NMB na CRDB

Utakomaa vipi ndugu labda unishauri, sina ndugu yangu mwenye nafasi kubwa huko kazini na hali ndiyo kama hii hamna pesa japo rushwa ni dhambi hata vitabu vya Mungu vimeangikwa.

Kazi ya benki huwa inahitaji refarii officially kabisa na anasaini kwenye application documents huyo ndio dhamana yako in case umeingizia benk loss.
 
Kumbukeni jamaa anasema "hata hakuitwa kwenye usaili" post yake iangaliwe vizuri jamani
 
Utakomaa vipi ndugu labda unishauri, sina ndugu yangu mwenye nafasi kubwa huko kazini na hali ndiyo kama hii hamna pesa japo rushwa ni dhambi hata vitabu vya Mungu vimeangikwa.

Umiza kichwa kijana usisubiri uitwe, everything is out there as ideas go and make them real
 
Wewe na huyo jamaa yako alyepata kazi mna degree za fani gani,labda tuanzie hapo?
 
Poleeeee
me nafanya kazi benkiii
ila nimeomba kazi serikalin mara mia na sijawahi itwa hata kwenye zile inteview za watu elfu nne!!
Sasa hapo nikianza kulaaan hamna wizara itakayo salimika
dooh
omba Mungu yeye n mwaminifu atakupatia stahili yako.
Pole sana
 
Cheti si uwezo baba. Huenda mwenzio alijibu kwa ufasaha maswali yote kushinda wewe na gpa yako. Siku hizi unaangaliwa uwezo na sio vyeti. Umenikumbusha forum flani, facilitators 5, mmoja wa USA, holland, uganda, kenya na mtz 1. Wote wana digrii moja moja ila mtz tu ndo ana phd. Akisimama kupresent mada unataka kuingia chini ya meza kujificha. Hata intern mkenya ana nafuu.

haujaelewa hoja mzee .jamaa sio ameshindwa maswali jamaa hajaitwa kabisa kwenye interview na amempita kwa kila kitu huyo aliyeitwa kwa matokea ya shule na chuo
 
kama atadumu kwa hiyo post by whatever means aliyotumia alikuwa kazi yake otherwise any thing can happen. Usikate tamaa wala kulaan kaka we endelea kupigana mchakato ni mrefu na mgumu sana.
 
Ndugu zangu wana JF ukisikia Bank za kipumbuvu katika kuajili wafanyakazi wake ndiyo hizi mbili, kwa mtazamo wangu ni Namba moja.Leo nitaielezea moja nayo ni NMB.

Hawa jamaa Namuomba Mungu Kama vp uongozi wa Highlands Zone walaaniwe na mabaya yawe juu yao. July,2012 walitangaza ajira zao kwa kubandika tangazo kwenye mti hapa ofisi zao Mbalizi Road Mbeya ambapo ndiyo makao makuu ya Highlands zone. Mimi na jamaa yangu tuliandika barua kwa kufuata viwango vya barua za ajira, namimi nina alama nzuri za kufaulu kuliko jamaa yangu katika kila hatua ya shule. Mwenzangu akatangulia kupeleka Maombi ya kazi lakini hukuambatanisha na cheti cha kuzaliwa, mimi nilivyopeleka mpokeaji akaniambia ambatanisha na cheti cha kuzalia, ikabidi nirudi kuchukua na kuambatanisha. Sasa jamaa yangu wala hakuambatanisha,Nadhani Siku ya Kupitia hayo maombi wakampigia simu alete hicho cheti na akaitwa kwenye usaili na kazi akapata, mimi hata kuitwa usili hawakuthubutu.

Swali: Hawa jamaa huwa wanatangaza kazi kwa ajiri ya kufurahia tunavyohangaika kuomba hizo nafasi au ili iwaje?Na ukweli ni kuwa huyo jamaa yangu kaka yake yupo hapa hapo hapo mbeya na anafahamiana na hawa wa NMB na ndiye alifanya mpango mzima.
Nilikuwa najaribu kuwajuza kuwa msione kwanini hamwitwi kwenye usaili na hali huku walitangaza na mliomba wanatuzuga tu hawa. HAKIKA WALAANIWE NA MWENYEZI MUNGU WENYE TABIA HIZI.

Pole sana. Interview ni kutimiza mradi wanakuwa wana ndugu zao kama walivyokufanyia. Pole sana, lakini Mungu yupo nawa
 
Usiwe na shaka kijana. Siku hizi kama hauna Network inabidi uwe mpole. Jaribu kumuuliza mwenzako michongo ipo vipi Hapo NMB Then kama kunauwezekano wa kupigiwa CROSS DONGO japo na ndugu yake. Maisha haya inabidi uwe mpole ili uweze kutoka. Watu wengi hatuna ajira but mwenzio akipata kazi inabidi iwe faraja kwako kwani hiki ni kipimo kua hata wewe upo njiani kuipata ajira.
 
kulalamikani dalili ya kushindwa.Mpe mungu nafasi na sio kutoa malalamishi .Ajira za sasa zinakujuana so ridhika kwa kila jambo.
 
Nadhani ikitangazwa nafasi ya kazi application zinakuwa nyingi mno, na mchujo unaanzia wakati wa kupitia hizo karatasi za maombi kabla ya interview yenyewe. Na watu wengi wanashindwa kufahamu kwamba karatasi za application zinatoa some picture of what type of person you are. Ndio maana wengine hata kwenye interview hawaitwi. Marks nzuri pekeyake sio ndio uhakika wa kuitwa kwenye interview
 
Watanzania bwana hamna hata jipya! hivi mimileo nataka kutoka kwenye ajira nianze kuwa mkulima hata huko kyela wewe unataka kuajiriwa, Tena uwe banker acha upuuzi huo umepitwa na wakati.kuwa mjasilia mali kaka
una upeo mdogo sana wa kufikiria wewe! hivi unadhani ukiamka asubuhi tu unaamua leo mimi ni mkulima basi mchana unaenda kulima shamba?
hv hujui kilimo kinahitaji mtaji mkubwa wa uhakika? huyu jamaa anao? hv ni watanzania wangapi wanamiliki ardhi safi zinazofaa kwa kilimo? huyu jamaa anayo?
fikiria kwa kutumia akili na si ma.kalio..
kwanza unangoja nini acha hiyo kazi ukawe mjasiria wanaotafuta kazi ni wengi mno
 
We mweka mada unaonekana unaringa saaana.. Ki GPA chako ndo ulingie ktk maisha ya street?? Una dharau kwanza.. Kwanza hueleweki unazungumzia NMB, hiyo CRDB umeitaja ya nini?? Nawas was na GPA yako
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom