Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Safari njema Nyaronyo, huenda mtakuwa katika mahusiano mazuri na Kikwete, maana wiki iliyopita ulilalamika kuachwa katika uteuzi wa wajumbe wa Bunge la Katiba, licha ya kukidhi vigezo vyote

Mkuu, naona hujamwelewa Kicheere. Huyu mwanasheria ni mshairi pia, hiyo habari ni 'satire' flani hivi. Hao ameongelea kinyume kabisa na mawazo ya wengi, kwamba kahamia CCM. Isome tena hiyo habari uielewe.
 
Aende tu,bora tufike 20 wenye nia 1 kuliko 1000 wanafiki na wasaliti.

ni mchumia tumbo sana.

Chadema imesambaratika kwa uzushi

kumbe ndiye huyu? the same Psychological problems as TSAVERY LWAITAMA.

Naam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu

CCM inapendwa jamani, tuache utani

Jina lenyewe ukiita tu vidonda vya tumbo hapo hapo.Kwani akihama lazima kila mtu ajue au sifa za kijinga tuu.

Sidhani kama CCM wanaweza kumpokea huyu hata wakipewa bure. Huyu ni mmoja wa waliomwandikia Rais KIMEMO cha kutaka ateuliwe kuwa Mjumbe wa Bunge la Katiba, taarifa zimevuja.

Kweli Mungu hakupi vyote!!!
 

Huyu si alisema Kikwete anamchukia bila ya sababu? Kafuata nini tena huko CCM?


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...cheere-kikwete-ananichukia-bila-sababu-3.html

Nyaronyo-Mwita-Kicheere.jpg

Mkuu, hukumuelewa mwandishi. Soma katikati ya mistari utaelewa kuwa ni kinyume cha mambo!
 
anayejiunga ccm atakuwa na matatizo ya akili huyo ccm imeshakufaaaaa
 
Naam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu
Nawe umeingia kichwa kichwa bila kufikiri. Rudia kusoma uelewe, au umeshapata sembe tayari.
 
Heko sana nyaroyo, nimefurahi kusoma bandiko lako. Watu wengi umewachanganya maana kwenda shule na kuto kwenda shule tofauti yake imeonekana leo. Wote ambao hawajaelewa ujumbe huu, jitahidi kuto kubishana nao maana shule ilikuwa ngumu kwao.
 
Huyu mzee ni kiboko anajua kuwasilisha kazi zake kifasihi zaidi ,kwa mtu uelewa wake kama wa panzi hatamuelewa kamwe.
 
Naam, ngoma inogile, tutampokea tundu lissu na pro.safari na baregu sio mda mrefu
Hakika wewe ulipata division 5,Somo la fasihi lilikupitia pembeni sana.Nakushauri soma between lines usilete UMACCM WAKO wa kipimbirism
 
Mungu wangu...watu hawasomi...lol...watanzania tuna tatizo kubwa
 
Kupitia uzi huu ndo natambua akili za watanzania...
Wengi wanazan kweli kahamia ccm

Jamani fasihi nzuri sana.... na wajinga wangali wengi sana taifa hili lafwa...

Eleweni mada kwa fasihi inastajabisha mtu anasema eti karbu ccm mara hawez kuja ccm mara huyu huyu aloandika kuulaani uteuz aje ccm...

Bongo bana.... nyaronyo kanyaga twende
 
Back
Top Bottom