa taifa as well, isn't it?
That was a recognition by an act of a parliament..... Kisheria! Before it wasn't "'in the books".

Karume day ipo kwa SMZ so yes, na yeye pia.

Public Holidays are '''LAWS" !
 
Mchambuzi, darasa lako ni zuri sana. Halihitaji mashairi kujibu, kupinga bali linahitaji data. Huo ndio ukweli unao tusukuma kumuenzi yule mzee. Mimi natamani mtu afanye research ili kujuwa hasa watu wanaomlalamikia Nyerere ni watu wa aina gani? Sidhani kama ni wa-Islam wa kweli. Tunatoka familia za wa-Islam wazuri tu lakini sijawahi kushuhudia chuki iliyopindukia dhidi ya Mwalimu kama ninavyoshuhudia kutoka baadhi ya watu hapa. Sidhani kama ni wa-Zanzibar kama Takashi, kuna wa-Zanzibar wanamsifu na kumuheshimu sana Mwalimu nawafahamu mimi. Je kuna uwezekano wa hao wanaolaani sana Mwalimu ni wahamiaji waliotoka mataifa ya nje au wale walionunua uraia... hili linahitaji research, na kama ni kweli basi nchi yetu bado iko mashakani huko tunakokwenda.


Asante sana ndugu Mchunguzi kwa analysis yako hii..

Inawezekana labda ulizaliwa baada ya yule mzee wenu uongozi kumshinda...Kwa waliokuwapo wakati yeye (Nyerere) yuko katika hatamu wanajua vizuri nini alikifanya. Usiingize mbegu za kidini kumtetea Dikteta. Hivi mumekaa angalau kujiuliza kwanini lawama zote atupiwe Nyerere? Kama chuki au udini ,kwanini yeye Nyerere na isiwe kwa wakatoliki wengine?
Msitegemee kila mtz ataungana na nyinyi kuimba "zudumu fikra za mwenyekiti" .Hapa kila mtu ana fikra zake .
 
Inawezekana labda ulizaliwa baada ya yule mzee wenu uongozi kumshinda...Kwa waliokuwapo wakati yeye (Nyerere) yuko katika hatamu wanajua vizuri nini alikifanya. Usiingize mbegu za kidini kumtetea Dikteta. Hivi mumekaa angalau kujiuliza kwanini lawama zote atupiwe Nyerere? Kama chuki au udini ,kwanini yeye Nyerere na isiwe kwa wakatoliki wengine?
Msitegemee kila mtz ataungana na nyinyi kuimba "zudumu fikra za mwenyekiti" .Hapa kila mtu ana fikra zake .
Hakuna lawama dhidi ya Nyerere, upo uzushi unaoundwa na kikundi cha watu wachache kama Takashi ambao hawana hoja, data wala ukweli. Wamejazwa hadi akili haziwezi kubaini kati ya kudanganya au kudanganywa.

Nimeweka maswali hapo juu hakuna anayejibu, bali tunaona watu wakibadili mada na kuleta udikteta, Zimbabwe, unit n.k.

Nikuulize wewe Takashi unayedhani huna chuki mdomoni lakini moyoni ni mweusi. Maswali ni haya:

1. Mwinyi, Mkapa, Kikwete wamejenga bara bara gani kwa pamoja kushinda Nyerere. Sio kuweka lami uelewe!

2. Watatu hao wamewekeza kiasi gani katika 'energy' kuliko Nyerere

3. Ni kitu gani kinafanyika sasa hivi ambacho hakina msingi alioweka Nyerere

Ukijibu maswali hayo nitajua upo kwa mjadala, usipojibu kaa kimya chuki itafaune nafasi yako.
 
Unajua haya ndiyo nasema kila siku, kama hujafanya uchunguzi au kusoma au kuuliza basi usiandike kitu.
Wewe unadhani uwepo wa internet Tanzania umeanza miaka kama 20 iliyopita. Usichokifahamu ni kuwa technology ya Internet haikuwepo kwa kila mtu duniani kama ilivyosasa mwaka 1984 Nyerere alipostaafu.
.
Nenda katika maktaba uone miaka 20 iliyopita ni nchi ngapi duniani zilikuwa na technolojia hiyo.

Mwaka 1995 wakati Bill anazindua window 95 lilikuwa ni tukio kubwa sana. Jiulize leo kuna software ngapi.

