Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Kuna watu wamejenga hoja ya kidini kuwa "katika Uislamu hakuna baba". Hii si kweli hata kidogo. Qurani Tukufu yenyewe inaweka wazi jambo hili kwamba wapo wanaoitwa "baba" kati ya wanadamu na tena ni waamini. Katika Surat Affat (37:102 na kuendelea) tunaona kuwa Ishmaeli anamuita Ibrahim "Baba". Waislamu wanaamini kuwa Mitume wote hata kabla ya Mohammed (SAW) walikuwa ni Waislamu. Kuwa hata Ibrahim alikuwa ni Muislamu. Kwa hiyo kama ni kweli hivi (Italiki na Msisitizo mweuzi wangu)

Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri (37:102)

Na katika sura hiyo hiyo Qurani inawasifia manabii wengine waliotangulia na inapofika kwa Nabii Ilyas (Elia) inasemwa hivi:

Na
A hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume
lipo waambia watu wake: Hamwogopi?
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani? 37:123-126

Kitu pekee ambacho kiko wazi katika Qurani na katika mafundisho ya Uislamu ni kuwa Mungu si Baba. Ukisoma mistari inayofuatia hapo chini hili liko wazi kabisa. Na kwa wanaosoma historia ya dini ni kuwa Uislamu umekataa kabisa toka mwanzo Kumuita Mungu "Baba" kwa sababu Wakristu walikuwa wanamuita Mungu "Baba" na iliaminika kana kwamba wanamaanisha Mungu alichukua mke akazaa naye. Hili Qurani Tukufu inalikataa hata kwenye sura hii:

Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume? 37:151-153

Pia tunaona katika Sura 33:6 kuwa wake wa Mtume ni "mama wa waamini" na ndio maana hata leo Waislamu wanamuona Bi. Khadijah kama "mama yao". Je, kama mke wa nabii (kama mstari unavyosema) ni "mama" wa waumini je nabii mwenyewe anaweza kuchukuliwaje? Hasa ukizingatia kuwa Qurani inawatambulisha wale manabii wa zamani (hiyo sura ya 37) kuwa ni "baba" wa zamani? Je manabii nao ni kama baba zetu?

Kumbe ni rahisi kuona kuwa:

a. Uislamu unatambua nafasi ya "ubaba" na kuwa haikatazi kumuita mtu "baba". Katika Biblia labda ni kali zaidi kwa sababu Yesu ndiye alisema wazi kuwa "Usimwite mtu yeyote baba hapa duniani kwani baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni!" Mathayo 23:9.

b. Uislamu unakataza kumuita Mungu "Baba" kwa sababu Mungu "hakuzaa wala hakuzaliwa". Na ni kinyume na mafundisho yaliyokuwepo ya Wakristu waliomuita Mungu "Baba yetu".

c. Kama ndivyo ilivyo kwamba Qurani inawatambulisha mitume waliotangulia kama "baba" ni wazi kuwa haikatazwi kumuita mtu "baba" moja kwa moja; inakataza kumuita Mungu "baba". Na tunafahamu inaposema wake wa nabii ni "mama" wa waamini sidhani kama kuna mtu anaamini kwamba inasema huyo "mama" alizaa waamini wote kimwili. Ni wazi ni cheo na nafasi ya heshima ambayo mama hao wanazo. Hili ni kweli pia kwa wale manabii. Wanapoitwa "baba" zetu si kwa sababu waliwaingilia mama zetu!


Hivyo, hoja ya kuwa Nyerere hafai kuitwa 'baba' haina msingi na kuwa mtu aliyezaa asiitwe 'baba' nayo haina msingi vile vile!


Nasimama kusahihishwa.

Acha uwongo aya ulizo quote Qur: 37:126

Ni batili naomba usipoteshe watu..ok

Omba msamaha haraka please..
 
Kwanza aombe msamaha huyu jamaa yako ni mnafiki mkubwa anachezea Aya za Allah...

