Njoo tulime tikiti ujikomboe

Njoo tulime tikiti ujikomboe

HISIA ZANGU NAAMINI ZINANIAMBIA UKWELI

"HIZI HABARI ZA TIKITI NA KILIMO CHA GREEN HOUSE HAZINA TOFAUTI SANA UKIZILINGANISHA NA ZILE HABARI ZA MAYAI YA KWARE"....

MWISHO WA KUNUKUHU.
 
Sisi tunalima hybrid ndani ya usiku 56
Hakuna tikiti linalojenga sukari kwa kiwango sahihi ndani ya hizo siku tajwa.
Ivi unatambua dalili za ukomavu wa tikiti mkuu?
Ndani ya siku 56 shina la tikikiti linatakiwa nimwagiliwe maji ya mwisho mwisho kabisa ambayo yata sustain uhai wa mmea kukamilisha ujengaji wa wekundu/pink ndani ya tunda.
Tikiti la hybrid ukilivuna kwa muda huo utafail kumeet qualifacations zifuatazo:
1)radha yake haitakuwa ile halisi.
2)rangi yake ya nje na ndani itakuwa sio halisi
3) tunda lake halitakaa rafuni(shelf life) zaidi ya siku14 na lita shrink/undergo deformation.
4) litaoza kwa mtindo wa madoadoa
5)punje zake(which is of vital importance) zitakuwa na radha mbovu na kwa muda huo zitakuwa bado zimeshikana na nyama ya tikiti na hazitafaa kukamliwa mafuta wala kupandwa tena.
5) juice ya hilo tikiti itakuwa na radha ya ukakasi make sukari yake ilikuwa haijatimia ktk kiwango chake. Etc etc
 
Hichi kilimo cha tikiti kinavutia sana ngoja nijipange vizuri nami niwekeze huko, kazi za kuajiriwa inakuwa kama mtumwa ebo. Hata wanawake tunaweza bwana kukamata jembe
 
Huu ni mchanganuo halisi kuhusu kilimo cha tikiti na nimekuwa nikitoa ushauri hapa jamvini kwa muda mrefu sana;

1)Kiufupi: shina la tikiti ili lizae vizuri, halitakiwi bugudha wakati wa kustawi kwake na majani yake hayapaswi kukaa na unyevu kwa muda mrefu.
2)Tunda lake hukomaa na kujenga sukari baada ya siku75 tokea linapoonyesha majani yake halisi.
Kutambua tikiti lililokomaa angalia kikonyo/coil ambacho kipo kama kikamba kilichojikunja mithiri ya spring karibu kabisa na tunda, kikianza kunyauka kuanzia kwenye ncha yake ya mwisho kabla hakijafikia maungio yake na shina kuu, chuma tunda lake.
3)Ikiwa umeandaa mfumo mzuri wa umwagiliaji, tikiti lafaa kumwagiliwa mara mbili tu kwa wiki na hakikisha unamwagilia mapema asubuhi na usiruhusu kulowanisha majani.
Baada ya siku ya 75 hutakiwi tena kumwagilia tikiti ili kuruhusu uwiano wa maji na sukari kwenye tunda. Kwa muda huo tikiti haliwezi kuongezeka kipenyo hivyo kitendo cha kulinyweshea maji kutapelekea kupasuka kwa tunda na kuharibu balance ya sukari.
 
Mi nataka ya kununua shambani, vpi upatikanaji wake?
 
Inaendelea...
4)Upandaji na umwagiliaji:
Kwa njia nyepesi na nafuu, tumia surface irrigation kwa furrow(forcing the flow of water under gravitational course). Hapa utadraft mifereji itakayoruhusu flow ya maji kulingana na sura ya shamba lako.
Hakikisha unapanda kwa mistari na utapishanisha mifereji yako walau kwa mita16(huu ni urefu wa vijaruba viwili) vitakavyo kuwa adjucent kwa kutenganishwa na mfereji. Panda tikiti zako pembeni kidogo ya mfreji wenye mita8 kwa kuchimba shimo lenye ukubwa wa kipenyo cha mpira wa mguu.
Panda matikiti yako punje2 kila shimo. Pishanisha mifereji kwa mita2 na kila shimo ruka mita1.
Mifereji yako inayopitisha maji kwenda kwenye mashimo yote ifanye iwe 60cms na ile itakayosafirisha maji iwe 30cms ili maji yakimbie haraka kuokoa mafuta!
4) Hakikisha unatunza kila shina walau likutolee matikiti mawili(2) yenye afya na ukubwa sawa.
Pogolea matikiti ili mmea ujitosheleze chakula chake.
Kawaida upogoleaji hufanyikwa kwa kukata channels zote zinazoota kwenye kamba toka shina kuu.
 
