Nitafungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi

Nitafungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi

Tatizo ni moja :
Watu wema wameamua kuwa chini ya waovu.

Bado bara la Afrika halijakombolewa.
Waafrika wanajazana Makanisani na Misikitini kutetea nafsi zao huku wakishiriki au wakitumika au wakinyamazia nafsi za Waafrika wenzao zikiwa zinaangamizwa na binadamu wenzao waliolewa madaraka na Mali.

Yaani Kikundi cha watu wachache waovu kimewakalia watu wema kwa nguvu ya pesa na Madaraka.

Kwa sasa CCM kwa kulitumia Jeshi la Polisi haina habari tena na kitu kinachoitwa siasa safi ya ushawishi na kuwaheshimu wapiga kura kwa kuwa wapende wasipende watashinda Kwa nguvu ya Polisi.

Hata hivyo Mleta mada kuna tatizo kwa wananchi bado hawajawaelewa wale wanaolalamika kuwa wanatekwa au kuteswa au ndugu zao kupotea.

Magereza yamejaa maskini huku wahalifu dhidi ya binadam na mali za umma wakiwa wanaheshimika na kukalia ofisi za umma kwa mitutu ya Bunduki.

Ni vyema sasa watu wema wanaojua wazi kuwa hawana hatia lakini wanashitakiwa kwa uongo wakaungana kwa pamoja na kutafuta watu waaminifu sana ,wakachanga fedha kwa ajili ya kugharamikia kesi dhidi ya watawala wanaotumia vibaya madaraka yao kuumiza na kupoteza watu.

Hata mitaani unakuta kibaka mmoja anawanyima watu zaidi ya 100 usingizi na kupora watu bila aibu . Yani kibaka mmoja anatoa vitisho na watu wote wanajifungia kwenye mageti kila mmoja na mlango wake. Badala ya watu 100 wema kuungana na kumdhibiti kibaka mmoja wao ndio wanadhibituwa na kibaka kwa hofu.

Afrika tumependa hivyo ndio maana watu wastarabu wanasema achana na siasa ni mchezo mchafu. Matokeo yake waovu wenye michezo michafu wanawahonga wenye mamlaka ya kidola ili waingie kwanye siasa na wao wanakula Mali za umma kama wanavyotaka . Wanakula bata tu.

Mwaka Jana watumishi wa umma zaidi ya 43000 wakiwemo Polisi walichukua fomu za kugombea Ubunge kupitia CCM. Ni Jeshi la wananchi pekee ndio ambao hawakuchanganya siasa na Jeshi kama Katiba inavyosema. Wengine wote walikimbilia CCM na kugombea kinyume cha katiba.

Wavunja sheria ndio wanaotangulia na kuwakamata watu wema.

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
Dhuruma kamwe haijawahi kuishinda haki.

Ipo siku haki itashinda tu
 
Kukamatwa kuna taratibu zake. Ka taratibu hizo hazikufuatwa, ni utekeji. Polisi wa hapa kwetu wanapenda zaidi kuteka kuliko kukamata.

Utasemaje mtu amekamatwa wakati kanyakuliwa bila ya kuambiwa huyo anayemnyakua ni nani, ana tuhuma gani, anapelekwa wapi. Anasafirishwa usiku kucha, anafikishwa kituo cha polisi anabadilishwa jina, anahamishwa hamishwa mahabusu kila mara?

Tusitetee uovu, tuseme ukweli, jeshi la polisi linafanya kazi kama genge la majambazi. Kuna wakati ni aheri ya majambazi maana wao wanakuvamia, wanakunyang'anya mali, wanakuacha. Lakini hawa, wanakunyang'anya mali, halafu wanakutesa, na wakati fulani kukua au kukupoteza.
"ukitekwa" huwezi kutambulika ulipo na usalama wako unakuwa mashakani.

"ukikamatwa" lazima utafahamika ulipo na usalama wako huzingatiwa.

Jeshi la Polisi huwa haliteki watu bali linakamata mtuhumiwa wa uhalifu au wahalifu na pia unaweza kukamatwa papo hapo bila kufuata taratibu endapo kuna hali ya udharura au kwa kufuata taratibu kulingana na mazingira.

Jeshi letu la Polisi linafanya kazi zake kwa weledi wa hali ya juu na kwa kuzingatia sheria na taratibu.
kuna mabadiliko makubwa sana ktk utendaji kazi wa Jeshi letu.
Pongezi za dhati kwa IGP Sirro.
 
Keyboard warrior's
Kwani wewe upo wapi? Acha kuishi kwa Akili za Le mutuz tumia Akili zako kujua kuwa haki husakwa kwa njia zote bila kujali changamoto na wapi ulipo
 
"ukitekwa" huwezi kutambulika ulipo na usalama wako unakuwa mashakani.

