Nitawashangaa sana AU wakikubali mapinduzi Zimbabwe!

Nitawashangaa sana AU wakikubali mapinduzi Zimbabwe!

Huo ndio Mwisho wa Madikteta siku zote...

Madikteta ni watu wa hatari sana uwa wanafikiri tofauti...

Jeshi likiamua ni muda wowote linamuondoa kiongozi dikteta madarakani..
 
Ghadaffi aliondolewa na kuuawa kinyama kwa maslahi ya wazungu na hatima ya nchi ya libya imekuwa ni mbaya sana na kupelekea vita visivyoisha na ukimbizi wa aina yake duniani.

leo hii tunashuhudia jaribio la kumuondoa Mugabe kwa mapinduzi baada ya mbinu za kidemokrasia kushindwa.

Kwa mujibu wa BBC wazungu wanaamini kuwa Zimbabwe imekuwa mismanaged kwa miaka zaidi ya 37...msimamo huu unahusianishwa na yeye kuwafukuza matajiri wachache kwa manufaa ya umma.

Leo hii wazungu wanatuaminisha kuwa nchi ya Zimbabwe imeharibika kutokana na kuondoa mazingira ya unyonyaji wa wawekezaji wa kizungu.

Siku zote wazungu wamesisitiza kuhusu kubadilisha utawala kwa njia ya demokrasia...kwa nini wachekelee mapinduzi? Kwa nini hawatumii maguvu yao kuzuia mapinduzi?Je mfumo wa mapinduzi ni sehemu ya njia bora za kubadilisha tawala?


Ni wakati AU kuonesha makucha yake na kukataa double standards katika Demokrasia.Au wanapaswa kupinga kwa kauli na matendo yote dhidi ya mapinduzi haya ya kijeshi.

AU wasipoponga au UN wasipopinga mapinduzi basi tusuwasikie tena kupinga mapinduzi sehemu yoyote duniani.


Inasemekana jeshi la Zimbabwe liliwasiliana na China ili kufanya hayo wanayotaka kufanya...kama hili ni kweli basi AU haina budi kumuonya China na ikiwezekana kumkataa kama muwekezaji kwani naye atakuwa amekubaliana na wazungu kuimaliza Afrika.


AU watakuwa na kikao kinachohusu usalama kesho...tusubiri tuone tamko lao.



Wananchi wa Zimbabwe wenyewe wamemchoka Mugabe, time has come for Africans kuleta mapinduzi. Hawa viongozi wote dizaini ya Mugabe, Kagame, Museveni, na wengine ni LAZIMA waondolewe kwa nguvu kwani wanachangia sana kutoleta maendeleo nchini mwao. Unakaa madarakani miaka 30, 40 au milele wakati hauleti maendeleo yeyote nchini what is the point? Unaambiwa unemployment rate Zimbabwe ni 95%, yet Mugabe anataka kumrithisha mkewe urais wakati hana uwezo wowote wa uongozi. Viongozi wote waliounga mkono mkewe Mugabe wamepewa uwaziri, Mnangagwa ambaye ndiye aliyekuwa makamu wa Mugabe alifukuzwa kazi mwezi uliopita kisa he didn't support agenda ya Grace Mugabe kuwa rais. Kumbuka, Grace Mugabe ni secretary tu na udokta alionao alipewa na Mugabe kwa kishikaji. People had enough.
 
Mleta uzi utakuwa CCM tu. Nani kakwambia wazungu ndio wanampindua??
 
Yule waziri sijui makamu aliyeenda kwa mganga kutaka kujua Mugabe anadanja lini lakini kutokana na intelijensi ya babu kuwemo mpaka huko gizani akaujua ukweli basi nahisi anahusika na hii issue.. Nasikia alitorokea bondeni
 
Hapa jingalao umekuwa mpole kidogo, utanisamee cm yangu bado Mpya hivyo typing error nivumilie kidogo,
Labda nianze Na kukuuliza swali sasa sisi waafrica tufanyaje? Maana watawala wanafanya hila kusaliaa madarakani, maana utakuta baadhi ya nchii raisi ndio anachagua mwenyekiti Wa tume, ana chagua makamishna, mpaka wasimamizi Wa majimboni, anachagua majaji, Na hata matokeo yakitangazwa licha ya kwamba yeye ndio kateua hao majaji, still bado hakuna Mahakama wala chombo chochote chenye mamlaka ya kuhoji Na kuamua vinginevyo Na tume ndio wenye kauli ya mwisho kumtangaza mshindi, Na bado katiba kwa sehemu kubwa ni kama ya mfumo Wa chama kimoja Na bado kwenye utakuta kuna majimbo yanachukua mpaka wiki mbili kutangazwa mbunge aliyeshinda, sasa mpaka hapa utaona jinsi mazingira yalivyo magumu upande Wa demokrasia Na ukitaka mabadiliko wenzio hawataki kwakuwa inawapendelea, sasa katika mazingira ya namna hii mheshimiwa sana jingalao ebu nisaidie tutaepusha vipi mbo ya ajabu ajabu kutokea ktk jamii zetu?
Ebu nisaidie uwenda kuna mahali sifahamu vizuri.
 
Watanzania mbona mu-wagumu kuelewa?? Wanaogombana ni chama tawala. Kumbuka ni msimamo wa jeshi la Zimbabwe kwamba hawatamuunga mkono Rais ambaye hakupigana vita ya ukombozi. Na makamanda wote ni memba wa vikao vya ZANU PF
 
AU ndo takataka gani? Wamegeuza nchi zao kama mashamba yao, nchi ya familia, wakae kimya kabisa waufyate maana hawana msaada wowote bali kulindana na kutaka kufia madarakani
 
AU wanadai hawatambuwi mabadiliko ya kiuongozi ya kimapinduzi, hapa naona wataongea na Comrade tu, kwamba yatosha, raia wanaumia, apumzike tu, Makamu rais ataongoza kwa muda, pamoja na kwamba wanadai Makamu hana tofauti kabisa na Comrade, twajuwa kilichotokea, yeye Comrade alitaka mazuri, unfortunately dunia inaongozwa na binadamu aliye mweupe, mwanaume, katili, mnyonyaji kufa, huyu binadamu akisema popote ulipo kwamba hufai sababu tu hujampigia magoti huwezi ongoza nchi, labda uwe na Nuclear Power, watayaongea, nchi ilifika pabaya sana aise..yatosha kwa faida ya raia...
Well said Jebs!
 
Wanaotaka kubadili uongozi sio wazimbabwe bali ni makabaila wa uzunguni.
Ni principle ya kawaida kwamba uongozi huondolewa kwa njia halali na za kidemokrasia
Sawa wanavyomtoa huwezi kumhonga mkeo nchi
 
Back
Top Bottom