Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

Mkuu sijui km hili swai wameshauliza
nilisumbuliwa sana na Puscells enzi zangu nikichezea timu za mitaani
na nilikuwa nikipima tu nikiona ni greater than < najua hapo nimeumia Gono , kaswende nk nabugia vidonge
sasa nipo kwenye ndoa miaka 10 na zaidi, kuna siku Wife kaenda akaandikiwa hivyohivyo kidogo nipigane
Je nilikuwa sahihi kuwa ni gonjwa la ngono km Gonoriaau ni mchafuko wa mikojo ulimtokea au ni usafi tu hakuzingatia
nisaidie ufafanuzi wa vipimi vya kuandikiwa puscel < 100 au <15 nini maana yake
 
Upimaji wa Tezi dume unakuwaje? hakuna njia nyingine za maabara zaidi ya hii ya Dr kukuingizia kidole
 
Hivi zile dk 5 za vipimo wanatupimaga kweli au wanatoa majibu tu
wanapima mkuu labda mahala hapo hao wasiwe waaminifu....
Kila kipimo kina muda wake wa kutoa majibu sahihi ....
vipo vya dakika kadhaa, masaa, siku , masiku ,wiki ,mawiki nk..
na ndo maana mtu anaweza akaja kwenye benchi amekukuta na akapata majibu kabla ya wewe uliekuwepo ...

majibu sahihi ni Yale yanayotolewa Kwa kufata muda sahihi wa kipimo kama inavyotakikana na manufacturer wa kipimo husika.
 
Mkuu sijui km hili swai wameshauliza
nilisumbuliwa sana na Puscells enzi zangu nikichezea timu za mitaani
na nilikuwa nikipima tu nikiona ni greater than < najua hapo nimeumia Gono , kaswende nk nabugia vidonge
sasa nipo kwenye ndoa miaka 10 na zaidi, kuna siku Wife kaenda akaandikiwa hivyohivyo kidogo nipigane
Je nilikuwa sahihi kuwa ni gonjwa la ngono km Gonoriaau ni mchafuko wa mikojo ulimtokea au ni usafi tu hakuzingatia
nisaidie ufafanuzi wa vipimi vya kuandikiwa puscel < 100 au <15 nini maana yake
mkuu najaribu kidogo ....🤓

Hapana pus cells hutolewa nje hasa unapokua na maambukizi katika njia ya mkojo (Urinary tract infections/UTI)..

Pus cells -dead white blood cells

unapopatwa na maambukizi katika njia ya mkojo ambapo bakteria huingia katika njia hii na kuleta shida huwa mwili Una detect na kuanza kupeleka Askari wa mwili (white blood cells ) .....sasa wakizidiwa huanza kuuliwa na kutolewa nje as dead white blood cells (pus cells) ....na wewe hapo huanza kujisikia homa na dalili zinginezo.

sasa mkuu hao unatakiwa ujue pia dalili za gonnorhoea (kisonono) na syphillis (kaswende) pia japo Kwa case yako nafikiri ulikua ni mchezaji peku wa mechi za mchangani (just a guess) na ndo maana pus cells zilikua hazikukosi...

Okay turudi kwenye case yako.....
wanawake ni wahanga wakubwa wa UTI sababu moja ama mbili haswa....

Kumbuka kwamba tumboni mwa binadamu upande wa njia ya haja kubwa ...kuna bakteria kibao ambao wao hapo huwa ni sehemu salama na hawana shida ....na husaidia pia kuuwa some bakteria wasio wenyeji wa eneo la hapo pindi ulapo chochote chenye shida na kazi zingine nimesahau c unajua mtaani muda mrefu mkuu....

Sasa pindi bakteria hawa wanapotoka hapo na kuhamia sehemu nyingine husababishwa shida .....na ndo hapo wanapotoka njia ya haja kubwa kwenda ndogo huleta maambukiz katika njia ya mkojo (UTI)

How?
Kwa wanawake hasa ni wakati wa kujitawadha pindi wamalizapo shughuli ya haja kubwa .....inaweza kupelekea kuwahamisha kutoka sehemu ya haja kubwa kwenda ndogo ....

why wao hasa?
moja......sababu distance Kati ya sehemu ya haja kubwa na ndogo kwao ni kama 1.5 inchi .....ni sehemu ndogo sana......wakati wanaume ni kama inch 7 kama sijakosea ko inakua ni rahisi wao....

