Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

U "baba" unatumika kanisani kuanzia "Mungu baba", "Baba Mtakatifu", "Baba Padri", na sasa tunalazimishwa "Baba wa Taifa". Utamlazimishaje Muislaam atumie vyeo vya kanisani wakati dini yake hamruhusu? kama si udini ni nini?

Huko juu nimetowa mpaka aya ya Qur'an inayokataza hata Mtume Muhammad kuitwa "baba" nimeonesha pia kuwa hata katika sifa za Mwenyeezi Mungu Kiislaam, hakuna sifa ya ubaba. Na pia kiislaam "baba" ni yule aliyekuzaa tu, hata mume mwingine wa baba yako hupaswi kumuita "baba" labda kwa wasiyoyaelewa mafundisho ya Kiislaam.

Nakushangaa unapoona mimi nnaelipinga hili la udini wa kulazimishana kumuita mtu baba kama wafanyavyo wakatoliki lakini wanaolazimisha hili huwaoni kuwa wadini. Unanshangaza sana.

Umeletwa ushahidi hapa kwamba nchi za kiislamu ama zilizo na idadi kubwa ya waislamu kama Uturuki, Pakistani, Saudi Arabia na india wanao watu wao wanaowaita "baba wa taifa".
Kwa ubishi wako unajifanya wewe ndiye muislamu kuliko wao. Yani dini wakuletee wao halafu wewe unajidai kuifahamu kuliko wao wenyewe! Kwamba wao hawafahamu kwamba neno baba ni la kikanisa!? kama huu ndio uislamu mnaofundishwa hapa Tanzania, basi mna kazi kubwa ya kufanya.
 
Aliyakuta zaidi ya hayo, usitujaze ujinga kuwa kayaleta yeye, neno "Sheikh" kiarabu ni kama Kiswahili "Mzee" kwa hiyo ukisikia mtu anaitwa Sheikh Nyerere wala usishangae. Ni simply imemaanishwa Mzee Nyerere, lakini si "baba". NO.

Mama Faiza Foxy unaumiza sana kichwa chako, wewe mwite unavyotaka, nao hao wanaotaka kumwita Baba wa Taifa, mjomba wa Taifa, babu wa Taifa waachie, hakuna kipengele kwenye katiba kinachokulazimisha kumwita Mwl. Nyerere Baba Taifa, hiyo ni heshima tu chagua unaloona linakufaa.

Chama
Gongo la Mboto DSM.
 
Hatutaki heshima za Kikatoliki, hukohuko kanisani, huo ndio udini wenyewe, kwanini mlazimishe kitu ambacho kinawaudhi wengine?

Mama Faiza Foxy labda mimi nilipitwa kuna siku ambayo serikali yetu iwe tangu mh. Raisi (mstaafu) Benjamini Mkapa au hii ya sasa ya mh. Jakaya Kikwete ilitoa shurutisho la kuwataka watanzania wamwite Mwl. Nyerere Baba wa Taifa? Wewe kwa nafsi yako ulipendelea tumwite vipi?

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Nimemuomba mwandishi wa hii article arekebishe kwanza. Marekani haina "Baba" as singular, pale kuna Plural "Fathers" as Founding Fathers.

Also, unashindwa kuelewa kwamba hayo mataifa uliyoyataja yaliwahi kutawaliwa na hao Wazungu (Wakristo) kabla ya kupewa Uhuru wao. Sas ni nini hoja yako.

Sijaelewa msingi wa hoja yako kwani universally, George Washington is regarded as father of his nation - USA;

Kuhusu hoja ya kutawaliwa na wazungu ndio kigezo cha kumuita mwanaharakati aliyeongoza mapambani dhidi ya ukoloni BABA WA TAIFA is a fallacy from the outset; China ina founding father wake Sun Yat - Sen, anaetambulika kidunia, katika jamii ambayo ilikuwa predominantly non - Christian;
 
Mkuu FairPlayer,

Swala la vita vya Kagera limekuwa likipotoshwa na watu kwa muda mrefu. Nina hakika kwamba maamuzi ya Nyerere kumpiga Idd Amin, yangeweza kufanywa na Rais yeyote yule ambaye angekuwa madarakani wakati huo. Huwezi ukavamiwa halafu ukakaa kimya bila kujitetea au kulinda mipaka yako.