Hakuna sehemu kwenye Quran katika aya alizoweka inayosema baba zenu..

This is third time jamaa anafanya makusudi kabisa na kitabu cha Allah???


Kwanza aombe msamaha huyu jamaa yako ni mnafiki mkubwa anachezea Aya za Allah...

Hakuna sehemu kwenye Quran katika aya alizoweka inayosema baba zenu..

This is third time jamaa anafanya makusudi kabisa na kitabu cha Allah???

Topical - tafuta tafsiri nyingine ya Kiswahili utaona inatumia maneno hayo ya "baba"; Tafsiri ninayotumia ni ya Shehe Barwani na inatumia maneno hayo. Hata tafsiri za Kiingereza kama ya Yusufali inatumia hivyo. HIyo ya 37:126 inasema "Al-Laha Rabbakum Wa Rabba 'Ābā'ikumuAl-'Awwalīna" Topical aya haisemi "wazee" inasema "baba zenu". Niko sahihi na wewe uombe radhi kwa kusema kitu ambacho Qurani haisemi!

Mkandara - ni kweli ninachoonesha ni kwamba kuwa wapo watu wanaoitwa "baba" kwa kuzaa. Kwamba mtu aliyekuzaa huwezi kumuita "baba" kama baadhi walivyokuwa wanadai. Ninachoonesha ni kuwa wapo "baba" katika Uislamu. Nipo napitia Hadithi hapa (Bukhari na Muslim) na naweza kuona mara kadhaa ambapo watu walipewa ushauri kwa "baba" zao au kuhusiana na "baba" zao. Kwamba, inaruhusiwa kumuita mtu "baba" halina shaka kama mistari hiyo inavyoonesha. Ama sivyo?
 
Mi nashauri mkubaliane kutokukubaliana. Mwandishi ameelezea utofauti kati ya Baba na Rais bora wa Taifa,kila mtu ameelewa,labda kama mtu hakubali. Halafu ameonyesha kuwa asili ya ubaba wa taifa ama jina hilo haikutokea kanisa katoliki wala si Roma wanaotoa jina hilo kwa viongozi wa nchi hapa duniani,iwe za kiislamu au kikristo. Hata hatukuwahi kusikia aliyetoa jina hilo alikuwa kardinali Rugambwa au Pengo! Mi nadhani imechukuliwa kifamilia zaidi kwamba...kiongozi wa familia huwa ni mwanamume. Na kwa bahati ni kwamba wanaharakati wengi katika ukombozi na mapinduzi ya nchi zao,walikuwa wanaume... Kifamilia kuna mambo ambayo hayakamiliki hadi baba aje.. Heshima ya ubaba,ni kuonesha uongozi,msimamo,ujasiri,vision,na maamuzi ambayo hata kama yatapingwa na watoto au wake zake,ya baba yanakuwa ya mwisho.. Someone can correct me ila huo ndiyo ufahamu wangu.

hoja hii ipo tangu saa 9! Haijapata majibu wala maoni! Sijui lugha iliyotumika ni ngumu ama vipi. Humu tunaelimishana.. Topical kama bado upo taf changia...
 
Topical - tafuta tafsiri nyingine ya Kiswahili utaona inatumia maneno hayo ya "baba"; Tafsiri ninayotumia ni ya Shehe Barwani na inatumia maneno hayo. Hata tafsiri za Kiingereza kama ya Yusufali inatumia hivyo. HIyo ya 37:126 inasema "Al-Laha Rabbakum Wa Rabba 'Ābā'ikumuAl-'Awwalīna" Topical aya haisemi "wazee" inasema "baba zenu". Niko sahihi na wewe uombe radhi kwa kusema kitu ambacho Qurani haisemi!