Mbili....maumbile yalivyokaa ,, wao pamoja na umbali mfupi but also n kama kashimo while wanaume ni tofauti ko uingiaji wa vijidudu/ mabaki yenye vijidudu ni changamoto kdg....

tatu...hata vyoo vya kukaa .....wao kujisaidia kwao mara nyingi mpk wakae wakati wanaume aweza simama mbaya zaidi ukute mtu ana UTI halafu anakojoa huku amesimama ko anakojolea juu ya eneo la kukaa la Choo ....ko akija mtu ni rahisi kupata UTI hasa Kwa wanawake....

na ndo maana ukiwa upo vizur Kwa mwanaume kupata UTI kama hukuwah umwa ni asilimia ndogo sana tofauti na wanawake......labda Tu ukaiCHOVYE mahali mkuu 🤓

ko usihofu mkuu Kwa wanawake huwa inatokea Sana .....na ni vyema aumwapo ni vizur wote mkapima na kutumia dawa wote sababu mnashare naniliu ko hata wewe waweza pata pia.....na sio mmoja tu atumie itakua ni kutwanga maji Kwa kinu.

Iyo < 100 or <15 ni reporting way mkuu ambayo inaweza kumsaidia daktar kuforecast ukubwa wa tatizo na kukupa dozi inayofaa.

ni muhimu wanawake wanapojiweka Safi baada ya haja , wajisafishe Kwa "kumuvuzisha" mkono wao kutoka mbele kwenda nyuma (yaani kutoka njia ya mkojo kwenda kule kwengine) na si kutoka nyuma kuja mbele sababu atahamisha vijidudu kuja katika njia ya mkojo...

Kuwa makini pia katika matumizi ya vyoo vya kukaa hasa public toilets ....


naamini umepata mwanga kidogo ....watakuja kuweka Sawa wenyewe mkuu....
 
Pole sana lab wachache sana ambao hawana kazi ungesema famasi sawa.

Una leseni ya usajili ? shida ya lab kujiajiri kwa prof yao ni msala hadi uwe na mtaji mzuri
 
Upimaji wa Tezi dume unakuwaje? hakuna njia nyingine za maabara zaidi ya hii ya Dr kukuingizia kidole
Mkuu tunajaribu..

awali ya yote maabara huwa kuna kipimo cha awali kabisa ambacho hupimwa kwenye damu ......damu huchukuliwa na kupelekwa maabara kupimwa Kwa kiasi cha protein ambayo huzalishwa na tezi dume (prostate gland) kipimo huitwa PSA yaani Prostate Specific Antigen....

kipimo hicho ni Kwa ajili Tu ya kufanya screening ....na si chenye kutoa majibu sahihi kwamba Una cancer ya tezi dume....

kiasi cha PSA (prostate specific antigen ) kina range yake kwenye damu lakini pindi kinapozidi huwa kina indicate kuna shida katika tezi dume .....inaweza ikawa cancer ama inflammation ama infections (prostatitis)....na husababisha kuzalishwa Kwa wingi kwenye damu.

hatua ya pili kwa mtu ambae daktar anahisi huenda ikawa mtu ana cancer ni digital rectal examination (DRE) sijajua na SIDHANI kama kuna njia nyingine tofauti mkuu ....kuangalia kuvimba na kuwa kugumu Kwa prostate gland ....sababu inahitaji (physical touching) ili kujiridhisha kwamba mgonjwa atolewe sampuli ama la.

Hatua ya tatu ni operation kuchukuliwa sampuli ya kwenye tezi dume kupelekea maabara ku confirm (kuthibitisha) cancer ya prostate.
 
Pole sana lab wachache sana ambao hawana kazi ungesema famasi sawa.

Una leseni ya usajili ? shida ya lab kujiajiri kwa prof yao ni msala hadi uwe na mtaji mzuri
kila kitu kipo mkuu ...kasoro koneksheni

Yah ni kweli mkuu... mtuombee mambo yamebadilika Sana.
 
naam uko sahihi mkuu, na asante kwa kunisaidia kumjibu kwa ufasaha na maelezo mazuri.

hiyo njia ya kwanza uliyosema ilikua wanaripoti kwa 1,2,3,4 nadhani ulimaanisha "QBC malaria"
hiyo ya 2 yes ndo inayotumika sana, yaan malaria against white blood cells na hyo ya 3 ni against red bloodcells,

nmefanya kazi sehemu wanatumia hyo ya 2, na pia mwaka huu nmefanta kazi sehemu inatumika hyo ya 3. .

hyo ya kwanza sijawahi kuitumia siwezi kuficha hilo maana hata kwenye mtaala wetu imeondolewa nadhani..
Wakisema 500wbc wanahesabu 1,2,3,4....hadi 500? Au kuna namna ya kutambua hizi wbc kwa haraka?
 
Je mfano mtu anapoambiwa ana maambukizi ya fangasi kwenye mkojo je kuna uhusiano na fangasi kwenye damu na pia vipimo vinavyohusika kupima fangasi hapo ni kipi na ni sampuli gani hupimwa.
mkuu em kidogo tujaribu..

Fangasi katika njia ya mkojo hupimwa kwa kutumia mkojo .....na ni maambukizi katika njia ya mkojo (UTI) urinary tract infections...

Fangasi katika damu hupimwa kwa kutumia damu.

hakuna mahusiano kwamba waliokuepo kwenye damu wanakuja kwenye mkojo hapana sababu fungus tofauti tofauti wana maeneo Yao ya kukaa Japo kwenye damu wanaweza kusambaa mahala tofauti kwenda kwenye ubongo, ini, figo nk

.....wapo ambao hukaa juu kwenye ngozi (superficial mycosis) , chini ya ngozi na ndani huko (deep within mycosis) kwenye damu huko.....

wapo fangasi wengi sana na wana majina tofauti tofauti kulingana na eneo wanapopatikana kwahiyo sampuli ya kuchukuliwa itategemeana na mahala husika fangasi wanapatikana...
 
Wakisema 500wbc wanahesabu 1,2,3,4....hadi 500? Au kuna namna ya kutambua hizi wbc kwa haraka?
zinahesabiwa mkuu hakuna ujanja ujanja.....🤓

sema c unajua wazungu mkuu wamerahisisha mengi......unakuwa unaangalia kwenye microscope huku pembeni Una kitu tunaita CELL COUNTER..... ko kila unapoona unabonyeza...kinahesabu taratibu chenyewe.
 
mkuu najaribu kidogo ....🤓

Hapana pus cells hutolewa nje hasa unapokua na maambukizi katika njia ya mkojo (Urinary tract infections/UTI)..

Pus cells -dead white blood cells

unapopatwa na maambukizi katika njia ya mkojo ambapo bakteria huingia katika njia hii na kuleta shida huwa mwili Una detect na kuanza kupeleka Askari wa mwili (white blood cells ) .....sasa wakizidiwa huanza kuuliwa na kutolewa nje as dead white blood cells (pus cells) ....na wewe hapo huanza kujisikia homa na dalili zinginezo.

sasa mkuu hao unatakiwa ujue pia dalili za gonnorhoea (kisonono) na syphillis (kaswende) pia japo Kwa case yako nafikiri ulikua ni mchezaji peku wa mechi za mchangani (just a guess) na ndo maana pus cells zilikua hazikukosi...

Okay turudi kwenye case yako.....
wanawake ni wahanga wakubwa wa UTI sababu moja ama mbili haswa....

Kumbuka kwamba tumboni mwa binadamu upande wa njia ya haja kubwa ...kuna bakteria kibao ambao wao hapo huwa ni sehemu salama na hawana shida ....na husaidia pia kuuwa some bakteria wasio wenyeji wa eneo la hapo pindi ulapo chochote chenye shida na kazi zingine nimesahau c unajua mtaani muda mrefu mkuu....

Sasa pindi bakteria hawa wanapotoka hapo na kuhamia sehemu nyingine husababishwa shida .....na ndo hapo wanapotoka njia ya haja kubwa kwenda ndogo huleta maambukiz katika njia ya mkojo (UTI)

How?
Kwa wanawake hasa ni wakati wa kujitawadha pindi wamalizapo shughuli ya haja kubwa .....inaweza kupelekea kuwahamisha kutoka sehemu ya haja kubwa kwenda ndogo ....

why wao hasa?
moja......sababu distance Kati ya sehemu ya haja kubwa na ndogo kwao ni kama 1.5 inchi .....ni sehemu ndogo sana......wakati wanaume ni kama inch 7 kama sijakosea ko inakua ni rahisi wao....

