Nitafungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi

Brigedia Chan-ocha

JF-Expert Member
Mar 7, 2014
1,353
2,842
Natarajia kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya jeshi la polisi, naitaka mahakama kuu itoe tafasiri na/ muongozo wa je Jeshi la polisi linaruhusiwa kuteka raia au kukamata raia? Na Je kukamata ni sawa sawa na kuteka? Na je utaratibu wa kuteka raia unatakiwa uweje? Yaani kabla raia hajatekwa ni hatua zipi za kufuata kabla ya tukio hilo? Na je ni haki zipi za mtu anayetekwa na polisi?

Utaratibu wa kukamata Raia unajulikana ila utaratibu wa kuteka raia haujulikani, kwa hiyo nitaiomba mahakama kuu itoe utaratibu mzima, na kama ni halali au haramu kwa polisi kuteka raia itamke waziwazi, na nitaiomba mahakama kama kuteka ni kitendo haramu basi itoe adhabu kali kwa polisi yeyote atakayejihusisha na utekaji raia.

Naiomba mahakama kuu isiogope kupokea na kusikiliza shauri hili, iige wenzao wa kenya wanavyotoa maamuzi bila kuangalia sura ya mtu.

Nawasilisha.
 
Best wishes Mkuu, Ila angalia isije Kesi ya Nyani Unaipelekea Ngendele." Kilio cha Samaki by Dr. Remmy Ongara Machozi Yanakwenda na Maji". In short Kuna Mstari Mwembamba Sana Kati ya Unaopanga Kuwashitaki na Mtoa Haki. Tuseme tu Umeshafail Kabla ya Kuanza Movie yako. But all in all best wishes, sisi tutakuja Kusikilizia Mitaa ya Kisutu.
 
Natarajia kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya jeshi la polisi, naitaka mahakama kuu itoe tafasiri na/ muongozo wa je Jeshi la polisi linaruhusiwa kuteka raia au kukamata raia? Na Je kukamata ni sawa sawa na kuteka? Na je utaratibu wa kuteka raia unatakiwa uweje? Yaani kabla raia hajatekwa ni hatua zipi za kufuata kabla ya tukio hilo? Na je ni haki zipi za mtu anayetekwa na polisi?

Utaratibu wa kukamata Raia unajulikana ila utaratibu wa kuteka raia haujulikani, kwa hiyo nitaiomba mahakama kuu itoe utaratibu mzima, na kama ni halali au haramu kwa polisi kuteka raia itamke waziwazi, na nitaiomba mahakama kama kuteka ni kitendo haramu basi itoe adhabu kali kwa polisi yeyote atakayejihusisha na utekaji raia.

Naiomba mahakama kuu isiogope kupokea na kusikiliza shauri hili, iige wenzao wa kenya wanavyotoa maamuzi bila kuangalia sura ya mtu.

Nawasilisha.
Mungu akulinde katika kutetea haki za watanzanua wenzako. Tunaunga mkono hatua hizi
 
Natarajia kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya jeshi la polisi, naitaka mahakama kuu itoe tafasiri na/ muongozo wa je Jeshi la polisi linaruhusiwa kuteka raia au kukamata raia? Na Je kukamata ni sawa sawa na kuteka? Na je utaratibu wa kuteka raia unatakiwa uweje? Yaani kabla raia hajatekwa ni hatua zipi za kufuata kabla ya tukio hilo? Na je ni haki zipi za mtu anayetekwa na polisi?

Utaratibu wa kukamata Raia unajulikana ila utaratibu wa kuteka raia haujulikani, kwa hiyo nitaiomba mahakama kuu itoe utaratibu mzima, na kama ni halali au haramu kwa polisi kuteka raia itamke waziwazi, na nitaiomba mahakama kama kuteka ni kitendo haramu basi itoe adhabu kali kwa polisi yeyote atakayejihusisha na utekaji raia.

Naiomba mahakama kuu isiogope kupokea na kusikiliza shauri hili, iige wenzao wa kenya wanavyotoa maamuzi bila kuangalia sura ya mtu.

Nawasilisha.
neno "kutekwa" limetumiwa vibaya na Adamoo, amelitumia neno hilo kwa maksudi kwa nia ya kupotosha.

Hata Mbowe alivyo kamatwa kule mwanza wafuasi na viongozi wa CDM walizusha kwa maksudi kuwa eti mbowe "Katekwa"!! huku wakifahamu fika kuwa kakamatwa na Jeshi la Polosi.

Wafuasi wa Mbowe na baadhi ya viongozi wenzake wamekuwa na tabia ya kuzusha na kupotosha habari kwa maksudi na kwa nia ya kuihadaa jamii kwa nia ya kuhalalisha maovu yao.
Jamii iwaelewe hivyo lkn pia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wanapaswa wajue tabia na nia ovu ya watu hao.
 
neno "kutekwa" limetumiwa vibaya na Adamoo, amelitumia neno hilo kwa maksudi kwa nia ya kupotosha.

