nisaidieni wana JF

Kalunguine

JF-Expert Member
Jul 27, 2010
2,543
134
waungwana! nilikuwa na mchumba,toka mwaka 2004,nikamtoa form four na sasa anamalizia degree ya education mwezi wa sita mwaka huu,mwaka jana mara tu baada ya kumlipia ada ya mwaka wa mwisho,kesho yake akani sms kuwa alikuwa hanipendi na alikuwa anataka tu asome! kijana nikaamua kuwa cool kwa kuwa nshapoteza pesa nyingi vibaya kwa huyu she,lakini katika masiku ya karibuni baada ya kupigika vibaya kwa mwanaume alokuwa nae eti sasa anataka kurudi kwangu na wakati hata pate yangu ya uchumba alishaitupa,na kamwe siwezi kumuamini tena,nifanyeje ndugu zangu
 
Duh,.
Umewahi sikia wimbo unaitwa "stell" sina uhakika lakini?

Jamaa kauza ng'ombe zake zote akampeleka mchumba wake kusomea udaktari Japan,siku anaenda kumpokea karudi na mtoto na pande la Mjapani!

Anyway,msaidie tu!
Usilipize kisasi,atleast kwa Mungu utakuwa umetenda jambo kubwa sana ila usimsaidie kama mke mtarajiwa maana hafai kuwa mke,...
Fanya tu kama ulikuwa una msaidia mtu usiye mjua!

Pole kaka
 
C alijifanya katema Big G kwa utamu wa karanga za kuonjeshwa? Wala ckushauri urudiane nae coz hana mapenz ya dhati alitaka aku2mie 2. Mpotezee
 
mpige chini kama mwizi huyoo...
kama unamsaidia msaidie kama rafiki...ila usiweke malengo naye hakufai huyo.
 
waungwana! nilikuwa na mchumba,toka mwaka 2004,nikamtoa form four na sasa anamalizia degree ya education mwezi wa sita mwaka huu,mwaka jana mara tu baada ya kumlipia ada ya mwaka wa mwisho,kesho yake akani sms kuwa alikuwa hanipendi na alikuwa anataka tu asome! kijana nikaamua kuwa cool kwa kuwa nshapoteza pesa nyingi vibaya kwa huyu she,lakini katika masiku ya karibuni baada ya kupigika vibaya kwa mwanaume alokuwa nae eti sasa anataka kurudi kwangu na wakati hata pate yangu ya uchumba alishaitupa,na kamwe siwezi kumuamini tena,nifanyeje ndugu zangu

...follow your heart, msamehe lakini usirudiane nae.
 
...follow your heart, msamehe lakini usirudiane nae.

Ushauri mzuri Mbu

Juzi alikuwa na wewe kwa sababu alijua ungemtimizia mahitaji yake

Kaenda kapigika na mahitaji yameisha anarudi tena...ukishamtimizia keshokutwa anatimka tena....Kwa nini ujuimize na kujipa Pressure ya moyo...

mwache atimke baba na muite tu vizuri kirafiki na umshauri kuwa maisha hayaendeshwi namna hiyo
 
mkuu
pole sana. kweli dunia ina mambo??

Nakushauri umsamehe, umepoteza vingi juu yake, na zaidi anakujali sana tu. Inawezekana alipata mtu wa kumdanganya, ndio maana akafanya jambo la kijinga.

Mpe nafasi nyingine. hakuna binadamu aliye sawa (perfect). wengine wanayafanya haya wakiwa ndani ya ndoa.. Lakini give her a chance..
Ukimsamehe toka moyoni, Mungu ni mwema, atarekebisha uhusiano wenu..Kwenye mahusiano kuna mambo mengi sana, ukitaka kuchukua hatua kwa kila tukio, utakufa mapema.

Wanadamu tuko hoi siku zote, pamoja na Mungu kutuma hata Mwanaye, lakini mambo bado sio mazuri kote misikitini na makanisani. MSAMEHE.

