Wana baadhi ya mapungufu yao sio wakamilifu sehemu zote lakini wamejitahidi kwenye hivi vitu
Hawana mtu wa ndani wala wa nje, ukienda kwao huna haja ya kutambulishwa umejiunga, kwamba fulani hebu simama watu wote kanisani wakuone umejiunga.
Hawajioni bora kuzidi wengine, makanisa mengine hutumia muda mwingi kujiona kama wao ndio wapo kwenye kanisa wataloenda mbinguni au wao ndio bora zaidi, ni kawaida kukuta dini nyingine wakibishana hadi mishipa kuwatoka shingoni kwamba wao ndio kanisa bora lakini mkatoliki huwa muda hana
Kanisa la Roma wamewekeza sana kwenye Elimu na ndio maana jamii zilizoendelea zina historia kubwa ya mchango wa kanisa la Roma kuwapa elimu kwenye shule za wamishenari, Elimu hio imejaza wahasibu, Madaktari, Wahandisi, Wanasheria, n.k. kwenye taasisi nyingi sana za serikali na makampuni. shule kama Saint Francis ni kawaida kuongoza kila mwaka na wanafunzi wachache wanabahatika kupata ufadhili kusoma nje ya nchi
hakuna ubaguzi wa ndoa, kuna baadhi ya makanisa wanataka kuoana wao kwa wao, hili limesababisha baadhi ya mabinti kuzalia kwao kwa kukataa kuolewa nje na baadhi ya waumini wa kiume kuzalisha nje ya imani bila kuoa.
Hawaingilii maisha ya ndoa, Hili limekuwa tatizo kubwa kwenye makanisa mengi sikuhizi, wachungaji wamekuwa viongozi wa wake za watu badala ya waume zao, kugeuza majukwaa ya mahubiri yawe majukwaa ya ushauri wa ndoa za watu bila kujali sumu wanayojaza kwa waumini inayochangia ndoa nyingi kuwa na migogoro na hata kuvunjika
Hawana mtu wa ndani wala wa nje, ukienda kwao huna haja ya kutambulishwa umejiunga, kwamba fulani hebu simama watu wote kanisani wakuone umejiunga.
Hawajioni bora kuzidi wengine, makanisa mengine hutumia muda mwingi kujiona kama wao ndio wapo kwenye kanisa wataloenda mbinguni au wao ndio bora zaidi, ni kawaida kukuta dini nyingine wakibishana hadi mishipa kuwatoka shingoni kwamba wao ndio kanisa bora lakini mkatoliki huwa muda hana
Kanisa la Roma wamewekeza sana kwenye Elimu na ndio maana jamii zilizoendelea zina historia kubwa ya mchango wa kanisa la Roma kuwapa elimu kwenye shule za wamishenari, Elimu hio imejaza wahasibu, Madaktari, Wahandisi, Wanasheria, n.k. kwenye taasisi nyingi sana za serikali na makampuni. shule kama Saint Francis ni kawaida kuongoza kila mwaka na wanafunzi wachache wanabahatika kupata ufadhili kusoma nje ya nchi
hakuna ubaguzi wa ndoa, kuna baadhi ya makanisa wanataka kuoana wao kwa wao, hili limesababisha baadhi ya mabinti kuzalia kwao kwa kukataa kuolewa nje na baadhi ya waumini wa kiume kuzalisha nje ya imani bila kuoa.
Hawaingilii maisha ya ndoa, Hili limekuwa tatizo kubwa kwenye makanisa mengi sikuhizi, wachungaji wamekuwa viongozi wa wake za watu badala ya waume zao, kugeuza majukwaa ya mahubiri yawe majukwaa ya ushauri wa ndoa za watu bila kujali sumu wanayojaza kwa waumini inayochangia ndoa nyingi kuwa na migogoro na hata kuvunjika