Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

hata hivyo nashukuru kwa lile swala la minyoo ya Tape worm
niliwafuata maDr wa muda mrefu katika kazi hizo wakarefeer huko nyuma
dawa siikumbuki ila vipimo vyetu na computer vijana hawajazimudu
naam mkuu changamoto hazikosekani .....
Microscope ni moja ila macho tofauti.
 
hata hivyo nashukuru kwa lile swala la minyoo ya Tape worm
niliwafuata maDr wa muda mrefu katika kazi hizo wakarefeer huko nyuma
dawa siikumbuki ila vipimo vyetu na computer vijana hawajazimudu
Jitahidi wawe wanaosha mikono Yao Kwa maji na sabuni vizuri, kutumia maji yalochemshwa kuosha matunda, mboga mboga ziive vizuri, nyama iwe ya ng'ombe ama pork ichemke vizuri iive na samaki aive vizuri.
itamsaidia asipatwe na minyoo hii ya tapeworm.
 
zinahesabiwa mkuu hakuna ujanja ujanja.....🤓

sema c unajua wazungu mkuu wamerahisisha mengi......unakuwa unaangalia kwenye microscope huku pembeni Una kitu tunaita CELL COUNTER..... ko kila unapoona unabonyeza...kinahesabu taratibu chenyewe.
Ok hapo sawa
 
Mkuu hongera kwa elimu uliyoamua kutupa bure

Ila mimi mkuu ninashida sana kwnye mwili wangu yapata miezi 10 sasa nina joto lisilo kwisha, ulimi unachemka, kizungu zungu kisichoisha, mikono na miguu inawaka moto, vitu vinayembea mwilini kma mdudu, nineshapima vipimo kama vyote kam

HIV
SUKARI
FIGO
INI/ HEPATATIS PANEL
UA
ECG/ NEUROPATHY
FULL BLOOD PICTURE
VDRL
BP
MRI BRAIN

Lakini vyote viko sawa sina shida yyte

Ila bdo maumivu nayasikia pale pale nimeshakula antiobitics nying lakin wapi

Sasa sijui hpo utanishauri nn mkuu cha kufanya tafadhali
mkuu hapo sina uhakika sana lakini nashauri uonane na daktari tena.. ambae atapendekeza vipimo kulingana na umri jinsia n.k
 
mkuu najaribu kidogo ....[emoji851]

Hapana pus cells hutolewa nje hasa unapokua na maambukizi katika njia ya mkojo (Urinary tract infections/UTI)..

Pus cells -dead white blood cells

unapopatwa na maambukizi katika njia ya mkojo ambapo bakteria huingia katika njia hii na kuleta shida huwa mwili Una detect na kuanza kupeleka Askari wa mwili (white blood cells ) .....sasa wakizidiwa huanza kuuliwa na kutolewa nje as dead white blood cells (pus cells) ....na wewe hapo huanza kujisikia homa na dalili zinginezo.

sasa mkuu hao unatakiwa ujue pia dalili za gonnorhoea (kisonono) na syphillis (kaswende) pia japo Kwa case yako nafikiri ulikua ni mchezaji peku wa mechi za mchangani (just a guess) na ndo maana pus cells zilikua hazikukosi...

Okay turudi kwenye case yako.....
wanawake ni wahanga wakubwa wa UTI sababu moja ama mbili haswa....

Kumbuka kwamba tumboni mwa binadamu upande wa njia ya haja kubwa ...kuna bakteria kibao ambao wao hapo huwa ni sehemu salama na hawana shida ....na husaidia pia kuuwa some bakteria wasio wenyeji wa eneo la hapo pindi ulapo chochote chenye shida na kazi zingine nimesahau c unajua mtaani muda mrefu mkuu....

Sasa pindi bakteria hawa wanapotoka hapo na kuhamia sehemu nyingine husababishwa shida .....na ndo hapo wanapotoka njia ya haja kubwa kwenda ndogo huleta maambukiz katika njia ya mkojo (UTI)

How?
Kwa wanawake hasa ni wakati wa kujitawadha pindi wamalizapo shughuli ya haja kubwa .....inaweza kupelekea kuwahamisha kutoka sehemu ya haja kubwa kwenda ndogo ....

why wao hasa?
moja......sababu distance Kati ya sehemu ya haja kubwa na ndogo kwao ni kama 1.5 inchi .....ni sehemu ndogo sana......wakati wanaume ni kama inch 7 kama sijakosea ko inakua ni rahisi wao....

