J.J Mnyika,
Habari za gardens zetu nimezipata toka humu:-
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=2993
We need level field(kwa maana ya mfumo) but we also need strong oppossition parties. They all have to be addressed kwa pamoja.
hapa mjomba sikubaliani kabisa!... hata mimi huu ni mtazamo wangu isije chukuliwa kama ndio mawazo ya kila mtu. Nitasema kwa nini nafikiri Mzee Es amewasakama.
J.J Mnyika, Mnashindwa kutenganisha vitu viwili muhimu hapa. Navyo ni kwamba nchi yenye demokrasia ya kweli ni ile yenye kutoa nafasi sawa kwa vyama - (Equal field level) ktk Kutangaza siasa zake. Sasa kama Tanzania hakuna ina maana hatuna haja kabisa ya kuwa na vyama vya Upinzani ktk mtazamo wa demokrasia (chama mbadala). Kila kunapokucha kazi za vyama vyetu ni kugombania nafasi sawa jambo ambalo CCM imewahakikishia kuwa haiwezekani sawa na serikali ya mkoloni ilivyokuwa ikitawala. Na bahati mbaya mnaendelea kupigania haki yenu ya demokrasia ambayo kwa mlalahoi hawezi kabisa kuelewa mnapigania kitu gani hali nchi yetu iko huru na kama ni demokrasia sii hiyo mnayo?..
First, wengi wetu hatuelewi nini demokrasia na inafanya kazi vipi ktk mazingira yapi - tunachofahamu zaidi ni kuisoma hiyo demokrasia ktk magazetini, kama vile fiction.
Kwa hiyo hapa nafasi ipo tu ktk upinzani kuchagua ni mbinu gani itangulie. Kama ni kutafuta Demokrasia, basi hakuna haja ya vyama kujiunga na uchaguzi wa aina yeyote na kuweka madai yenu ktk kutafuta hiyo level. Hapa viongozi hamhitaji chama hata kidogo kwa sababu kuwepo kwa chama na kushiriki kwake ni sababu moja tosha kuwepo kwa level sawa ya demokrasia (quote n qoute) huko nje. Ikiwa hampewi nafasi sawa dawa yake ni kutoshiriki...
Mapambano yenu yanakuwa ktk kuwaelemisha wananchi kama walivyofanya akina MLK, Malcom na kadhalika yaani vyama vya UPINZANI..
Nafikiri leo inabidi nikupe wazi msemo wako mwenyewe kuwa Chadema sio chama cha
UPINZANI ila ni Chama
MBADALA. Na hupendi kabisa watu wanapokiita Chadema chama cha Upinzani.
This is where mawazo yenu na ya wananchi yanapopishana.
J.J Mnyika, huwezi kuwa chama mbadala ktk mfumo ambao hauna leve field sawa. Huwezi kuwa chama Mbadala hali madai yako mengi yatakuwa yakikwamishwa na katiba iliyopo ambayo inakumbatia chama kimoja. Hapa mnakuwa hamna mwelekeo kwa sababu wananchi wanashindwa kufahamu hasa vyama hivi vinapigania kitu gani!. Kibaya kuliko yote ni kwamba mnajaribu kuyafanya yote kwa pamoja..
1. Kutafuta uwanja sawa huku mkiwa bado ndani ya ligi...
2. Mnacheza mechi hali mnafahamu marefa, linesmen wote ni vibaraka wa timu mnayocheza against!..huku mkitegemea kwa baraka zake Mungu labda kutatokea muujiza wa ushindi!... heeeeelll No haiwezekani hata kidogo.
Kisha baada ya mechi mnataka wananchi wafahamu kuwa mlishindwa kwa sababu... blaaa blaaa blaa! lakini kwa nini mmejiunga na ligi? hali mnafahamu toka mwanzo ligi hii ni feki?.. inapangwa kama mechi za boxing za mzee Don King! unless nanyi ni washiriki wazuri ktk mchezo huu kutafuta ngawila!...
That is Mzee Es point. kama kweli mnataka kuwakilisha wananchi mnatakiwa chama cha UPINZANI na mfanye kazi zenu kama Wapinzani. Madongo tuuuuuu kila kukicha!.. Wananchi watakuja kuona mwanga na ndio siku CCM wataweka uwanja sawa na pengine mnaweza kuchukua imani za wananchi ktk Upinzani kuliko ktk mfumo mliokuwa nao leo....Ati vyama mbadala ktk mfumo usiokuwa na haki.