Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Status
Not open for further replies.
Haya bwana kila la kheri 'Kamanda', hope utarudi salama.

Naufaham vizuri huu mtego, msije mkashangaa kusikia Lisu na Mnyika wamekufa mazoezini jeshini pindi watakapokwenda na wao.
 
Wana JF, salam!

Nategemea kushiriki mafunzo ya JKT yatakayoshirikisha wabunge vijana. Nafanya hivyo kwa ajili ya NCHI YANGU, VIJANA WENZANGU NA CHAMA CHANGU.

Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.

Safari njema
 
Wana JF, salam!

Nategemea kushiriki mafunzo ya JKT yatakayoshirikisha wabunge vijana. Nafanya hivyo kwa ajili ya NCHI YANGU, VIJANA WENZANGU NA CHAMA CHANGU.

Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.

kila la heri. Ila najua nyie waheshimiwa, tena wa chama tawala hamtahenyeshwa. La msingi jiepushe na dada zetu tu...
 
Mkuu Pasco, si wote wanaobadilika positively.
Huyu Lameck Madelu, kwa akili zake ndio anaweza kutoka huko akiwa wa ovyo kabisa.
Mkuu Mkeshaji, "give a dog a bad name and hang it!", just wish him the best, and hope for the best that hell be the best!.
P.
 
Wana JF, salam!

Nategemea kushiriki mafunzo ya JKT yatakayoshirikisha wabunge vijana. Nafanya hivyo kwa ajili ya NCHI YANGU, VIJANA WENZANGU NA CHAMA CHANGU.

Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.

Mwigulu, mimi kama Afande wako nakuasa yafuatayo; La kwanza Ukifika Kikosini Jina lako si Mwigulu Nchemba tena bali ni Kuruta Mwigulu.
Pili. Kama ulidhani kujua hesabu ni kusaidia kujongo basi kwa taarifa yako Jeshini hesabu mwisho TATU kule hakuna NNE wa KUMI.
Tatu. Hakuna ITIKADI ZA VYAMA KULE. Usiende na nguo yoyote kuashiria wewe ni CCM Damu Hakuna.
Nne. Jeshini hakuna uchafu utakao zagaa mbele yako hadi vyoo mtashika kwa mikono mkitafuta risasi iwapo mmoja wenu kwa bahati mbaya akatumbukiza wakati akikamua "King'amuzi" chake.
Tano. Jeshini hakuna neno "SAWA AFANDE" Bali kuna "NDIYO AFANDE" Usawa hakuna wewe ni kuruta una usawa gani na Ofisa wewe.
Sita. Usijaribu KUGOMA au Kunung'unikia jambo utakuwa umewatia sumu Maafande wako utakoma.
Saba. Lazima ujue nyimbo za Kilugha, wewe ni Mnyiramba lazima ujue kuimba Kinyiramba kuna Disco kule, DJ ni wewe Kuruta.
Sidhani kama mtaruhusiwa kuwa na simu mifukoni mwenu enzi zetu redio ilikuwa ni kitu hatari kuwa nacho HANGANI yaani sehemu ya kulala

Ni imani yangu mkimaliza mkataba wenu hizo itikadi zenu za vyama zitaisha wote mkirudi mtakuwa ni Wazalendo wenye NIA MOJA TU KULINDA NA KUIENDELEZA NCHI YA TANZANIA.

Mengine nitakujuza.

 
Nenda ukirudi utukamatie lile jangili la tembo bila kujali kama ni boss wako vinginevyo dr.kitila tunampa jimbo
 
kila la kheri Mwigulu natumaini ukirudi huko hauta tetea tena mambo ya kipuuzi puuzi na kutukana viongozi wako,Mafunzo mema mkuu
 
Hiyo ni semina sio mafunzo ya JKT. Hayo mafunzo yana mtaala wake ambao huwezi kumaliza hata kwa miezi mitatu. Nyie mnatafuta umaarufu wa kisiasa na sio mafunzo ya JKT. Chezea national service weye!
 
nyie waheshimiwa hamsomeki isije tukasikia mmetengewa bilion kadhaa yani budget special ya wk 3 mkiwa mafunzoni alafu mnarudi mtaani na vitambi vyenu mmekwishatafuna kodi zetu kavp kausheni tu ila waandalieni vijana mazingira mazuri ya depo
 
Wana JF, salam!

Nategemea kushiriki mafunzo ya JKT yatakayoshirikisha wabunge vijana. Nafanya hivyo kwa ajili ya NCHI YANGU, VIJANA WENZANGU NA CHAMA CHANGU.

Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.
sikupi hongera mpaka utakapohitimu mafunzo na kupewa force number.

Kule kuna misemo kama hii utaikuta pale main gate tu siku unaripoti:
1. Kuruta hujui kutembea
2. Trankadoso kafike kwenu
3. Kalinyekalinye
4. Songombingo
5. Disko (hapa utapenda maana ni wakati wa kuimba nyimbo za utaifa, kupeana moyo baada ya kazi ngumu ya kutwa nzima)
6. Kichele (sina uhakika kama mtakuwa mnalipwa posho mwisho wa mwezi, tulikuwa tunapata Tsh 300/- those days
7. Kujongomea - Kutoroka, huwezi kumaliza Jeshi bila kutoroka kwa hiyo mh. jiandae kwa hilo vinginevyo unaweza kushusha tani 10 za mahindi toka kwenye Fuso peke yako ukijifanya mlokole na kule hakuna sheria.
8. Usawa wa Gudulia - msosi time, mestine kiunoni (maafande huita appetile yako)
9. Utajibu ndiyo afande katika kila amri yoyote utakayopewa -- hakuna kuhoji.


Utafanya kazi kubwa na Kopro's - hawa jamaa ni hatari sana, kwa ufupi tu wana V mbili chini ya bega.

nafikiri ukirudi huko utakuwa umebadilika sana....
 
hiyo kichwa ya NCHEMBA ni ngumu sana kuelewa hizo week hazimtoshi! huyo kama ni gari imenock injini anatakuwa over hole
 
Hongera sana mkuu, nimekuona sasa hivi hapo Vodacom Mlimani City, kitambi chako ni kikubwa sana mheshimiwa, jitahidi kupasha kabla hujaenda huko, unaweza rudi baada ya siku tatu tu, hizo wiki tatu zitakuwa nyingi sana kwako

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
mkuu jitaidi kupiga kazi na usitege wiki tatu si haba kwani kupata hakuna kidogo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom