Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

Niulize chochote kuhusu vipimo vya Maabara za Afya

Kipimo cha FBP kina saidia kujua Magonjwa gani?
mkuu kipimo cha FBP=Full Blood Picture ni kipimo ambacho kinaonesha idadi ya seli zilizopo kwenye damu na wingi wa damu(Haemoglobin-HB)..

sasa unapopata infection ya aina yoyote hizi cell hua zinaongezeka na kupungua, kulingana na infection uliyo nayo pia kama ukipungukiwa damu kwa namna yoyte ile.

hivyo kupitia hiki kipimo daktari wako anaweza kujua nini hasa ni tatizo kulingana na seli zilivokaa kuongezeka/kupungua au kama ziko sawa..
 
Bro nashukuru umenipa mwanga maana mimi natamani sana kusoma medical laboratory kwa kuwa ni rahisi kujiajiri hata kama ukiwa na diploma ushauri wangu tafuta capital kidgo anza kujiajiri anzisha duka la madawa muhimu karibu na hiyo maabara uvute mpunga.
Ni kweli mkuu, hii fani ina emphasize katika kujiajiri ila wengi wetu tunakwama kwenye tatizo la Funds, pia mkuu nashukuru sana kwa wazo lako.
 
High level ya phosphate kwenye mkojo inaashiria nini? Na kipimo gani kingine kifanyike kugundua tatizo hilo?
High level ya phosphate inaashiria kua kuna either tatzo katika figo hususani kidney stones(vijimawe kwenye figo), pia inaweza kusababishwa na kula sana chakula chenye madini mengi ya phosphorus.

kipimo cha kufanya ni Urine Analysis(Urinalysis).
 
high level ya phosphate inaashiria kua kuna either tatzo katika figo hususani kidney stones(vijimawe kwenye figo), pia inaweza kusababishwa na kula sana chakula chenye madini mengi ya phosphorus.

kipimo cha kufanya ni Urine Analysis(Urinalysis).
Kwa nini damu ya kidoleni haifai kupima blood group? (Lakini kwenye kupima malaria inatumika)
 
Je, upimaji wa magonjwa ya binadamu yamegawanyika katika makundi makuu mangapi? Mfano ni hapo kwenye kipimo cha MRI na utrasound kulingana na maelezo yako ni kitengo kinachojitegemea kimaabara. Kitaalam unaweza ukasoma mambo yote yahusuyo maabara kwa ujumla kama course huko vyuoni?

Kuna wakati ukienda hospitali unaambiwa anayehusika na kupima ugonjwa, mwili (au sampuli) hayupo na utapangiwa wakati mwingine wa kuchukuliwa vipimo akiwepo.
 
Kuna mchezo niliufanya wa kuweka chai kwenye chupa na kumpa mpimaji bila yeye kujua kwa sababu kila ukipima pale UTI lazima ukutwe nayo, hii kitaalamu ikoje?
 
Kwa nini damu ya kidoleni haifai kupima blood group? (Lakini kwenye kupima malaria inatumika)
Mkuu damu ya kidoleni unaweza kuitumia kupimia blood group, lakini kwa sababu za kiwango cha damu kinachohitajika inatubid kuchukua ile ya kwenye mshipa na pia ili kuepuka possible error yoyte inayoweza kujitokeza.

Kuna baadhi ya vituo hua wanapima kwa kutumia ya kidoleni, ukitembelea vituo vya afya vya kiserikali utaona hili.
 
Je, upimaji wa magonjwa ya binadamu yamegawanyika katika makundi makuu mangapi? Mfano ni hapo kwenye kipimo cha MRI na utrasound kulingana na maelezo yako ni kitengo kinachojitegemea kimaabara. Kitaalam unaweza ukasoma mambo yote yahusuyo maabara kwa ujumla kama course huko vyuoni?

Kuna wakati ukienda hospitali unaambiwa anayehusika na kupima ugonjwa, mwili (au sampuli) hayupo na utapangiwa wakati mwingine wa kuchukuliwa vipimo akiwepo.
Mkuu hapo unazungumzia fani(taaluma) mbili tofauti ambazo ni maabara na mionzi(radiology).. vipimo kama MRI, Ultrasound, X ray na CT Scan ni vipimo vya radiolojia, ambayo ni taaluma inayojitegemea na tofauti kabisa na maabara..

katika aina ya vipimo kuna
1. In vivo( hivi mtu anapimwa kipimo ndani ya mwili bila sampuli kuchukuliwa mfano ni vipimo vya radiolojia).

2. In vitro, hvi ni vipimo ambavyo sampuli inachukuliwa na kupimwa nje ya mwili( hapa vingi ni vipimo vya maabara.

NB: mtaalam wa maabara ni tofauti kabisa na mtaalam wa radiolojia, ni taaluma mbili tofauti..
 
Kuna mchezo niliufanya wa kuweka chai kwenye chupa na kumpa mpimaji bila yeye kujua kwa sababu kila ukipima pale UTI lazima ukutwe nayo, hii kitaalamu ikoje?
Mkuu hapo kitaalam hiyo naweza kuiita "competence assesment", ni katika kuhakikisha kua huyo mpimaji je anajua anachokifanya!?.

Nimewahi kushuhudia na kuletewa sampuli ya mtori badala ya sampuli ya haja kubwa (mtu aliekua anaharisha) .. hiyo sampuli ilipimwa na watu wa4 kuna ambao hatukuona kitu ila wenzetu wawili kila mtu akasema kaona mnyoo ilhali hakuna kitu, kwahyo hicho ni kama kipimo cha kujua mtaalam je anajua au anabahatisha!?... ila pia sishauri sana kuwajaribu jaribu wataalam maana moja ya vitu ambavyo vinakufanya upate matibabu bora ni kuwaamini wanaokuhudumia.

mfano: ulisema umewahi kuweka chai kwenye kichupa ukampelekea mtaalamu apime, tuseme hyo chai ni nyeusi, yy akianza kuexamine sampuli atanote kuanzia rangi hadi anamalizia kwenye kuuangalia kwa microscope.. sasa kama ulipeleka chai akaona weusi ina maana ata report black urine ambayo daktari wako ataihusisha na homa ya manjano, huoni ww mgonjwa itakucost!?. kwakua umepeleka sampuli sio.
 
Vile vichupa mnavyotupaga tukakojolee huwa mnaviosha na nini?

Nauliza sababu vinakuwaga used ikimaanisha kichupa kimoja kinatumiwa na mtu zaidi ya mmoja
Hicho kichupa ni cha glass au plastic!?.. hua vinaoshwa na sabuni na baada ya hapo vinapitishwa kwenye dis-infectant.. kama ni vya glass, tunamalizia kwa kuvichemesha kwenye autoclave..

Sasaivi hvi vya plastic hua kinatumika mara moja tu baada ya hapo tunatupa, japo baadhi wanalazimika kuosha kulingana na ukosefu wa vitendea kazi vya kutosha.
 
Shukrani sana kwa majibu mazuri mkuu

Swali

Dhana ya idadi ya vijidudu wa malaria kwenye majibu ya blood slide ikoje?. Kwa mfano, mtu kuwa na malaria 45, 200 au 3, je ukubwa wa namba unaashiria severity ya ugonjwa? Na nini implication ya kutaja idadi ya vijidudu ilhali dosage itatolewa vile vile??
 
hicho kichupa ni cha glass au plastic!?.. hua vinaoshwa na sabuni na baada ya hapo vinapitishwa kwenye dis-infectant.. kama ni vya glass, tunamalizia kwa kuvichemesha kwenye autoclave..

sasaivi hvi vya plastic hua kinatumika mara moja tu baada ya hapo tunatupa, japo baadhi wanalazimika kuosha kulingana na ukosefu wa vitendea kazi vya kutosha.
Nilishawahi kupewa cha glass kimemeguka kwa juu nikamwita yule dada pembeni kumlalamikia akasema kipo salama.

Asante kwa kunielewesha mkuu
 
Nilishawahi kupewa cha glass kimemeguka kwa juu nikamwita yule dada pembeni kumlalamikia akasema kipo salama.

Asante kwa kunielewesha mkuu
pole sana mkuu, hakitakiwi.. ulitakiwa upate ambacho hakina dosari, na kama una mashaka na vifaa vyake una haki ya kukikataa mkuu.. kumbuka afya yako ni jukumu lako namba moja.
 
Shukrani sana kwa majibu mazuri mkuu

Swali:
Dhana ya idadi ya vijidudu wa malaria kwenye majibu ya blood slide ikoje?... Kwa mfano.. mtu kuwa na malaria 45, 200 au 3... je ukubwa wa namba unaashiria severity ya ugonjwa?? Na nini implication ya kutaja idadi ya vijidudu ilhali dosage itatolewa vile vile??
mkuu naomba nikukosoe hapo sio "dhana" bali ni technique ya kureport majibu.

unapoambiwa kua una malaria tuseme 45/200wbc ambazo hzo 200 ni idadi ya white bloodcells, kwahyo hapo ni sawa na aseme kua ameona vimelea 45 vya malaria katika seli nyeupe 200, hvyo mwilini utakua na wastani wa vimelea 45 kwa kila seli nyeupe 200..

hyo idadi daktari anaitumia kuamua ukubwa wa dose na dawa gani atumie,..

NB:- Jihadhari na idadi ya malaria 1, 2 3 4 mara nyingi sio ukweli huo.. mtaalam akipima akakuta kuna malaria chini ya kumi katika seli 200 anatakiwa aendelee mpaka zitakapofika seli 500.. hvyo naweza kusema kua malaria chini ya 8 inaashiria kuna ukakasi kidogo ( simaanishi kua hua haitokei, ila ni nadra sana sana).
 
Shukrani sana kwa majibu mazuri mkuu

Swali:
Dhana ya idadi ya vijidudu wa malaria kwenye majibu ya blood slide ikoje?... Kwa mfano.. mtu kuwa na malaria 45, 200 au 3... je ukubwa wa namba unaashiria severity ya ugonjwa?? Na nini implication ya kutaja idadi ya vijidudu ilhali dosage itatolewa vile vile??
ukubwa wa namba huashiria ukubwa wa ugonjwa ndio.
 
ukubwa wa namba huashiria ukubwa wa ugonjwa ndio.
Nadhani wanaoripoti kwamba malaria 1,2 nakadhalika wana base kweny mRDT sababu kile huonesha kwa mistar, so nafikiri hicho ndicho wanachomaanishaga kwamb ukiwa na Malaria 1 means mRDT Positive kwa Plas.Fascipalum na Malaria 2 kwa Mixed Infection ya Malaria parasites, ila ni mawazo yangu tuu
 
Nadhani wanaoripoti kwamba malaria 1,2 nakadhalika wana base kweny mRDT sababu kile huonesha kwa mistar, so nafikiri hicho ndicho wanachomaanishaga kwamb ukiwa na Malaria 1 means mRDT Positive kwa Plas.Fascipalum na Malaria 2 kwa Mixed Infection ya Malaria parasites, ila ni mawazo yangu tuu
hapana mkuu, MRDt inaripotiwa katika mfumo wa POSITIVE na NEGATIVE...
 
huwa maabara mkipima ukimwi mnatumia kipimo gani? nimesikia mahali mnatumia kama hivi hivi tunavyouziwa wananchi tuji pime wenyewe? kuna ukweli ktk hilo
 
Back
Top Bottom