Changamoto za kupata mtoto mchanga ukiwa umri wa kustaafu, unakuwa ni Baba Babu. Dawa ni kujipanga kabla, vinginevyo ni kubebesha watu mizigo yako

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,571
Leo Ijumaa ya Tarehe 8 April, ni siku yangu ya kuzaliwa, nikiwa nimeipiga mingi nikikaribia 60! ambao ndio umri rasmi wa kustaafu, nikiwa tayari ni father of 8 +1= 9, Grand Pa of 6, and about to retire!.

Sababu ya makala hii ya leo sio kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali kutoa mbinu za changamoto za ulezi katika umri mkubwa, huku unajiandaa kustaafu, huku vichanga vinaendelea kuzaliwa!.

Naomba kutoa taarifa ya ujio wa mgeni mwingine kwenye familia yangu, ujio wa mgeni huyu, ume concide na tarehe yangu ya kuzaliwa, mgeni huyu mpya, amebisha hodi hapa duniani leo, tarehe 8 April, 2022 majira ya saa 4:00 asubuhi, katika hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam, na kwa vile mgeni mwenyewe ni Jnr kidume, hivyo nimetoa jina langu la Pasco, hivyo ataitwa Pasco Mayalla -Jnr na kuanzia leo mimi nimebadili jina na kuwa Pasco Mayalla Snr baada ya ujio wa Pasco Jnr!.

Kupata mtoto katika umri mkubwa kama huu, kuna changamoto zake, changamoto ya kwanza, ni watoto wangu wakubwa 3, tayari wana watoto!, yaani mimi ni Babu, halafu unapata mtoto mdogo kuliko mjukuu!, hivyo kwa wajukuu wa watoto wangu wa kiume, huyu Pasco Jnr ni baba yao mdogo! na wajukuu wa mabinti huyu ni mjomba wao!, baba mdogo na mjomba kuwa ni mdogo kuliko wajukuu, haipendezei saana kivile!.

Kuna watu wataona ni ajabu kwa mtu over 50 kupata mtoto, japo nikweli sio kawaida sana, watu wanapaswa kujenga familia wakiwa wangali vijana, while still energetic, ukifika umri wa miaka 50 ni umri wa kujiandaa kustaafu na kuitwa babu, sio tena umri wa kuanza kulea vichanga na kuitwaa baba wakati umri ni wa babu!, lakini amini usiamini, kupata mtoto at 50 plus Kiafrika, ni kawaida sana!, tuna mfano mingi tuu, ukitafuta umri wa Chief Burito Nyerere wakati Julius Kambarage anazaliwa, hutashangaa!. Hata Nabii Ibrahim alipomzaa Isaka alikuwa na umri wa miaka 90!. Mfano mzuri wa karibu ni yule Mzee wetu fulani, Al maarufu na mashuhuri, alipata watoto twins at 74 years!, hivyo mimi kupata mtoto at 50 plus, ni bado kijana sana!, ila huyu Pasco Jnr ni last born!.

Lengo la makala hii ya leo ni kutoa somo la kujiandaa kustaafu, ili ustaafu bila stress. Kitendo tuu cha mstaafu mtarajiwa kupata mtoto at 50 +, hiyo peke yake tayari ni stress tosha!, kwasababu mtoto anatakiwa kutimiza the age of majority, akiwa total dependant!. Pesa za mstaafu, haziwezi kumlipia shule nzuri mtoto huyu, unless nikubali akasome St. Kayumba!. Kama hao wenzake 8, hakuna aliyesoma St. Kayumba, hivyo huyu kitinda mimba wa Baba Babu, kuja kusoma St. Kayumba, itakuwa sio kumtendea haki, hivyo I need kujipanga kweli kweli!. Hivyo makala hii, itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa wazee wenzangu na wale wote wenye umri mkubwa, huku wakikabiliwa na changamoto za ulezi.

