Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,996
Kama Tanzania inaamini nusu ya Ziwa Nyasa ni mali yake kwanini wanasubiri kuwabembeleza Wamalawi kuhusu suala la kusitisha utafiti wa mafuta ili kupisha majadiliano? HIvi tumekuwa wasahaulifu hivi kiasi kwamba hatujui suala hili nusura litulete katika vita na Kamuzu Banda?
Tanzania inaamini mpaka wake na Malawi umepita kwenye Ziwa Nyasa. Sasa kama hii ni imani ya Kikwete na Membe na serikali yetu kwa ujumla kwanini wanataka kupoteza muda wa kuwashawishi Wamalawi? Jambo rahisi ni Serikali kuanza utafiti wa mafuta na gesi kwenye "upande wetu" na kutoa kibali kwa makampuni ya kimataifa kufanya hivyo. Wamalawi watafanya nini?
Unless tuna jeshi lisiloweza kulinda mipaka yetu! Kama Wamalawi wameweza kuingia "nusu yetu" ni nini kinatuzuia kuwazuia? Si Idi Amin naye alisema sehemu ya ardhi yetu ni yake akateua hadi Mkuu wa Wilaya?
Lakini nani anafikiri kuna kiongozi anayeweza kusimama vikali hivi? Watu wameng'ang'ania ati JWTZ lilinde mitambo ya umeme ya Tanesco! na mipaka analinda nani?
Tanzania inaamini mpaka wake na Malawi umepita kwenye Ziwa Nyasa. Sasa kama hii ni imani ya Kikwete na Membe na serikali yetu kwa ujumla kwanini wanataka kupoteza muda wa kuwashawishi Wamalawi? Jambo rahisi ni Serikali kuanza utafiti wa mafuta na gesi kwenye "upande wetu" na kutoa kibali kwa makampuni ya kimataifa kufanya hivyo. Wamalawi watafanya nini?
Unless tuna jeshi lisiloweza kulinda mipaka yetu! Kama Wamalawi wameweza kuingia "nusu yetu" ni nini kinatuzuia kuwazuia? Si Idi Amin naye alisema sehemu ya ardhi yetu ni yake akateua hadi Mkuu wa Wilaya?
Lakini nani anafikiri kuna kiongozi anayeweza kusimama vikali hivi? Watu wameng'ang'ania ati JWTZ lilinde mitambo ya umeme ya Tanesco! na mipaka analinda nani?