Ni ukweli ambao haupingiki kwamba mapinduzi ya Obote hayakumfurahisha Nyerere. Obote alikimbilia Tanzania na kuomba hifadhi lakini pia alikuwa bado anatamani kurudi madarakani. Kitendo cha Nyerere kukubali kumweka Obote Dar es Salaam kwa namna yoyote ilikuwa ni kujitakia matatizo kwa sababu Idd Amin lazima alijua kwamba Obote anaweza kuitumia Tanzania kuandaa mashambulizi ya kumrudisha madarakani, kwa hiyo kitendo cha Obote kukubaliwa kuishi Dar es Salaam kiliongeza kutoaminiana kati ya Uganda na Tanzania na given kwamba Nyerere hakuitambua serikali ya Idd Amin mara baada ya mapinduzi.

Hilo la Obote kutaka kurudi madarakani ni kweli lilifanyiwa majaribio mwaka 1972, lakini liliwahusisha akina Museven na wapinzani wengine ambao walikuwa ni vijana wa Obote. Obote alijua kwamba alikuwa na support kubwa within Uganda na kumbe he was wrong na ndio maana hawakufanikiwa. Kwa bahati mbaya kabisa zoezi hilo halikufanikiwa na matokeo yake ilikuwa ni kumfanya Amin arushe mabomu Mwanza na Bukoba. Kwa kuwa Nyerere alijua kosa lake, wala majeshi ya Tanzania na serikali yake hawakujibu kitu waliishia kimya kimya.

Tension iliendelea kwa muda mrefu, akina Museven walifungua kambi za mafunzo ya vijana wa kutoka Uganda ambao walikuwa wamekimbilia Tanzania. Lakini kwa kuwa kitengo cha usalama cha Amin kilikuwa makini sana, habari zilimfikia Amin kuwa Tabora (to be specific, Kigwa) kulikuwa na kambi za vijana wa Uganda chini ya Museveni. Kwenye makubaliano ya Mogadishu ya ku-difuse tension kati ya Tanzania na Uganda, Uganda ilitoa condition ya kufungwa hiyo kambi ya Kigwa na Nyerere alikubaliana nao na ilifungwa. Ndipo Museven alipohamia Nachingwea ambako ilikuwa ni ngumu sana kwa Amin kujua kinachoendelea kwani mikoa ya huko kusini ilikuwa na askari wengi sana na wengine walikuwa masalia ya askari wa marehemu Samora. Wakati haya yote yakitokea Nyerere alisha-give up plan yoyote ya kumsaidia Obote kurudi madarakani baada ya makubaliano ya Mogadishu.

Mimi nilikuwa mmoja wa watu waliokuwa wakiamini kwamba Tanzania ndio ilimchokoza Idd Amin mwaka 1978, lakini ukweli ni kwamba Amin ndiye aliichokoza Tanzania. Tanzania haikuwa imejiandaa kwa vita ya aina yoyote ile na Uganda na ndio maana ilichukua karibu mwezi mzima kwa Tanzania kuanza vita rasmi tangu siku askari wa Amin walipobomoa daraja la mto Kagera na kupandisha bendera ya Uganda ndani ya mpaka wa Tanzania.

Kuthibitisha hili, askari waliokwenda frontline mwanzoni kabisa mwa vita walitoka Songea, vikosi vya kusini ndio pekee ambavyo vilikuwa tayari na ninadhani ni kwa sababu Nyerere alikuwa anahofia zaidi nchi za kusini kuliko nchi za kaskazini na magharibi mwa Tanzania. By then Banda alikuwa haeleweki na pia hali ya Msumbiji ilikuwa bado iko tete na Angola pia moto ulikuwa unawaka na Zimbabwe walikuwa bado hawajapata uhuru. So, vikosi vya kusini vyote vilikuwa viko ready masaa 24 kwamba lolote likitokea ni swala la kusogeza zana na kazi inaanza.

Hii clip angalia/sikiliza kuanzia 05:22 na kuendelea mbele kidogo ili umsikilize Amin kwa kauli yake mwenyewe akiwa anatamba na bendera ya CCM.

