King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 60,341
- 88,512
Machinga Complex ipo Sokoni.
Mwambieni Mbowe arudishe mkopo wa NSSF ambao amepanga kuwatapeli. Watu aina ya Mbowe ndio hao hao wanaoshiriki kuikwamisha mifuko yetu ya kijamii.
walijenga wajiuzie wenyeweMachinga Complex ipo Sokoni.
Kimkopo cha Mbowe cha 76m. Ambacho kila akilipa anabadilishiwa hesabu hakiwezi kuwa sababu ya mfuko kufilisika.
Wabunge wa upinzani tunaomba muihoji serikali Bungeni kuhusu hili, wabunge wa CCM hawawezi hata kama wanaumia.
Mpaka sasa serikali imekopa kiasi gani NSSF?
Katika bajeti ya mwaka huu 2015/16 serikali imetenga kisai gani kupunguza deni la NSSF?
Liquidity ya mfuko wa NSSF iko je mpaka sasa? i.e. Uwezo wa kulipa mafao kwa wafanyakazi NOT assets.
Afadhali nilihamia LAPF
Wabunge wa upinzani tunaomba muihoji serikali Bungeni kuhusu hili, wabunge wa CCM hawawezi hata kama wanaumia.
Mpaka sasa serikali imekopa kiasi gani NSSF?
Katika bajeti ya mwaka huu 2015/16 serikali imetenga kisai gani kupunguza deni la NSSF?
Liquidity ya mfuko wa NSSF iko je mpaka sasa? i.e. Uwezo wa kulipa mafao kwa wafanyakazi NOT assets.
so!!
unatushaurije? tuhame au..
Mkuu wake bado yuko ofisini tu!
Suala hili ingawaje mtoa mada hana reliable source ya habari yake lakini halina budi kufanyiwa uchunguzi haraka sana kuokoa fedha za michango ya wanachama wa mfuko huu,si la kupuuzwa abadani,linajirudia rudia sana,inawezekana kuna ukweli ndani yake
Suala hili ingawaje mtoa mada hana reliable source ya habari yake lakini halina budi kufanyiwa uchunguzi haraka sana kuokoa fedha za michango ya wanachama wa mfuko huu,si la kupuuzwa abadani,linajirudia rudia sana,inawezekana kuna ukweli ndani yake
MFUKO WA TAIFA WA HIFADHI YA JAMII (NSSF)
Mheshimiwa Spika, mfuko wa hifadhi ya jamii, NSSF, ni mojawapo ya mifuko ambayo mbali ya kutoa mafao ya kustaafu na huduma zingine kwa kadri dira na dhima yake lakini bado inajishughulisha katika uwekezaji kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa takwimu zilizopo ni kwamba mbali ya kuwekeza kwenye ujenzi wa majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma na Daraja la Kigamboni, pia NSSF ina miradi ifuatayo ya ujenzi wa nyumba;
i. Nyumba 300 za Mtoni Kijichi (PHASE I &II) Nyumba hizo zilikwisha uzwa tayari
ii. Nyumba 800-Flats 500 na Villas 300 (PHASE III) ambao umegharimu shilingi bilioni 137.
iii. Mradi wa AZIMIO SATELITE -Kigamboni wenye Nyumba 7160 (Flats &Villas) Utagharimu shilingi bilioni 871
iv. Mradi wa Dungu Farm-Kigamboni (Flats 568) Utagharimu shilingi bilioni 140
v. Mradi wa MZIZIMA TOWER nyumba ya Ghorofa 32 unaotarajiwa kumalizika Juni 2017, ambao utagharimu shilingi bilioni 233. Lakini hadi sasa bado mradi haujaanza.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi sio kama inapinga uwekezaji unaofanywa na NSSF, je uwekezaji huo unafanywa kwa kuangalia kipindi ambacho miradi hiyo itarejesha faida za uwekezaji (return on investment)?
Aidha, kwa mujibu wa kifungu cha 3.12 cha mwongozo wa Msimamizi wa Mifuko ya Hifadhi(SSRA) wa mwaka 2003, pamoja na kanuni zake kuhusu uwekezaji salama wa mifuko na marejeo yake ya mwaka 2012 ni kwamba, mifuko inatakiwa kuwekeza asilimia 70 ya mali zake kwenye dhamana (T-Bills) na hati fungani ( T-Bonds), asilimia 25 ya mali zake kwenye Miundombinu, asilimia 30 ya mali zake kwenye mali isiyohamishika (Real Estates).
Je, ni kwa kiasi gani NSSF imefuata Sheria na kanuni kuhusu uwekezaji wake mpaka sasa kwa kufuatia mgawanyo uliotajwa?
Mheshimiwa Spika, NSSF walinunua majengo ya Manji (EPZ-Project) kwa jumla ya shilingi bilioni 47.5 mwaka 2006, kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, ni kuwa majengo hayo hayakuwa na thamani hiyo wakati NSSF inayanunua. Pamoja na hayo, mradi huu unasemekana mpaka sasa kutorudisha thamani ya uwekezaji kwa muda. Kambi ya Upinzani Bungeni inahusisha upandishaji huo wa thamani isiyo halisi kuwa ni mojawapo ya mianya ya watendaji wa NSSF kujipatia 10% kwa miradi isiyo na tija.
Aidha, kodi ya mwaka ya Jengo hilo inayotokana na upangaji, haijaweza kuakisi marejesho ya faida ya uwekezaji huo kwa kuwa mradi huo mpaka sasa umeshindwa kurudisha hata nusu ya fedha zilizowekezwa na hivyo kuhatarisha uwezo wa mfuko kutoa marejesho kwa wanachama wake.
Kwa mujibu wa sheria ya SSRA, Benki Kuu ndio mamlaka ya kuhakikisha mifuko inafanya uwekezaji makini, je kwa uwekezaji huu ambao taarifa ya CAG ilisema kuwa unauweka mfuko katika hali ya kuweza kufilisika na hivyo wanachama kukosa mafao, Wizara ya Fedha inatoa majibu gani?
Mheshimiwa Spika, kuonesha kuwa uwekezaji wa NSSF umekuwa ukiongozwa na matakwa ya watu binafsi, kuna jengo la ghorofa 4 lililojengwa Kigoma kwa gharama ya shilingi Bilioni 7 na limekamilika sasa ni miaka 2, lakini hadi muda huu halijapata mpangaji. Kambi ya Upinzani inahitaji kupata majibu ya uhakika kuhusu uwekezaji huu usio na tija ni nini hatma ikiwemo uwajibikaji wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi kwa kushindwa kuusimamia mfuko ipasavyo?
Mheshimiwa Spika, NSSF imenunua ardhi mikoa kadhaa kwa bei ambayo ni zaidi ya ile ya soko (Inflated price) na mwishowe viwanja hivyo vinakosa wanunuzi. Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kuwa NSSF kukataa kuwekeza kwenye dhamana za Serikali na kuwekeza kwenye majengo ni wa kutia shaka na ni mwanya wa watendaji wake kupokea rushwa au makampuni yanayopewa kandarasi za ujenzi ni makampuni yao na hivyo uwekezaji huo kuwanufaisha wao binafsi na si wanachama wa mfuko.
Kambi ya Upinzani Bungeni, inataka majibu ya kina kutoka kwa Wizara juu ya uwekezaji mzima unaofanywa na NSSF bila kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo kwa kuwa ni dhahiri kuwa uwekezaji mkubwa usio na tija unaofanywa na NSSF unahatarisha kwa kiwango kikubwa uhai wa mfuko huu.