Nitaendelea kutokuwa na dini

Nitaendelea kutokuwa na dini

Matatizo yako soma Summa Theologica. Kwa sababu posting yako ni kama ukurasa unetolewa katika Summa Theologica. Mapadre wanajiuliza,sisi mapadre tunaposema Mungu yupo,tuna uhakika gani?
Mmmh hio "summa theological" inapatikana wapi? Ni kitabu au mada?
Mapadre wanajiuliza uhakika wa uwepo wa Mungu?
 
Huwezi fanya mabadiliko kwenye Biblia. I think huna shule kabisa kuhusu theology! Hebu kasome CANONICITY. Hatuhitaji kuongeza au kupunguza kitu chochote ktk Biblia. Kinachokusumbua wewe ni shule ndogo ya haya mambo
 
Huwezi fanya mabadiliko kwenye Biblia. I think huna shule kabisa kuhusu theology! Hebu kasome CANONICITY. Hatuhitaji kuongeza au kupunguza kitu chochote ktk Biblia. Kinachokusumbua wewe ni shule ndogo ya haya mambo
Sasa amba si ndo ninachokiongelea hapa. Nafahamu kwamba huwezi kuongeza kitu ktk biblia lakini nafahamu pia maisha yanabadilika na yanapokea mabadiliko makubwa. Sasa kama maisha yanabadilika kwanini biblia isipokee mabadiliko? Amini maneno yangu itafikia kizazi ambacho kila neno ktk biblia litakua ni msamiati mgumu mno kwani mambo yote yaluyoandikwa hayatakuwepo kabisa katika kizazi chao. Kama hatia zisipichukuliwa za kufanyia mabadiliko vitabu hivi vitakatifu nyakati zitatucheka.
 
Kutokuwa na dini wakati unaamini Mungu yupo sio mtazamo sahihi hata kidogo. Nimezingatia hoja zako zote nimeona ni za kijamii badala ya uchambuzi wa kujua mfano kiini cha dini ya Kikristo nini. Uhusiano wa dini na Mungu ninini. Dini inanafasi gani kwa mwanadamu yeyote.
Niseme machache kwako na wengine kwa leo;
1. Mungu unayeamini kama yupo anamaagizo aliyotoa kwa walioamua kumtii
2. Ili ujifunze na kujua maagizo na maelekezo hayo lazima ufundishwe na uhakikishe unachofundishwa ndicho kilichoandikwa kwenye biblia.
3. Dini ya kweli kazi yake ni kukulea mwamini katika msingi huo ili mwamini ajue Mungu anataka nini na hataki nini.
4. Dini ya kweli inajenga ushirika kati ya mwamini na Mungu wa pekee wa kweli aliyeumba mbingu na Nchi.
5. Dini ya kweli inamuandaa mwamini na kumfanya aishi maisha ambayo baada ya kumaliza safari ya Dunia asiishie kwenye taabu ya milele mikononi mwa shetani bali aende mbinguni kwenye raha ya milele. Au huamini kwamba kuna maisha mengine ya milele baada ya haya ya Duniani?
6. Jifunze ujue historia ya uumbaji kwenye biblia, historia ya dini utagundua kuwa Ulaya nao waliletewa Ukristo na Wayahudi/Israel wala haukutoka kwao.
7. Neno la Mungu sio kama Siasa kwamba linachuja kutokana na maendeleo ya kijamii. Alichosema Mungu kilifaa juzi, jana kinafaa leo, kitafaa kesho na milele.
8. Kama ambavyo Ulaya walivyokuwa hawana Dini kabla ya kupokea Ukristo Israel ndivyo ilivyokuwa kwenye Imani za Kiafrika. Tuliamini miungu mingine uchawi nakadhalika. Kumbuka imani ya vita vya majimaji.
8.Mungu anakusaidia Duniani na milele. Mpokea Yesu uone uzuri na siri zilizomo kwenye Ufalme wa Mungu.
9. Mambo ya Mungu ni halisi sio dhana.
 