Kutokana na maandalizi duni ya kustaafu, wastaafu wengi hujikuta hawana vitega uchumi vya kutosha kuwa sustain baada ya kustaafu, hivyo kuishi maisha ya stress, wengine kusumbua watoto kwa kupiga muzinga, hali inayopelekea ikiona tuu simu ya dingi, unahisi ni mzinga, hivyo ukijiona uko apeche alolo, unaogopa hata kupokea simu ya dingi wako ukidhani ni mzinga!, kumbe sometimes, simu nyingine za madingi, wala sio mizinga!, ni dingi tuu amekukumbuka na anakupigia ili kukusalimia tuu!, hivyo natoa kwa wote, ukiona simu ya dingi, pokea tuu!, ila madingi nao sometimes wanazi!, anakupigia simu, uko very busy, hupokei!, ukiona anafululiza kupiga, unapokea ukijua, anashida!,
"haloo, shikamoo baba".
"marahaba mwanangu, nilikupigia kukusalimia tuu, nina kiu!"
unatamani kukata!.
Wa Maza hawanaga simu za hivi, maza akikupigia simu anashida ujue ni shida kweli!.

Kitu kinacholeta stress kubwa Kwa wastaafu wengi, ni wengi kutofanya biashara yoyote wakati wa utumishi wao, halafu akiisha staafu yale malipo ya mafao ya pensheni ya mkupuo kuyatumia kama mtaji wa kuanzisha biashara, biashara isipokwenda vizuri, matokeo yake ni kupata stress, kuchoka mapema na kuchakaa, na hapo hapo maradhi ya depression na mwisho ni kufa mapema kwa ma pressure, heart attacks, maumivu ya viungo, organ failure etc.

Ili kuzuia stress za kustaafu, kama unapanga kufanya biashara fulani baada ya kustaafu, start small!, anza kidogo kidogo ukingali kazini kupata uzoefu wa kutosha ukiona unaweza ndipo ukistaafu ujikite zaidi.

Ushauri wangu wa the best way ya kustaafu, ni zile fedha za mafao yako ya kustaafu ambayo umelipwa kupitia benki, wastaafu wengi huziweka fedha hizo Benki kama akiba, na kuzitumia kidogo kidogo.

Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu sana. Fedha hizo zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni kwa kuwekeza kwenye ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 12%!.

Sasa tupige hesabu ya pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 12. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 6 kila miezi 6.

Ukiisha nunua bonds zile Bondi certificate ni dhamana ya uhakika ya kupata mkopo Benki yoyote kufanyia biashara yoyote.

Nakushauri, fanya utaratibu na Benki yako, badala ya kusubiri kupokea gawio lako la milioni 12 kwa mwaka, unaomba ulipwe shilingi milioni 1,000,000 kila mwezi kwa muda wa miaka 25, bado wewe mstaafu utakuwa na stress au kusumbua kupiga mizinga watoto?.

Wastaafu wenzangu watarajiwa, ni muhimu sana kupanga uzazi, ni muhimu kupanga familia, ni muhimu kujipanga kustaafu bila stress, ila ikitokea umepata ugeni kama wa Pascal Mayalla Jnr, mida ya machweo, mpokee tuu mgeni with positivism after all kila mtoto anakuja na rizki yake!,
Karibu Pascal Mayalla Jnr.
Happy Born Day Pascal Mayalla Jnr
Happy Birthday Pascal Mayalla Snr
Paskali
Update ya Kilichopelekea Kuendelea Kutengeneza Watoto Post 50 Years!.
Pasco, umezaa na mkeo? Watoto 8 ni wengi sana. Wanatumia financial, physical and emotional resources nyingi sana kuwahudumia na kuwalea. I think it wasn’t the wisest decision for you to have a baby at this point in your life. Hapo umefulia mzee. Big time.
Mkuu Goldschmidt , kwanza asante sana kwa kuwa mkweli, bonafide genuine, watu huwa hatupendi kuambiwa ukweli mchungu, hiki ulichosema hapa ni ukweli mchungu!.

