Nini kilikufanya ugundue Umri umeenda?

Nini kilikufanya ugundue Umri umeenda?

Mawele

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2023
Posts
999
Reaction score
3,549
Kuna muda mtu unakuwa na mambo mengi hadi unasahau kama upo kwenye "Age go" unaongeza miaka ila ni kama unajiona bado mdogo tu mpaka ukutane na jambo fulani ndio unastuka kumbe umri wangu ushaenda hivyo.

Kuna wengine ongezeko la shikamoo ndio linawastua wengine kuitwa kwneye vikao vya ukoo nk.

Kipi kilikufanya ujue umri ushakutupa mkono?
 
Mimi ni young forever, ishu inayonifanya nione nina umri mkubwa ni kwamba nina miaka 4 sijawahi kuvaa jeans . Nimepoteza interest kwenye vitu vingi ; kuanzia chakula mpaka show off . Nikienda town kununua suruali na T shirt kama nitanunua naweza nisivae ... Nina Tshirt mpya kama tano sijavaa hata moja , napenda kuvaa kanzu kuliko nguo yoyote ile .

Yaani kifupi hata kupiga picha naona ni ushamba , kushangaa maghorofa . Nikipata fresha na nikikosa fresh , kitu naogopa ni magonjwa tu ila kifo sijawahi kuogopa .. Vitu vingi nilivyozoea kufanya sina mzuka navyo , kila kitu naona kawaida , sipendi kelele wala kujichanganya na watu .

Sipendi kuona mtu anaonewa wala kupata tabu .
 
Back
Top Bottom