Vita vya Kagera (Kagera War) - Part 1 of 4 - YouTube

Sasa swali linakuja, je, baada ya huo uhuni alioufanya, ni Rais gani wa nchi angekaa kimya bila kujibu? Ndugu zangu wachagga hata ukiingia hatua moja ndani ya mpaka wa kihamba yake atakutokea na panga. Ndio ije kuwa umevuka mpaka, umevunja daraja na kuua wananchi wake halafu akuache tu?

Kuna wengi ambao wanasema kwamba tulitakiwa ku-reclaim ardhi ambayo ilikuwa imechukuliwa na then tuishie hapo. Lakini kuishi ujirani na mtu kama Amin ni kujitakia matatizo, maana huwezi jua next atakuja na nini. Nyerere alishafanya assessment ya na kujiridhisha kwamba Amini alikuwa anapigika tu na kwa msaada wa akina Museveni ambao walikuwa na contacts within Uganda. Kama Tanzania ingefanya kosa la kumwacha Idd Amin madarakani basi tungeendelea kuwa kwenye tension siku zote na kusubiri mpaka Mungu amchukue Amin na huwezi jua ni nani angefuata baada ya Amin.

Ni kweli Tanzania tulikumbwa na hali ngumu ya uchumi mwanzoni mwa miaka ya 80 na kuendelea, lakini it

Sasa hueleweki, kitendo cha kuwahifadhi na kuwapa mafunzo ya kijeshi wapinzani wa Idd Amini ndani ya aridhi yetu kinaashiria nini kama siyo dalili za uchokozi? Umekubali kuwa baada ya mwanza kupigwa Tanzania haikujibu, kwa nini? Je waliotaka kumpindua Amin mwaka 72 si walikuwa wanatokea katika aridhi ya Az, je huo sio uchokozi? Kwa ni nini Nyerere alikiuka mkataba wa Mogadishu, alikuwa na nia gani?
 
Aliyakuta zaidi ya hayo, usitujaze ujinga kuwa kayaleta yeye, neno "Sheikh" kiarabu ni kama Kiswahili "Mzee" kwa hiyo ukisikia mtu anaitwa Sheikh Nyerere wala usishangae. Ni simply imemaanishwa Mzee Nyerere, lakini si "baba". NO.

Maana yangu hapa ni kwamba upande mwingine wa dini, watanzania wengi hawajali kuwaita neno lolote la kuonyesha heshima kwao hata kama haitokani na dini yao, iwe ina maana ya neno kaka, mjomba, ndugu n.k; hiyo ndio Tanzania ya Nyerere ninayoizungumzia na nitakayojivunia mpaka tamati yangu duniani kama Mtanzania;
 
Al Haj sio "title" ya kitaifa ni "title" ya Kiislaam kwa aliyekwenda kuhiji Makkah, na kwa wanawake ni Hajat, kama utamuita ni sawa na kama hujamuita ni sawa, si "title" ya Kitaifa.

"Baba" ni title ya kikatoliki sasa tuambiwe na yeye alikuwa analitumikia kanisa ndio anapewa hiyo "title" maana kitaifa hakuna "title" hiyo na Waislaam hatuikubali kwani inakwenda kinyume na mafundisho yetu, na hii nchi si ya wakatoliki pekee. Hatuwezi kuwa na vyeo vya kanisani "unless" mtuambie kuwa Nyerere alikuwa "baba" wa kanisa, na tutamuita hivyo, "baba wa kanisa" na si baba wa taifa. Mbona ma "padri" hatuna shida nayo tunawaita hivyo? kwani ni vyeo vyao vya kanisani.
FF ni mabaki yale ya 1990s ya kutaka kusilimisha Africa baada ya kushindwa "HASIRA KAMA MTOTO MWENYE UTAPIAMLO" kila siku uislam , ukristo. uislam, ukristo, uislam ukristo these parots"!!!!
 
Hivi nyerere ni baba wa taifa wa zanzibar?

Kama ndiyo, then how?
Kama siyo, then atakuwaje baba wa taifa la tanzania, wakati hakualify kuwa baba wa taifa wa zanzibar ambayo ni nchi, na pia ni sehemu ya tanzania?

