Njia ya kumuachisha mtoto kunyonya kidole

Njia ya kumuachisha mtoto kunyonya kidole

backtobasics

Member
Joined
Apr 24, 2024
Posts
26
Reaction score
40
Wana JF,

Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...

Sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?

===
Ufuatiliaji wa JamiiCheck

Je, kunyonya vidole kwa mtoto ni hali ya kawaida?

Tovuti ya Hopekins medicine kupitia makala yake yenye kichwa “Finger sucking in children” wanabainisha kuwa watoto huzaliwa na uwezo wa wachanga huzaliwa na uwezo wa asili wa kutafuta na kunyonya, wakati mwingine hata kabla ya kuzaliwa.

Watoto hunyonya vidole kwa sababu kufanya hivyo huwafariji basi wanaweza kujenga tabia ambayo inaweza kuwa ngumu kuja kuiacha. American Dental Association na American Academy of Pediatric Dentistry wanashauri kuwa watoto wanapaswa kuacha kunyonya vidole kati ya umri wa miaka 2 hadi 4.

Tovuti ya colgate inaeleza kuwa hali hii humpa mtoto faraja, na anapokua inaweza kumsaidia kujihisi salama na mwenye furaha. Pia watoto wengi wachanga na wadogo hutumia kama njia ya kujikimu wanapokuwa na wasiwasi au wametengana na wazazi wao. Tabia hii pia husaidia kupata usingizi, ndiyo maana baadhi ya watoto hunyonya vidole vyao jioni kabla ya kulala.

Mtoto akiendelea kunyonya vidole baada ya kufikisha miaka 4 nini hutokea?

Kama ilivyoelezwa hapo awali angalu kwa kawaida inategemea mtoto aache kunyonya vidole kati ya akiwa na miaka miwili (2) hadi minne (4). Iwapo mtoto ataendelea kunyonya vidole zaidi ya hapo anaweza kukutwa na baadhi ya changamoto.

Iwapo mtoto ataendelea kunyonya vidole zaidi ya hapo inaweza kupelekea kuathiri mpangilio wake wa meno, Pia kunaweza kuathiri sehemu ya juu ya ndani ya mdomo inayojulikana kama kaakaa la juu (palate). Hatari ya matatizo ya meno huwa kubwa zaidi ikiwa watoto hunyonya vidole kwa muda mrefu na mara kwa mara.

Hopkins Medicine wanabainisha pia kuwa Kunyonya vidole mara nyingi si tatizo hadi meno ya kudumu ya mtoto yanapoanza kuota. Hata hivyo, tabia ya kunyonya vidole kwa muda mrefu inaweza kusababisha:

  • Mfumo usio wa kawaida wa kumeza au kuzungumza kwa kusukuma ulimi mbele, ikiwemo lafudhi ya kutamka vibaya baadhi ya herufi.
  • Ulimi kukaa katika nafasi isiyo ya kawaida ukiwa umetulia.
  • Kupungua kwa nguvu ya ulimi.
  • Kupungua kwa uwezo wa ulimi kusogea vizuri (kama kuinuliwa au kusogezwa upande kwa upande), jambo linaloweza kuathiri matamshi na ulaji.
  • Meno ya mbele kubaki wazi (open bite), hali inayoweza kuathiri kung’ata, kutafuna na kuzungumza.
Nini cha kufanya ili mtoto aache tabia ya kunyonya vidole

Tabia hii mara nyingi hukoma yenyewe bila kuwa na tatizo kubwa au juhudi maalum. Mara nyingi, njia bora ni kuipuuza tu. Watoto huja kugundua wenyewe kupitia mazingira ya kijamii na ushawishi wa wenzao kwamba tabia hiyo haikubaliki tena. Hata hivyo, ikiwa itaendelea baada ya umri wa kwenda shule ya awali, basi unaweza kufanya yafuatayo;