It's true watoto 8, now 9 ni wengi!. Mimi ni a modern man, niliao a classmate sweetheart mimi nikiwa at 25 years mwenzagu at 21, straight chuo TSJ, into kujenga familia!, tukahama nchi kwenda UK tukapata mtoto wa kwanza a girl then tukahamia US tukapata mtoto wa pili, a boy tukaamua that is it. Hatuhihitaji tena kuongeza watoto!.

Wife akapata full sponsored fellowship ya 4 years US mimi ndio niwe house husband na babysitter wa watoto wetu wawili. Very unfortunately, nilishindwa nikamwacha wife US na kurudi Bongo!.

Long distance relationships doesn't work well kwa baadhi ya makabila, so does maisha ya u Marioo, yaani mke ndio mwenye kazi, pesa, mimi niwe Marioo!. Wasukuma ni one of such tribes!, nilishindwa!.

Hivyo niliporudi kuishi bongo huku wife US, nikajikuta wametokelezea watoto 3 wengine!. 2 boys and a girl hivyo I had 5 kids!. (naomba usiulize ufafanuzi wowote kuhusu hawa watoto 3 please!).

Wife baada ya kumaliza shule with news ya uwepo wa watoto wengine wa3, wife akaamua kugomea US hivyo mimi nikawa sina jinsi bali kurudi Bongo na kuendelea kuendesha life.

Mwaka 2008 I suffered a bad terrible motor accident, I was confirmed to a wheelchair!. Hapa akajitokeza kabinti fulani with a heart of gold, she came with love and care , kiukweli mtu ukiwa invalid confined to a wheelchair, akatokea mtu kupenda hivyo ulivyo, ni very rare and amazing love.

She told me something was telling her tukijaribu pengine, nitaweza kupona. She made some efforts tukahangaika huku na kule, tukaenda South gharama zikatushinda , tukaenda India, ndiko nilikoponea na kusimama tena!.

Baada ya kupona na kurudi Bongo,
kwanza nilitoa shukrani kwa yote niliyopitia Waraka wa Pascal Mayalla - Asanteni Sana! nikajikuta zawadi pekee kwa huyu binti ni ndoa!, hivyo 2010 nikaoa tena, by then nikiwa over 40!.

Kabinti kakanizalia 3 beautiful daughters the number was 8, ilipotokea tena dalili ya ugeni, we didn't say no!, then ndio hiyo jana kaleta kidume, na kiukweli hapo sasa ndio mwisho.
P
 
Happy Birthday kaka Pascal, hongera kwa kuwa baba mpya. Pamoja na kumuomba Mungu akujalie afya njema pia chukua tahadhari zote za kiafya ikiwa ni pamoja na kuongeza ulaji wa matunda na mboga za majani , kufanya mazoezi na kunywa maji mengi.

Malezi ya mtoto si pesa tu bali uwepo wako physically ni muhimu sana. Kumfunza maadili yaliyo mema. Junior akiwa na miaka 10 wewe utakua na miaka 70. Yale magenge ya vishawishi na hormonal changes yakianza kumtokea Junior utakua na nguvu za kukimbizana navyo?

Bahati nzuri anao waliomtangulia. Ninamtakia Junior maisha ya furaha na Afya njema.
 
Ijumaa ya Tarehe 8 April, ni siku yangu ya kuzaliwa, nikiwa nimeipiga mingi nikikaribia 60! ambao ndio umri rasmi wa kustaafu, nikiwa ni father of 8 +1= 9, Grand Pa of 6, and about to retire!.

Sababu ya makala hii ya leo sio kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali kutoa taarifa ya ujio wa mgeni mwingine kwenye familia yangu, ujio wa mgeni huyu, ume concide na tarehe yangu ya kuzaliwa, na kwa vile mgeni mwenyewe ni kidume, hivyo nimetoa jina langu la Pascal, hivyo ataitwa Pascal Mayalla, Jnr na kuanzia leo mimi nimebadili jina na kuwa Pascal Mayalla Snr baada ya ujio wa Pascal Mayalla Jnr.