Sasa amba si ndo ninachokiongelea hapa. Nafahamu kwamba huwezi kuongeza kitu ktk biblia lakini nafahamu pia maisha yanabadilika na yanapokea mabadiliko makubwa. Sasa kama maisha yanabadilika kwanini biblia isipokee mabadiliko? Amini maneno yangu itafikia kizazi ambacho kila neno ktk biblia litakua ni msamiati mgumu mno kwani mambo yote yaluyoandikwa hayatakuwepo kabisa katika kizazi chao. Kama hatia zisipichukuliwa za kufanyia mabadiliko vitabu hivi vitakatifu nyakati zitatucheka.
Mkuu umesoma CANONICITY? Kama hujasoma tafuta kujua juu ya CANONICITY utapata majawabu yote. Lakini napenda ujue kuwa Biblia haijapitwa na wakati na haitapitwa na wakati. The Bible is the Oldest book currently existing in the world! Vitabu vya agano la kale vilikuwepo hata kabla ya Kristo na bado tunavisoma ni kila siku vinaonekana vipya. Sasa wewe wa juzijuzi ndo unasema eti Bibla itashindwa kwendana na wakati!
 
Mkuu umesoma CANONICITY? Kama hujasoma tafuta kujua juu ya CANONICITY utapata majawabu yote. Lakini napenda ujue kuwa Biblia haijapitwa na wakati na haitapitwa na wakati. The Bible is the Oldest book currently existing in the world! Vitabu vya agano la kale vilikuwepo hata kabla ya Kristo na bado tunavisoma ni kila siku vinaonekana vipya. Sasa wewe wa juzijuzi ndo unasema eti Bibla itashindwa kwendana na wakati!
Mkuu nimesoma idea ya canonicity tangu jana lakini sijaona point yyte ya kueleweka.
 
Sina hata cha ku comment maana umeongea fact tupu. Unajua watu ambao wameingia katika dini wanakuwa blind folded hata ufanye nini hawawezi kuuona ukweli na hivyo ndivyo mafunzo ya dini nyingi yanavyowatengeneza ili wasije wakastuka. Yaani utakapojidai kutaka kujua undani tu unaambia unakufuru na ndo inakuwa full stop yako. Hahaha dini bwana!
Ukristo na Uislamu ambao kila moja kuna matawi mengi ndani yake ndicho wengi hawataki kihojiwe.Siamini chochote kile kati ya hivyo,ila naamini kuwa ni utaratibu na taratibu tu hizo,Maana hata ukisoma vilivyoandikwa vinatokea na vinatendwa na watu na ni sehemu ya maisha ya binadamu kila siku.Na vilikuwa sehemu za watu kipindi hicho.Ukisoma hivyo vitabu ni vinazungumzia jinsi ya kuweka njia na kumfanya anaelewa kuishi maisha tu kama siku zote,sasa shida huja hapa tunalazimisha kubadilisha jinsi tulivyoumbwa na kulazimishwa uhalisia wa binadamu kupitia hivyo vitabu.Ndio chanzo cha haya machafuko yoote na kila mtu kuona anavyoona.Tulikaririshwa bila kuhoji toka enzi,na waliokuja walitumia nafasi za kibinadamu kutumaliza.
 
KUNA MTU KAULIZA HUMU HIYO IMANI YA KUAMINI MUNGU IMELETWA NA NANI PIA? Na mimi naongezea hivi ni Imani zipi ambazo waafrika tulikuwanazo kabla ya kuletewa dini na dini zilileta mafundisho gani?
 
