Kwanza umenikumbusha jamaa mmoja hivi alikuwa anaitwa
Tyta siku hizi hata simuoni naona kubadili jina la hapa JF au kutoka kabisa au ndo kaja kwa jina lingine.
Maneno yako na yake ni hayo hayo sana sana hapo umesahau kuweka neno syndrome. Heheheheheheee nawapa pole sana.
Pili, wewe ni Daktari? Na clinic yako haina wagonjwa? Hivo unawasaka wagonjwa kinguvu ili ujidai unawatibia kumbe lengo lako uuze madawa? Daaah watu wana mbinu nyingi ila with Kasie. .... you need to go an extra mile.
Tatu na mwisho, kuna akili inaniambia kuna watu huwa wana aina zao flani hivi za utongozaji.... utaona kila mahali anamfatilia mtu anayetaka kumtongoza na kumghasi ghasi. .... halafu sasa aidha ni aibu au kumtongoza hajui au ndo kujifanya sitaki nataka kumbe anajenga mazoea ili apate kula nyama hahahahahhahahaahaa looh. Shida ya kigagula Kasie keshapitia aina zote hizo na akiona tuu huwa anawagundua mapemaaaa.
Basi huwa nawaonea huruma tuu wanavohaha. Itabidi nianzishe chuo au shule ya kufundisha jinsi ya kutongoza maana hizi ni aibu na ni aibu mwanaume kuwa nazo hahahahhahahaaa.
Ngoja niwape siri moja ya Kasie, Kasie bana udhaifu wake ni kutongozwa kilugha hata kama hicho kilugha sikijui yaaani nakuwa nyoronyoroo ndembendembee. Ila kwa sasa haiwezekani tena maana dadiiiiii alishanitongoza na kilugha chake mwenyewe akiniongelesha masikioni naanza kucheka cheka mara nasinzia huku natabasamu. .. mara nasikia nimebanwa na haja ndogo lakini haitoki basi ni burudani na raha isiyo kifani.
Kasie matata.