Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Nyaronyo Kicheere 'ahamia CCM'

Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha, Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.

Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----

mwambie akamchukulie mke ndiyo atajua ni mtu wa kusamehe au la.
 
Inaelekea Fasihi andishi na fasihi simulizi na uandishi wa kutumia picha ilishia miaka ya 1990.Sidhani kama watoto wetu leo wanalishwa vizuri elimu hii.
 
[h=2]Kweli ukiambiwa una akili ya hawa ndugu unaweza ukalia, hivi hawajasoma fasihi kwenye lugha ya kiswahili, wameshindwa kumuelewa Nyaronyo Kicheere mpaka wanamshangilia kwa hizo sababu, kweli CCM janga la elimu Tanzania[/h]
 
Hii inaitwa "ironic" writing. Au kejeri kejeri hivi. Without reading between lines lazima kama ni CCM ishangilie kama ni CDM ulie.
Kwa waliosoma literature miaka ile wanaweza kukumbuka Chief Nanga wa kitabu cha "a man of the people(Achebe) na Dr. Stalkman wa "an enermy of the people (Ibsen) ni nani hasa ali reflect title ya kitabu husika.
 
Nyaronyo jembe, ukifika huko muombee na Babu Seya msamaha na waliochota hazina majuzi wasikamatwe
 
hahahaha,Nyaronyo akisoma comment yako atakudharau! mkuu.
 
Mwandishi Mahiri wa Makala na Mwanasheria wa Jijini Dar es Salaam Nyaronyo Mwita Kicheere amehamia CCM, kati ya sababu kubwa zilizomhamisha CHADEMA, anasema Viongozi wake hawana sura ya Tabasamu, tofauti na viongozi wa CCM, Kikubwa zaidi anasema ameamua kuipenda CCM kwa kuwa Mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ni mtu Rahimu, anayependa watu wake na kuwahurumia kutokana na magumu ya maisha, Juzi juzi ametangaza jinsi alivyopelekewa orodha ya majangili 40 wanaotikisa mbuga zetu lakini hakuwachukulia hatua yeyote kwa kuwa wanafanya ujasiriamali kujikimu na wanaweza kuwekeza. Nyaronyo amesema pia, anahamia CCM kwani kesho au keshokutwa akikamatwa na ngozi ya Chui, ya Mamba, au meno ya Tembo atapata msamaha kama wale 40 waliosamehewa na Kikwete.

Nyaronyo anasema, CHADEMA wangekuwa madarakani leo, ambao viongozi wao hawana tabasamu, akamtaja Mbowe Slaa, Lissu na Lwakatare nchi isingekalika, maana ni wazee wa visasi, maana Wezi wangekamatwa, watekaji wangesakwa, wauza dawa za kulevya wangekuwa wote gerezani.

Tena akaongeza kuwa hii si mara ya kwanza Kikwete kusamehe. Amesamehe Majangili 40, kama alivyosamehe wezi wa EPA, Nyaronyo anasema Tumshukuru Mungu kwa kuwa na Kikwete, Rais anayesamehe. = Chanzo gazeti la -----

Yes, this is what we call "Ironic language", it contain educative, informative and reasonable journalism, while, disgustingly, killing the party to which you pretend to be in common understanding.....loooh!! Thank you so much Learned Brother, Counsel Nyaronyo Kicheere, for your critical makala.
 
Nyaronyo ni Fanani na Mtambaji pia.....hadhira yapaswa kuwa makini ili kung'amua ujumbe.
 
Back
Top Bottom