Kupata mtoto katika umri mkubwa kama huu, kuna changamoto zake, changamoto ya kwanza, ni watoto wangu wakubwa tayari wana watoto, yaani mimi ni Babu, halafu unapata mtoto mdogo kuliko mjukuu, hivyo kwa wajukuu wa watoto wangu wa kuume, huyu Pascal Mayalla Jnr ni baba yao mdogo ni mdogo kuliko wajukuu!.

Kuna watu wataona ni ajabu kwa mtu over 50 kupata mtoto, japo nikweli sio kawaida, watu wanajenga familia wakiwa vijana, ukifika miaka 50 ni umri wa kujiandaa kustaafu na sio tena kuanza kulea na kuitwaa baba wakati umri ni wa babu, lakini amini usiamini, kupata mtoto at 50 plus ni kawaida sana, tuna mfano mzuri wa yule Mzee fulani, maarufu na mashuhuri, alipata watoto at 74 years hivyo mimi kupata mtoto at 50 plus ni bado sana.

lengo la makala hii ya leo ni kutoa somo la kujiandaa kustaafu, ili ustaafu bila stress. Kitendo tuu cha mstaafu mtarajiwa kupata mtoto at 50, hiyo peke yake tayari ni stress, hivyo makala hii, itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa wale wote wenye umri mkubwa, huku ukikabiliwa na changamoto za ulezi.

Kutokana na maandalizi duni ya kustaafu, wastaafu wengi hujikuta hawana vitegauchumi vya kutosha kuwa sustain baada ya kustaafu, hivyo kuishi maisha ya stress, wengine kusumbua watoto Kwa kupiga muzinga, hali inayopelekea ikiona tuu simu ya dingi, unahisi ni mzinga, hivyo ukijiona uko apeche alolo, unaogopa kupokea!, kumbe ni dingi amekukumbuka tuu na anakupigia kukusalimu.

Kitu kinacholeta stress kubwa Kwa wastaafu wengi, ni wengi kutofanya biashara yoyote wakati wa utumishi wao, halafu akiisha staafu yale malipo ya pensheni ya mkupuo kuyatumia kama mtaji wa kuanzisha biashara, biashara isipokwenda vizuri, matoi yake ni kupata stress, kuchoka mapema na kuchakaa, na hapo hapo maradhi ya depression na mwisho ni kufa mapema kwa ma pressure, heart attacks, maumivu ya viungo, organ failure etc.

Ili kuzuia stress za kustaafu, kama unapanga kufanya biashara fulani baada ya kustaafu, start small!, anza kidogo kidogo ukingali kazini kupata uzoefu wa kutosha ukiona unaweza ndipo ukistaafu ujikite zaidi.

Ushauri wangu wa the best way ya kustaafu, ni zile fedha za mafao yako ya kustaafu ambayo umelipwa kupitia benki, wastaafu wengi huziweka fedha hizo Benki kama akiba, na kuzitumia kidogo kidogo.

Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu Sana. Zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni Kwa kuwekeza Kwa ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 16%!.

Sasa tupige hesabu ya Pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 16. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 8 kila miezi 6.

Ukiisha nunua bonds zile Bondi certificate ni dhamana ya uhakika ya kupata mkopo Benki yoyote kufanyia biashara yoyote.

Nakushauri, fanya utaratibu na Benki yako, badala ya kusubiri kupokea gawio lako la milioni 16 kwa mwaka, unaomba ulipwe shilingi milioni 1,300,000 kila mwezi kwa muda wa miaka 25, bado wewe mstaafu utakuwa na stress au kusumbua kupiga mizinga watoto?.

Wastaafu wenzangu watarajiwa, ni muhimu sana kupanga uzazi, ni muhimu kupanga familia, ni muhimu kujipanga kustaafu bila stress, ila ikitokea umepata ugeni kama wa Pascal Mayalla Jnr, mida ya machweo, mpokee tuu mgeni with positivism after all kila mtoto anakuja na rizki yake,
Karibu Pascal Mayalla Jnr.
Happy Born Day Pascal Mayalla Jnr
Happy Birthday Pascal Mayalla Snr
Paskali
Pasco, umezaa na mkeo? Watoto 8 ni wengi sana. Wanatumia financial, physical and emotional resources nyingi sana kuwahudumia na kuwalea. I think it wasn’t the wisest decision for you to have a baby at this point in your life. Hapo umefulia mzee. Big time.
 
