Peter Mwaihola
JF-Expert Member
- Jun 23, 2022
- 227
- 333
Wanaume nisikilize mimi, ukikutana na mwanamke mzuri muoe zaa nae watoto jenga familia pamoja naye.
Anaweza kuwa rafiki yako bora, msiri wako, mfanya biashara wako mshirika.
Na Unaweza kumuona kama mshirika wako wa karibu kwenye maombi pindi utakapomua kwani wanandoa huanza kufanana wakidumu pamoja.
Lakini usisahau nguvu iliyowaunganisha inaweza kuingia kutu kulingana na muda na kubadilika kwa moyo.
Mke wako sio ndugu yako wa damu na upendo wake unaweza kubadilika kuwa chuki ndani ya usiku mmoja.
Nisikilize mimi mpendwa kaka yangu, kwenye Wakati wa mahaba, kwenye kilele cha mafanikio yako, mkumbuke kaka yako aliesimama na wewe wakati haupo imara na umkumbuke dada yako aliekusafisha wakati ukiumwa sana.
Wakumbuke pia waliotumia muda wao kukuambia usitupe maji ya baridi kwenye mgongo wako, mikono yako na kukuandalia maji moto yaliyoilea ngozi yako.
Usiwafungie milango watoto wanapokuja mbele ya uzio wako wakiwa na miguu yenye vumbi na nguo zilizochanika wakitaka msaada wako.
Usizibe pua yako ikiwa wananuka harufu mbaya, usizibe masikio yako ili usisikie matumbo yao yakiunguruma kutokana na kukosa shibe.
Wakaribishe kwa mikono mikunjufu fungua milango yako waite wale juu ya meza yako na watendee kadri ungependa utendewe.
Yajayo ni kama upepo yanaweza kuwa hayatabiriki kabisa unaweza ukajikuta upo kama ayubu wa kwenye biblia ukiwa mtupu mwenyewe kwenye kisiwa cha matatizo.
Dada yako aliyekuokota ukiwa unaumwa hujiwezi Kama mtoto asiye na matumaini atakutafuta akusaidie tena.
Ndugu yako katakushika mkono katika mapito yako yote kwakuwa nguvu iliyowaunganisha kwenye damu itazongwa na upepo lakini kamwe haiwezi kutenganishwa.
Peter Mwaihola
Elvinah Obuya, The Standard Kenya.
Anaweza kuwa rafiki yako bora, msiri wako, mfanya biashara wako mshirika.
Na Unaweza kumuona kama mshirika wako wa karibu kwenye maombi pindi utakapomua kwani wanandoa huanza kufanana wakidumu pamoja.
Lakini usisahau nguvu iliyowaunganisha inaweza kuingia kutu kulingana na muda na kubadilika kwa moyo.
Mke wako sio ndugu yako wa damu na upendo wake unaweza kubadilika kuwa chuki ndani ya usiku mmoja.
Nisikilize mimi mpendwa kaka yangu, kwenye Wakati wa mahaba, kwenye kilele cha mafanikio yako, mkumbuke kaka yako aliesimama na wewe wakati haupo imara na umkumbuke dada yako aliekusafisha wakati ukiumwa sana.
Wakumbuke pia waliotumia muda wao kukuambia usitupe maji ya baridi kwenye mgongo wako, mikono yako na kukuandalia maji moto yaliyoilea ngozi yako.
Usiwafungie milango watoto wanapokuja mbele ya uzio wako wakiwa na miguu yenye vumbi na nguo zilizochanika wakitaka msaada wako.
Usizibe pua yako ikiwa wananuka harufu mbaya, usizibe masikio yako ili usisikie matumbo yao yakiunguruma kutokana na kukosa shibe.
Wakaribishe kwa mikono mikunjufu fungua milango yako waite wale juu ya meza yako na watendee kadri ungependa utendewe.
Yajayo ni kama upepo yanaweza kuwa hayatabiriki kabisa unaweza ukajikuta upo kama ayubu wa kwenye biblia ukiwa mtupu mwenyewe kwenye kisiwa cha matatizo.
Dada yako aliyekuokota ukiwa unaumwa hujiwezi Kama mtoto asiye na matumaini atakutafuta akusaidie tena.
Ndugu yako katakushika mkono katika mapito yako yote kwakuwa nguvu iliyowaunganisha kwenye damu itazongwa na upepo lakini kamwe haiwezi kutenganishwa.
Peter Mwaihola
Elvinah Obuya, The Standard Kenya.