Kama Uasisi wa Taifa la Tanzania ndiyo kigezo cha kuwa baba wa Taifa, Je mzee Karume?, naye si ni muasisi wa Tanzania?, kwa nini yeye siyo baba wa Taifa wa Tanzania. Zanzibar na Tanganyika si ziliungana kama equal partners au?, sasa vipi muasisi mmoja ndo aonekane kuwa baba wa Taifa na si mwingine?.

Mahatma Gandhi hakuwa raisi wala Wazirimkuu wa India, lakini mmemuita baba wa Taifa la India, kumbe basi UNAWEZA KUPEWA HESHIMA YA BABA WA TAIFA PASIPO KUWA RAISI WA KWANZA WA TAIFA HILO.

TANZANIA TUNA FATHERS OF THE NATION, SIYO FATHER OF THE NATION(MMOJA), MIONGONI MWAO NI WALE 17 WALIOTAJWA NA JK, NA WENGINE AKINA KARUME, ABDULRAHMAN BABU, NASSORO MOYO, KAWAWA , KAMBONA ETC.

NI VIZURI HAWA WOTE TUKAWAPA HESHIMA YA UBABA WA TAIFA NA SI NYERERE PEKE YAKE.

Suala la Nyerere na ubaba wa muungano nimelielezea kwa kina kwenye hoja yangu ya msingi, tafadhali rejea;

Kuhusu Mahatma Ghandi, kama ulinisoma vizuri, nilisema kwamba mara nyingi, sio wakati wote, kiongozi wa harakati hizo uendelea na kuwa Rais wa kwanza wa taifa huru husika. Na ondokana na mtazamo kwamba ubaba wa taifa unakuja pale tu mapambano ya uhuru yanapoisha na kiongozi huyo kuwa rais wa kwanza; Nyerere hakuwa baba wa taifa mwaka 1961 au Mwaka 1970; Hata kina Ghandi na wengineo, heshima hiyo haikuja kwa namna hiyo; naomba utumie muda kidogo kutafakari mambo na pia uwe unafanya utafiti kidogo, itasaidia mjadala huu utawaliwe na hoja za kutojirudia rudia na badala yake hoja ya kusonga mbele;

Kuhusu Kambona, naona haujui historia ya nchi hii vizuri, jaribu kuisoma kidogo uelewe nafasi ya Kambona katika harakati hizo kama inafanana na kina Nyerere, Kunambi, Kandoro na wengineo;

Ni muhimu ukasoma historia ya harakati za taifa hili ili ubaini what qualifies taifa letu - father of the nation au founding fathers; mtazamo wako ni kama as if hata mapambano ya kumtoa mkoloni Mwalimu aliwaburuza watu na kutumia mabavu na udikteta, kitu ambacho sio inherent na mapambano yoyote ya kujikomboa; soma historia ya nchi yako Tanzania ili uelewe nini kilichojiri mpaka mwalimu akastahili sifa hiyo badala ya kina kawawa na wengineo;
 
Sisingizii dini yangu napinga kuletewa "title" za kikatoliki "kidini" zikawa za kitaifa huo ni udini wa hali ya juu, halafu mtu akipinga nyie ndio wa kwanza kumuita mdini, wakati ukweli mnauona.

Neno Rais linatokana na Kiarabu "Ray'es". Kumbuka unaongea na FF hapa, ni cheo kipi cha kanisa ni Rais? ustake kuzuga hapa.
TEC inaongozwa na nani? Pope unamlinganisha na nani hapa nchini? Sheria tulizonazo zimetoka wapi? Unazikumbuka zile AMRI 10 za Mungu? FF huyu wa sasa sio yule wa mwanzo!
 
Suala la Nyerere na ubaba wa muungano nimelielezea kwa kina kwenye hoja yangu ya msingi, tafadhali rejea;

Kuhusu Mahatma Ghandi, kama ulinisoma vizuri, nilisema kwamba mara nyingi, sio wakati wote, kiongozi wa harakati hizo uendelea na kuwa Rais wa kwanza wa taifa huru husika. Na ondokana na mtazamo kwamba ubaba wa taifa unakuja pale tu mapambano ya uhuru yanapoisha na kiongozi huyo kuwa rais wa kwanza; Nyerere hakuwa baba wa taifa mwaka 1961 au Mwaka 1970; Hata kina Ghandi na wengineo, heshima hiyo haikuja kwa namna hiyo; naomba utumie muda kidogo kutafakari mambo na pia uwe unafanya utafiti kidogo, itasaidia mjadala huu utawaliwe na hoja za kutojirudia rudia na badala yake hoja ya kusonga mbele;

Kuhusu Kambona, naona haujui historia ya nchi hii vizuri, jaribu kuisoma kidogo uelewe nafasi ya Kambona katika harakati hizo kama inafanana na kina Nyerere, Kunambi, Kandoro na wengineo;

Ni muhimu ukasoma historia ya harakati za taifa hili ili ubaini what qualifies taifa letu - father of the nation au founding fathers; mtazamo wako ni kama as if hata mapambano ya kumtoa mkoloni Mwalimu aliwaburuza watu na kutumia mabavu na udikteta, kitu ambacho sio inherent na mapambano yoyote ya kujikomboa; soma historia ya nchi yako Tanzania ili uelewe nini kilichojiri mpaka mwalimu akastahili sifa hiyo badala ya kina kawawa na wengineo;

Wacha kuruka ruka wewe, inaelekea hujui Nyerere ameanza kuitwa baba wa Taifa lini, kwa kukusaidia tu ni kwamba hoja yako iko emotional, ina flaws nyingi.

Wewe unadai heshima ya BABA WA TAIFA NI SUALA LA KISHERIA, Lete hiyo Sheria basi inayotamka kwamba Nyerere ni Baba wa Taifa la Tanzania, unazunguka zunguka.

nakukumbusha kwenye hoja yako ya msingi unasema hivi:
Ubaba wa taifa sio Mapenzi ya mtu mmoja mmoja aidha kwa kutumwa au kwa juhudi binafsi bali ni heshima kwa mujibu wa sheria kama tulivyokwisha ona

LETE HIYO SHERIA MJOMBA, INAYOSEMA NYERERE NI BABA WA TAIFA.
 
Baba wa Taifa ni mmoja na ni Hayati Julius Nyerere....


Tena imetokea sana hii tabia hasa katika uongozi wa awamu nne na ninasikia BOSi mwenyewe hajawahi kumuita Baba wa taifa na hataki na wala haamini kuwa Nyerere ni baba wa taifa ILA ANAMUITA MZEE NYERERE SAWA NA WAZEE WENGINE. KUNA MTU ALINUAMBIA NA KWELI MKIMFUATILIA KATIKA HOTUBA ZAKE ZOTE HAJAWAHI KUMUITA BABA WA TAIFA.
 
safi sana kwa hoja. wanaomchafua baba wa taifa kuficha madhaifu yao wanajisumbua watanzania hawa si wale wa jana kifikra wanajua wapi mbivu wapi mbichi na wanaoingiza udini tusibishane nao coz ni kupitiwa kwa elimu ndio tatizo ila nawaombea tuelemishane zaidi kihoja kama member wangu ulivyofanya thank u
 
CHINA INA HISTORIA ZAIDI YA MIAKA 5000, KUNA EMPERORS, TANG, QIN, ZHOU, NA DYNASTIES KIBAO! NA WACHINA WANAJIVUNIA SANA HISTORIA YAO HIYO, CHINA ISHAKUWA SUPERPOWER MIAKA MAELFU KABLA YA HUYO SUN-YAT-SEN.

SASA UNAPOKUJA NA HOJA ETI, UBABA WA TAIFA NI WA MILELE NA MTU AKISHAUPATA HAUMPONYOKI, WACHINA WATAKUCHEKA.

WACHINA WAO WAMECHARACTIZE HISTORIA YAO KATIKA (1) ANCIENT CHINA (2) MODERN CHINA, AKINA SUN-YAT-SEN ARE FATHERS OF MODERN CHINA, NA EMPERROR KAMA Qin Shi Huang( FIRST Emperror) Ni father of Ancient China. SASA SWALI KWAKO NI JE KWA MUJIBU WA HOJA YAKO YA "UBABA WA TAIFA MTU AKIISHAUPATA HAUBADIRIKI" WEWE UNAONA FATHER WA CHINA NI NANI KATI YA HAO WAWILI?.