Mbili....maumbile yalivyokaa ,, wao pamoja na umbali mfupi but also n kama kashimo while wanaume ni tofauti ko uingiaji wa vijidudu/ mabaki yenye vijidudu ni changamoto kdg....

tatu...hata vyoo vya kukaa .....wao kujisaidia kwao mara nyingi mpk wakae wakati wanaume aweza simama mbaya zaidi ukute mtu ana UTI halafu anakojoa huku amesimama ko anakojolea juu ya eneo la kukaa la Choo ....ko akija mtu ni rahisi kupata UTI hasa Kwa wanawake....

na ndo maana ukiwa upo vizur Kwa mwanaume kupata UTI kama hukuwah umwa ni asilimia ndogo sana tofauti na wanawake......labda Tu ukaiCHOVYE mahali mkuu 🤓

ko usihofu mkuu Kwa wanawake huwa inatokea Sana .....na ni vyema aumwapo ni vizur wote mkapima na kutumia dawa wote sababu mnashare naniliu ko hata wewe waweza pata pia.....na sio mmoja tu atumie itakua ni kutwanga maji Kwa kinu.

Iyo < 100 or <15 ni reporting way mkuu ambayo inaweza kumsaidia daktar kuforecast ukubwa wa tatizo na kukupa dozi inayofaa.

ni muhimu wanawake wanapojiweka Safi baada ya haja , wajisafishe Kwa "kumuvuzisha" mkono wao kutoka mbele kwenda nyuma (yaani kutoka njia ya mkojo kwenda kule kwengine) na si kutoka nyuma kuja mbele sababu atahamisha vijidudu kuja katika njia ya mkojo...

Kuwa makini pia katika matumizi ya vyoo vya kukaa hasa public toilets ....


naamini umepata mwanga kidogo ....watakuja kuweka Sawa wenyewe mkuu....
asante Doctor maana wewe sio Lab Technician
nina swali la kiDr sasa linagawanyika katika sehemu km 2
  1. wakati wa kukojoa hasa urushaji wake unapungua tofautu na mtoto au wale teenage, na hata urushaji wake unaweza kukuta mtu kaushikilia kabisa au akichelewa anajikojolea bila ya kuwa na habariJe ni kawaida au ni mambo ya sukari na presha?
  2. Uzibaji wa njia ya mkojo, hasa kwa umri mkubwa, ni kwa maradhi au tundu linaziba na zile hisia za kuusukuma zinapotea?
 
Nina mwanangu wa umri chini ya miaka 7 tulimgundua ana minyoo ya Tape worm maana akiwa amekaa vipande vipande vya minyoo vinamtoka katika njia ya haja kubwa. Tukaenda hizi Hospital za BIMA NHIF, wakipima choo chake hawapati kitu
nikaenda Dispensary za mitaani wakanipatia dawa kweli minyoo wakatoka
sasa Tape waorm wanakipimo gani na Dawa yake halisi ni ipi?
 
Nina mwanangu wa umri chini ya miaka 7 tulimgundua ana minyoo ya Tape worm maana akiwa amekaa vipande vipande vya minyoo vinamtoka katika njia ya haja kubwa. Tukaenda hizi Hospital za BIMA NHIF, wakipima choo chake hawapati kitu
nikaenda Dispensary za mitaani wakanipatia dawa kweli minyoo wakatoka
sasa Tape waorm wanakipimo gani na Dawa yake halisi ni ipi?
Mkuu hapo sijafahamu nini exactly kilitokea japo navyofahamu Mimi changamoto Kwa wataalamu bado ipo na juhudi lazima ifanyike kupata wataalamu bora na walio vizur.


Kikwetu kwetu hapa Kipimo ni hicho hicho cha " stool analysis" japo kinahitaji mtu mzoefu kutazama Kwa makini kuweza tambua Aina gani ya minyoo ili kupata tiba sahihi.

Nachofahamu mimi tapeworm dawa yao (drug of choice) hutumia Praziquantel japo pia huweza kutumia albendazole na nyinginezo (madaktar ndo wajuzi zaidi)

nafikiri alitibiwa kwa dawa ambazo ni (broad spectrum drugs) Kwa minyoo ....ambazo ukitumia ni kama unapiga jiwe moja kwenye ndege kama 100 ukiamini hutokosa hata mmoja .....na kweli ikakubali..

Wajuzi watanisaidia mkuu najaribu tu.🤓
 
asante Doctor maana wewe sio Lab Technician
nina swali la kiDr sasa linagawanyika katika sehemu km 2
  1. wakati wa kukojoa hasa urushaji wake unapungua tofautu na mtoto au wale teenage, na hata urushaji wake unaweza kukuta mtu kaushikilia kabisa au akichelewa anajikojolea bila ya kuwa na habariJe ni kawaida au ni mambo ya sukari na presha?
  2. Uzibaji wa njia ya mkojo, hasa kwa umri mkubwa, ni kwa maradhi au tundu linaziba na zile hisia za kuusukuma zinapotea?
Mkuu huku kiukweli sifahamu labda waje wajuzi watusaidie...🙌
 
Mkuu huku kiukweli sifahamu labda waje wajuzi watusaidie...🙌
hata hivyo nashukuru kwa lile swala la minyoo ya Tape worm
niliwafuata maDr wa muda mrefu katika kazi hizo wakarefeer huko nyuma
dawa siikumbuki ila vipimo vyetu na computer vijana hawajazimudu
 
Shikamooni wakuu.

Mimi ni muhanga wa tatizo la ajira, na pia kabla ya hilo ni mtaalamu(mteknolojia) wa maabara(Laboratory technician) mwenye diploma ambayo nimeipata kutoka BUGANDO mwaka 2018..

Pia, katika kukaa sana mtaani nimegundua kua nina muda mwingi sana, japo baadhi hua nautumia katika kutafuta kazi.

Nimetafakari sana na kujiona mimi ni mbinafsi maana kila siku natafuta ajira kwa manufaa yangu na familia yangu.. hivyo nimeamua kwa elimu hii niliyonayo niwanufaishe na wengineo, maana hakuna msaada mwingine nnaoweza kuutoa kwenu zaidi ya elimu yangu.

Sasa naomba kutumia fursa hii, kuwapa ruksa na kuwaomba mniulize chochote kuhusiana na maabara ya afya, ku-interpret vipimo ama kutoa ushauri wa juu ya kipimo gani ufanyiwe.

Kama umeona sehemu ukakasi naweza kukusaidia katika namna ambayo nitaweza, ama kama una mashaka na majibu uliyopewa sehemu pia naweza kukuelezea vizuri kadri niwezavyo kwani kwenye kazi hii nna uzoefu wa utendaji kazi kwa miaka 2..

NB: napokea michongo ya kazi pia kupitia 0786744401,

NIULIZE, NIKUSAIDIE.
Utaratibu wa kufanya kipimo cha DNA tafadhali
 
ANA TEST inapimwaje
Mkuu hicho unachukuliwa Tu damu inapelekwa maabara Kwa ajili ya kupimwa hizo anti nuclear antibody (ANA) .....
maana tunavyojua antibody huzalishwa kufight foreign substances mfano bacteria, virus, nk.... kwenye mwili.

Sasa kuna muda antibodies hizi mbadala wa kuattack vitu nlivyovitaja hapo juu huanza kuvamia cells za mwili wako mwenyewe.....na ndo husababisha Auto (self) Immune diseases mfano systemic lupus erythromatus etc....

maabara kuna njia kama mbili ivi unaweza tumia .....moja immunoassay na mbili indirect fluorescent antibody (IFA) ambazo ndizo hutumika kudetect hizo ANtinuclear antibody (ANA) kwenye damu yako sababu Hilo ni hematological disorder (tatizo lililopo kwenye damu yako) na inarithisha.
naamini kidogo umenipata.
 
Nliandikiwa hiki kipimo na hakipo mkoani kwangu hadi niende dar
Yah ni ngumu mkuu huku mikoani kwetu kukipata ....sababu kinahitaji wataalamu wenye maujuzi, kinachukua mda kidogo , reagent zake za kupimia ni gharama kidogo, nk.....

Naamini kidogo umepata kitu ......wajuzi watakuja kunirekebisha.
 
Back
Top Bottom