"ukikamatwa" lazima utafahamika ulipo na usalama wako huzingatiwa.

Jeshi la Polisi huwa haliteki watu bali linakamata mtuhumiwa wa uhalifu au wahalifu na pia unaweza kukamatwa papo hapo bila kufuata taratibu endapo kuna hali ya udharura au kwa kufuata taratibu kulingana na mazingira.

Jeshi letu la Polisi linafanya kazi zake kwa weledi wa hali ya juu na kwa kuzingatia sheria na taratibu.
kuna mabadiliko makubwa sana ktk utendaji kazi wa Jeshi letu.
Pongezi za dhati kwa IGP Sirro.
Jeshi letu wewe na nani? Weledi upi? Kufukuza watu mahakamani ni weledi? Pongezi kwa IGP kwa lipi? Kuwabambikia kesi wapinzani ni kufanya kazi kwa weledi? Kingai mahita kuwatesa watu kuwafunga pingu mikono miguu saa 24 ni kufanya kazi kwa weledi?
 
Kuna watu watakuwa wanabeza au kudharau kuwa hawezi kuwashitaki mapolisi mahakamani.

Lkn wanasahau kuwa hata mchicha ulianza kama mbuyu.

Waulize wananchi wa sudan walianzaje kutafuta mageuzi pale Khartoum?

Tumpe moyo mleta uzi anaweza akaingizwa kwenye maandiko ya msingi kwenye vitabu hapa Tanzania.
Polisiccm hushitakiwa sana ingawa wengi hawajui kuwa hakuna aliye juu ya Sheria na hapo ndipo Polisiccm hutumia huo udhaifu wa kutojua haki na Sheria kuwatesa watu kuwapiga kuwalipa wakubali ugaidi ambao haupo , kuhoji watu kwa kuwapiga kutojua maana ya PGO nk
 
Hata usiposhinda Itasaidia kufanya watu waanze kuamka na kujua polisi wanafanya utekaji na kupoteza watu, go for it!
 
Natarajia kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya jeshi la polisi, naitaka mahakama kuu itoe tafasiri na/ muongozo wa je Jeshi la polisi linaruhusiwa kuteka raia au kukamata raia? Na Je kukamata ni sawa sawa na kuteka? Na je utaratibu wa kuteka raia unatakiwa uweje? Yaani kabla raia hajatekwa ni hatua zipi za kufuata kabla ya tukio hilo? Na je ni haki zipi za mtu anayetekwa na polisi?

Utaratibu wa kukamata Raia unajulikana ila utaratibu wa kuteka raia haujulikani, kwa hiyo nitaiomba mahakama kuu itoe utaratibu mzima, na kama ni halali au haramu kwa polisi kuteka raia itamke waziwazi, na nitaiomba mahakama kama kuteka ni kitendo haramu basi itoe adhabu kali kwa polisi yeyote atakayejihusisha na utekaji raia.

Naiomba mahakama kuu isiogope kupokea na kusikiliza shauri hili, iige wenzao wa kenya wanavyotoa maamuzi bila kuangalia sura ya mtu.

Nawasilisha.
Kabla ya kuhangaika sana ebu tutolee ufafanuzi kati ya kutekwa na kukamata kwa mujibu wa uelewa wako wewe!

Siku hizi CHADEMA mmekuja na mbinu ya kutangazia umma mnatekwa wakati ukweli ni kwamba mnatenda jinai, halafu mkikamatwa mnakinbilia kutangaza mitandaoni uzushi wa kutekwa.

Mbona hamuendi vituo vya polisi kutoa taarifa ya kutekwa kwenu?

Lini mtaacha hizi siasa UCHWARA?
 
Wafungulie kesi ya moja kwa moja watu wawili mahita na kingai kwa kutesa kuwapiga kuwafunga pingu mikono miguu saa 24 kila siku walinzi wa mbowe, hii itakuwa kesi ya wachache lakini itasaidia kuwafungua macho wapenda haki wote Duniani
 
Hata usiposhinda Itasaidia kufanya watu waanze kuamka na kujua polisi wanafanya utekaji na kupoteza watu, go for it!
Sheria inasema Polisiccm anapokwenda kumkamata mtu lazima awe na RB na pia amweleze mtuhumiwa sababu ya kumkamata na ndugu wa mtuhumiwa wanapewa taarifa alipo ndugu yao, na pindi akifikishwa kituoni ndani ya saa 48 anatakiwa awe amefikishwa mahakamani, pia ipo Sheria inayomruhusu mtuhumiwa kudai fidia endapo amekamatwa kimakosa kwa uonevu ama kwa Bahati mbaya, Sheria hizo zipo lakini kwa kuwa wananchi hawajui haki zao wamekosa wajibu wa kuzitumia na Polisiccm kuendelea kuwakamata kuwaweka vituoni hata week mwezi pasipo kufikishwa mahakamani
 
Kwa kuwa kajitoa mhanga ni mara 100 aombe mawakili wa kimataifa ili waweze kuweka hiyo kesi kidunia iwe kama alama ya kuonyesha mapungufu ya Polisiccm kwenda idara ya ukamataji na mahojiano
Hao mawakili wa kimataifa si ndio kina Amsterdam?

