TGInnocent
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 1,088
- 576
Hujawahi kukutana na Mwanaume king'ang'anizi, huyu ni kiboko nimetumia ubabe nimegonga mwamba, naitaji njia nzuri nimalizane naye kwa amani.
Do you mean bado mna date?
Hujawahi kukutana na Mwanaume king'ang'anizi, huyu ni kiboko nimetumia ubabe nimegonga mwamba, naitaji njia nzuri nimalizane naye kwa amani.
Ningekuwa sina mtu isingekuwa shida, kuondoka kagoma namtishia kumlipua kwa mkewe wala hatishiki ila akinilipua mm ndo basi nawaza kujilipua kabla hajanilipua ila sijui Kama ntaeleweka, yamenifika haswa.
Well ana weza kuusaidia mchepuko utulie tuliiiiiiiiiiiiiii kama majiya mtungi. And i was thinking of EXTORTION and BLACK MAIL, he will be too broke and afraid to sleep arround. It is bloody difficult but it can be done!
Generalization is WRONG. Hata kama wewe na jamaa zako wote unaowajua wana michepuko bado haina maana kwamba WANAUME wote wana michepuko.
mbona simpo sana. wewe jitahidi uanzishe urafiki na mkewe, jamaa lazima ataslow down
Hahahahaaa! SASA ALIE OLEWA KAPATA NINI KAMA BADO MUME ANAPIGIA MAGOTI NYUCHI HUKU NJE? Manake naona ndo kala hasara zaidi. Atazaa mitoto haramu mpaka basiii.
Nenda kwa mke wake kisha jitambulishe kuwa wewe ni mchepuko. Then tukutane hapa hapa kwa ajiri ya mrejesho!
HAHAA good approach, hapo hawezi kuwa kung'ang'anizi tenedaaaah mkuu ka unanijua vile! hii ndo dawa yangu always, mtu anayejifanyaga pendapenda mi hiwa natafuta kumjua mkewe au mchumba...!!!
nikimpata tu kwisha habar yako!! najitahid niwe karibu nawe halafu mtu anatoka ndukiiii! from there me tuliiiii naendelea kula maisha
Achana nae uyo hakupendi anakutumia tu tafuta wa kwako wa maisha. Mwambie unataka kuolewa asikusumbue.
Kajambeee huko, dhambi zako zimekushinda zawrngine zinakutoa povu. Wale ndugu zako wasioolewa wameishia kuzalishwa nyumbani huwaoni ama?????
Embu nitolee giza mtoto mdogo mie hata hiyo 25 naisikia kwa wengine, Tengeneza ww urafiki na Mungu kama unaweza mwisho wa siku kila mtu na msalaba wake, hunijui sikujui huna ushauri pita mbali usinimwagie povu lako hapa.
wanaume bana mi hata siwaelewagi yani!!!!
Hahahahah angelita wewe ni mtoto?!
Usijidanganywe mwaya, huyo jamaa is just taking advantage of you. Hakuna cha kuwa taaban wala nini. I mean think about it, mmekutana akiwa na mchumba, mkawa pamoja na akakolea kweli kweli lakini recently ameamua kumuoa huyo aliyekuwa anajuta kuna na commitment nae?! We unaona nini hapo?!
Kama angekuwa hoi,taaban or whatever he tells you aingemuoa huyo aliyemuoa bali angekuoa wewe. Sababu ya kumuoa aliyemuoa ni kwamba ANAOGOPA KUMPOTEZA ila wewe hana wasiwasi na wewe hata kidogo. Na ndio maana wewe unajua kuhusu mwenzio na anakutumia apendavyo bila kuwa na future na wewe wakati mwenzio ana-treat-iwa delicately.
Fungua macho uone kisha utafute maisha yako mwenyewe. Huyo mwanaume anakuona wewe ni ----- na anajua huna ujanja juu yake. Wewe ndo uko taaban, amka mama utafute na wewe wa kukufia mpaka atake kuji-commit kwako na sio kwa mwenzio.
Hatueleweki dada mahondaw
ver simple method...anzaa kumchuna vitu vikubwa vikubwa akununulie gari,mara akujenge nyumba akusaidie kumpeleka mdogo wako chuo kikuu,,automatic atajiengua mwenyewemwaka na miezi kazaa tangu nimjue sasa, nakumbuka kuna tatizo lilitokea ikabidi nimuone yeye ofisini kwao, ndo ukawa mwanzo wa penzi letu kuchipua.
Aliniweka wazi kwamba ana mchumba, ila yuko nje ya mji haikuwa shida sababu nilikuwa na stress zangu za mapenzi niliona nimepata pakuzitolea labda nitamsahau yule aliyekuwa mpenzi wangu, kwa takribani miaka minne sasa nitamsahau na kupata pakuanzia.
Ingawa sikuwa single kwa wakati huo, kuna mtu ambaye nilikuwa naye kwa muda mrefu, alinizidi umri sana na ni mume wa mtu, nilihitaji mtu wakuwa naye huru na kwakuwa huyu mchumba wake alikuwa mbali na mie moyo wa kupenda ulikufa sikuona shida kusogeza muda naye.
Kadiri siku zilivyosonga niliona mwenzangu anazidi kukolea, ikabidi nikate mawasiliano, mana ilifika kipindi anajutia kuwa kwenye commitment.ni mwezi sasa na siku kazaa tangu aoe, bado ananiganda anataka tuendelee na mahusiano, binafsi siko tayari kuendelea naye nishatumia njia zote kumkatisha tamaa bado kang'ang'ana.
Tafadhari wale wakurusha mawe pita mbali, hapa ni ushauri jinsi ya kunusuru ndoa ya watu idumu tu.
Ndio nyinyi mnafeli mtihani kwa genye zenu zakuharakia kujibu bila kusoma vizuri.
Soma bandiko vizuri uelewe, aliyekwambia nilitaka anioe nani, huna ushauri pita mbali nilishatoa onyo mwisho wa bandiko.
Tulikuwa na kawaida ya kupima, bahati mbaya ananijua Sana kiundani ndomana nakosa njia za kumuepuka.