Hata Mbowe alivyo kamatwa kule mwanza wafuasi na viongozi wa CDM walizusha kwa maksudi kuwa eti mbowe "Katekwa"!! huku wakifahamu fika kuwa kakamatwa na Jeshi la Polosi.

Wafuasi wa Mbowe na baadhi ya viongozi wenzake wamekuwa na tabia ya kuzusha na kupotosha habari kwa maksudi na kwa nia ya kuihadaa jamii kwa nia ya kuhalalisha maovu yao.
Jamii iwaelewe hivyo lkn pia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wanapaswa wajue tabia na nia ovu ya watu hao.
Kukamatwa kuna taratibu zake. Ka taratibu hizo hazikufuatwa, ni utekeji. Polisi wa hapa kwetu wanapenda zaidi kuteka kuliko kukamata.

Utasemaje mtu amekamatwa wakati kanyakuliwa bila ya kuambiwa huyo anayemnyakua ni nani, ana tuhuma gani, anapelekwa wapi. Anasafirishwa usiku kucha, anafikishwa kituo cha polisi anabadilishwa jina, anahamishwa hamishwa mahabusu kila mara?

Tusitetee uovu, tuseme ukweli, jeshi la polisi linafanya kazi kama genge la majambazi. Kuna wakati ni aheri ya majambazi maana wao wanakuvamia, wanakunyang'anya mali, wanakuacha. Lakini hawa, wanakunyang'anya mali, halafu wanakutesa, na wakati fulani kukua au kukupoteza.
 
Tatizo ni moja :
Watu wema wameamua kuwa chini ya waovu.

Bado bara la Afrika halijakombolewa.
Waafrika wanajazana Makanisani na Misikitini kutetea nafsi zao huku wakishiriki au wakitumika au wakinyamazia nafsi za Waafrika wenzao zikiwa zinaangamizwa na binadamu wenzao waliolewa madaraka na Mali.

Yaani Kikundi cha watu wachache waovu kimewakalia watu wema kwa nguvu ya pesa na Madaraka.

Kwa sasa CCM kwa kulitumia Jeshi la Polisi haina habari tena na kitu kinachoitwa siasa safi ya ushawishi na kuwaheshimu wapiga kura kwa kuwa wapende wasipende watashinda Kwa nguvu ya Polisi.

Hata hivyo Mleta mada kuna tatizo kwa wananchi bado hawajawaelewa wale wanaolalamika kuwa wanatekwa au kuteswa au ndugu zao kupotea.

Magereza yamejaa maskini huku wahalifu dhidi ya binadam na mali za umma wakiwa wanaheshimika na kukalia ofisi za umma kwa mitutu ya Bunduki.

Ni vyema sasa watu wema wanaojua wazi kuwa hawana hatia lakini wanashitakiwa kwa uongo wakaungana kwa pamoja na kutafuta watu waaminifu sana ,wakachanga fedha kwa ajili ya kugharamikia kesi dhidi ya watawala wanaotumia vibaya madaraka yao kuumiza na kupoteza watu.

Hata mitaani unakuta kibaka mmoja anawanyima watu zaidi ya 100 usingizi na kupora watu bila aibu . Yani kibaka mmoja anatoa vitisho na watu wote wanajifungia kwenye mageti kila mmoja na mlango wake. Badala ya watu 100 wema kuungana na kumdhibiti kibaka mmoja wao ndio wanadhibituwa na kibaka kwa hofu.

Afrika tumependa hivyo ndio maana watu wastarabu wanasema achana na siasa ni mchezo mchafu. Matokeo yake waovu wenye michezo michafu wanawahonga wenye mamlaka ya kidola ili waingie kwanye siasa na wao wanakula Mali za umma kama wanavyotaka . Wanakula bata tu.

Mwaka Jana watumishi wa umma zaidi ya 43000 wakiwemo Polisi walichukua fomu za kugombea Ubunge kupitia CCM. Ni Jeshi la wananchi pekee ndio ambao hawakuchanganya siasa na Jeshi kama Katiba inavyosema. Wengine wote walikimbilia CCM na kugombea kinyume cha katiba.

Wavunja sheria ndio wanaotangulia na kuwakamata watu wema.

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
Mungu akulinde katika kutetea haki za watanzanua wenzako. Tunaunga mkono hatua hizi
Kuna watu watakuwa wanabeza au kudharau kuwa hawezi kuwashitaki mapolisi mahakamani.

Lkn wanasahau kuwa hata mchicha ulianza kama mbuyu.

Waulize wananchi wa sudan walianzaje kutafuta mageuzi pale Khartoum?

Tumpe moyo mleta uzi anaweza akaingizwa kwenye maandiko ya msingi kwenye vitabu hapa Tanzania.
 
Back
Top Bottom