Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Hili la baba wa taifa tuachane nao wanopinga wakameze wembe... turudi kwenye mada yetu.Kipande hiki nimekipenda sana na hakika nitachangia kwa wale wasiojua mahesabu ili wapate kujua kama kweli tulishindwa ama kulichangiwa sababu nyingine kabisa..

Nitawapa mfano mdogo sana:-
- Kuanzia mwaka 1972 hadi 1982, Tanzania tulikuwa na mashamba ya Kahawa Hectares 126,000 zikizalisha kahawa wastani wa tani 46,000kila mwaka - yields about 390 kilo per hectare...
- Na sasa hivi tuna hectares za kilimo cha kahawa zaidi ya 300,000 tunazalisha kahawa kwa wastani watani 60,000 kwa mwaka -yields ni about 320 per hectare...

Sasa waungwana kweli unaweza kusema leo hii tumeendelea kwa sababu tu leo hii Kahawa imepanda bei wakati uzalishaji ndio kama mnavyoona hapo juu.
Hivi kweli mama mpika vitumbua alokuwa akiuza vitumbua 1,000 kwa siku mwaka jana kwa bei ya Tsh 500 ana nafuu zaidi mwaka huu kwa sababu anauza vitumbua 600 kwa bei ya Tsh 1000? kwa sababu tu watu wanatazama pato la kutoka laki tano kwenda laki 7 bila kuzingatia matumizi na kupoteza wateja 300!...

Naomba wasomi wa uchumi mnielimishe..
Kwanza kabisa population dynamics zinaifanya hiyo 60,000 kuwa less than 46,000.
Pili, productivity inasuta uwezo wetu bearing in mind technology imeongezeka duniani.
 
nimeogopa baada ya kuona comment zimefika 666 naombeni samahani nimeogopa tu.
 
Na foleni za chakula wakati wa Nyerere mbona huzisemi?

Hivi unafahamu hata wakati wa Great Depression in most advanced economies like the US kulikuwa na foleni pia za chakula? Haina maana kwamba tatizo hili Tanzania was justifiable on such grounds, lakini ni muhimu uelewe how the business cycle works.
 
Kabla ya hapo mbona husemi? 1961 - 1967 alivyopewa madaraka na alipotaifisha? na 1985 alipoondoka.

Hivi hoja yako kimsingi ni nini, uongozi kiuchumi chini ya Mwalimu Vis-a-Vis Kiongozi Unayempenda Wewe OR Uchumi chini ya Ujamaa vis-a-vis Free Market?

1961-1966 - Free Market (miaka 5); [Nyerere]
1967-1985 - Command/Planned Economy (miaka 18); [Nyerere]
1986 - 2011 - Free Market (Miaka 25); [Mwinyi, Mkapa, Kikwete]

Miaka 30 chini ya Soko huru Vs Miaka 18 chini ya Ujamaa.

Unaweza kuwa muwazi kidogo nini haswa unalenga?
 
Hivi hoja yako kimsingi ni nini, uongozi kiuchumi chini ya Mwalimu Vis-a-Vis Kiongozi Unayempenda Wewe OR Uchumi chini ya Ujamaa vis-a-vis Free Market?

1961-1966 - Free Market (miaka 5); [Nyerere]
1967-1985 - Command/Planned Economy (miaka 18); [Nyerere]
1986 - 2011 - Free Market (Miaka 25); [Mwinyi, Mkapa, Kikwete]

Miaka 30 chini ya Soko huru Vs Miaka 18 chini ya Ujamaa.

Unaweza kuwa muwazi kidogo nini haswa unalenga?
Mkuu, kama nilivyokwambia awali ...... Ni ubaguzi wa kidini ndiyo unaozungumziwa hapo!, watu waliozaliwa Bara (i.e other than Dar) au wageni wa mji hawana nafsi mbele ya vigagu kama hivyo.


Usipoteze muda wako....... she's too shallow to even compromise.
 
Hivi hoja yako kimsingi ni nini, uongozi kiuchumi chini ya Mwalimu Vis-a-Vis Kiongozi Unayempenda Wewe OR Uchumi chini ya Ujamaa vis-a-vis Free Market?

1961-1966 - Free Market (miaka 5); [Nyerere]
1967-1985 - Command/Planned Economy (miaka 18); [Nyerere]
1986 - 2011 - Free Market (Miaka 25); [Mwinyi, Mkapa, Kikwete]

Miaka 30 chini ya Soko huru Vs Miaka 18 chini ya Ujamaa.