Kwa mwanaume Miaka 60 aweza zaa mtoto strong tu

Ila kwa mwanamke mwisho Miaka 40 zaidi ya hapo kuzaa anatafuta matatizo aweza zaa mtoto zezeta au lenye akili nusu.Jinga hasa.
Wanawake pia hukauka mapema hivyo ni vyama kwa mwanamke kuwahi kuzaa mapema ukifika 40 ndio uzae last born vinginevyo utagombana na manesi na waweza zaa kwa operation

Anyway Mayala Mkeo ana umri gani? Kama beyond Miaka 40 be prepared. For the worse
 
Leo Ijumaa ya Tarehe 8 April, ni siku yangu ya kuzaliwa, nikiwa nimeipiga mingi nikikaribia 60! ambao ndio umri rasmi wa kustaafu, nikiwa tayari ni father of 8 +1= 9, Grand Pa of 6, and about to retire!.

Sababu ya makala hii ya leo sio kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa, bali kutoa mbinu za changamoto za ulezi katika umri mkubwa kwa huku unajiandaa kustaafu, huku vichanga vinaendelea kuzaliwa!.

Naomba kutoa taarifa ya ujio wa mgeni mwingine kwenye familia yangu, ujio wa mgeni huyu, ume concide na tarehe yangu ya kuzaliwa, na kwa vile mgeni mwenyewe ni kidume, hivyo nimetoa jina langu la Pascal, hivyo ataitwa Pascal Mayalla, Jnr na kuanzia leo mimi nimebadili jina na kuwa Pascal Mayalla Snr baada ya ujio wa Pascal Mayalla Jnr.

Kupata mtoto katika umri mkubwa kama huu, kuna changamoto zake, changamoto ya kwanza, ni watoto wangu wakubwa tayari wana watoto, yaani mimi ni Babu, halafu unapata mtoto mdogo kuliko mjukuu, hivyo kwa wajukuu wa watoto wangu wa kiume, huyu Pascal Mayalla Jnr ni baba yao mdogo ni mdogo kuliko wajukuu!.

Kuna watu wataona ni ajabu kwa mtu over 50 kupata mtoto, japo nikweli sio kawaida sana, watu wanajenga familia wakiwa vijana, ukifika miaka 50 ni umri wa kujiandaa kustaafu na sio tena kuanza kulea na kuitwaa baba wakati umri ni wa babu, lakini amini usiamini, kupata mtoto at 50 plus ni kawaida sana, tuna mfano mingi tuu, ukitafuta umri wa Chief Burito wakati Julius Nyerere anazaliwa, hutashangaa!. Hata Nabii Ibrahim alipomzaa Osaka alikuwa na miaka 90!. Mfano mzuri wa karibu ni yule Mzee wetu fulani, Al maarufu na mashuhuri, alipata watoto at 74 years hivyo mimi kupata mtoto at 50 plus ni bado sana.

lengo la makala hii ya leo ni kutoa somo la kujiandaa kustaafu, ili ustaafu bila stress. Kitendo tuu cha mstaafu mtarajiwa kupata mtoto at 50, hiyo peke yake tayari ni stress, hivyo makala hii, itakuwa ni msaada mkubwa sana kwa wale wote wenye umri mkubwa, huku ukikabiliwa na changamoto za ulezi.

Kutokana na maandalizi duni ya kustaafu, wastaafu wengi hujikuta hawana vitegauchumi vya kutosha kuwa sustain baada ya kustaafu, hivyo kuishi maisha ya stress, wengine kusumbua watoto Kwa kupiga muzinga, hali inayopelekea ikiona tuu simu ya dingi, unahisi ni mzinga, hivyo ukijiona uko apeche alolo, unaogopa kupokea!, kumbe ni dingi amekukumbuka tuu na anakupigia kukusalimu.