KUNA MTU KAULIZA HUMU HIYO IMANI YA KUAMINI MUNGU IMELETWA NA NANI PIA? Na mimi naongezea hivi ni Imani zipi ambazo waafrika tulikuwanazo kabla ya kuletewa dini na dini zilileta mafundisho gani?
Mbona jamii nyingi za Africa zilikuwa na imani zao kabla ya kuja kwa wazungu.
Hebu pitia"how europe underdevelop africa" cha walter lodney
 
Mbona jamii nyingi za Africa zilikuwa na imani zao kabla ya kuja kwa wazungu.
Hebu pitia"how europe underdevelop africa" cha walter lodney
Sikatai kuwa zilikuwepo imani ila nataka uzitaje,na ueleze zilipokuja dini zikaja kufundisha nini?
 
Inayosema watu wakifa wasizikwe Na majeneza! Kumbe sababu ya ukame Na Jangwa kipindi cha Mtume! Kupelekea kutokuwepo kwa miti ambayo inngekatwa mbao!?
Mbona wakati wa kuzika maiti mbao pia zinawekwa
 
Upo sahihi.Dini sasa hivi ni biashara kubwa kuliko zote.Angalia maaskofu wa makanisa mengi makubwa ni mabilionea wa kutupwa!
Umeona Maaskofu Tu, Hujaiona Makka Inavyowatumbua Waislam Wenzio? Wanapiga Hela Kwenye Hija Si Mchezo
 
Summa Theologica ipo katika sacred-texts.com. Imeandikwa na St.Thomas Aquinas.
 
Umeona Maaskofu Tu, Hujaiona Makka Inavyowatumbua Waislam Wenzio? Wanapiga Hela Kwenye Hija Si Mchezo
Ndugu yangu tuyaongee ya kwetu,wasije jilipua hapa.Mwaka jana maelfu ya watu wamekufa kisa,mwana ukoo wa kifalme ambae ni waziri wa ulinzi aliamua kufunga barabara muhimu kwa dharura ili apite yeye na wapambe wake bila kujali ratiba ilionyesha mahujaji maelfu kwa maelfu wanatakiwa wapite hapo.Kwa unafiki wa watu hilo suala limepita kimyaaaaaaaa...
 
Ndugu yangu tuyaongee ya kwetu,wasije jilipua hapa.Mwaka jana maelfu ya watu wamekufa kisa,mwana ukoo wa kifalme ambae ni waziri wa ulinzi aliamua kufunga barabara muhimu kwa dharura ili apite yeye na wapambe wake bila kujali ratiba ilionyesha mahujaji maelfu kwa maelfu wanatakiwa wapite hapo.Kwa unafiki wa watu hilo suala limepita kimyaaaaaaaa...
me nashangaa suala kama hili lilipitaje pitaje kimyaaa.na hawa jamaa hata hawakucomplain.yaaan kule macca eashachukulia watu kufa ni jambo la kawaida hata kama kuna uzembe wa hali ya juu!
 
Habari wana jamvi.
Kwanza kabisa naomba niwiwe radhi kwa nitakachozungumza hapa kama nitawakwaza baadhi ya watu, ashankum si matusi.
Pili napenda niweke wazi kuwa ninaheshimu imani ya kila mtu na mimi natumaini kila mtu ataheshimu imani na msimamo wangu.

Ninapatwa wakati mgumu sana pale ninapotaka kuzungumza kuhusu dini na mungu kwani mambo haya yanatazamwa kwa mtazamo tofauti endapo mtu atathubutu kusema hakuna mungu ama hakuna dini.
Mimi naamini mungu yupo(kama sitapata shaka ya kutokuwepo)

Lakini ninaamini pasi na shaka kwamba ideology ya dini ni propaganda na si kitu sahihi kukifuata.
Labda niweke sababu chache ambazo zimenifanya nisiamini kwa dini yeyote (Islam and Christianity to bespecific)

1.Dini zimetoka wapi?
Dini kubwa zinazodominate Tanzanian zimeletwa na wageni. Islam imetoka Asia na Christianity imetoka Europe. Lakini unadhani kabla ya wazungu na waarabu kuja tulikua sisi waafrika hatuna imani? Je hizo imani zetu zimeenda wapi? Wazungu na waarabu walizipiga vita imani zetu na kuziita primitive na wao wakaleta imani zao na dini zao "civilization" Hivi unadhani kati ya imani tulizokua nazo sisi na hizo walizoleta waarabu na wazungu zipi ni "primitive"