Unaweza kuwa muwazi kidogo nini haswa unalenga?
Mchambuzi unajua watu wenye chuki hata ufanye nini hawatakuelewa kwasababu chuki ndio inaongoza hisia zao na imeziba nafasi zote za uelewa.

Watu wakiongelea Nyerere hata siku moja hawaelezi alichukua nchi katika hali gani kiuchumi, alikabiliwa na changamoto gani, alizikabili changamoto vip, aliwekeza vipi na nini, alipoondoka aliacha nini n.k.

Ninashangaa kuna mtu alisema Nyerere alivamia uganda kwa kutuma askari waende wakabake waganda mwaka 1978. Masikini mtu huyu amesimuliwa bila kutafuta ukweli wa ugomvi kati ya Tanzania na Uganda. Amini aliwahi kuishambulia Tanzania miaka kabla ya hapo na alipiga mabomu Mwanza na Kagera. Kati ya watu waliosuluhisha mgogoro ule alikuwa marehemu Haile Sellasi na kwa msaada wa kidiplomasia wa Somalia. Vita vya Kagera ilikuwa beyond tolerance na Nyerere alijua outcome yake lakini alisimama kuilinda nchi.

Mtu anasema Nyerere aliacha foleni blia kujiuliza foleni ilianza lini na kwanini.
Yupo anayesema Nyerere aliacha mashimo na mahandaki, tukiuliza kati ya Mwinyi, Mkapa na Kikwete nani amejenga bara bara kwa kuvunja majabali hatupewi jibu. Watu wameelekeza vichwa vyao katika lami utadhani lami inaweza kutandikwa porini au juu ya majabali.

Wapo wanaosema hakuacha miundo mbinu, hao hawajiulizi reli ya Mnyuzi-Ruvu au Tazara zimejengwa na nani. Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamjenga reli yenye urefu gani inayolingana na ile ya Mnyuzi(Korogwe) hadi Ruvu. None!

Nyerere ameacha mashiirika zaidi ya 400 yakitoa huduma na ajira. Kikwete anakwenda Kampala kulalamika kuwa vijana wasipopata ajira ni hatari. Ni hatari kweli, lakini hajiulizi ajira zipi na kwa mazingira yapi aliyoyaandaa.

Labda kwa ufupi niseme kuwa Nyerere ndiye Rais peke yake aliyewekeza katika nchi hii kuliko marais wote watatu kwa pamoja. Hakuna kiongozi anayejenga bara bara wote wanaweka lami. Hakuna kiongozi anayewekeza katika elimu kwasababu wao ni zao la uwekezaji wa Nyerere. Hakuna kiongozi aliyewekeza katika miundoo mbinu, afya kama Nyerere.

Kama yupo au wapo, naomba mtu anieleze ni kitu gani kinafanyika nchini sasa hivi ambacho si uwekezaji wa Nyerere.
Nielezwe kiongozi gani amefanya kitu ambacho Nyerere hakuthubutu kukifanya katika uongozi wake tangu uhuru
Nielezwa katika nchi za EAC ni ipi inayoweza kusimama na kusema ni tofauti na Tanzania katika hali za watu wake.
 
Hivi hoja yako kimsingi ni nini, uongozi kiuchumi chini ya Mwalimu Vis-a-Vis Kiongozi Unayempenda Wewe OR Uchumi chini ya Ujamaa vis-a-vis Free Market?

1961-1966 - Free Market (miaka 5); [Nyerere]
1967-1985 - Command/Planned Economy (miaka 18); [Nyerere]
1986 - 2011 - Free Market (Miaka 25); [Mwinyi, Mkapa, Kikwete]

Miaka 30 chini ya Soko huru Vs Miaka 18 chini ya Ujamaa.

Unaweza kuwa muwazi kidogo nini haswa unalenga?


Sasa unataka kucompare wakati wa Njaa wa Nyerere na huu wa Free Market? Nyerere na Ujamaa wake ulishindwa vibaya na Nyerere mwenyewe alikiri hivyo.

Sasa unabisha nini?
 
Hivi unafahamu hata wakati wa Great Depression in most advanced economies like the US kulikuwa na foleni pia za chakula? Haina maana kwamba tatizo hili Tanzania was justifiable on such grounds, lakini ni muhimu uelewe how the business cycle works.