Unajua Right nikikuambia kitu kinaitwa Telex ni kigeni kwako. Mwaka 1980 dunia ilikuwa inawasiliana kwa telex, technology iliyokuwa sophsicated kuliko Fax. Hizo computer zilikuwa ni kwa ajili ya kazi maalumu na military operation. Nyerere hakuzuia computer maana hata Kenya na Uganda hazikuwa nazo, huko alikuwepo Nyerere!

Wewe hukuona the other side, umezaliwa ukaikuta internet basi unachojua ni kuwa imeletwa na kikwete. Ni ubishi usio na hoja wala kujitafutia ufahamu, ndio maana hukujua kitu kinaitwa Canon law, watu wakakaa kimya kwasababu hadi hapo kila mtu alijua kuna kazi kiasi gani kukusaidia kuelewa. Usiwe mbishi tu, tulia ujifunze kwa wenzako.

Nakusihi kama jambo hulielewei kaa kimya ujifunze.

Tuyaache hayo na nikuulize swali la msingi. Ni Jambo gani linalofanyika bila msingi wa Nyerere.


Hata TV, mafridge yalikuwepo duniani wakati Nyerere yupo madarakani; lakini WTZ hawakuruhusiwa kuwa navyo. Wanajeshi WTZ walipoivamia Uganda walishangaa kuona Waganda wana TV, fridge, lakini bongo kulikuwa hakuna kitu.

Bado tunaendelea kukumbuka ule unga "Yanga" kwa sababu ya Ujamaa.

Bado tunaendelea kukumbuka ile foleni mafuta.

Ebu, acha ubishi wa Simba na Yanga.
 
Inawezekana labda ulizaliwa baada ya yule mzee wenu uongozi kumshinda...Kwa waliokuwapo wakati yeye (Nyerere) yuko katika hatamu wanajua vizuri nini alikifanya. Usiingize mbegu za kidini kumtetea Dikteta. Hivi mumekaa angalau kujiuliza kwanini lawama zote atupiwe Nyerere? Kama chuki au udini ,kwanini yeye Nyerere na isiwe kwa wakatoliki wengine?
Msitegemee kila mtz ataungana na nyinyi kuimba "zudumu fikra za mwenyekiti" .Hapa kila mtu ana fikra zake .
Mkuu anatupipa lawama kwa sababu yeye ndiye alikuwa rais..Na hizi chuki zenu haziwezi wafikisha popote zaidi ya kuwa maadui wa nafsi zenu wenyewe na umaskini hauwezi kuondoka.
 
Hapa kulikuwa hakuna uongozi bora. Nchi iliyokuwa inauza mazao nje kuja yule Mzee asiyejuwa kuongoza katuletea dhiki moja kwa moja. Mpaka anaachia madaraka mambo yakabadilika na akaanza kuona chuki na kumuitia waandishi na kumshambulia Mwinyi waziwazi. Yote ilikuwa ni roho mbaya tu ya kuona mwenzake kaweza within a short period yaliyomshinda yeye kwa zaidi ya miaka 23.

Hata mseme nini ukweli unabaki kuwa ukweli. Tanzania kulikuwa na "great depression"? Au kulikuwa na mageti ya kipindupindu. Unanshangaza.

Hivi kwanini mnatafuta justification ya kushindwa? Badala ya kutafuta "solution"?

Ni kipi alichoweza Mwinyi within a short period? Ni kwamba tu mambo mengine sio ya kujadili hapa, tusije tukakamatwa kama Mwigamba, lakini ujue tu kwamba Nyerere alifanya kazi ya ziada kuokoa hali tete miaka ya mwanzo ya tisini. tusingekuwa hapa katika hali hii ya leo;
 
Hata TV, mafridge yalikuwepo duniani wakati Nyerere yupo madarakani; lakini WTZ hawakuruhusiwa kuwa navyo. Wanajeshi WTZ walipoivamia Uganda walishangaa kuona Waganda wana TV, fridge, lakini bongo kulikuwa hakuna kitu.

Bado tunaendelea kukumbuka ule unga "Yanga" kwa sababu ya Ujamaa.

Bado tunaendelea kukumbuka ile foleni mafuta.