Mkandara - ni kweli ninachoonesha ni kwamba kuwa wapo watu wanaoitwa "baba" kwa kuzaa. Kwamba mtu aliyekuzaa huwezi kumuita "baba" kama baadhi walivyokuwa wanadai. Ninachoonesha ni kuwa wapo "baba" katika Uislamu. Nipo napitia Hadithi hapa (Bukhari na Muslim) na naweza kuona mara kadhaa ambapo watu walipewa ushauri kwa "baba" zao au kuhusiana na "baba" zao. Kwamba, inaruhusiwa kumuita mtu "baba" halina shaka kama mistari hiyo inavyoonesha. Ama sivyo?

Acha unafiki wewe..

Qurani inasema " Wazee wenu" hakuna sehemu inayosema baba zenu

Omba msamaha mkuu acha tricks??

Usilazimishe mambo ya kanisani kwenu kwenye uislamu ok..

omba msamaha mku tafadhali
 
Topical - tafuta tafsiri nyingine ya Kiswahili utaona inatumia maneno hayo ya "baba"; Tafsiri ninayotumia ni ya Shehe Barwani na inatumia maneno hayo. Hata tafsiri za Kiingereza kama ya Yusufali inatumia hivyo. HIyo ya 37:126 inasema "Al-Laha Rabbakum Wa Rabba 'Ābā'ikumuAl-'Awwalīna" Topical aya haisemi "wazee" inasema "baba zenu". Niko sahihi na wewe uombe radhi kwa kusema kitu ambacho Qurani haisemi!

Mkandara - ni kweli ninachoonesha ni kwamba kuwa wapo watu wanaoitwa "baba" kwa kuzaa. Kwamba mtu aliyekuzaa huwezi kumuita "baba" kama baadhi walivyokuwa wanadai. Ninachoonesha ni kuwa wapo "baba" katika Uislamu. Nipo napitia Hadithi hapa (Bukhari na Muslim) na naweza kuona mara kadhaa ambapo watu walipewa ushauri kwa "baba" zao au kuhusiana na "baba" zao. Kwamba, inaruhusiwa kumuita mtu "baba" halina shaka kama mistari hiyo inavyoonesha. Ama sivyo?
Hapana mkuu nadhani umevamia mada. kilichosemwa ni kwamba huwezi kumwita mtu yeyote baba katika Uislaam isipokuwa yule alokuzaa... Ubishi huu umetokana na Nyerere kuitwa baba wa Taifa, Faizafoxy akasema hawezi kuwa baba wa Taifa wala babayake kwani hakumzaa..Watu ndio waka quote semi za waraabu na nchi za kiislaam kama Pakistan, saudia na kadhalika bila kujua kwamba hata hawa ni watu wa makabila na wanazo tamaduni zao mbali na dini..
 
Kabla ya baba JULIUS nyerere alikuwepo baba ABDULWAHID sykes ( ametufundishwa hivyo baba Mohamed said). na hakuna kupinga hilo sababu yeye amejadiliana hayo hadi na waprofessor wa USA kwa "paper".

Nani anabisha ajitokeze
 
Hapana mkuu nadhani umevamia mada. kilichosemwa ni kwamba huwezi kumwita mtu yeyote baba katika Uislaam isipokuwa yule alokuzaa... Ubiushi huu umetokana na Nyerer kuitwa baba wa Taifa na watu waka quote semi za nchi za kiislaam kama Pakistan, saudia na kadhalika bila kujua kwambahata hawa tu wanazo tamaduni zao mbali na dini..

Mkandara, mstari ambapo Nabii Ilyas anawaambia Waisraeli kuhusu "baba" zao wa zamani; unafikiri inamaanisha wale waliowazaa au wazee waliowatangulia?
 
Hapana mkuu nadhani umevamia mada. kilichosemwa ni kwamba huwezi kumwita mtu yeyote baba katika Uislaam isipokuwa yule alokuzaa... Ubishi huu umetokana na Nyerere kuitwa baba wa Taifa, Faizafoxy akasema hawezi kuwa baba wa Taifa wala babayake kwani hakumzaa..Watu ndio waka quote semi za waraabu na nchi za kiislaam kama Pakistan, saudia na kadhalika bila kujua kwamba hata hawa ni watu wa makabila na wanazo tamaduni zao mbali na dini..

