Nini tunahitaji kwanza? - (tazama picha na amua)

Tatizo hapa ni uongozi ikiwa hii ndio njia pekee ya kumfikisha mgonjwa hospital maana kiongozi anashindwa hata kuwahamasisha wananchi wakaona umuhimu wa kuchangishana na kununua ambulance hata kama itachukua miaka miwili ama mitatu hili ni tatizo.viongozi haohao wanaongoza kuuza mashamba na viwanja vya wazi na kwa manufaa yao.,,,think twice.


SAHIBA.

Suala hapa sio kuhamasisha wananchi na kununua ambulance. Suala hapa ni kupatikana gari a aina yoyote. Mwananchi anapotumia mkokoteni wa kuvutwa na ng'ombe au punda ni udhibitisho kwamba hana uwezo wa kukodi gari au hakuna gari kabisa katika mazingira yanayomzunguka. Mimi nimebahatika kufanya utafiti flani na kampuni moja katika mkoa wa Shinyanga, na hasa katika wilaya ya Kahama. Hali ya huko vijijini ni mbaya kwa kweli. Na suala hapa sio tu kuhamasisha kununua ambulance, bali ni kuweka miundo mbinu ya kuiwezesha hiyo ambulance kupita. Barabara ni mbovu, na kwenye mito hakuna madaraja. Kipindi cha masika hali ni mbaya sana huko. Hakupitiki kwa magari kwa kifupi.

Kama hoja ya Mwanakijiji inavyosema, nadhani tunahitaji miundo mbinu bora kwanza. Dar es Salaam inahitaji kupanguliwa na kupangwa upya. Issue ya mifereji na mitaro ya kupitisha maji ni ya siku nyingi mno. Ujenzi usio na mpangilio maalumu ni sehemu tu ya kero za jiji hili.
 
kutembelea au kutotembelea nchi za nje wala sio hoja. if you got "it" then you got "it", if you don't then you don't, hence Ndivyo Tulivyo

Kwani wao watu wa nchi za nje walienda kwenye nchi gani ya nje?



icon10.gif
icon10.gif
icon10.gif
icon10.gif


You are politically incorrect.
 
Suala hapa sio kuhamasisha wananchi na kununua ambulance. Suala hapa ni kupatikana gari a aina yoyote. Mwananchi anapotumia mkokoteni wa kuvutwa na ng'ombe au punda ni udhibitisho kwamba hana uwezo wa kukodi gari au hakuna gari kabisa katika mazingira yanayomzunguka. Mimi nimebahatika kufanya utafiti flani na kampuni moja katika mkoa wa Shinyanga, na hasa katika wilaya ya Kahama. Hali ya huko vijijini ni mbaya kwa kweli. Na suala hapa sio tu kuhamasisha kununua ambulance, bali ni kuweka miundo mbinu ya kuiwezesha hiyo ambulance kupita. Barabara ni mbovu, na kwenye mito hakuna madaraja. Kipindi cha masika hali ni mbaya sana huko. Hakupitiki kwa magari kwa kifupi.

Kama hoja ya Mwanakijiji inavyosema, nadhani tunahitaji miundo mbinu bora kwanza. Dar es Salaam inahitaji kupanguliwa na kupangwa upya. Issue ya mifereji na mitaro ya kupitisha maji ni ya siku nyingi mno. Ujenzi usio na mpangilio maalumu ni sehemu tu ya kero za jiji hili.

Ambulance ya nini jamii. Nimeshaona mkuu wa kitengo amechukua Ambulance kufuata majani ya kulisha ng'ombe wake wa maziwa.
 
Ambulance ya nini jamii. Nimeshaona mkuu wa kitengo amechukua Ambulance kufuata majani ya kulisha ng'ombe wake wa maziwa.

Sasa unaleta utani....but knowing us (Miafrika), I wouldn't put that past anybody...
 
kwa nini sisi hatukuwa wa kwanza kwenda kwao? kwikwikwiiiiii

sisi tumeridhika tangu longtaiiiimu. Tunaruka hatua za maendeleo. Tunaacha wengine wanahangaika, sisi tunabypass steji ya utafiti. kwa mfano tumeruka simu za ndani hadi mobile, mitandao iko richebo (heheee, hivi hapo hatujampiga bao mmarekani?).
Tukimaliza ID, tunampango wa kuweka CCTV uswahilini.
 
Sasa unaleta utani....but knowing us (Miafrika), I wouldn't put that past anybody...

Niliviona vitu vinavyofanana na hivyo nikiwa mitikasini DSM. Friji ya bosi mmoja ilikuwa mbovu na ikatumika ambulance kuipeleka kwa mafundi.
 