Unachanganya mambo. Usifananishe Great Depression ya 1930s na Ujamaa wa Nyerere kabisa. Usichanganye mambo. Ujamaa wa Nyerere ulishindwa vibaya ndiyo maana nchi yetu ipo maskini sasa kwa sababu ya matatizo yaliyosababishwa na Ujamaa wa Nyerere.
 
Mchambuzi unajua watu wenye chuki hata ufanye nini hawatakuelewa kwasababu chuki ndio inaongoza hisia zao na imeziba nafasi zote za uelewa.

Watu wakiongelea Nyerere hata siku moja hawaelezi alichukua nchi katika hali gani kiuchumi, alikabiliwa na changamoto gani, alizikabili changamoto vip, aliwekeza vipi na nini, alipoondoka aliacha nini n.k.

Ninashangaa kuna mtu alisema Nyerere alivamia uganda kwa kutuma askari waende wakabake waganda mwaka 1978. Masikini mtu huyu amesimuliwa bila kutafuta ukweli wa ugomvi kati ya Tanzania na Uganda. Amini aliwahi kuishambulia Tanzania miaka kabla ya hapo na alipiga mabomu Mwanza na Kagera. Kati ya watu waliosuluhisha mgogoro ule alikuwa marehemu Haile Sellasi na kwa msaada wa kidiplomasia wa Somalia. Vita vya Kagera ilikuwa beyond tolerance na Nyerere alijua outcome yake lakini alisimama kuilinda nchi.

Mtu anasema Nyerere aliacha foleni blia kujiuliza foleni ilianza lini na kwanini.
Yupo anayesema Nyerere aliacha mashimo na mahandaki, tukiuliza kati ya Mwinyi, Mkapa na Kikwete nani amejenga bara bara kwa kuvunja majabali hatupewi jibu. Watu wameelekeza vichwa vyao katika lami utadhani lami inaweza kutandikwa porini au juu ya majabali.

Wapo wanaosema hakuacha miundo mbinu, hao hawajiulizi reli ya Mnyuzi-Ruvu au Tazara zimejengwa na nani. Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamjenga reli yenye urefu gani inayolingana na ile ya Mnyuzi(Korogwe) hadi Ruvu. None!

Nyerere ameacha mashiirika zaidi ya 400 yakitoa huduma na ajira. Kikwete anakwenda Kampala kulalamika kuwa vijana wasipopata ajira ni hatari. Ni hatari kweli, lakini hajiulizi ajira zipi na kwa mazingira yapi aliyoyaandaa.

Labda kwa ufupi niseme kuwa Nyerere ndiye Rais peke yake aliyewekeza katika nchi hii kuliko marais wote watatu kwa pamoja. Hakuna kiongozi anayejenga bara bara wote wanaweka lami. Hakuna kiongozi anayewekeza katika elimu kwasababu wao ni zao la uwekezaji wa Nyerere. Hakuna kiongozi aliyewekeza katika miundoo mbinu, afya kama Nyerere.

Kama yupo au wapo, naomba mtu anieleze ni kitu gani kinafanyika nchini sasa hivi ambacho si uwekezaji wa Nyerere.
Nielezwe kiongozi gani amefanya kitu ambacho Nyerere hakuthubutu kukifanya katika uongozi wake tangu uhuru
Nielezwa katika nchi za EAC ni ipi inayoweza kusimama na kusema ni tofauti na Tanzania katika hali za watu wake.


Hivi wewe ungeweza kuandika hapa kama Nyerere angekuwepo? Ubishi wa Simba na Yanga ushapitwa na wakati.
 
Hivi wewe ungeweza kuandika hapa kama Nyerere angekuwepo? Ubishi wa Simba na Yanga ushapitwa na wakati.
Unajua haya ndiyo nasema kila siku, kama hujafanya uchunguzi au kusoma au kuuliza basi usiandike kitu.
Wewe unadhani uwepo wa internet Tanzania umeanza miaka kama 20 iliyopita. Usichokifahamu ni kuwa technology ya Internet haikuwepo kwa kila mtu duniani kama ilivyosasa mwaka 1984 Nyerere alipostaafu.
.
Nenda katika maktaba uone miaka 20 iliyopita ni nchi ngapi duniani zilikuwa na technolojia hiyo.

Mwaka 1995 wakati Bill anazindua window 95 lilikuwa ni tukio kubwa sana. Jiulize leo kuna software ngapi.

