Nitatoa zawadi ya 200,000

Nitatoa zawadi ya 200,000

Kuna mtu alinitimia elfu 43 voda, akanipigia simu kunijuza nami nikamrudishia pesa zote aisee huyo mtu hadi leo amekuwa rafiki yangu, tunachat na kusalimiana kama ndugu. Pesa kwa wengine huonekana maana haramu hadi kutokomea kusikojulikana..pole sana
 
Vijana wa daslamu wanapenda sana maisha ya mteremko.....

Wanapenda sana ganda la ndizi au mteremko.....ndio hao wanaopaka mpaka lipstick midomoni na kutwa wanashinda vijiweni......

Naamini kabisa hiyo hela ingemfikia mtu muhangaikaji kama wewe nina hakika angekurudishia......tena bila hata ya kumuuliza......

Mtoto wa kiume unakulaje hela ya mwanaume mwenzio kulaini laini tu.....watoto dizaini hiyo ndio wanaovunjiwa mayai huko nyuma.......

Muone midomo yake anaonekana hata kunyanyua chupa ya soda hawezi atawezaje kubeba zege kujipatia ridhiki yake....!!!??

Ndugu nenda kwa watu wa mtandao...waambie wakupe namba zake tatu alizokuwa anazipigia mara kwa mara hakika utampata tena haiishi hata week......

Chakufanya ukishapata hizo namba kwanza zijaribu kama ni za wanaume basi mtafute binti mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni......ajifanye kama amekosea namba.....nina hakika hata week haiishi....mtakuwa mmeshamtia mikononi huyo bwana mdogo......kila la kheri ndugu....

Usikatishwe taamaa na makelele ya watoto wa mama humu wanaoshangilia huo upuuzi......
 
pole,atapatikana huyo,namba ya simu iko kwenye kitambilisho cha mpiga kura,uraia,leseni ya gari,ni rahisi tu,hili ni funzo tunapotuma fedha tuwe makini kwa kuwa kila kitu unaweza kuhakiki mwenyewe,kama jina unalijua ukifika pale neno la siri mtandao utakupa Jina,linganisha ndio ugonge 1.ndio gonga moja baada kujiridhisha,si hivyo,
mh! hela toka benk kwenda kampuni za simu haioneshi jina. Ingekuwa simu kwenda simu, kweli.
 
huo ni kuchafuana brand!una uhakika gani kama ndio yeye?kosa ni kako au lake?kwa nini umejipa kazi ya polisi na mahakama?kama sio yeye uko tayari kumlipa fidia?achaupuuzi
HEEE Maajabu!
 
Kaka niliwahi nami kupoteza hela kwa njia hii hii nilimtumia hela mtu nikawa nimekosea digit moja then aliyetaka hiyo hela akaniambia hakupata nikatuma tena then badae kuja kucross check nikakuta badala ya kuandika 21 nikaandika 51 akazima cmu hadi leo ila nachoamini nae atakuja fanyiwa kama mimi nilivyofanyiwa.Kimsingi alipost hii thread hajafanya sawa anatakiwa afuate taratibu zilizopo na atampata mhusika bila tabu
 
Mkuu...
Huyu jamaa nilimtumia pesa kwa bahati mbaya nikiwa nafanya malipo kwa watu kadhaa.... Sasa baada ya kuwalipa wengine wote, nikapata sim toka kwa jamaa mmoja akiulizia malipo yake. Nami nikamjibu kwamba tayari nimefanya malipo kwa watu wote, lakini nikaamua kurudi kuhakiki kama nilikua sahihi.... Toba... , nikakuta nimezituma kwa Venance Chiwalala.
Hapo nikaamua kumpigia sim na kumtaarifu kuhusu kilicho tokea king makosa kwa kumtumia pesa asio stahiki, kisha huyu jamaa akakubali na akaniahidi kuirudisha baada ya muda mchache, nami bila hiyana nikamwambia achukue 50,000 kwakua amekua muungwana.
Baada ya kuona muda unapita, ndipo nikaamua kumpigia tena na jamaa akawa amezima sim.
Hajapatikana kwenye namba ile hadi leo.
Hapo nikaamua kwenda toa taarifa police kuhusu tukio lile, na nikafungua kesi ya kuibiwa kwa njia ya mtandao.
Hapo bila kuchelewa nikaanza kufanyia kazi jambo hili na nikapata informations zake kadhaa
Acha upuuzi,hiyo ni fursa!Usimdhalilishe mtu kwa uzembe wako!Unajua shida zake?Mbuzi kafia kwa muuza supu!
 
