NMB na CRDB

Cheti si uwezo baba. Huenda mwenzio alijibu kwa ufasaha maswali yote kushinda wewe na gpa yako. Siku hizi unaangaliwa uwezo na sio vyeti. Umenikumbusha forum flani, facilitators 5, mmoja wa USA, holland, uganda, kenya na mtz 1. Wote wana digrii moja moja ila mtz tu ndo ana phd. Akisimama kupresent mada unataka kuingia chini ya meza kujificha. Hata intern mkenya ana nafuu.
Nimependa hii Watanzania wengi tunabweteka tukishakuwa na marks nyingi tunafikiria kuwa ni kigezo cha kupata kazi sasa hivi kinachoanagliwa efficiency yako.Upendeleo upo sawa lakini hatuwezi kuconclude kuwa jamaa kapendelewa,huenda jamaa alitoa maelezo ya kujitosheleza kuliko yule anayetegemea vyeti tu ndo vimbebe,kumbuka sasa hivi tupo kwenye liberalism.
 
haujaelewa hoja mzee .jamaa sio ameshindwa maswali jamaa hajaitwa kabisa kwenye interview na amempita kwa kila kitu huyo aliyeitwa kwa matokea ya shule na chuo
Si kweli kama kampita kila kitu je hata katika uandishi wa barua kampita,je hiyo kozi na fani aliyomba zinaendana?Pengine barua aliyoandika haikuendana na aina ya vyeti alivyo navyo? so kuna many factors japo katika kuomba kazi yahitaji uvumilivu huwezi pata siku moja kazi.
 
tehe tehe tehe wewe ulidhani NMB ni NECTA ambao wanaangalia ufaulu wako wakupe post au ulidhani NMB ni TCU wangalia ufaulu wako wajue uende chuo gani na kozi ipi haaa haa open ur eyes bro hiyo ndiyo elimu mtaani yani ukinicheka shambani takucheka sokoni umeona sasa
 
CRDB inahusikaje? Hata NMB umetaja tawi tu wala siyo makao makuu!
Bado sana kijana, kuajiri mtu wanaangalia vitu vingi sana, unaweza kuwa na div 1 au GPA ya 5 lakini ukashindwa maswali ya interview. Siku hizi baadhi ya waajiri hawaitaji vyeti.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom