Katika kupima U.T.I kuna sampuli ambayo inayoweza kupimwa tofauti na mkojo? Na vipi ukubwa wa ugonjwa huu mfano Ukiwa sugu vipimo vyake vinasomekaje mfano unakuta unaambiwa una U.T.I ipo 55
mkuu najaribu kidogo ,wenyewe watakuja kujibu Kwa ufasaha.
U.T.I ni kifupi cha urinary tract infections yaani maambukizi katika njia ya mkojo.
maambukizi haya mara nyingi husababishwa na bakteria ambao huvamia eneo la haja ndogo na kuleta maambukizi mahala hapo.
mara nyingi hawa bakteria hutoka katika njia ya haja kubwa ambapo huko hawana madhara ila wakija kwenye njia ya haja ndogo huleta madhara.
sampuli navyofaham ni mkojo tu.
Standard inaelekeza kwamba ili kupata majibu ya uhakika ya mtu mwenye U.T.I ni vizuri kufanya test inaitwa "urine culture"
mkojo unapandwa kwenye special prepared media ambazo zina content maalum zinazowezesha wadudu kuota baada ya kuwekwa kwenye mazingira Sawa na mwilini mwa binadamu ....at 37 degree centigrade kwenye incubator Kwa masaa 24.
Baada ya hapo wadudu huota. Kwa sampuli ambayo ina U.T.I na ambayo haina wadudu hawatoota.
Baada ya hapo hufanyiwa antimicrobial susceptibility testing Kwa maana unatest ni dawa zipi ambazo zitakua zinamtibu ama zimekua sugu Kwa mdudu huyo. Kwa hiyo kupitia kipimo hicho unaweza pata Aina ya mdudu na dawa ipi ni nzuri inaua mdudu na ipi imekua sugu.
Ila kutokana na uhaba wa vifaa na gharama ya vifaa, mahitaji ya watu ambao ni Wana ujuzi wa kutosha ...kipimo hiki unaweza kipata kwenye maabara kubwa na hospitali za mikoa ,rufaa hasa.
sasa huku chini ambako huwez kufanya kipimo hiki , kinachofanyika ni kupima namba ya WBCs tu zinazoonekana kwenye mkojo (pus cells-died WBCs) na kuangalia urine presence of nitrites.
inaaminika kwamba ... Bakteria hawa wakivamia sehemu ya haja ndogo huanza kuzaliana 😊 na kuongezeka in number kufikia namba ambayo wanaanza kusababisha shida na wewe kuanza kusikia homa, na dalili zinginezo ambapo hapo unakua umepata maambukizi katika njia ya mkojo.
kwann tunapima WBCs? sababu hawa ndo walinzi wa mwili hivyo kunapokua na shida huanza kupambana ...na wakishindwa huuliwa na kuanza kutolewa kwenye mkojo na ww huanza kujisikia homa Kwa case hii ya mtu mwenye maambukizi katika njia ya mkojo.
Kwa hiyo kinachopimwa ni died WBCs ambazo kadiri zinapokua nyingi "huenda" ukawa umeathirika pakubwa na hao bakteria.
Njia hii haiwezi kukuonesha ni dawa zipi zimekua sugu na haioneshi idadi ya wadudu. japo ni ya gharama nafuu na haichukui muda na ndo wengi huitumia kulingana pia na uchumi wetu wa kitanzania.
naamini umepata kidogo picha ...wajuzi watakuja kunirekebisha.