Mbona hatujaona matunda ya kazi yao zaidi ya kupiga hela za Tundu?

Muwe mnajitahidi kusoma mambo ya Dunia ili mfunguke uelewa.

Duniani kuna mambo mengi ya msingi ambayo yanaisumbua Dunia na siku za usoni kuliko hizi sarakasi zenu za kibongo bongo.

Vitu kama Climate change,Covid19,Taliban na hatari ya kuigeuza Afghanistan kuwa chaka la ugaidi au kashfa za kifisadi kama zilizoibuliwa juzi na na Pandora Documents!

Nyinyi CHADEMA endeleeni kuchezea keyboard tu.

Hakuna kipindi kigumu mtapitia kama hiki,poleni sana.

Lowassa aliwaambia, Sumaye pia aliwaambia,na hata Nyalandu pia wote hawa waliwausia kwamba kuna siasa za kistaarabu na kiharakati bila nidhamu.
Nyinyi mkaishia kuwatusi woote mkiongozwa na Lema na Halima mdee.
Leo hii Lema haongei na Mdee na Lema anatukana kutokea Canada

Lissu anatukana kutokea Ubelgiji
Leo ndio mnaelewa maneno ya wale wazee yalikuwa mazito.

Laana ya Doctor Wilbroad Slaa itawaumiza sana!
 
Kabla ya kuhangaika sana ebu tutolee ufafanuzi kati ya kutekwa na kukamata kwa mujibu wa uelewa wako wewe!

Siku hizi CHADEMA mmekuja na mbinu ya kutangazia umma mnatekwa wakati ukweli ni kwamba mnatenda jinai, halafu mkikamatwa mnakinbilia kutangaza mitandaoni uzushi wa kutekwa.

Mbona hamuendi vituo vya polisi kutoa taarifa ya kutekwa kwenu?

Lini mtaacha hizi siasa UCHWARA?
Siasa uchwara unazo wewe Yaani umejitoa fahamu zote hata hujui umeandika nini? Chadema wamefanya jinai gani? Kuwabambikia kesi ndiyo jinai zako? Tueleze alipo moses lijenje? Tueleze alipo mwenyekiti wa baraza la wazee chadema?
 
Natarajia kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya jeshi la polisi, naitaka mahakama kuu itoe tafasiri na/ muongozo wa je Jeshi la polisi linaruhusiwa kuteka raia au kukamata raia? Na Je kukamata ni sawa sawa na kuteka? Na je utaratibu wa kuteka raia unatakiwa uweje? Yaani kabla raia hajatekwa ni hatua zipi za kufuata kabla ya tukio hilo? Na je ni haki zipi za mtu anayetekwa na polisi?

Utaratibu wa kukamata Raia unajulikana ila utaratibu wa kuteka raia haujulikani, kwa hiyo nitaiomba mahakama kuu itoe utaratibu mzima, na kama ni halali au haramu kwa polisi kuteka raia itamke waziwazi, na nitaiomba mahakama kama kuteka ni kitendo haramu basi itoe adhabu kali kwa polisi yeyote atakayejihusisha na utekaji raia.

Naiomba mahakama kuu isiogope kupokea na kusikiliza shauri hili, iige wenzao wa kenya wanavyotoa maamuzi bila kuangalia sura ya mtu.

Nawasilisha.

Kwenye kesi itabidi uthibitishe nani katekwa?Alitekwaje tekwaje?Nani aliyetekwa!Mwisho Mahakama inaweza kukubaliana na wewe kwamba utekaji haurusiwi kisheria na hautamkwi na sheria yoyote na ni kosa.Ikaishia hapo na kukuacha kwenye “vacuum” kubwa.Na matukio unayoita ya Utekaji (badala ya Ukamataji) yakaendelea.

Hoja hapa ni lazima uwe “specific” na “matukio” na ni taratibu hizi hasa unazolalamikia kukiukwa ili mahakama “ione”kama kulikuwa na “Utekaji” badala ya “Ukamataji”.
 
Natarajia kufungua kesi mahakama kuu dhidi ya jeshi la polisi, naitaka mahakama kuu itoe tafasiri na/ muongozo wa je Jeshi la polisi linaruhusiwa kuteka raia au kukamata raia? Na Je kukamata ni sawa sawa na kuteka? Na je utaratibu wa kuteka raia unatakiwa uweje? Yaani kabla raia hajatekwa ni hatua zipi za kufuata kabla ya tukio hilo? Na je ni haki zipi za mtu anayetekwa na polisi?

Utaratibu wa kukamata Raia unajulikana ila utaratibu wa kuteka raia haujulikani, kwa hiyo nitaiomba mahakama kuu itoe utaratibu mzima, na kama ni halali au haramu kwa polisi kuteka raia itamke waziwazi, na nitaiomba mahakama kama kuteka ni kitendo haramu basi itoe adhabu kali kwa polisi yeyote atakayejihusisha na utekaji raia.

Naiomba mahakama kuu isiogope kupokea na kusikiliza shauri hili, iige wenzao wa kenya wanavyotoa maamuzi bila kuangalia sura ya mtu.

Nawasilisha.
Kwa majina bandia hapa unafoka , watu dhaifu hujitutumua kwenye keyboards za simu ,watu wakikamatwanasema wametekwa

USSR
 
Hao mawakili wa kimataifa si ndio kina Amsterdam?

Mbona hatujaona matunda ya kazi yao zaidi ya kupiga hela za Tundu?

Muwe mnajitahidi kusoma mambo ya Dunia ili mfunguke uelewa.

Duniani kuna mambo mengi ya msingi ambayo yanaisumbua Dunia na siku za usoni kuliko hizi sarakasi zenu za kibongo bongo.

Vitu kama Climate change,Covid19,Taliban na hatari ya kuigeuza Afghanistan kuwa chaka la ugaidi au kashfa za kifisadi kama zilizoibuliwa juzi na na Pandora Documents!

Nyinyi CHADEMA endeleeni kuchezea keyboard tu.

Hakuna kipindi kigumu mtapitia kama hiki,poleni sana.

Lowassa aliwaambia, Sumaye pia aliwaambia,na hata Nyalandu pia wote hawa waliwausia kwamba kuna siasa za kistaarabu na kiharakati bila nidhamu.
Nyinyi mkaishia kuwatusi woote mkiongozwa na Lema na Halima mdee.
Leo hii Lema haongei na Mdee na Lema anatukana kutokea Canada

Lissu anatukana kutokea Ubelgiji
Leo ndio mnaelewa maneno ya wale wazee yalikuwa mazito.

Laana ya Doctor Wilbroad Slaa itawaumiza sana!
Dr slaa hana laana aliacha chadema kwani alinunuliwa na CCM kwa dola milion 2 na kupewa nyumba Canada hana mfano wa kuigwa ni mzee wa hovyo tu, Lowasa na Sumaye walitishwa na marehemu magufuli wakiogopa wakarudi CCM, wewe ndiyo uendelee kuchezea keyboard huna unachokijua zaidi ya kujiona unajua vingi kumbe hujui kitu, wewe kama CCM na Polisiccm wanakusikiliza basi wakataze wasiwe wanawabambikia kesi wapinzani na CCM wafanye siasa safi tume huru ya uchaguzi uone nguvu ya wapiga kura bila uchakachuaji wenu
 
Kwenye kesi itabidi uthibitishe nani katekwa?Alitekwaje tekwaje?Nani aliyetekwa!Mwisho Mahakama inaweza kukubaliana na wewe kwamba utekaji haurusiwi kisheria na hautamkwi na sheria yoyote na ni kosa.Ikaishia hapo na kukuacha kwenye “vacuum” kubwa.Na matukio unayoita ya Utekaji (badala ya Ukamataji) yakaendelea.

Hoja hapa ni lazima uwe “specific” na “matukio” na ni taratibu hizi hasa unazolalamikia kukiukwa ili mahakama “ione”kama kulikuwa na “Utekaji” badala ya “Ukamataji”.
Walinzi wa mbowe walikaa vituoni zaidi ya masaa 48 pasipo kufishwa mahakamani kisheria hata akianza na hapo tu atakuwa kapata pa kuanzia
 
Kwa majina bandia hapa unafoka , watu dhaifu hujitutumua kwenye keyboards za simu ,watu wakikamatwanasema wametekwa

USSR
Kwani wewe hilo ni jina lako? wewe upo mbele ya keyboard? si na wewe upo nyuma ya keyboard kama unaona wanajitutumua hata wewe unajitutumua kusaka uteuzi kwa kujiandikia andikia chochote ili uonekane unawatetea CCM mitandaoni upate cheo kwa njia haramu za kishetani
 
Hilo swali lako mkuu mi naona ni maisha yamekupiga tu huku mtaani polisi wana kamata ila waasi, magaidi au majambazi hao ndio watekaji ili wapate pesa au kitu fulani au kulipiza kisasi lakini pia hata vitani wanaoshindwa wanakuwa mateka lakini kwa upande mwingine mkamataji kwanza anajitambulisha na anakwambia sababu ya kukukamata pia kama kosa lako linadhamana unadhaminiwa.
 
Back
Top Bottom