Siafiki wala kuunga mkono ujinga wake huyo dada, isipokuwa wanadamu tunateleza sana, kama sio leo basi ni kesho. She is yours, unamjua vizuri sana na yeye vivyo.. Nakuhakikishia kuwa atakuwa na heshima kuliko wakati mwingine wowote..Mshirikishe Mungu katika uamuzi wake.

thanks
 
Pole sana mkaka, je baada ya hapo ulianzisha mahusiano mengine? Unampenda kutoka moyoni huyo bibie wa zamani? Naweza kuchangia nikipata majibu ya hayo.
 
mkuu
pole sana. kweli dunia ina mambo??

Nakushauri umsamehe, umepoteza vingi juu yake, na zaidi anakujali sana tu. Inawezekana alipata mtu wa kumdanganya, ndio maana akafanya jambo la kijinga.

Mpe nafasi nyingine. hakuna binadamu aliye sawa (perfect). wengine wanayafanya haya wakiwa ndani ya ndoa.. Lakini give her a chance..
Ukimsamehe toka moyoni, Mungu ni mwema, atarekebisha uhusiano wenu..Kwenye mahusiano kuna mambo mengi sana, ukitaka kuchukua hatua kwa kila tukio, utakufa mapema.

Wanadamu tuko hoi siku zote, pamoja na Mungu kutuma hata Mwanaye, lakini mambo bado sio mazuri kote misikitini na makanisani. MSAMEHE.

Siafiki wala kuunga mkono ujinga wake huyo dada, isipokuwa wanadamu tunateleza sana, kama sio leo basi ni kesho. She is yours, unamjua vizuri sana na yeye vivyo.. Nakuhakikishia kuwa atakuwa na heshima kuliko wakati mwingine wowote..Mshirikishe Mungu katika uamuzi wake.

thanks

Me naona amsamehe na amsapoti amalizie masomo yake ila hafai kuwa mke,amsaidie kiubinadamu tu
 
Pole sana mkaka, je baada ya hapo ulianzisha mahusiano mengine? Unampenda kutoka moyoni huyo bibie wa zamani? Naweza kuchangia nikipata majibu ya hayo.

karibu Kibiritingoma..

natumaini ulipata msaada kwenye msaada wa kuacha ***o..

all the best
 
Pole sana mkaka, je baada ya hapo ulianzisha mahusiano mengine? Unampenda kutoka moyoni huyo bibie wa zamani? Naweza kuchangia nikipata majibu ya hayo.
Rudia kusoma..amesema "baada ya kupigika kwa mwanaume aliyekua nae...."
Nwyz unaweza kumsamehe ila kurudiana nae sikushauri!Alikutumia kusoma sasa anataka kukutumia kuweka maisha yake sawa!Ukijitosa uwe tayari kuambiwa tena ulikua hupendwi alitaka tu umwekee maisha yake sawa!
 
waungwana! nilikuwa na mchumba,toka mwaka 2004,nikamtoa form four na sasa anamalizia degree ya education mwezi wa sita mwaka huu,mwaka jana mara tu baada ya kumlipia ada ya mwaka wa mwisho,kesho yake akani sms kuwa alikuwa hanipendi na alikuwa anataka tu asome! kijana nikaamua kuwa cool kwa kuwa nshapoteza pesa nyingi vibaya kwa huyu she,lakini katika masiku ya karibuni baada ya kupigika vibaya kwa mwanaume alokuwa nae eti sasa anataka kurudi kwangu na wakati hata pate yangu ya uchumba alishaitupa,na kamwe siwezi kumuamini tena,nifanyeje ndugu zangu

Blue
alichokuambia alimaanisha na hata ukiangalia alikuambia wakati ambao haitaji tena msaada wako.
Ni wazi hakukupenda na baada ya kutimiza malengo akaondoka.
HAKUPENDI!