Mkuu Ushimen nimemcheki kijana Facebook yake naona yupo tu anatamba ila Instagram ndio kaweka Private!

Nahisi kumpata ni rahisi ila kuipata hela ndio inaweza kuwa ngumu!

Halafu dogo anafanana na Bashite nahisi wana undugu!
Umenifanya nicheke kwa sauti
 
Huu ni wizi kwani kajulishwa kuwa imekosewa na kuahidiwa ajimegee za usumbufu, lakini kaona apotee nazo zote. TUSIMTETEE, HUU NI WIZI.
huyo si mwizi uyo kakosa uhungwana alafu yawezekana alikuwa nashida mungu huwa anamakusudi
 
  • Thanks
Reactions: y-n
no vitu vingne jarbu kutumia common sense leo umepost pics za mtu humu kwa jina alosajiria line
tz kuna watu kibao wanatumia line ambazo hazisajiliwa jina lake kama mm hapa
je mwenye hio pics akikufungulia kesi ya uzalilishaji utakua umeonewa??na ushafikiria odds za kishndwa na utaoteza shilling ngap zaidi???
Huyo huyo akipatikana atasaidia kumpata muhusika huwezi kuomba kisajili line na kitambulisho cha mtu wa mbali lazima atakuwa ndugu jamaa au Rafiki
Mie kuna siku wakala aliniwekea 800,000/- badala ya 80,000/- nikaona baadae kuwa kazidisha hela. Kesho yake nikarudi nikamuuliza jana umeniwekea sh ngapi akasema elfu themanini. Nkamwambia angalia meseji zako. Mama wa watu alitahamaki nikamrudishia 720,000/- huyo mama kila akiniona anahadithia watu maana hakuamini.

Maisha haya ni uaminifu tu. Mtu akikosea sio sababu ya kuona una bahati maana huwezi kujua shida utakazomuachia. Pia ni laana na mikosi kumdhulumu mtu usiyejua tabu zake
 
Huyo huyo akipatikana atasaidia kumpata muhusika huwezi kuomba kisajili line na kitambulisho cha mtu wa mbali lazima atakuwa ndugu jamaa au Rafiki
Patamu hapo! Ndo mwenye kitambulisho atapojua kuwa kitambulisho ni transferable au la!
 
Ila umekosea kumwita MWIZI kwani wewe ndio Mwenye makosa hukua makini wakati wa kutuma pesa kwani yeye hajafanya biashara yeyote na wewe ameshangaa mzigo umeingia kwa nn asiende kutoa atumie wakati malaika kamshushia zigo la hela kwenye sim
Na inawezekana hiyo pesa yako sio ya halali ndio uliko itoa au inapokwenda
 
Ila umekosea kumwita MWIZI kwani wewe ndio Mwenye makosa hukua makini wakati wa kutuma pesa kwani yeye hajafanya biashara yeyote na wewe ameshangaa mzigo umeingia kwa nn asiende kutoa atumie wakati malaika kamshushia zigo la hela kwenye sim
Na inawezekana hiyo pesa yako sio ya halali ndio uliko itoa au inapokwenda
Ni kosa kisheria kutumia pesa ambayo umeipokea kimakosa, sheria inakushurutisha kurudisha sehemu ilipotoka
 
Back
Top Bottom