Nitamuachaje mmama huyu anae nizidi miaka tisa?

Nitamuachaje mmama huyu anae nizidi miaka tisa?

Tafuta ujasiri wa kumshawishi Bi mkubwa ili aone umuhimu wa huyu mrembo kuendelea kuwemo ndani ya maisha yako wewe ndiye utakayeishi na mkeo si Bi Mkubwa. Na huu wimbo wako wa umri mkubwa unaanza kuudhi sasa hebu achana nao, ama muoe ama umpige chini ukiamua kumpiga chini mpe milioni tano au sita ya kumuwezesha kuendelea na maisha yake, lakini nakuhakikishia ukimpiga chini huyu utakuja kumkumbuka sana pamoja na kukupeanda anavyokupenda, kukuheshimu, kuwa mwaminifu kwako na mtendaji mzuri kwenye biashara lakini yote haya hukuyathamini ukaona tofauti ya miaka 9/10 kati yenu ndilo kikawa kipaumbele chako ili umpige chini. Wanawake kama huyu katika dunia ya leo wanatafutwa sana na wengi, lakini ndiyo hivyo waswahili walisema kwenye miti hakuna wajenzi. Usiendelee kumpotezea muda wake kwa kuendelea kumdanganya utamuoa ukimaliza shule miezi michache ijayo.
Mkuu asante sana na pia nimekuelewa sana.
 
BAK kwanza kabs atuambie huyo mke ni kabila gani
tupo apa yaani akimtema tu kama huyu mama/binti anampenda yaan atamloga adi akome
atajazwa minuksi adi aone maisha yamesmama...................
hakuna kaitu kibaya kama kucheza na hisia za mtu

duh!! huu ushauri unaotoa wiki hii ni kiboko aiseee!!
 
Last edited by a moderator:
duh!! huu ushauri unaotoa wiki hii ni kiboko aiseee!!

ujue ndg yangu watu hawapend hata kidogo kuambiwa ukwel
sikufichi ukweli utamskia mtu akisema wazi mie nimelogwa jaman
ama fulan kalogwa. asa mie nuwaga nawauliza ivi mtu anaanzaje kukuloga ivi ivi??
ukichunguza ni mpaka kumekuwa na chanzo ambacho kinamfanya afanye ivyo na chanzo kikubwa ni mapenzi.
sasa huyu kacheza na hisia za mwenzie al those yrs leo eti hameet standards zangu.........kweli hii ni haki?
atapigwa nuksi ya myai viza na mavi adi aisome namba.
 
Huyo mwanamke ni mjasiria mali haswaa,kwa concern yako ya umri tafuta siku moja uongee naye juu ya hilo.Kama wenzako walivyosisitiza kwenye michango yao milichuma pamoja kwenye hiyo biashara yenu inabidi huyo mama umpatie mgao wake.Nami ninapendekeza umwachie shs 5M ili aendeleze hiyo shughuli yake.Ongeeni katika hali ya maelewano ili asije akaweka bifu ikawa mahusiano ya paka na panya hahaha.
 
kiukwel huyo mwanamke anakupenda sana na sio rahisi kumwambia muachane afu akubali kiurahisi,
hawezi kukubali hata kidogo chamsingi piga moyo konde ukiwakama mwanaume then fuata hisia zako,ingawa itamuuma sana kwa kumuacha,lakin baada ya miez kadhaa atarudi kweny hal yake,ila mpe 7Miln kama shukrani.
 
wanawake wenye umri mkubwa wanajua mapenzi na kukaba penalt sanaa.mpe hela aendelee na biashara,we oa mwanamke mwingine ata poa tu,na maisha yataendelea
 
Wakuu salama,

Kipindi nipo form five,nilipata demu mmoja hivi tulie kuwa tunalingana nae hakika tulipendana sana. Baada ya kumaliza form six sote tulifaulu, tukawa tumechaguliwa chuo, lakini tulienda vyuo tofauti. Baada ya kufika chuo tulipomaliza semister ya kwanza, huyo msichana alianza kuniletea mizinguo nikamvumilia sana mwisho wa siku tukaachana.

Sasa baada ya kuachana nae nilipokuwa naenda likizo nyumbani huko mkoani, niliona nikatafute mwanamke anae nizidi umli labda yeye atatulia. Sasa nilipofika nyumbani mta kama wa tatu kutoka nyumbani, alikuwepo mwanamke fulani hivi mwenye watoto wawili. Ambae mume wake alifariki kwa ajali ya gari.

Nikawa nimemtokea akawa amekubali lakini kiumri alikuwa mkubwa kwangu, alkuwa ananizidi miaka tisa.Sasa baada ya kuanza mahusiano nae baada ya kama miezi mitano na kwa vile alionyesha kuniheshimu sana na kunijali sana. Nilimshauli tuanza nae biashara akawa amekubali. Nilianza na mtaji wa laki nne ambayo nilikuwa nmeibana kutoka kwenye BUM.

Nikaanza kwa kununua madira na vitenge nikawa navisafirisha kwenda mkoani, akawa anauza kwa mkopo kwa wanawake wenzake. Kila mwisho wa mwezi akawa ananitumia hela nanunua mzigo nausafirisha anaupokea dhen anauza.

Tumefanya biashara hiyo ndani ya miaka miwili, nampaka ninavyoongea hivi sasa kanizalishia faida ya milioni kumi na moja nimeihifadhi benki na bado tunaendelea kufanya nae kazi na kugegedana pia.

Lakini sasa mwaka huu namaliza course yangu ya Mechanical Engineer na tatizo anadai nikimaliza nimuoe. Kusema kweli simpendi hata kidogo lakini nipo nae kwa ajili ya kumgegeda na kufanya nae biashara hiyo.

Sasa waungwana mpaka sasa sijui nimuachaje maana nmeshafanya majaribio ya kumuacha mwaka huu takribani mara mbili lakini wapi! maana kaniganda sana.Sasa kiukweli mie siwezi kumuoa na wala simpendi na tatizo kubwa ni umri wetu mimi na yeye. Kwahiyo wakuu nifanyeje huyu mwanamke niweze kuachana nae?

Naombeni ushauri

Asanteni sana

yani wewe ni chizi ila hujijui.huyo mke utamkumbuka na laana zitakuandama yani mmechuma nae sasa unamnyanyapaa.nyambafu
 
Kwa Usalama Wako Huyo Mjasliamali Mwachie Pesa Zote Kama Unajipenda!
 
Nimeshakufahamu maana ulishawahi kunipa hii story ngoja nimwambie unachotaka kufanya.
 
Usimpoteze huyo mama.....ila mwambie ukweli kwamba hamtaweza kuowana lkn endelea naye kama partner Wa kibiashara
 
Unaweza owa unayelingana umri ukafulia vibaya kama hana matatizo muowe
 
Mkuu medisonmuta sawa nimekuelewa lakini angalia tofauti ya umri wetu.

Wewe kweli wachu, kalimanzila nk ukimwacha mwanamke huyo hutampata mwingine. Age is nothing but number. Grow up. Wanawake wa namna hiyo siku hizi hawapo unapata gold unaitupa. Nakwambia ukimwacha utapata utajuta
 
Back
Top Bottom