Ninaamini kwamba dini zilikuja na wageni kwa mission zao (ukoloni na biashara) na baada ya mishen hizo kwisha wametuachia ujinga waafrika wa kukomaa na dini wakati wao wameshaacha huo upuuzi zamani. Tujaribu kuona misa za makanisa ya ulaya zinavyokosa waumini na tulinganishe mafuriko ya waumini wa makanisa na misikiti yetu afrika.

2. Dini zote hazitaki kupokea mabadiliko

Vitabu vikubwa vya dini ni Qur'an na biblia. Lakini maandishi yaliyo kwenye vitabu hivi na matakatifu na hatuwezi kubadilisha kwa namna yoyote.
Kama vitabu hivi viliandika zaidi ya miaka 1000 iliyopita basi vilikuwa valid kwa watu wa kipindi hiko na si kwa kizazi hiki ambacho kina mabadiliko makubwa katika kila nyanja ya maisha. Na sawa nabkutunza funguo yako ya gari la zamani na kulazimisha iendeshe kila gari jipya utakalonunua.

3. Dini ni mifumo mikubwa inayowanyonya ndugu zangu masikini walioamini.
Kama umefanikiwa kwenda katika vijiji vya hapa Tanzanian basi endapo utaona jenho zuri lolote lilioezekwa kwa bati na kujenga kwa tofali na kupakwa rangi vizuri ilihali majengo yote maeneo hayo ni tope na nyasi basi dhahiri jengo hilo litakuwa kanisa ama msikiti. Ni upuuzi kuona tuna makanisa manne na miskiti minane katika kijiji chetu ilihali hatuna hata zahanati. Pesa za ujenzi wa kanisa tulichanga lakni kanisa halina hata msaada mkubwa kilunganisha na dhahanati.
Sitaki kuzungumzia mashekh, maaskofu , mapadri na maimamu ambayo wanaishi maisha ya kitakatifu na anasa ilihali mimi muumini wananikwangua mpaka jasho langu la mwisho eti namtolea bwana.

Nina mengi ya kuzungumza na ninaahidi nitatoa sababu nyingine tele zinzofanya nisiwe na dini pundi nitakapopata wasaa.
Nawasilisha
Kwanza kabisa yakupasa uelewe maana ya dini,Dini ni mfumo wa maisha ya binadamu, si sahihi kusema huna dini kwani jinsi unavyoishi ndo dini yako
 
Kijana ukiwa hauna cha kuandika kaa kimya tu sio unaandika utumbo ambao hata mtu anayeumwa matatizo ya Akili hawezi kukuunga mkono JAHILI mkubwa wewe tena uliyekosa yakuzungumza hajui kuwa haifai kuzungumzia mambo ya dini bila ya Elimu eti Uislam ulitoka Asia kwa Ushaidi gani ? Hivi mbona unanuka ujinga wakupindukia tena nataka nikujuze yakuwa Mashaytwaan wamegawanyika sehemu mbili

1) Shaytwaan wakijini ambao huwa wanawaingia wanadamu kama tunavyoona has a Dada zetu kila siku wanahaha kwa matatizo ya majini mahaba na mengineyo

2) Shaytwaan wa kibinadamu ambaye kazi yake ni kupotosha watu ili wakachomwe moto siku ya malipo sasa wewe unaonekana ni SHAYTWAAN tena pepo mchafu anayetaka watu waache Iman zao sahihi kisha waangamie

Naomba watu wakuupuuze na UONGO wako ulio uwokota majalalani UONGO ambao vitabu vitakatifu unavipinga potea peke yko na fikra zako chafu!!!!
 
Back
Top Bottom