Wakuu salama,
Kipindi nipo form five,nilipata demu mmoja hivi tulie kuwa tunalingana nae hakika tulipendana sana. Baada ya kumaliza form six sote tulifaulu, tukawa tumechaguliwa chuo, lakini tulienda vyuo tofauti. Baada ya kufika chuo tulipomaliza semister ya kwanza, huyo msichana alianza kuniletea mizinguo nikamvumilia sana mwisho wa siku tukaachana.
Sasa baada ya kuachana nae nilipokuwa naenda likizo nyumbani huko mkoani, niliona nikatafute mwanamke anae nizidi umli labda yeye atatulia. Sasa nilipofika nyumbani mta kama wa tatu kutoka nyumbani, alikuwepo mwanamke fulani hivi mwenye watoto wawili. Ambae mume wake alifariki kwa ajali ya gari.
Nikawa nimemtokea akawa amekubali lakini kiumri alikuwa mkubwa kwangu, alkuwa ananizidi miaka tisa.Sasa baada ya kuanza mahusiano nae baada ya kama miezi mitano na kwa vile alionyesha kuniheshimu sana na kunijali sana. Nilimshauli tuanza nae biashara akawa amekubali. Nilianza na mtaji wa laki nne ambayo nilikuwa nmeibana kutoka kwenye BUM.
Nikaanza kwa kununua madira na vitenge nikawa navisafirisha kwenda mkoani, akawa anauza kwa mkopo kwa wanawake wenzake. Kila mwisho wa mwezi akawa ananitumia hela nanunua mzigo nausafirisha anaupokea dhen anauza.
Tumefanya biashara hiyo ndani ya miaka miwili, nampaka ninavyoongea hivi sasa kanizalishia faida ya milioni kumi na moja nimeihifadhi benki na bado tunaendelea kufanya nae kazi na kugegedana pia.
Lakini sasa mwaka huu namaliza course yangu ya Mechanical Engineer na tatizo anadai nikimaliza nimuoe. Kusema kweli simpendi hata kidogo lakini nipo nae kwa ajili ya kumgegeda na kufanya nae biashara hiyo.
Sasa waungwana mpaka sasa sijui nimuachaje maana nmeshafanya majaribio ya kumuacha mwaka huu takribani mara mbili lakini wapi! maana kaniganda sana.Sasa kiukweli mie siwezi kumuoa na wala simpendi na tatizo kubwa ni umri wetu mimi na yeye. Kwahiyo wakuu nifanyeje huyu mwanamke niweze kuachana nae?
Naombeni ushauri
Asanteni sana