Red
Ni ngumu kuishi na mtu ambaye mwenyewe unakiri huwezi kumuamini na pia aliwahi kukwambia hakupendi kwa dhati anafuata msaada wako tu.
Sasa unapata ugumu gani kufanya maamuzi?
 
Blue
alichokuambia alimaanisha na hata ukiangalia alikuambia wakati ambao haitaji tena msaada wako.
Ni wazi hakukupenda na baada ya kutimiza malengo akaondoka.
HAKUPENDI!

Red
Ni ngumu kuishi na mtu ambaye mwenyewe unakiri huwezi kumuamini na pia aliwahi kukwambia hakupendi kwa dhati anafuata msaada wako tu.
Sasa unapata ugumu gani kufanya maamuzi?

maisha wakati mwingine hayaendi kwa formula kama hivyo..
wote tunazifahamu akili za wanafunzi wakiwa vyuoni..kuna peer pressure, na mengine kama mob-psychology!

Simtetei huyo dada, ila kama huyo binti ameona kosa lake na anaomba msamaha, mie ninaona AMPE nafasi nyingine.
 
Rudia kusoma..amesema "baada ya kupigika kwa mwanaume aliyekua nae...."
Nwyz unaweza kumsamehe ila kurudiana nae sikushauri!Alikutumia kusoma sasa anataka kukutumia kuweka maisha yake sawa!Ukijitosa uwe tayari kuambiwa tena ulikua hupendwi alitaka tu umwekee maisha yake sawa!

nadhani mleta thread hajatamka kama ni binti alimuomba amlipie ada, au aliamua kuwekeza tu kwa kufikiri mambo yatakuwa mazuri mbeleni..kwa hiyo huwezi kusema kama binti alikuwa anamtumia..inabidi mleta mada aje aweke sawa kuhusu hili..

mambo ya mapenzi ni magumu, ni muhimu yajengwe katika misingi ya kusameheana.. wametoka mbali since 2004, sio mchezo
 
Atakuumiza mimi nishayaona na kunikuta mwambie ukweli mimi nina gf wangu ajanikosea hivyo sitopenda kumuumiza mtu asiyenitendea kosa lazima itamtachi zaidi kama unamtu mwingine unhisi unampenda naye anakupenda mwambie tukio zima hii itakusaidia wewe kujikuta umekabwa na penzi la ulaghai!!
 
..kwa hiyo huwezi kusema kama binti alikuwa anamtumia..inabidi mleta mada aje aweke sawa kuhusu hili..

mambo ya mapenzi ni magumu, ni muhimu yajengwe katika misingi ya kusameheana.. wametoka mbali since 2004, sio mchezo
"akanitumia sms kwamba ALIKUA ANATAKA TU ASOME" umeona hayo maneno?Yana maana gani?Sijakurupuka kujibu!Na kutoka kwao mbali hamna aliyesema ni mchezo.
 
"akanitumia sms kwamba ALIKUA ANATAKA TU ASOME" umeona hayo maneno?Yana maana gani?Sijakurupuka kujibu!

ok, nimekupata..

lakini nilitamani kujua makubaliano yao ya kulipiana ada yaliaanzaje??
Kumbuka walishavishana hadi pete ya uchumba.
 
Rudia kusoma..amesema "baada ya kupigika kwa mwanaume aliyekua nae...."
Nwyz unaweza kumsamehe ila kurudiana nae sikushauri!Alikutumia kusoma sasa anataka kukutumia kuweka maisha yake sawa!Ukijitosa uwe tayari kuambiwa tena ulikua hupendwi alitaka tu umwekee maisha yake sawa!

swali ni kwa mkaka baada ya hayo alianzisha uhusiano mwingine?? Yeye mkaka.
 
karibu Kibiritingoma..

natumaini ulipata msaada kwenye msaada wa kuacha ***o..

all the best

asante, jana nitoa thread ya shukran naona imehamishiwa sijui jukwaa la wazee. Its almost half done, tunamsubiri mume wangu arudi tu.
 
Back
Top Bottom