Mkuu laurentie hongera kwa kuwahamasisha raia kuhusu kuzikamatia fulsa zilizopo shamba!

Mimi ni mkulima mzoefu wa mazao karibu yote ya bustani.

Nimesoma na kujionea picha zako ulizo bandika hapa;
Zipo kasoro nyingi sana nimeziona kwenye hili bandiko. Ningependa kuweka masahihisho ya jumla iwe kama tahadhari kwa wale waliovutiwa na huu uzi hatmae kuja kufanya kazi.
1) Ipo kasoro kwenye upandaji wa hizo tikiti. Umepanda kienyeji sana. Upandaji wako utaathiri huo mmea kipindi cha umwagiliaji maji hasa kwa hiyo hybrid(zebra)
2) kuna mapungufu katika uainishaji wa gharama za uendeshaji. Kwanini huwi realistic kuchambua hatua kwa hatua mpaka mavuno.
Nk nk nk
Nikipata muda, ntatoa mchanganuo wa upandaji, cost na kipato halisi kwa ekari moja ya tikiti ili kuwarahisishia watakaovutika kuingia kwenye sekta hii na hatmae wajue mbivu na mbichi kuhusu kilimo.
Nakusubiri mkuu...

Naomba uje utujuze kiundani zaidi
 
Mimi ni mfanya biashara wa matunda hususani hayo matikiti maji, lakini nifanyacho mimi ni ulanguzi...
Nimefurahi kukutana na uzi huu, kwa yoyote anaehitaji trading partner naomba anijurishe, nahitaji sana mtu ambae ni mwaminifu hawezi kuniuzia bidhaa zitakazonipa hasaraa
 
umemaanisha kuwa tunadanganywa ama nini? what do you mean
Hapana, fuatilia mtiririko wa uzi vizuri. Nipo hapa kuboresha pale aliposahau mleta mada make wadau wamehitaji ufafanuzi zaidi wa uhalisia wa hiki kilimo.
Mimi nnauzoefu wa hiki kilimo na bustani kwa ujumla wake. Nimetoa ufafanuzi wa awali then nikawaalika wachangiaji kushare nami na kama ipo haja ya kuendelea kutoa darasa basi muulize maswali.
 
Mimi ni mfanya biashara wa matunda hususani hayo matikiti maji, lakini nifanyacho mimi ni ulanguzi...
Nimefurahi kukutana na uzi huu, kwa yoyote anaehitaji trading partner naomba anijurishe, nahitaji sana mtu ambae ni mwaminifu hawezi kuniuzia bidhaa zitakazonipa hasaraa
Hongera sana mkuu. Wewe ni mdau mhimu sana kwangu. Siku zote kwenye biashara tunategemeana pande zote mbili. Endapo upande mmoja ukikiuka vigezo na viwango, lazima hasara itatokea upande mmoja. Nipo tayari kufanya kazi na mtu anaejali muda na rasilimali make ndo mwanzo wa kufanikiwa.
Tuungane maana tunategemeana.
Nakukaribisha sana na nipo tayari kufanya kazi na wewe endapo uaminifu utazingatiwa kama ulivyotangulia kusema.
Karibu sana.
 
Inaendelea...
5)Makisio ya gharama kwa ekari1 ya tikiti.
Kama nilivyosema mwanzo, endapo miundombinu ya umwagiliaji ipo vizuri na ukitumia waterpump 3" hp5.5( cost yake ni sh300,000) deliverypipe 50metres(sh 100,000) inlet pipe(price cost per ft sh15000 i.e ft6=sh80000)
Shamba la ekari1 litamwagiliwa kwa tanki2 lenye ujazo wa 3litres(total 6litres) so cost/acre/whole period 2000sh*6litres*{20'}= sh 240,000(hii ni gharama ya petrol) nb {20'} ni idadi ya awamu za umwagiliaji wa shamba toka kupanda hadi kukomaa kwa tikiti siku ya 75.
6) Gharama za mbegu na viuatilifu;
Bei inatofautiana kulingana na sehemu na aina ya mbegu.
Hybrid SukariF1 ama SugarQueen kopo la gram500 lina range kuanzia sh250,000-270,000/- ambayo ndani yake kuna karibu punje4000. Inatosha kwa ekari1 ila itakulazimu uwe na mbegu ya dhiada endapo mashimo mengine hayataota.

