Godoro la kioo
JF-Expert Member
- Aug 2, 2025
- 436
- 934
Salaam. wakuu kina kitu kidogo nilitaka walau kwenu nyinyi mtazamo wenu je hakitoleta shida huko mbeleni
Inshu nzima iko hivi . kuna demu flani nilikutana nae maeneo flani demu kiukweli nikatokea kumuelewa
Basi nikaamua kumtokea na nikamueleza lengo langu kubwa nahitaji kuwa nae
Demu alizungusha zungusha kidogo kama mnavyojua lakini baadae akakubali, na tukaanza mahusiano
Lakini kadri tulivyozidi kwenda demu akawa mtu wa vizinga sana, ikafikia hatua nikitaka tuonane anaanza kuelezea shida zake mara ana shida na elfu kumi .au elfu kumi na tano
Siyo siri ile hali ikawa inanikwaza maana kama kweli alikuwa na shida na namba yangu anayo na tunawasiliana kila siku kwanini asiniambie mapema, iweje nikitaka kuonana nae ndo anaanza hizo sababu
Mwanzoni nilivumilia lakini baadae nikaona huyu hapana halaf ukijumlisha mimi mwenyewe bado najitafuta nikaamua kutemana nae na tukapotezeana kila mtu akawa hana habari na mwenzake
Sasa nilikuwa na jamaa angu tumeshibana sana.. sasa mshikaji ikawa kila siku ananisimulia mapenzi yanamchanganya kila akijaribu mahusiano anapigwa za uso
Kama nauli ashatuma sana kwa wanawake nauli inaliwa na hamna anachoambulia
Sasa alikuwa ameamua ajiweke mbali na mapenzi , kwa kiasi chake juhudi za kujiweka mbali na wanawake alifanikiwa lakini akawa anasumbuliwa sana na upweke kiasi kwamba ilifika hatua akawa hana hata mwanamke wa kumjulia hali kitu ambacho kilikuwa kinamuumiza
Akawa ananiomba kama kuna demu namjua hana shida nimfanyie mchongo apate mwanamke
Kwanza nikamuuliza unataka mwanamke wa kuoa au wa kusaidiana tu kwa hapa na pale
yeye akadai vyovyote vile kama akimuelewa na wakakubaliana anaweza kumuoa
Basi ikabidi nimpasie namba ya huyo ambae alikuwa demu wangu yaani ex wangu
Mshikaji akashukuru pale ila nikamwambia huyo demu kwa wewe ulivyo huyo demu anakufaa {mshikaji pesa sio shida sana kwake}
Basi bhana akaja akamcheki demu akaanza kumuuliza maswali ikiwemo wewe ni nani, namba yangu umeitoa wap, n,k
Jamaa akajitetea anavyojua basi akaanza kumwaga sera zake
Baada ya kama wiki walikuja kuonana uso kwa uso wakapiga story za hapa na pale kwa mujibu wa maelezo ya jamaa {kumbuka alikuwa ananisimulia kila tukio}
Kama utani mahusiano yao yakakolea na jamaa akawa anashukuru sana kumkutanisha na huyo mwanamke mpaka akasema anataka amuoe
Sasa mimi sina shida isipokuwa nawaza je. itakuwaje siku tutakapokutana na huyo ambae ni shemeji yangu mpya
Je. atajisikiaje atakapogundua kuwa mimi ndo niliegawa namba yake
na je. kama mshikaji akija kugundua kuwa huyo demu ambae sasa ndo mke wake niliwahi kuwa nae na mimi ndo niliempa namba atajisikiaje
TOENI MAWAZO YENU/MTAZAMO WENU JE . HALITOLETA SHIDA HUKO MBELENI
Inshu nzima iko hivi . kuna demu flani nilikutana nae maeneo flani demu kiukweli nikatokea kumuelewa
Basi nikaamua kumtokea na nikamueleza lengo langu kubwa nahitaji kuwa nae
Demu alizungusha zungusha kidogo kama mnavyojua lakini baadae akakubali, na tukaanza mahusiano
Lakini kadri tulivyozidi kwenda demu akawa mtu wa vizinga sana, ikafikia hatua nikitaka tuonane anaanza kuelezea shida zake mara ana shida na elfu kumi .au elfu kumi na tano
Siyo siri ile hali ikawa inanikwaza maana kama kweli alikuwa na shida na namba yangu anayo na tunawasiliana kila siku kwanini asiniambie mapema, iweje nikitaka kuonana nae ndo anaanza hizo sababu
Mwanzoni nilivumilia lakini baadae nikaona huyu hapana halaf ukijumlisha mimi mwenyewe bado najitafuta nikaamua kutemana nae na tukapotezeana kila mtu akawa hana habari na mwenzake
Sasa nilikuwa na jamaa angu tumeshibana sana.. sasa mshikaji ikawa kila siku ananisimulia mapenzi yanamchanganya kila akijaribu mahusiano anapigwa za uso
Kama nauli ashatuma sana kwa wanawake nauli inaliwa na hamna anachoambulia
Sasa alikuwa ameamua ajiweke mbali na mapenzi , kwa kiasi chake juhudi za kujiweka mbali na wanawake alifanikiwa lakini akawa anasumbuliwa sana na upweke kiasi kwamba ilifika hatua akawa hana hata mwanamke wa kumjulia hali kitu ambacho kilikuwa kinamuumiza
Akawa ananiomba kama kuna demu namjua hana shida nimfanyie mchongo apate mwanamke
Kwanza nikamuuliza unataka mwanamke wa kuoa au wa kusaidiana tu kwa hapa na pale
yeye akadai vyovyote vile kama akimuelewa na wakakubaliana anaweza kumuoa
Basi ikabidi nimpasie namba ya huyo ambae alikuwa demu wangu yaani ex wangu
Mshikaji akashukuru pale ila nikamwambia huyo demu kwa wewe ulivyo huyo demu anakufaa {mshikaji pesa sio shida sana kwake}
Basi bhana akaja akamcheki demu akaanza kumuuliza maswali ikiwemo wewe ni nani, namba yangu umeitoa wap, n,k
Jamaa akajitetea anavyojua basi akaanza kumwaga sera zake
Baada ya kama wiki walikuja kuonana uso kwa uso wakapiga story za hapa na pale kwa mujibu wa maelezo ya jamaa {kumbuka alikuwa ananisimulia kila tukio}
Kama utani mahusiano yao yakakolea na jamaa akawa anashukuru sana kumkutanisha na huyo mwanamke mpaka akasema anataka amuoe
Sasa mimi sina shida isipokuwa nawaza je. itakuwaje siku tutakapokutana na huyo ambae ni shemeji yangu mpya
Je. atajisikiaje atakapogundua kuwa mimi ndo niliegawa namba yake
na je. kama mshikaji akija kugundua kuwa huyo demu ambae sasa ndo mke wake niliwahi kuwa nae na mimi ndo niliempa namba atajisikiaje
TOENI MAWAZO YENU/MTAZAMO WENU JE . HALITOLETA SHIDA HUKO MBELENI