TUKIACHANA NA YOTE HAYO BWANA MCHAMBUZI, WEWE UMELIHUSISHA SUALA LA HESHIMA YA UBABA WA TAIFA KUWA LA KISHERIA, UKISHINDWA KUTHIBITISHA HILI, MUOMBE MOD AONDOE HII THREAD, KWA SABABU ITAKUWA IMEJENGWA KATIKA FLAWED PREMISES NA WRONG ARGUMENTATION PRINCIPLE!.

PIA NAOMBA UJENGE CASE VIZURI YA KWA NINI MWALIMU NYERERE APEWE HESHIMA YA UBABA WA TAIFA "PEKE YAKE", SO FAR ULICHOKIELEZEA KATIKA MADA YAKO NI SIFA NYINGI SANA ZA GEORGE WASHINGTON NA SI ZA MWALIMU, THEN UKACONCLUDE BY "ASSOCIATION" KWAMBA THEREFORE MWALIMU NDO AWE BABA WA TAIFA "PEKE YAKE".

WEKA POINT ZAKO MCHAMBUZI, KWA NINI NYERERE AWE BABA WA TAIFA LA TANZANIA NA SI KARUME SENIOR?(MAANA MIMI NA WEWE TUNAKUBALIANA KWAMBA KUWA RAISI WA KWANZA SI KIGEZO CHA KUWA BABA WA TAIFA, TUKATOLEA MFANO WA MAHTMA GANDHI WA INDIA)
NATAKA a,b,c,d THEN TUTAZICHAMBUA HIZO POINTI, NA PIA USISAHAU KUTULETEA SHERIA INAYOSEMA KWAMBA NYERERE NI BABA WA TAIFA KAMA ULIVYOSEMA KWAMBA IPO.
 
Kwanza kabisa mimi sikubaliani na hilo "baba" wa Taifa, huo ni ukatoliki na hutumika kanisani kuwaita wachungaji "baba", kumuita "papa" "baba" mtakatifu.

Hii nchi Nyerere aliikuta ina watu wa imani tofauti na ameondoka ametuwacha watu wa imani tofauti, kwanini mtubambikie vyeo vya kikatoliki na Kikristo? hamuoni kuwa huo ni "udini" wa wazi wazi?

Hakuna "baba" wa Taifa, huo ubaba alipewa na nani na kwa ridhaa ya nani? msitujaze ujinga.
Magonjwa ya asili haya. Vipi kule uchina ambapo imani ya kikiristo na ukatoliki ni uhaini? Je hawaiti Baba wa taifa?
 
Hayo yote unaotetea yanakwenda kinyume na mafundisho ya Uislaam. Hakuna baba zaidi ya baba yako aliyekuzaa. Huo mwingine wote ni Ukatoliki.
Nikikuita Mama FaizaFoxy hautaitika. Huku kungine kuna Mama Maria Nyerre, Mama Salma Kikwete,...DINI yako inaruhusu kuwaita hivi hawa?
 
Aliyakuta zaidi ya hayo, usitujaze ujinga kuwa kayaleta yeye, neno "Sheikh" kiarabu ni kama Kiswahili "Mzee" kwa hiyo ukisikia mtu anaitwa Sheikh Nyerere wala usishangae. Ni simply imemaanishwa Mzee Nyerere, lakini si "baba". NO.
Unataka kutuambia na kale katoto kalikokuwa kanafanya "miujiza" kakaitwa Sheikh Sharifu mlikuwa mnamaanisha Mzee Sharifu?
 
Hatutaki heshima za Kikatoliki, hukohuko kanisani, huo ndio udini wenyewe, kwanini mlazimishe kitu ambacho kinawaudhi wengine?
Mbona wale wazee Ustaadh wapigania uhuru maarufu waliona na ku-surrender na kumpa uongozi na urais kafiri yule Julius Kambarage Nyerere? unaakili fupi kweli wewe. zimejaa ma-biases!!!!
 
Jihabari reefu, kuandika kooote huko unataka tumuite Nyerere "baba"? Unanchekesha, huo ni ukatoliki. Hata Kikwete sijamsikia akimuita hivyo Nyerere. Upelekeni ubaba kanisani, huku wananchi tuwacheni tumuite Mwalim Nyerere.

Hakuna Muislaam anaefata Uislaam wake atathubutu kumuita Nyerere baba, labda wale mnakutana kwenye mabaa.

Mwandishi ameelezea utofauti kati ya Baba na Rais bora wa Taifa,kila mtu ameelewa,labda kama mtu hakubali. Halafu ameonyesha kuwa asili ya ubaba wa taifa ama jina hilo haikutokea kanisa katoliki wala si Roma wanaotoa jina hilo kwa viongozi wa nchi hapa duniani,iwe za kiislamu au kikristo. Hata hatukuwahi kusikia aliyetoa jina hilo alikuwa kardinali Rugambwa au Pengo! Mi nadhani imechukuliwa kifamilia zaidi kwamba...kiongozi wa familia huwa ni mwanamume. Na kwa bahati ni kwamba wanaharakati wengi katika ukombozi na mapinduzi ya nchi zao,walikuwa wanaume... Kifamilia kuna mambo ambayo hayakamiliki hadi baba aje.. Heshima ya ubaba,ni kuonesha uongozi,msimamo,ujasiri,vision,na maamuzi ambayo hata kama yatapingwa na watoto au wake zake,ya baba yanakuwa ya mwisho.. Someone can correct me ila huo ndiyo ufahamu wangu.
 
Kwanza kabisa napenda kumpongeza mwandishi kwa kuwa jasiri wa kutoa hisia zake bila woga. Hisia zilizojikita zaidi katika itikadi yake ya chama. Lakini amekuwa mwalimu zaidi badala ya kuwa mwenye kujadili. Amejitahidi sana kuonyesha heshima zinapatikanaje. Tumemuelewa.Lakini wakati unaanzisha mada kama hii lazima ufahamu kuwa wapo watu wanaomfahamu zaidi Julius Kambarage Nyerere kuliko wewe. Nina maana waliotawaliwa na Nyerere wakiwa watu wazima, wakfanya kazi naye na wakaonja matamu na machungu ya utawala wake. watu hao wakipewa uhuru wakueleza hisia zao naona wanaweza kukamatwa Haitoshi kutafuta uhuru ikawa tiketi ya kupewa heshima milele. Naomba nimjuze mwandishi kuwa mada yako inaweza ikahamasisha watu wakatoa michango ambayo badala ya kujenga heshima ya Nyerere ikamshusha zaidi sijui kama hili nalo uliliangali kabla hujaamua kuandika. kwa sababu mwandishi amekuwa wazi ni vema akatujuza hicho cheo cha baba wa taifa alipewa na nani wapi na kwa utaratibu upi. Siku nyingine usijaribu kuwashawishi watu waamini kile unachoamini wewe na kudai wanaotoa maoni wasiachiwe kutoa maoni. kama kuna mpotoshaji ambaye ameandika kabla ya kuijua historia ya Tanzania basi ni wewe.
 
Mchambuzi, I have just read this article from the Economist (Bonyeza hapa) na nipofika kwenye hizi para nikakumbuka maandishi yako. Kudos mkuu!!!!!

x5z6nl.jpg




Sure, the founding fathers of most countries are pretty warty when you look at them up close. George Washington massacred Native Americans. David Ben-Gurion ordered Israeli troops to carry out ethnic cleansing during the War of Independence; Yitzhak Shamir was personally involved in assassinating the morally irreproachable Swedish diplomat Folke Bernadotte.

Mahatma Gandhi...well, he was apparently exploitative with the ladies. But the fact is that the liberation strategy of terror against Israeli civilians that Yasser Arafat and the Palestinian leadership selected in the 1960s-80s was really pretty grotesque and inexcusable, even compared to the sins committed by a lot of other founding fathers. Given repeated chances to pull a Nelson Mandela in the 1990s, he never quite managed to rise to the occasion, and to some extent his people are still paying the price, though obviously Binyamin Netanyahu and Israeli religious-nationalist fanaticism have played a very large role as well.

Nonetheless, Mr Arafat remains the founding father of the Palestinian national movement

Anywayz anachokielezea mwandishi hapo juu ni kwamba pamoja na madhila na mapungufu ya hao aliowataja bado wanabaki kuwa the founding fathers.
 
Back
Top Bottom