7)gharama ya viutilifu: fungiside ridomily au ebony kilo1 sh40,000 kwa ajili ya ukungu
Insectside blasty kikopo cha mil500*10*sh8000=80,000.
Dawa ya panya pia mhimu.
 
Inaendelea...
5)Makisio ya gharama kwa ekari1 ya tikiti.
Kama nilivyosema mwanzo, endapo miundombinu ya umwagiliaji ipo vizuri na ukitumia waterpump 3" hp5.5( cost yake ni sh300,000) deliverypipe 50metres(sh 100,000) inlet pipe(price cost per ft sh15000 i.e ft6=sh80000)
Shamba la ekari1 litamwagiliwa kwa tanki2 lenye ujazo wa 3litres(total 6litres) so cost/acre/whole period 2000sh*6litres*{20'}= sh 240,000(hii ni gharama ya petrol) nb {20'} ni idadi ya awamu za umwagiliaji wa shamba toka kupanda hadi kukomaa kwa tikiti siku ya 75.
6) Gharama za mbegu na viuatilifu;
Bei inatofautiana kulingana na sehemu na aina ya mbegu.
Hybrid SukariF1 ama SugarQueen kopo la gram500 lina range kuanzia sh250,000-270,000/- ambayo ndani yake kuna karibu punje4000. Inatosha kwa ekari1 ila itakulazimu uwe na mbegu ya dhiada endapo mashimo mengine hayataota.

7)gharama ya viutilifu: fungiside ridomily au ebony kilo1 sh40,000 kwa ajili ya ukungu
Insectside blasty kikopo cha mil500*10*sh8000=80,000.
Dawa ya panya pia mhimu.
300000+100000+80000+240000+80000= so total ni laki nane sio?
 
Inaendelea...
8)Gharama ya spray tank sh 40,000/=

9)Gharama ya mbolea.
Kupandia, DAP sh 70,000 mfuko1 na kukuzia CAN sh70,000 Booster kopo2 za 1litre@12000=sh24000 TOTAL=164,000/-
8) Gharama ya vibarua +ulimaji haitazidi sh150000 mpaka kuvuna.
9)Upandaji na makisio ya matunda mazuri kwa ekari moja.
Eneo la ekari1 ina 4000sqm
Hivyo idadi ya mashimo ni 4000sqm/(2m*1m)=2000.
Idadi ya mashina kkt ekari1 kama utapanda punje2 kila shimo 2000*2=4000.
Ukifanikiwa kutunza matunda mawili makubwa katika kila shina, ekari1 utapata matunda 4000*2=8000.
Kadilio la chini kabisa la bei ya tikiti shambani ni sh1000.
TOTAL YIELD; 1000*8000= SH 8000,000/=
Fuatilia vipengele vyote vya gharama kisha DEDUCT toka kwenye total yeald utapata RETURN ya hii project.
Nyongeza;
Epuka kuspray viuatilifu mida ya asubuhi ili kujenga urafiki na nyuki ambao ndo wahusika wakuu ktk uchavishaji.
Usimwagilie maji usiku kuepuka kulowanisha majani ya tikiti yatashindwa kukauka mapema.

Karibuni kwa maswali.
cc Lizarazu etc
 
Mods wa jukwaa hili unaweza kuunganisha post zangu pamoja ili wadau wapate mtiririko kwa pamoja.
Kuna baadhi ya gharama unaweza ku omit endapo itatokea ukawa na baadhi vifaa vinavyotakiwa kabla ya project.
Cc Mulhat Mpunga Baba yenu etc
 
Hongera sana mkuu. Wewe ni mdau mhimu sana kwangu. Siku zote kwenye biashara tunategemeana pande zote mbili. Endapo upande mmoja ukikiuka vigezo na viwango, lazima hasara itatokea upande mmoja. Nipo tayari kufanya kazi na mtu anaejali muda na rasilimali make ndo mwanzo wa kufanikiwa.
Tuungane maana tunategemeana.
Nakukaribisha sana na nipo tayari kufanya kazi na wewe endapo uaminifu utazingatiwa kama ulivyotangulia kusema.
Karibu sana.

Naam mkuu ni jambo la heri sana kuona kuna mtu aliyetayari kwa ushirikiano ninao hitaji... kikubwa ni kuwa honesty na kutanguliza utu ukiishinda roho ya tamaa. Siku zote biashara nzuri ambayo hata Mungu ana ibariki ni inayofanyika for equally mutual benefits.

Kama nilivyoweka kwenye mabandiko yangu ya awali, binafsi sina tatizo ni utayari tu wa muhusika. Hivyo fanya unione kwa inbox kwa ajiri ya mawasiliano yenye ukaribu zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom