Rais yeye aliyajuaje majangili, alikwenda mbugani?
Hiki ni kichekesho cha mwaka, MKURUGENZI anatakiwa afanye kazi MBUGANI ya kudhibiti MAJANGILI wanaojulikana na mh.Rais
Serikali ni nini? Waziri sio serikali? Use ur brain effectivelyHivi inakuwaje kuajiriwa na Serikali na ufukuzwe na Waziri?
Mbona Pinda anawagwaya wateule wengine? Au wanafukuzwa wasio na Mizizi yao Magogoni?
Naona majangili 40 wangetajwa kwanza then ije hii ya kinafiki!!Hivi tusaidiane jamani, ni tangazo gani lilipaswa kuja mwanzo (what to come 1st):
Kutangaza majina ya 'majangiri' 40 na kiongozi wao aliyeko Arusha au kumfukuza mkurugenzi wa wanayamapori!!??
yangu macho
Sawa mkuu, ni suala la mda tuYangu masikio
mwacheni kijana wetu nyarandu afanye kazi tuliyo mtuma,hatutataki siasa kwenye kazi.hakuna cha profesa wala mkufunzi tena.go go nyarandu
Mkuu sio swala la kuwataja tu bali kuwakamata weka behind bars na sheria ikachukua mkondo wake,bila shaka rais alipotamka tayari alikuwa na uhakika na kauli yake.Naona majangili 40 wangetajwa kwanza then ije hii ya kinafiki!!
Hiki ni kichekesho cha mwaka, MKURUGENZI anatakiwa afanye kazi MBUGANI ya kudhibiti MAJANGILI wanaojulikana na mh.Rais
Rais anateua watu wengi sana mwishowe inaleta mtafaruku katika utendaji.
Waziri na mkurugenzi wote wanateuliwa na rais, waziri akitaka kumuwajibisha mkurugenzi kwa kumtimua, mkurugenzi anamwambia "I serve at the pleasure of the president, he put me here, he will be the one to take me out"
Solution.
Rais apunguziwe nafasi za watu anaowateua.
Badilisha hapo kwenye Red! Sema Boliwood!Tunafanya kazi kama sinema za Holliwood...si mchezo.
Ugumu wa Wizara ya Maliasili
Katika kipindi cha miaka minane ya Serikali ya Awamu ya Nne, Wizara ya Maliasili na Utalii imeongozwa na mawaziri sita. Alianza Anthony Diallo, Profesa Jumanne Magembe, Shamsa Mwangunga, Ezekiel Maige, Balozi Khamis Kagasheki, na sasa Lazaro Nyalandu.
Tangu mwaka 2005 makatibu wakuu waliopitia wizara hiyo ni Salehe Pamba, Blandina Nyoni, Dk. Ladslaus Komba, na Maimuna Tarishi.
Ugumu wa Wizara hiyo unathibitika pia kwenye idadi ya Wakurugenzi wa Idara ya Wanyamapori; sehemu ambayo inatajwa kuwa ni nono mno.
Tangu mwaka 2005 Rais Kikwete alipoingia madarakani, Idara hiyo imeongozwa na Emmanuel Severe, Erasmus Tarimo, Obeid Mbangwa, Profesa Alexander Songorwa (aliyetimuliwa leo), na sasa nafasi yake inakaimiwa na Sarakikya.
Idadi kubwa ya Wakurugenzi wa Idara ya Wanyamapori imekuwa ikiondoka kwenye wadhifa huo kutokana na misukosuko mingi ya kiutendaji. Itakumbukwa kuwa Severe aliingia kwenye malumbano makubwa na Waziri Diallo; akipinga kuwa waziri hakuwa na mamlaka kisheria ya kumwondoa madarakani.
Februari 11, mwaka 2013 Rais Kikwete alitengua madaraka ya Mkurugenzi wa Wanyamapori, Tarimo na kumpatia likizo akisubiri kustaafu.
Kwa mujibu wa kifungu 8(1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya Mwaka 2002, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii aliteua Mbangwa kuwa Mkurugenzi wa Idara hiyo.
Hata hivyo, Mbangwa hakudumu kwenye nafasi hiyo kwani baadaye aliachishwa kazi kutokana na kashfa ya usafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi, wakati huo akiwa mwenye dhamana na kitengo kilichohusu masuala hayo.
Hiyo idara inatkiwa wapewe WAMASAI wenyewe ndiyo wanatawalinda wanyama wao.