Nitamwambiaje Mke wangu mimi ni 'Atheist'?

Nitamwambiaje Mke wangu mimi ni 'Atheist'?

Sasa mtoto mdogo wa kuzaliwa leo anawezaje kuwa na msimamo wa kwamba hakuna Mungu?
Kwahyo mtoto aliyezaliwa leo anaamini uwepo wa Mungu?.
Kuwa atheist sio lazima uwe na msimamo Hakuna Mungu hata kutoamini uwepo wake either kwa kutokujua pia ni Atheism.
Chukulia mtoto azaliwe na akulie porini na wanyama..Je dini yake itakuwa ipi?Uislam au Atheism?
 
Ndugu wala huwezi kuwa harsh hata kidogo ni swala la kumueleza tu kua huamini katika hizo dini akaelewa na maisha yakaendelea !Alafu kwani usipoamini ndio mwisho sa maisha yako ndugu.....Sema sasa wafia dini watakupinga sana kana kwamba ndio walileta hizi dini
 
Kuna masuala ya bima, likizo, posho mbalimbali na likizo pia mkuu, ukiwa kwenye ndoa (hasa mke) unakua na advantage kubwa kuliko ambaye hajaolewa
Ndio na mm najua hilo, wengi mbona wamefungishana ndoa za mahakamani ili wapate vyeti ili wapate stahiki za mke pongezi sana nao ni uamuzi mkubwa
 
Wakuu habari,

Mimi ni siamini kuhusu masuala ya dini, ila naamini binadamu tunapaswa kuishi kwa upendo kati yetu na tuwapende pia viumbe wengine, naamini hii ndio 'perfect' na 'universal dini'.

Matatizo kama vita, njaa, mauaji, talaka, pengo kati ya matajiri na masikini n.k vyote hivi tungevipunguza kwa kiasi kikubwa kama tungezingatia hii 'universal dini' zaidi kuliko nyingine

Mke wangu ni mtu wa Dini sana, ametokea familia ya walokole.

Amekuwa akinisumbua kuhusu kwenda kanisani kila mara, nimekuwa nikimpa visingizio vya hapa na pale ili nisiende naye kanisani, ila naona visingizio vimeisha.

Sasa nimechoka kelele za kuhusu kanisani, nafikiria nimchane kuwa siamini masuala yake ya kanisani na sitaki usumbufu tena.

Nitakuwa harsh sana au kuna mbadala wa kuyamaliza?
Mtumie huu ujumbe atakuelewa vizuri mkuu
 
Ishi ndani ya mlengo wa imani yako, usiyumbishwe na huyo mkeo, muambie ukweli ili uwe huru.
 
Kwahyo mtoto aliyezaliwa leo anaamini uwepo wa Mungu?.
Kuwa atheist sio lazima uwe na msimamo Hakuna Mungu hata kutoamini uwepo wake either kwa kutokujua pia ni Atheism.
Chukulia mtoto azaliwe na akulie porini na wanyama..Je dini yake itakuwa ipi?Uislam au Atheism?
Atazaliwa aje polini wakati yeye sio mnyama poli? hapo ndio ukuu wa Mungu unawazidi maarifa
 
Masimulizi yanaweza kutungwa tu mkuu, anyway mimi sio muumini wa Ukristo wala Uislam au dini nyingine kuu
Lakini Nina independent philosophy yangu nikiamini kuwa kila binadamu anapaswa kumpenda binadamu mwingine na viumbe wengine, wanaaonyesha upendo huo wanakuwa rewarded na 'Mamlaka nyigine iliyo Juu' ambayo unaweza kuita mungu or whatever
Kwa maelezo yako paragraph ya mwisho unaonyesha unamtambua Mungu basi tu umeamua kusumbua watu
 
Hao wote wana matatizo ya akili, kama wanakubali simu imetengenezwa na kuwa hivi ilivyo, vipi Dunia na vinginevyo visiwe na muumbaji ? Hizi akili wanazitumia vibaya sana, ila bishara mbaya kwao.
Na huyo muumbaji aliumbwa na nani...?
 
Kama simu imetengenezwa haimaanishi aliyetengeneza alijitengeneza
Bali ina maanisha nini ? Yaani aliyeitengeneza amefanya nini ?

Pili, hili la kutomaanisha aliyetengeneza alijitengeneza limetokana na na nini, yaani munasaba wake na nilicho kiandika ni wapi au ni nini ?
Kama dunia na vinginevyo viliumbwa haimaanishi aliyeumba alijiumba au haitaji muumbaji
Bali ina maanisha nini ?
Ukisema muumbaji wa ulimwengu hana muumba unakua huna tofauti na anayekubali simu ina mtengenezaji ila ulimwengu hauna muumbaji
Ili niwe sawa na huyo wa kwanza, naomba unipe sababu tano tu zinazo onyesha ya kuwa muumbaji anabidi awe ameumbwa. (Japo najua hili huwezi kulifanya ila naonyesha kwa namna gani ulivyo dhaifu wa kufikiri).

Atakaye sema Ulimwengu hauna muumna inabidi atuambie amejuaje kama ulimwengu hauna muumba na atupe ithibati.
 
Wote tumezaliwa tukiwa atheist, dini tulikuja kuzifata baada ya kuja kuwa indoctrinated

Mtu kuwa atheist haimaanishi kabadili asili yake bali kairejea asili yake ambayo mwanzo aliikacha
Nithibitishie ya kuwa sote tumezaliwa tukiwa "Atheist".
 
Hii point ila huwa inanipa maswali hadi nahisi kuchanganyikiwa na huwa naachana nayo. Huyo mwumbaji wa dunia yeye nani alimwumba???? Nikijibiwa hili vizr nakuwa mchungaji mwaka huu😇😇
Kwanza nipe sababu na unionyeshe haja ya muumbaji wa mbingu na ardhi kuwa na yeye ameumbwa.
 
Back
Top Bottom