Nitamuachaje mmama huyu anae nizidi miaka tisa?

Nitamuachaje mmama huyu anae nizidi miaka tisa?

Mdau ulikuwa na mawazo kama ya kwangu big up sana mdau

Mpaka sasa simuelewi huyu jamaa kwa kweli mkuu. Huyo ni mwanamke wa maana sana ila halioni hilo sasa mpaka aweke paka asieshiba ndani ya nyumba yake ndio ataelewa. Kuna watu wana stress kila kukicha kisa mwanamke walie nae ni mtumiaji asiefaa, akionyeshwa pesa tu anakuwa mwehu wakati kuzitafuta hajui.
 
Kama hiyo story sio ya kutunga kama tulivyozoea kwa watu wa aina yako huku kwanza nakuambia yafuatayo:
Wewe inaonyesha unajivuna halafu hujatulia hata hiyo course sidhani kama ni kweli umesoma wewe muongo ni story tuu
Pili hakuna mwanamke utakae mpa laki 4 gafla aje azalishe milioni 11 na bado ana familia ya watoto 2 leo hii unakuja kupost story za kumuacha
Tatu ka ulikuwa humpendi utampaje hela wewe bila shaka upo darasa la saba na story za mapumziko ya saa nne wakati unasubiri uji

umetisha mkuu
 
Hahahaha jf banaaa rahaa...ww mtaji wa laki nne azalishe milioni 11 kwa miaka minne au mitano??...mama anawatoto 2..hali wala kwenda njoo huyo..hawaugui???...uongo mwingine bhana duu...
 
Mkuu tatizo umri mi na miaka 24 dheni yeye ana 34,We huoni gap lililopo?,Asume nimemuoa atazaa hata watoto watatu kwa umri wake?.

Si mbaya mkuu ata kama akikuzalia watoto wawili, wana tosha kwa sasa, huyo amekupenda sana mkuu.kwanza mwingine angeshaakupa hata gonjwa hatari. We uoni kuwa ni mwaminifu huyo.
 
katika kitu cha kuepuka ni kuachana na mtu kwa ugomvi, kaa nae mueleze atakuelewa mtu mzima huyo, possibly mambo mengine yakaendelea :teeth:
 
Tofauti ya miaka kumi unampeleka wapi???
Yani kabisa unaoa mmama alokuzidi ten good yrs?
Kwani yeye tu ndo anaweza kuzisaka pesa?
Hujui kuwa huyo amabembeleza kuishi na weye? Au hujui kuwa wanawake wa miaka hii wanabembeleza ndoa?
Huyo akiwa ndani ya ndoa aweza kukusimbua kama mwanamke yoyote yule....
Ni maoni tu..
 
Heshima kwako mkuu.
KALINZI NYUMBANI

Huyo ana uwezo wa kizaa hata watoto wawili. Siwezi kukushauri umuoe, kwani ni dhahiri humpendi kabisa ila umri umeiona kuwa ni sababu strong ya kujustify kumuacha kwa sababu angekuwa moyoni mwako, swala la umri ungeliweka pembeni na swali ambalo ungelileta hapa lingekuwa jinsi ya kuwashawishi ndugu na jamaa zako ili wampokee kama sehemu ya familia.

Usichokiona kwa sasa ni kuwa, huyo ni mwanamke anaejua maisha kwani alikwishayaanza kabla yako na akakomazwa kwa ndoa na uzazi. Hahitaji training kwani ana akili na uwezo wa kutambua na kufanya maamuzi sahihi yenye manufaa kwake na kuweka pembeni yasiyo ya msingi tofauti na mtu alie na umri mdogo au alie immature kiakili.

Kuna watu wameoa wanawake wanaojua sana label za bia, lakini hawawezi hata kununua au kuingiza units za luku. Wengine wanajua kuvaa na kutumbua sana ila mpe mtaji umwambie; "Baby, hebu izungushe hii milioni 5, usomeshe watoto wetu na kile nachopata mimi (mume) tukitumie kumalizia mjengo wetu". Ndani ya mwezi tu atakwambia biashara imemshinda kwa sababu hajazoea kupigizana kelele na wateja, kukaa sehemu moja au kuzunguka. Sasa muulize ulipo mtaji uliompa. Hapo ndipo utakapozusha ugomvi ambao hutausahau.

Kipindi ulipozinguliwa, uliapa kutafuta mtu mzima, ukampata anaefaa kabisa, ila unapokaribia kugraduate, unamuona hafai na inawezekana na tayari umeishampoint unaemwona anafaa zaidi, sasa yakijirudia wakati hizo ml 11 zimeishapukutishwa benki, uje utupe mrejesho pia.
 
Hahahaha jf banaaa rahaa...ww mtaji wa laki nne azalishe milioni 11 kwa miaka minne au mitano??...mama anawatoto 2..hali wala kwenda njoo huyo..hawaugui???...uongo mwingine bhana duu...
Mkuu unaweza kuona ni uongo lakini itabaki kuwa kweli.We hujiulizi maisha ya mkoani huko baada ya kuukuza mtaji na kuchukua mzigo wa milioni mbili na faida inafika milioni moja point tatu.Asume yeye na familia ake baada ya kuukuza mtaji kwa mwezi atumie laki tatu tu,Ingawa ni nyingi kwa mkoani then awe anasev milioni moja tu kwa mwezi.

Mimi huku nikiishi kwa Bum na hela ya field tu.kwahiyo sishangai unavyosema ni uongo maana kuna wengine milioni kumi ni hela ya mboga ya siku moja.
 
Mpaka sasa simuelewi huyu jamaa kwa kweli mkuu. Huyo ni mwanamke wa maana sana ila halioni hilo sasa mpaka aweke paka asieshiba ndani ya nyumba yake ndio ataelewa. Kuna watu wana stress kila kukicha kisa mwanamke walie nae ni mtumiaji asiefaa, akionyeshwa pesa tu anakuwa mwehu wakati kuzitafuta hajui.
Mkuu nimekuelewa sana asante kwa ushauri wako.
 
Tofauti ya miaka kumi unampeleka wapi???
Yani kabisa unaoa mmama alokuzidi ten good yrs?
Kwani yeye tu ndo anaweza kuzisaka pesa?
Hujui kuwa huyo amabembeleza kuishi na weye? Au hujui kuwa wanawake wa miaka hii wanabembeleza ndoa?
Huyo akiwa ndani ya ndoa aweza kukusimbua kama mwanamke yoyote yule....
Ni maoni tu..
Mkuu nimekuelewa.
 
Back
Top Bottom