  • Tengeneza ratiba au mfumo wa zawadi kufuatilia maendeleo ya mtoto katika kuacha tabia hiyo.
  • Mhimize na umsifie mtoto anapojaribu kuacha.
  • Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno ili kujifunza faida za kuacha tabia hiyo.
  • Tambua visababishi. Ikiwa mtoto wako hanuniwi lakini bado ananyonya kidole, jaribu kugundua kinachomfanya ajisikie hivyo. Unaweza kumpa faraja kwa kumbatio au maneno ya kumtuliza. Pia unaweza kumpa mto au mdoli wa kukumbatia ili ashike na kujituliza.
  • Endelea kumkubusha kwa upole. Ikiwa mtoto wako ananyonya kidole bila kujitambua, mkumbushe kwa upole aache. Epuka kumkemea au kumkosoa mtoto wako.
Mayo Clinic wanaeleza kuwa mara chache wataalamu wa afya hushauri kutumia ,pamoja na kupaka kitu chenye ladha chungu kwenye kucha ya kidole, kufunga bandeji kwenye kidole, kutumia kifaa maalum cha mdomoni au kufunika mkono kwa soksi wakati wa usiku.

Nini cha kufanya iwapo njia zote hazitozaa matunda?

Kwa baadhi ya watoto, kunyonya kidole ni tabia ngumu sana kuacha. Jaribu kutokuwa na wasiwasi sana. Usiweke shinikizo kubwa kwa mtoto kuacha kunyonya kidole kwani kunaweza kuchelewesha zaidi mchakato huo. Zungumza na daktari wa meno wa meno ikiwa unahitaji msaada zaidi.
 
Wana JF,
Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?
Mkuu achana nayo hiyo mdogo wangu ana miaka 30 kwa sasa na ana nyonya!

Nilikua kaacha siku moja nadhani ni pasaka hii tukalala kitanda kimoja kule kijijini kwa wazee nikasikia kama mtu anafyonza kitu kumuangalia ananyonya madole.

Nadhani hawaachi dogo karithi kwa babu mdogo upande wa baba na yeye hadi anakufa alikuwa akijisahau anatia dole mdomono dole lile hadi lilikuwa lishabadilika
 
Mkuu achana nayo hiyo mdogo wangu ana miaka 30 kwa sasa na ana nyonya!

Nilikua kaacha siku moja nadhani ni pasaka hii tukalala kitanda kimoja kule kijijini kwa wazee nikasikia kama mtu anafyonza kitu kumuangalia ananyonya madole.

Nadhani hawaachi dogo karithi kwa babu mdogo upande wa baba na yeye hadi anakufa alikuwa akijisahau anatia dole mdomono dole lile hadi lilikuwa lishabadilika
duuuh😂😂 !!!hii hatari sasa huyu mtoto wa kiume si ni noma sana
 
Wana JF,

Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?
Kama anatmebea unamvalisha kaptula bwanga kiunoni attention inahamia kuzuia kaptula isidondoke.
Tafuta mwenzake wa kucheza naye kukimbizanakimbizana kunafanya asaahau kunyonya kidole
 
Mkuu achana nayo hiyo mdogo wangu ana miaka 30 kwa sasa na ana nyonya!

Nilikua kaacha siku moja nadhani ni pasaka hii tukalala kitanda kimoja kule kijijini kwa wazee nikasikia kama mtu anafyonza kitu kumuangalia ananyonya madole.