Kitu kinacholeta stress kubwa Kwa wastaafu wengi, ni wengi kutofanya biashara yoyote wakati wa utumishi wao, halafu akiisha staafu yale malipo ya pensheni ya mkupuo kuyatumia kama mtaji wa kuanzisha biashara, biashara isipokwenda vizuri, matoi yake ni kupata stress, kuchoka mapema na kuchakaa, na hapo hapo maradhi ya depression na mwisho ni kufa mapema kwa ma pressure, heart attacks, maumivu ya viungo, organ failure etc.

Ili kuzuia stress za kustaafu, kama unapanga kufanya biashara fulani baada ya kustaafu, start small!, anza kidogo kidogo ukingali kazini kupata uzoefu wa kutosha ukiona unaweza ndipo ukistaafu ujikite zaidi.

Ushauri wangu wa the best way ya kustaafu, ni zile fedha za mafao yako ya kustaafu ambayo umelipwa kupitia benki, wastaafu wengi huziweka fedha hizo Benki kama akiba, na kuzitumia kidogo kidogo.

Kitendo cha fedha hizo kukaa Benki kwenye account ya savings, faida yake ni kiduchu Sana. Zingekaa kwenye a fixed deposit account, FDA, zingezalisha faida kubwa kidogo, lakini mpango mzima wa ukweli na wa uhakika wa uwekezaji wa mafao yako ni Kwa kuwekeza Kwa ununuzi wa dhamana za serikali, yaani Government Bonds, ambazo huuzwa na Benki Kuu ya Tanzania ambapo hutoa riba ya mpaka asilimia 16%!.

Sasa tupige hesabu ya Pamoja.
Tuseme mafao yangu ya kustaafu ya mkupuo ni milioni 100. Nikinunulia Government Bonds za miaka 25, kila mwaka nitapata shilingi milioni 16. Bonds wanalipa gawio mara 2 Kwa mwaka, kila baada ya miezi 6. Hivyo nitalipwa shilingi milioni 8 kila miezi 6.

Ukiisha nunua bonds zile Bondi certificate ni dhamana ya uhakika ya kupata mkopo Benki yoyote kufanyia biashara yoyote.

Nakushauri, fanya utaratibu na Benki yako, badala ya kusubiri kupokea gawio lako la milioni 16 kwa mwaka, unaomba ulipwe shilingi milioni 1,300,000 kila mwezi kwa muda wa miaka 25, bado wewe mstaafu utakuwa na stress au kusumbua kupiga mizinga watoto?.

Wastaafu wenzangu watarajiwa, ni muhimu sana kupanga uzazi, ni muhimu kupanga familia, ni muhimu kujipanga kustaafu bila stress, ila ikitokea umepata ugeni kama wa Pascal Mayalla Jnr, mida ya machweo, mpokee tuu mgeni with positivism after all kila mtoto anakuja na rizki yake,
Karibu Pascal Mayalla Jnr.
Happy Born Day Pascal Mayalla Jnr
Happy Birthday Pascal Mayalla Snr
Paskali
😍
 
A very Happy Birthday to you Pascal Mayalla. Kusema kwako unakaribia 60yrs kumenifanya nitafakari ni jinsi gani wakati unakimbia. Nakumbuka kuanza kukusikia nikiwa kijana mdogo na mpaka sasa naelekea kuuacha ujana.

Mungu akupe umri zaidi na afya tele bro. In your own ways you have been an inspiration to many. Be blessed.
HBD Pascal Mayala

Sent from my SM-J530F using JamiiForums mobile app
 
Komredi hongera sana kwa Mwenyezi Mungu kukupatia Paschal Mayalla Jnr👍

Mwenyezi Mungu ampe PM Jnr uhai mrefu ,afya njema na mafanikio tele....afuate NYAYO za babu na bibi yake katika utumishi wa taifa letu pendwa ,amen🙏

Happy birthday 🙏

Kudos👍
 
Back
Top Bottom