Tarakilishi
JF-Expert Member
- May 19, 2013
- 2,180
- 2,454
Hata hivyo ww umefanya makosa ama kwa uzembe, kutojua au kwa bahati mbaya. Hukutakiwa kumpigia yeye, bali ulitakiwa kuwapigia customer care ya mtandao uliotumia kutuma pesa wangeblock na wangekurudishia hiyo hela. Usirudie kufanya makosa ya namna hiyoKaniumiza parefu sana aiseeeee.....
Kwasababu ulichelewa kuwapa taarifaWatu wa mtandao husika hawana msaada mkuu....
Niliwasiliana nao siku ya tukio na wakanijibu kwamba tayari amesha zitoa na hawana la kunisaidia zaidi nikafungue kesi police
Nadhani neno sahihi ni tapeli, sio mwizi.Ila umekosea kumwita MWIZI kwani wewe ndio Mwenye makosa hukua makini wakati wa kutuma pesa kwani yeye hajafanya biashara yeyote na wewe ameshangaa mzigo umeingia kwa nn asiende kutoa atumie wakati malaika kamshushia zigo la hela kwenye sim
Na inawezekana hiyo pesa yako sio ya halali ndio uliko itoa au inapokwenda
Utalindaje brand ya mwizi!Naomba nikupuuze aiseeeee......
Ipo siku nawe yatakukuta
Inaelekea ni muumini wa kkkt kimara, nenda kanisani ukafanye upelelezi utampataKama sio yeye, kwanini alikubali kua amezipokea na akazitoa?
Kama sio yeye kwanini alikubali kwamba anazirudisha?
Kama sio yeye kwanini amepotea kwenye namba ya simu nili mtumia?
Kama nilimtumia hiyo pesa tarehe 23 March, jaribu kuoanisha na alichokuja kuki post kwenye account yake ya facebook tarehe 26 March
Yashanikuta,bahati nzuri haikuwa pesa kubwa nikapotezea baada ya niliyemtumia kuingia mitini!Hayajakukuta. Kuna siku Italia kilio cha mbwa meno hayaumani.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Jumapili nenda hapo kkkt kimara utamuona anasimama hapo alipopigia picha, akitaka kupiga nyingine au umwambie mchungaji atangaza hapo kanisani!
Lakini isije ikatokea ukamwaga machozi hapo kanisani maana ndipo hapo Bashite alipomwaga machozi!
Sasa nani ana kosa? Wewe au yeye?Mkuu...
Huyu jamaa nilimtumia pesa kwa bahati mbaya nikiwa nafanya malipo kwa watu kadhaa.... Sasa baada ya kuwalipa wengine wote, nikapata sim toka kwa jamaa mmoja akiulizia malipo yake. Nami nikamjibu kwamba tayari nimefanya malipo kwa watu wote, lakini nikaamua kurudi kuhakiki kama nilikua sahihi.... Toba...[emoji87] [emoji87], nikakuta nimezituma kwa Venance Chiwalala.
Hapo nikaamua kumpigia sim na kumtaarifu kuhusu kilicho tokea king makosa kwa kumtumia pesa asio stahiki, kisha huyu jamaa akakubali na akaniahidi kuirudisha baada ya muda mchache, nami bila hiyana nikamwambia achukue 50,000 kwakua amekua muungwana.
Baada ya kuona muda unapita, ndipo nikaamua kumpigia tena na jamaa akawa amezima sim.
Hajapatikana kwenye namba ile hadi leo.
Hapo nikaamua kwenda toa taarifa police kuhusu tukio lile, na nikafungua kesi ya kuibiwa kwa njia ya mtandao.
Hapo bila kuchelewa nikaanza kufanyia kazi jambo hili na nikapata informations zake kadhaa
Acha hadithi za uongoTusizunguke mbuyu, Huyo Jamaa ni mwizi maana Kama pesa Imeingi Kwenye ac yako halafu hujui imetoka wapi ni busara kusubiri na kuona nani atakupigia, Mimi ilishanitokea siku moja hela iliingia kwangu yakutosha kiss nikasema doh, mambo yamekaa poa ila roho ikaniuma sana, nilikuwa na rafki yangu akanishauri tukaitoe fasta nikaona ni mwenye Tamaa nikampa ukweli kuwa sili jasho la mtu kwanza sijui kaipata vipi, nimekaa masaa mawili nishasahau nasikia sim inaita kupokea nasikia mama analia nikamuuliza vipi mbona walia na sikufahamu akaniambia amenitumia pesa kimakosa nikamuuliza sasa anacholia ni nini akaanza kujieleza mambo meengi nikamwambia pesa yake ipo salama cha msingi aongee na Huduma kwa Mteja wairudishe na kuanzia wakati huo sitafanya muamala wowote mpaka anijulishe kuwa amerudishiwa hela yake mama alifurahi sana, sikuona nimeshinda njaa kwasababu nimeachia pesa isiyo halali yangu, hivyo Mimi napitisha kabisa kuwa huyo mtu ni mwizi kabisa tena alaaniwe
Wewe ulifanya busara sana. Na huyo jamaa angechukua hata laki tu si mbaya. Kutokomea ndo kosa.Yashanikuta,bahati nzuri haikuwa pesa kubwa nikapotezea baada ya niliyemtumia kuingia mitini!
Kuna siku nikiwa chuo,nilikuwa nimepigika kinoma na rafiki yangu!Hatukuwa na hata mia ya kula mchana!Ilikuwa jmos,basi tukawa tumelala tu hostel kila mtu akihangaika na simu kucheki ndugu wa kututoa kwenye majanga!Mimi nilikuwa nimepiga mzinga watu kama watatu hivi!Nikawa nasubiri,ghafla 100,000/= ikaingia!Kilichofuata nikamshtua jamaa twende tukale mzigo umeingia!Kwa njaa niliyokuwa nayo hata sikuangalia nani katuma,nikaenda kutoa 30,000 tukaenda kula!Tukiwa katikati ya msosi,nikapigiwa simu na mama mmoja akaniambia amekosea kutuma hela!Daah nilisinyaa!Ikabidi nimueleze hali halisi bila kuficha!Nikamuomba nimrudishie 70,000 ikiyokuwepo kwny simu then nikipata nitamtumia kiasi kilichobaki!Huyo mama hakuamini,akasema mwanangu basi tu usitume hata hiyo 70,000!Itakusaidia na usome kwa bidii!Mpaka leo huyo mama tunawasiliana na kujuliana hali!
Ukikosea kutuma pesa basi fanya kama umepoteza tu,usiihesabie kabisa!Halafu mtu huwezi muanika kisa ameingia mitini na hela uliyomtumia kimakosa!
Umeona ushimeni alivyofanya makosa... Huyu mtu akienda mahakamani Ushimen haponi...Mkuu Ushimen nimemcheki kijana Facebook yake naona yupo tu anatamba ila Instagram ndio kaweka Private!
Nahisi kumpata ni rahisi ila kuipata hela ndio inaweza kuwa ngumu!
Halafu dogo anafanana na Bashite nahisi wana undugu!
Kichefuchefu cha kutetea wezi na majambazi kila uchao kinazidi, tunakunywa maji mengi kuzuia kutapika, lakini inashindikana hadi tunatapika sasa.huo ni kuchafuana brand!una uhakika gani kama ndio yeye?kosa ni kako au lake?kwa nini umejipa kazi ya polisi na mahakama?kama sio yeye uko tayari kumlipa fidia?achaupuuzi
Wakurupukaji kama wewe huwa hamkosekani aisee!huo ni kuchafuana brand!una uhakika gani kama ndio yeye?kosa ni kako au lake?kwa nini umejipa kazi ya polisi na mahakama?kama sio yeye uko tayari kumlipa fidia?achaupuuzi
Na usiishie tu hapa jf, mpeleke mpaka facebook huko ili dunia yote imjue.maana amekosa ubinadam kabisa.Hawa watoto tatizo kwakua wanatuona tunashinda nao humu na kutaniana nao, wanadhani tunafanana nao.
Kama jamaa ameshindwa kua muungwana, nami sioni ajizi kumuanika aiseeeee.... Na hii itakua fundisho kwa wenye tabia kama yake
Mimi sijatoa hadithi nimetoa ukweli sasa wewe mbuzi wa kafara endelea kuwaza uongo ivyo ivyoAcha hadithi za uongo