Nitaendelea kutokuwa na dini

Nitaendelea kutokuwa na dini

Sitaki kufikia hatua nikazungumza na nikaonekana nakashifu imani za watu wengine kwa sababu mm naheshimu sana imani zote. Lakini ww inakuingia akilini eti yameandika yaliyomo na yatakayokuja ktk Qur'an! Si dhihaka ila unawwza kuniambia kama ktk Qur'an iko aya inayosema watu watawasiluana kupitia internent? Je kuna hadithi mtume aepanda tren ya umeme ama ndege! Haya mambo huwezi kuyakuta kabisa ila unaweza kuona ngamia, jahazi punda nk kwa sababu zama hizi ndo vitu vilivyokuwepo. Sasa Qur'an nzima tunaambia mara ngamia mara punda wakati kizazi chetu cha treni za umeme huyo ngamia tunamuona zoo tu na wewe bado unaamini kuwa kwa kitabu hiki faded uongoze maisha yako ya sasa. Tafakari
Katika quran kuna vipando vingine bado mpaka leo havija gundulika hapa ulimwenguni mpaka leo hii unalijua hilo? Rejea sura ya 17 uone Muhamad 'Rehema na amani zimwendee huko aliko' alivyokwenda Jerusalemu usiku kutokea Maka kwa muda mfupi kabisa na akarudi usiku huohuo.
 
Na ndiyo maana katika familia mkizaliwa na baba mmoja na mama mmoja wote mnakuwa kabila moja, Sasa sisi hizi dini zimekujaje kujaje na kwa faida ya nani,tuna heshimu dini za watu woote. Ila si lazima wote tuwe na dini
 
Katika quran kuna vipando vingine bado mpaka leo havija gundulika hapa ulimwenguni mpaka leo hii unalijua hilo? Rejea sura ya 17 uone Muhamad 'Rehema na amani zimwendee huko aliko' alivyokwenda Jerusalemu usiku kutokea Maka kwa muda mfupi kabisa na akarudi usiku huohuo.
Sura ya 17 aya gani? Nambie na sura inaitwaje niko na Qur'an hapa.
 
siwez kamwe kupuuza mchango wa dini kwenye kuunganisha watu kwa ajili ya civilization, na maendeleo.Kuna mahali kama sio hof ya dni pasingekalika, zahanat zsingekuepo etc. Validity na reliability ya hivi vitab sina uwezo wa kuvidefend ila kwa kutumia sabab za hapo juu acha dini ziwepo
 
Sura ya 17 aya gani? Nambie na sura inaitwaje niko na Qur'an hapa.
Ukiambiwa sura ya 17 maana yake uisome yote, pia ukisema inaitwajwe ni ubabaishaji kwani kama Qur an unayo ungeshaiangalia na ukajua yaitwajwe, soma suratul Israa aya ya kwanza inakufungua maarifa. 17:1
 
Dini watu zimewangia mpaka wanauwa wenzako ukiwauliza ohhh tunapigania dini.haya sasa huyo mwenyewe aliyezileta si angetoa msaada kwa upande unaoonewa, hapa nahisi kuna tatizo hapa si bure
 
Mleta uzi inaonekana hujui maana ya dini ndiyo maana unasema utaendelea kutokuwa na dini...kutokuwa muislam au mkristo haimaanishi huna dini! Mfumo mzima wa maisha, jinsi unavyoishi na kishirikiana na wenzako, kupenda wenzako na kuwasaidia, busara, kuishi kwa kufuata taratibu zilizowekwa na wanajamii, utashi ulionao juu ya kuwatatulia wenzio matatizo, kutekeleza wajibu wako, n.k hiyo ndio dini tena iliyo safi...tafuta maana sahihi ya dini kutoka vyanzo mbalimbali halafu uone je ni kweli huna dini,? Kiukweli hakuna binadamu asiye na dini, kila mmoja ana imani yake!
 
Kuamini au kutoamini uwepo wa Mungu ni uamuzi wako binafsi.Pia kumbuka matokeo yake ni yako binafsi.Lakini hofu yangu inakuja kwamba wewe unaamini hakuna Mungu kutokana na uelewa wako wewe mwenyewe bila kupata taarifa sahihi kutoka vyanzo sahihi.Sasa wewe hujui na inatoa hitimisho hakuna Mungu kwa huko kutokujua kwako,huoni kwambo unakuwa mwongo?Suala sio kuwepo au kutokuwepo kwa Mungu bali ni kukosa taarifa za kuhusu Mungu
Mungu yupo kwamba unamkubali au humkubali.Naomba nijibu tu nn chanzo cha ulimwengu na vilivyomo?Halafu kuanzia hapo utaanza kujiuliza maswali ambayo yatakufanya uyafute majibu ya maswali yako badala ya kujijibu kutokujua kwako.Swala la watu kujenga nyumba za ibada nzuri na kuwa na makazi duni hilo haliusiani na uwepo wa Mungu au kutokuwepo bali mahusiano ya watu na Mungu kwa hiyo halina mantiki kwa hali duni za watu.Kingine Mungu ni SUPREME BEING anajua yote kwa hiyo hayo mabadiliko unayoyaona ukiyachunguza wala hayana chochote cha kufanya maandiko matakatifu kwani vyote vitabadilika ila Mungu anabaki kuwa yule yule.
 
Naona umejiridhisha kuwa dini ya kipagani ndio muafaka kwako.
 
Back
Top Bottom