Monstgala
JF-Expert Member
- Aug 25, 2009
- 1,079
- 1,037
Nyerere alikuwa anataka Taifa lijitegemee, halafu Mkandara na wengineo wanasema Wazungu wanataka kununua bidhaa zetu kwa bei ya chini. Sasa mbona mnajicontradict wenyewe. Kwa nini mnataka kuuza mazao yetu ya Ujamaa kwa West? hao wenye Free Market na advance Technology? Nyerere alikuwa anataka WTZ tujitegemee halafu anataka mazao yetu tuuze kwa nchi za West!! Je Nyerere hakujua hilo? Hapo ndipo ujue kwamba Mwalimu Nyerere hakujua anachokifanya.
Nyerere alijua Mkulima wa Jembe ataweza kucompete na nchi za West zenye Free Market with advance technology? Inaonekana ALISHINDWA kufikiri kwamba kuna Competitive Advantage.
Nyerere alikuwa MZUNGUMZAJI MZURI SANA!! lakini Utendaji wake ni ZERO.
Huyu jamaa ni bingwa wa kujichanganya...
1.Unapoongelea kujitegemea huna maana ya kwamba usifanye trade la hasha! Ila katika hiyo trade uepuke vigezo vitakavyokunyonya, mfano unaweza kuwa na soko la pamoja, au biashara kati ya mataifa yasiyokuwa ya kibepari etc. Hiyo ndio point na pia katika sera ujamaa si kwamba usitumie technology nani alikuambia hilo? Enzi za U.S.S.R walirusha chombo chao mwezini na walikuwa ni wajamaa haswa.
2.Unaongelea competitive advantage kana kwamba mkulima wa Tanzania alitakiwa kucompete na mkulima wa West kitu ambacho si kweli. Ujamaa sio competition na hilo umechajichanganya vibaya sana. Bali sera ya kiuchumi illikuwa ni comparative advantage yani mkulima wa Tanzania azalishe kile ambacho ana-advantage zaidi (absolute advantage) mfano kahawa ambayo kwa sababu za kijiografia haistawi nchi za magharibi na yule wa mkulima wa nchi za magharibi azalishe kile ambacho ana advantage zaidi mfano mahindi kwa marekani. Hujiulizi kwa nini Ivory Coast na Ghana ndio wazalishaji wakubwa wa cocoa kwa nini hao mabepari wa west wasizalishe wenyewe na ndio watumiaji wakubwa wa cocoa beans. Unadhani Ivory coast na Ghana wana advanced tech kiliko nchi za magharibi? au unadhani nchi za magharibi si walaji sana wa chocolate ni sie kina mgalanjuka wa Africa.
Ukishajiuliza maswali hayo utaona wazi kwamba Nyerere alifikiria mbali zaidi ya wewe na kizazi chako.