Ambulance ya nini jamii. Nimeshaona mkuu wa kitengo amechukua Ambulance kufuata majani ya kulisha ng'ombe wake wa maziwa.

Kama nilivyosema, ambulance hapa sio suluhisho. Suluhisho ni kuwa na zahanati ya karibu yenye madaktari na madawa ya kutosha. Nimewahi kushuhudia mgonjwa kwenye mkokoteni wa punda akisafirishwa for 65kms kwenda kwenye zahanati (sio hospitali). You can just imagine the pain mtu anapitia katika hali kama hiyo. Unajiuliza, maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi? Ahadi za Rais vipi? Kuna vitu ni basic human needs, lakini wenzetu hawazipati. Watu wanashangaa kuhusu mauaji ya vikongwe katika mkoa wa Shinyanga. Lakini sababu inasingiziwa ni imani za kishirikina. But what is the root cause? Hakuna vituo vya afya vijijini. Mtu akiugua, wanakwenda kupiga ramli badala ya kumpeleka hospitali. Huko anaambiwa kalogwa na kikongwe fulani. Baada ya hapo ni mauaji ya kikongwe huyo. Hii ndio hali halisi ya vijiji vingi huko Shinyanga.
 
Je viongozi ni nani ??? Si wanachaguliwa kutoka miongoni mwa wananchi.

Zakumi taabu wananchi wanawaamini mno viongozi kuwa ni jawabu ktk matatizo yao....yet viongozi wako ktk direction tofauti..wizi ..uongo..kujilimbikizia mali n.k

pesa hizi2 wanazoiba wanawahonga wananchi maskini wali na kanga kubaki madarakani..na wananchi wanawachagua!

Ndo nikasema taabu ni wananchi na sii viongozi!

Sasa kama wananchi hawataki kubadilika ...je tufanyeje?

Angalia Mzindakaya amekuwa mbunge Sumbawanga miaka 30 na 2010 watamchagua tena!
 
We are always wailing ''the government is not doing anything for us'', what are we doing for us? the loudest among us in this forum are not even residing in Tanzania, let alone contributing anything other than bla, bla, bla...
 
Mkuu mimi nimeshakataa hiki kigezo cha wananchi kupigia kura viongozi wabovu na wanasingizia umasikini! Its damn stupid. Sasa huo umasikini utaishaje? Infact hapa village kwangu hili nimeshawaambia na wanalijua kabisa.

Honestly, bila wananchi TANZANIA kuamka na kujua wajibu wetu...tutaendelea kuwa masikini milele! Na wala siyo cheche ya mwanakijiji wala kelele za akina Kubenea, Ulimwengu et al...zitakazoleta mabadiliko. Ni sisi wenyewe..ila tunakwepa jukumu!

We have to own up our problems. Wananchi tumezidi na ujinga..haiwezekani tunawachagua watu wale wale kila baada ya miaka mitano..harafu tunategemea mabadiliko..kama siyo ujinga ni nini? mi nadhani hata wabunge akina AZANI ambao ni form four wanatuona wajinga mno sisi wananchi..maana wanagombea ubunge sehemu kama KINDONDONI ambako ndo kumejaa the so called wasomi (ambao ungetegemea watofautishe mchele na pumba) Lakini wanachaguliwa kwa kishindo..sasa kweli...tutegemee mabadiliko yapi?


Ushauri wangu: wafanyakazi kwa wakulima Tanzania..tuwe wawajibikaji..haijalishi uko ulaya au uko Mbinga..tuangalie ni namna gani..tunaweza kuisaidia nchi yetu. Ujenzi wa taifa siyo mtu mmoja mmoja..ni sote tunawajibika...Yanayotokea hapa kwenye nchi yetu yanasikitisha sana..you dont need to be a scientist to know this..lakini what are we doing? Hata kama upinzani siyo jawabu...tuwape..wakivurunda..tunawatimua tunaweka wengine..Hivi akili zetu zina nini? Duh!

Labda MATATIZO yetu ni inherent kwenye DNA!
 
Dar Es Salaam,
Please, Hivi wewe kweli unafikiria hayo maendeleo unayoyaona kwa watu nyumbani bila ndugu/marafiki zao nje tungefika hapo tulipo..
Trust me mkuu, kila kitu unachokiona madukani, mitaani na kwingineko kuna Mtanzania aliyeko/ anaishi nje anahusika...
 
Dar Es Salaam,
Please, Hivi wewe kweli unafikiria hayo maendeleo unayoyaona kwa watu nyumbani bila ndugu/marafiki zao nje tungefika hapo tulipo..
Trust me mkuu, kila kitu unachokiona madukani, mitaani na kwingineko kuna Mtanzania aliyeko/ anaishi nje anahusika...