Ebu, acha ubishi wa Simba na Yanga.
Kama wewe ni mchumi utasema ule ndio ulikuwa wakati wa Great Depression ya Tanzania na facts zinajieleza wazi. Tazama Marekani canada na nchi za magharibi wakati wa great depression halafu nambie kuna nchi hata moja wanamlaumu kiongozi wao?... hapana ni Midanganyika tu iliyokumbwa na udini kama vile Nyerere alikuwa na uungu fulani..Kwa jinsi mnavyoandika mnaonyesha wazi kwamba ni nyie wenye imani za mizimu yaani mlitegemea Nyerere angeweza kutuokoa pengine kama angekuwa Muislaam lakini kwa Ukristu wake ndio maana alishindwa. Wapuuzi kweli nyie na mnatia aibu Uislaam..
 
Hata TV, mafridge yalikuwepo duniani wakati Nyerere yupo madarakani; lakini WTZ hawakuruhusiwa kuwa navyo. Wanajeshi WTZ walipoivamia Uganda walishangaa kuona Waganda wana TV, fridge, lakini bongo kulikuwa hakuna kitu.

Bado tunaendelea kukumbuka ule unga "Yanga" kwa sababu ya Ujamaa.

Bado tunaendelea kukumbuka ile foleni mafuta.

Ebu, acha ubishi wa Simba na Yanga.

I see, kumbe benchmark yako ni TV, FRIJI, PASI na mambo kama hayo kuwepo madukani, okay;
 
1) Nyerere kajenga barabara ipi zaidi ya Dar-Tunduma?

Ni barabara chache sana, tena sana ambazo ni mpya baada ya 1985, kilichotokea, tena sana sana wakati wa Mkapa ni kuzipiga lami zile zilizokongoroka, au zile ambazo mwalimu alizichonga; tumia busara kufikiria kama umewahi sikia wakati wa utu uzima wako kama kuna mradi mpya wa bara bara ambao ume involve watu kukata miti na mapori tanzania hii ili kutokea upande mwingine wa nchi; hadi leo, mradi wa makaa ya mawe ya mchuchumua liganga inabakia ndoto kwasababu hata wawekezaji wanapelekwa na Helikopta, kwani hata barabara ya kuchonga haipo; barabara mpya, iwapo zitatokea, ni zile zinazohusu Mtwara corridor;
 
Kama wewe ni mchumi utasema ule ndio ulikuwa wakati wa Great Depression ya Tanzania na facts zinajieleza wazi. Tazama Marekani canada na nchi za magharibi wakati wa great depression halafu nambie kuna nchi hata moja wanamlaumu kiongozi wao?... hapana ni Midanganyika tu iliyokumbwa na udini kama vile Nyerere alikuwa na uungu fulani..Kwa jinsi mnavyoandika mnaonyesha wazi kwamba ni nyie wenye imani za mizimu yaani mlitegemea Nyerere angeweza kutuokoa pengine kama angekuwa Muislaam lakini kwa Ukristu wake ndio maana alishindwa. Wapuuzi kweli nyie na mnatia aibu Uislaam..

Mkandara

Usichanganye mambo. Ile Great Depression ni part of the flactuation ktk uchumi. In order, kwa free market to sustain lazima iwepo recession au zaidi ya recession. Ndiyo maana hata 2007-9 tumeona another recession lakini haikuwa kubwa kama ile ya 1930s.

Ujamaa system ilikuwa ni maisha ya kila siku haikuwa short term kama recession ktk free market. Tunabishana bure, wakati Nyerere alitoa hotuba mwenyewe na alikiri kushindwa kwa Ujamaa TZ.
 
I see, kumbe benchmark yako ni TV, FRIJI, PASI na mambo kama hayo kuwepo madukani, okay;

Umeandika kwa urefu sana article kuhusu Ujamaa na Nyerere ideology za self determination. Lakini, kitu kimoja lazima uelewe kuhusu, Nyerere. Nyerere alifanya vile ili kuwa against na West na siyo kwa maslahi ya nchi.

Nyerere alikuwa anapenda sifa. Alijua fikra zake za Ujamaa zitakuwa bora iwapo hatakuwa na urafiki wa kibiashara na West. Wakati hiyo idea ilifeli hata kwa Warusi, na Wachina pia.


Unajaribu kucompare nchi zilizokuwa ktk Ujamaa na Market economy? Mbona siku nyingi hiyo comparison imeshapata jibu. Ujamaa umeshindwa vibaya duniani, na nchi zote duniani zimeamua kuwa na market economy; ikiwemo TZ.
 
Back
Top Bottom