Mbili....maumbile yalivyokaa ,, wao pamoja na umbali mfupi but also n kama kashimo while wanaume ni tofauti ko uingiaji wa vijidudu/ mabaki yenye vijidudu ni changamoto kdg....

tatu...hata vyoo vya kukaa .....wao kujisaidia kwao mara nyingi mpk wakae wakati wanaume aweza simama mbaya zaidi ukute mtu ana UTI halafu anakojoa huku amesimama ko anakojolea juu ya eneo la kukaa la Choo ....ko akija mtu ni rahisi kupata UTI hasa Kwa wanawake....

na ndo maana ukiwa upo vizur Kwa mwanaume kupata UTI kama hukuwah umwa ni asilimia ndogo sana tofauti na wanawake......labda Tu ukaiCHOVYE mahali mkuu [emoji851]

ko usihofu mkuu Kwa wanawake huwa inatokea Sana .....na ni vyema aumwapo ni vizur wote mkapima na kutumia dawa wote sababu mnashare naniliu ko hata wewe waweza pata pia.....na sio mmoja tu atumie itakua ni kutwanga maji Kwa kinu.

Iyo < 100 or
ni muhimu wanawake wanapojiweka Safi baada ya haja , wajisafishe Kwa "kumuvuzisha" mkono wao kutoka mbele kwenda nyuma (yaani kutoka njia ya mkojo kwenda kule kwengine) na si kutoka nyuma kuja mbele sababu atahamisha vijidudu kuja katika njia ya mkojo...

Kuwa makini pia katika matumizi ya vyoo vya kukaa hasa public toilets ....


naamini umepata mwanga kidogo ....watakuja kuweka Sawa wenyewe mkuu....
asante sana mkuu.. umeelezea vizuri kuliko ambavyo ningeelezea kwasababu ya changamoto za kuandika muda mrefu.
 
Pole sana lab wachache sana ambao hawana kazi ungesema famasi sawa.

Una leseni ya usajili ? shida ya lab kujiajiri kwa prof yao ni msala hadi uwe na mtaji mzuri
ndio mkuu leseni ya usajili ninayo.
 
asante sana mkuu.. umeelezea vizuri kuliko ambavyo ningeelezea kwasababu ya changamoto za kuandika muda mrefu.
Yah shukrani mkuu.....
nilikua najaribu tu walau nachofahamu kwenye uzi ulouanzisha..
palipo na mapungufu naomba uweke sawa wananzengo wapate faida ....🙏
ni Jambo jema kukuona upo nasi tena.
 
Yah shukrani mkuu.....
nilikua najaribu tu walau nachofahamu kwenye uzi ulouanzisha..
palipo na mapungufu naomba uweke sawa wananzengo wapate faida ....[emoji120]
ni Jambo jema kukuona upo nasi tena.
nashukuru sana mkuu.
 
Sawa mkuu!
View attachment 1640080View attachment 1640085
Ila mRDT inaweza kukupa majibu kwamba ni one parasite infection au mixed infection, nadhani hapo ndo majibu ya malaria moja na mbili inaanzia.

Kwa mfano picha nilotuma hapo juu inaonesha mtu ana mixed infection ya falciparum na wengine
Wewe umeelekezwa vizuri tu huko juu...mbona unang'ang'ania Moja, mbili?!?!?!??!?!!?!?!

MRDT majibu ni Aidha "Positive or Negative" haitaji namba...Sana sana itaandikwa ""POSITIVE (P.f)"" au ""POSITIVE (P.f and Pan).

Achana na hayo mawazo.yako ya 1, 2 ,3 , 4 ,5.
 
Nashukuru umeelewa!

Maana kuna watu wanakataa tu bila kujua mantki ya suala lenyewe.

Vijijin huku watu wakiambiwa wana malaria 2 wanajua huyu mgonjwa anaweza kua na hali mbya tofauti na 1 ingawa ki- professionalism yoyote kat ya mwenye 1 au 2 anaweza pata severe form ya Malaria.

So kiujumla wataalam wa maabara wanatumia maneno mepesi kuwaeleza watu hasa wenye elim ndog kuelewa majibu yao ya vipimo.

Ahsante
Ona tena[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umerudia moja mbili zako...[emoji134]
 
Mkuu mleta mada...Hongera sana, unajua sana.
Mungu akubariki sana, upate hitaji la Moyo wako[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Mleta mada Fundisanifu uko vizuri sana. Ninatamani upate Ajira then ujikusanye upate mtaji ufungue laboratory yako. Yaani you are the smartest Lab Physician. Keep it up
 
Uko vizuli kaka mimi ni NurseMidwife Anaesthetist
vyote ulivyoeleza kwa wanazengo hamna hata sehemu moja uliyoteleza uko smart... Congratulations broo
Mungu akusaidie upate hitaji la moyo wako
 
Back
Top Bottom