Unajua Right nikikuambia kitu kinaitwa Telex ni kigeni kwako. Mwaka 1980 dunia ilikuwa inawasiliana kwa telex, technology iliyokuwa sophsicated kuliko Fax. Hizo computer zilikuwa ni kwa ajili ya kazi maalumu na military operation. Nyerere hakuzuia computer maana hata Kenya na Uganda hazikuwa nazo, huko alikuwepo Nyerere!

Wewe hukuona the other side, umezaliwa ukaikuta internet basi unachojua ni kuwa imeletwa na kikwete. Ni ubishi usio na hoja wala kujitafutia ufahamu, ndio maana hukujua kitu kinaitwa Canon law, watu wakakaa kimya kwasababu hadi hapo kila mtu alijua kuna kazi kiasi gani kukusaidia kuelewa. Usiwe mbishi tu, tulia ujifunze kwa wenzako.

Nakusihi kama jambo hulielewei kaa kimya ujifunze.

Tuyaache hayo na nikuulize swali la msingi. Ni Jambo gani linalofanyika bila msingi wa Nyerere.
 
Kabla ya mjadala huu na mingine iliyotangulia na inayoendelea kuibuka juu ya Mwalimu sikuwa nafahamu kwamba Mzee huyu bado yumo mioyoni na akilini mwa watu kwa kiwango hiki. Hatutakuwa na Nyerere mwingine nchi hii miaka mingi ijayo.
 
Kabla ya mjadala huu na mingine iliyotangulia na inayoendelea kuibuka juu ya Mwalimu sikuwa nafahamu kwamba Mzee huyu bado yumo mioyoni na akilini mwa watu kwa kiwango hiki. Hatutakuwa na Nyerere mwingine nchi hii miaka mingi ijayo.

WildCard, umesema kweli tupu! Mimi niliwahi kusema kuwa, ili wale wanaompinga Nyerere waweze kufanikiwa kumfanya afutike mioyoni mwa wa-Tanzania/Tanganyika waache maneno ya matusi dhidi yake, bali wafanye vitendo vya kutufurahisha watu wote. Tuone sera nzuri zinazohusu watu wote zikitekelezwa kwa ajili ya watu wote, hasa wale wanyonge. Tunataka ardhi ya watu iwe salama mikononi mwa serikali au watu wenyewe. Tunataka elimu na huduma za afya bora kwa ajili ya watu wote.

Hatutaki lawalawa, pipi na plastic kujazana madukani na mafisadi kuongezeka, na madini yakiibwa makontena kwa makontena usiku na mchana na kubaki na mashimo ya machimbo...

Tunataka tuone uzalendo uliotukuka kwa viongozi wetu nk ...Tukiyaona hayo, tutamsahau Nyerere, tutakubali kumtukana Nyerere, tutamlaani Nyerere .... tutampokonya na heshima tuliyompa ya baba wa taifa. Lakini yupo kiongozi wa namna hiyo? Labda Faiza Foxy anaweza kufanya makubwa kumshinda huyo marehem Nyerere. Mimi nipo tayari kumwita F/Foxy kuwa mama wa taifa akiyafanya yote hayo.
 
public holidays act.

Nyerere day, pia ipo kwenye employent ordinance na bank of tanzania act.... Bank days huwa zipo internationally recognized. Nyerere day is internationally and nationally recognized by law.

So his legacy as the father of the nation is legally recognized by those acts.

nyerere day and "ubaba" wa taifa are two different things- remember nyerere had been called "baba" wa taifa long before nyerere day ever existed!, so what do you want to say, wasn't he a "baba" wa taifa until when nyerere day was set up?.

By the way, we have "karume" day as well- i think that infer the legacy of karume as a "baba" wa taifa as well, isn't it?
 
HTML:
Mchambuzi unajua watu wenye chuki hata ufanye nini hawatakuelewa kwasababu chuki ndio inaongoza hisia zao na imeziba nafasi zote za uelewa.

Watu wakiongelea Nyerere hata siku moja hawaelezi alichukua nchi katika hali gani kiuchumi, alikabiliwa na changamoto gani, alizikabili changamoto vip, aliwekeza vipi na nini, alipoondoka aliacha nini n.k.

Ninashangaa kuna mtu alisema Nyerere alivamia uganda kwa kutuma askari waende wakabake waganda mwaka 1978. Masikini mtu huyu amesimuliwa bila kutafuta ukweli wa ugomvi kati ya Tanzania na Uganda. Amini aliwahi kuishambulia Tanzania miaka kabla ya hapo na alipiga mabomu Mwanza na Kagera. Kati ya watu waliosuluhisha mgogoro ule alikuwa marehemu Haile Sellasi na kwa msaada wa kidiplomasia wa Somalia. Vita vya Kagera ilikuwa beyond tolerance na Nyerere alijua outcome yake lakini alisimama kuilinda nchi.