Hana lolote anataka kulazimisha kwa kuandika Quran ambandavyo yeye?? aya inasema wazee wenu wala si baba yenu..

Mnafiki mwambie aombe msamaha.
 
Acha unafiki wewe..

Qurani inasema " Wazee wenu" hakuna sehemu inayosema baba zenu

Omba msamaha mkuu acha tricks??

Usilazimishe mambo ya kanisani kwenu kwenye uislamu ok..

omba msamaha mku tafadhali


Weka hilo neno la kiarabu ambalo linaamanisha "wazeee wenu"... na si "baba zenu"...
 
Mkandara, mstari ambapo Nabii Ilyas anawaambia Waisraeli kuhusu "baba" zao wa zamani; unafikiri inamaanisha wale waliowazaa au wazee waliowatangulia?

Mstari upi mkuu??

37: 126 unasema wazee wenu hakuna baba zenu..

usipotoshe kitabu cha Allah
 
Mkandara said:
ukisema - Mungu mkubwa haikufanyi wewe uwe mkristu lazima useme Allahu Akbar ndio uwe muislaam wakati hata waarabu wakristu watasema hivyo hivyo..hii ni lugha tu lakini mwambie Mdanganyika akisikia Allahu Akbar basi ndio Uislaam.

Mkandara nimefuatilia bandiko lako na nimejaribu kukupata.

However mkuu wangu hilo la kusema ni just lugha si kweli kwa upande mwingine kwasababu kuna ule usemi kuwa "There is no God but Allah"

Kwahiyo unaweza kuona shida ilipo mkuu...
 
mnataka kuanzisha mambo yenu sasa muaribu thread yote, neno baba kwenye thread ni kama metaphor tu ya muasisi, muanzilishi na mengineo to do with political field-specific lexis. Hizo maana zenu azituhusu humu ndani kwani nyerere tunajua ajatuzaa wote humu sasa sijui kwanini mntaka kutuletea hizo maana zenu humu kwenye jukwaa la siasa. Baba humu inamaana nyingine kwetu ingawa tunajua ajatuzaa huyu mwl na wala hatuna uhusiano nae kibailojia hila neno limesimama kama mtu wa kupewa hesima zote kitaifa kutokana na aliyotufanyia.

jamani tafadhalini hivi kwani jukwaa la dini limefungwa these days au vipi mods?
 
Sheikh Abdullah Saleh Al-Farsy

Well, tafrisi ya Sheikh Al-Farsy ilitangulia tafsiri ya Barwani. Yeye Barwani anasema hivi kuhusu tafsiri yake: "Kwa hivyo kama ilivyo mkinika Tafsiri hii ya AL-MUNTAKHAB imejaribu kuepuka khitilafu za kimadhehebu katika mambo ya Fiqhi na Itikadi. Kwa sababu hii na kwa kuwa imejaribu kueleza mambo ambayo yamekwisha hakikishwa na ilimu za sayansi, ndio nikavutika nayo mimi na nikataka kuiandika kwa lugha ya Kiswahili, ili Waswahili wenzangu wasio jua Kiarabu wapate nao kuifahamu na iwaongoze kama ilivyo niongoza mimi. Kwa kuwa urefu wake ni wa wasitani, wa kutosha kufahamisha, na si wa kuchosha, basi nimeona ni mnasaba sana kwa wasomaji wa Kiswahili ambao wamekwisha onjeshwa utamu wa Qur'ani kwa tafsiri za Sheikh Al-amin bin Aly Mazrui na Sheikh Abdulla Saleh Al-Farsy au walio isikia ikisomwa tafsiri ya Jalaleini misikitini."

Tafsiri ya Barwani iko karibu sana na maana ya Kiarabu.


weka mstari mzima wa 37:126
 
Back
Top Bottom