If you can make it nje, kwa nini usiweze hapa?
 
Kama nilivyosema, ambulance hapa sio suluhisho. Suluhisho ni kuwa na zahanati ya karibu yenye madaktari na madawa ya kutosha. Nimewahi kushuhudia mgonjwa kwenye mkokoteni wa punda akisafirishwa for 65kms kwenda kwenye zahanati (sio hospitali). You can just imagine the pain mtu anapitia katika hali kama hiyo. Unajiuliza, maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi? Ahadi za Rais vipi? Kuna vitu ni basic human needs, lakini wenzetu hawazipati. Watu wanashangaa kuhusu mauaji ya vikongwe katika mkoa wa Shinyanga. Lakini sababu inasingiziwa ni imani za kishirikina. But what is the root cause? Hakuna vituo vya afya vijijini. Mtu akiugua, wanakwenda kupiga ramli badala ya kumpeleka hospitali. Huko anaambiwa kalogwa na kikongwe fulani. Baada ya hapo ni mauaji ya kikongwe huyo. Hii ndio hali halisi ya vijiji vingi huko Shinyanga.

Zero:


Sehemu kubwa ya matatizo ya afya Tanzania ni poor Hygiene.
 


Zakumi taabu wananchi wanawaamini mno viongozi kuwa ni jawabu ktk matatizo yao....yet viongozi wako ktk direction tofauti..wizi ..uongo..kujilimbikizia mali n.k

pesa hizi2 wanazoiba wanawahonga wananchi maskini wali na kanga kubaki madarakani..na wananchi wanawachagua!

Ndo nikasema taabu ni wananchi na sii viongozi!

Sasa kama wananchi hawataki kubadilika ...je tufanyeje?

Angalia Mzindakaya amekuwa mbunge Sumbawanga miaka 30 na 2010 watamchagua tena!

Kwani sasa tusirudi CCM na tukipata nafasi tufanye mapinduzi ndani ya CCM ???

Kuna mNigeria alijifanya ameokoka na kukaa na mwanamke wa kizungu kwa zaidi ya miaka mitano. Pale mzungu alipomwani tu jamaa alikusanya pesa zote na kuanza.

TumuombE mwanakijiji arudi CCM na ajitulize tu. Na siku wakimpa nafasi aanze kuleta CHECHE.
 
Wakati flani humkosea Muumba na hunipelekea kuamini sisi watu weusi tuna dosari/tatizo kwa asili. Hudiriki kukubaliana na nadharia mbalimbali za kibaguzi......

Hatuna sababu ya maana kuwa maskini kiasi hiki. Labda ndio maana hata Kikwete alipoulizwa kwa nini TZ ni maskini, alisema hajui! Tuna kila aina ya neema kwenye maliasili...lakini duh..

Tatizo la kwanza ni uongozi wetu, hasa wa juu kabisa ya nchi. Ni uongozi dhaifu, usio na vision, hauna uwezo kabisa wa akili. Ni viongozi hawa wanaoshindwa kuamua kwa usahihi vipaumbele vyetu na mwelekeo imara wa taifa letu. Hawaioni Tanzania yetu kwa muono wa miaka 200 au zaidi ijayo. Wanaiona ya leo na kesho. Wakijitahidi sana, miaka 5!

Tatizo lingine ni mfumo wetu wa kuwapata viongozi bora, wenye uwezo na wa maana. Mfumo wetu upo loose mno, dhaifu na haufai kiasi kwamba mtu yeyote (hata awe zuzu) anaweza kupenyeza na kuiongoza nchi yetu. Anaweza kuwa rais, mbunge, waziri, RC, DC, Mkurugenzi Mkuu, Commisioner, Mkuu wa Majeshi, e.t.c Mifano ni mingi tunayo na tunaijua. Binafsi, najua baadhi ya wabunge ambao hata darasa la saba hawakumaliza..!

Tatizo la tatu, likihusiana na MFUMO, ni kukosekana kwa misingi imara kwa maendeleo ya taifa (foundations necessary for development; institutions and structures). Kwa mfano katiba yetu (mbovu) ina mruhusu kila rais ajaye kujiamulia binafsi UKUBWA wa serikali! Au serikali (executive) inakuwa na nguvu hata zaidi ya bunge! Mahakama!

Taifa lazima lifikirie upya namna ya kuwapata viongozi wetu, kujenga misingi imara ya maendeleo. Lazima tujitathmini, tujipange upya, tutafakari, tumuombe Mungu. TUANDIKE chini namna tunataka nchi yetu iwe. Ikishindikana, we need a visionary and patriotic dictator!

YOU AND I, CAN DO SOMETHING. Let us act now!
 
Back
Top Bottom