Mtu anasema Nyerere aliacha foleni blia kujiuliza foleni ilianza lini na kwanini.
Yupo anayesema Nyerere aliacha mashimo na mahandaki, tukiuliza kati ya Mwinyi, Mkapa na Kikwete nani amejenga bara bara kwa kuvunja majabali hatupewi jibu. Watu wameelekeza vichwa vyao katika lami utadhani lami inaweza kutandikwa porini au juu ya majabali.

Wapo wanaosema hakuacha miundo mbinu, hao hawajiulizi reli ya Mnyuzi-Ruvu au Tazara zimejengwa na nani. Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamjenga reli yenye urefu gani inayolingana na ile ya Mnyuzi(Korogwe) hadi Ruvu. None!

Nyerere ameacha mashiirika zaidi ya 400 yakitoa huduma na ajira. Kikwete anakwenda Kampala kulalamika kuwa vijana wasipopata ajira ni hatari. Ni hatari kweli, lakini hajiulizi ajira zipi na kwa mazingira yapi aliyoyaandaa.

Labda kwa ufupi niseme kuwa Nyerere ndiye Rais peke yake aliyewekeza katika nchi hii kuliko marais wote watatu kwa pamoja. Hakuna kiongozi anayejenga bara bara wote wanaweka lami. Hakuna kiongozi anayewekeza katika elimu kwasababu wao ni zao la uwekezaji wa Nyerere. Hakuna kiongozi aliyewekeza katika miundoo mbinu, afya kama Nyerere.

Kama yupo au wapo, naomba mtu anieleze ni kitu gani kinafanyika nchini sasa hivi ambacho si uwekezaji wa Nyerere.
Nielezwe kiongozi gani amefanya kitu ambacho Nyerere hakuthubutu kukifanya katika uongozi wake tangu uhuru
Nielezwa katika nchi za EAC ni ipi inayoweza kusimama na kusema ni tofauti na Tanzania katika hali za watu wake.

Bw, Mkubwa... Hakuna mtz aliyezaliwa kumchukia Nyerere, kama kukosolewa kwakwe ,kwako wewe ni sawa na chuki ,hiyo juu yako na kasumba zako. Nyerere anavuna alicho panda (lima). Wapo waliopoteza ndugu zao wakati wa Udikteta wake na kamwe hawatakaa kimya . Mnae muuabudu fanyeni hivyo kwa maslahi yenu binafsi.
 
Bw, Mkubwa... Hakuna mtz aliyezaliwa kumchukia Nyerere, kama kukosolewa kwakwe ,kwako wewe ni sawa na chuki ,hiyo juu yako na kasumba zako. Nyerere anavuna alicho panda (lima). Wapo waliopoteza ndugu zao wakati wa Udikteta wake na kamwe hawatakaa kimya . Mnae muuabudu fanyeni hivyo kwa maslahi yenu binafsi.

Takashi, just out of curiosity, hayo madai ya nyerere na maisha ya watu, ni Nyerere Per Se meaning it was a direct order ya watu kuuwawa au ni kwa hoja kwamba mauaji yalitokea chini ya utawala wake? Ni mauaji gani hayo if you dont mind to share info?
 
Takashi, just out of curiosity, hayo madai ya nyerere na maisha ya watu, ni Nyerere Per Se meaning it was a direct order ya watu kuuwawa au ni kwa hoja kwamba mauaji yalitokea chini ya utawala wake? Ni mauaji gani hayo if you dont mind to share info?
Wewe Mchambuzi unapoteza muda wako bure kujibizana na huyo Taka shi... hao wanajulikana dunia nzima katika JF kuwa wapo kinyume na Nyerere kwa sababu alitetea wanyonge na kuwaadabisha wezi na waporaji wa wakati huo.

Kitu cha ajabu ni kuwa, shutuma zingine haziwezi hata kuthibitika isipokuwa isipokuwa kuthibitisha chuki zao wenye vijiba na hududa. Wanamrushia taka taka zao Nyerere na kuwahifadhi wauwaji wanaojulikana mchana kweupe. Ipo siku kila mtu atatowa hesabu ya maneno yake, chuki zake, ukosefu wa nidham, matukano yake ... na siku hiyo hakutakuwepo na mabishano ya JF.
 
Back
Top Bottom