Nadhani hawaachi dogo karithi kwa babu mdogo upande wa baba na yeye hadi anakufa alikuwa akijisahau anatia dole mdomono dole lile hadi lilikuwa lishabadilika
Mwanaume unalala na dume lenzako kitanda kimoja? Maajabu
 
Wana JF,

Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?
Hii ni janga mimi kuna mtoto wa mdogo wangu ana miaka sita ananyonya mno na ni kweli zinaharibu dental formula
 
Wana JF,

Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?
Muache unampa mateso makubwa hivyo vitu ni automatically

Mtoto kunyonya kidole ni tabia ya kawaida ambayo mara nyingi huanza tangu akiwa tumboni au punde tu baada ya kuzaliwa. Hizi hapa ni sababu kuu zinazomfanya mtoto afanye hivyo:

Kujituliza na Kujifariji:
Hii ndiyo sababu kuu. Mtoto hutumia kidole kama njia ya kujipoza anapokuwa na wasiwasi, anapochoka, au anapotaka kulala. Kulingana na maelezo ya wataalamu katika Gazeti la Mwananchi, kunyonya kidole huwasaidia watoto kujisikia salama na wenye furaha.

Asili ya Kunyonya (Sucking Instinct): Watoto huzaliwa wakiwa na hamu ya asili ya kunyonya kwa ajili ya kupata chakula. Wakati mwingine, hata kama ameshiba, ile hamu ya kunyonya bado inakuwepo, hivyo hutumia kidole kuitosheleza.

Njaa:
Mara nyingine mtoto anaweza kuanza kunyonya kidole ikiwa hajapata maziwa ya kutosha au anahisi njaa na anasubiri kulishwa.

Kuondoa Upweke:
Mtoto anaweza kunyonya kidole anapojihisi mkiwa au mpweke kama njia ya kujiliwaza mwenyewe.

Kukua kwa Meno:
Wakati meno yanapoanza kuchomoza, fizi huwasha au kuuma, hivyo mtoto huweka kidole mdomoni ili kupunguza muwasho huo.Wataalamu wengi wanashauri usimlazimishe mtoto kuacha tabia hii akiwa na umri wa chini ya miaka 4, kwani watoto wengi huacha wenyewe kadiri wanavyokua na kuanza kupata njia nyingine za kujiliwaza.
 
Wana JF,

Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?
Nimewahi kuona njia nyingi wanatumia wazazi na walezi.Kuna zingine sikuzipenda kama vile kupiga,kuwawekea pilipili na hata vitisho vingi.Jaribu kuwa unamvalisha gloves za nguo zisizoumiza ili akiweka kidole mdomoni kisishawishi kukinyonya.
 
Wana JF,

Ni njia gani isiyo na madhara ya kumfanya mtoto aache kunyonya vidole, ana miezi 7 sasa ila naona kwa kasi anayoenda nayo yaani hadi usingizini yeye yuko navyo tu...sitamani afike umri mpaka anaanza shule awe ananyonya na pia nasikia vinaharibu dental formula hivyo nawezaje kumsaidia?
Hili siyo tatizo. Ataacha mwenyewe hasa akianza shule. Usihangaike. Kna watu tuna watoto walinyonya vidole .... yaani kila mtoto wangu alinyonyalakini waliaacha wenyewe.
 
Endelea kusema ukatili mpaka mtoto awe na magego na meno yaliyoparanganyika.
Kumbuka kuwa meno ya utotoni hung'oka mtoto akifikia umri kati ya miaka 5-8. Hivyo hiyo dental formula itajipanga upya kama kawaida.
Mimi nilikuwa na tabia ya kutafuna peni wakati wa kujisomea hasa maswali magumu ya pure maths kipindi nabukua usiku wa manane. Lakini leo hii sifanyi hivyo.

Mtoto ataacha mwenyewe kadri umri unavyokuwa mkubwa.
 
Mwanaume unalala na dume lenzako kitanda kimoja? Maajabu
Asee wacha namimi nikushangae ...ebu nambie kosa la kulala na mwanaume mwenzio kitanda kimoja?

Ujue bro sio kila mtu ana element za ushoga kama wewe na jamii inayokuzunguka la wengine hatuko hivyo.

Ebu nambie tofauti na ushoga ulio kujaa kwenye ubongo wako Kuna tatizo Gani kulala na mdogo wako wa kiume kitanda kimoja?
 
Back
Top Bottom