Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Status
Not open for further replies.
Hiyo ni semina sio mafunzo ya JKT. Hayo mafunzo yana mtaala wake ambao huwezi kumaliza hata kwa miezi mitatu. Nyie mnatafuta umaarufu wa kisiasa na sio mafunzo ya JKT. Chezea national service weye!

umenikuna. Anaenda semina,mafunzo ya JKT miez chini ya 3 na upewe cheti?
 
Watafanya miezi sita kwa sasa, ila hawa waHeshimiwa nasikia wanaenda Wiki 3 tu.
Mafunzo gani mtu unaenda kwa wiki tatu?Kama ni hivyo sioni wanachoenda kujifunza zaidi ya kupata sifa tu kuwa walienda JKT
 
Mkuu hayo sio mafunzo ya kijeshi labda kama unaenda kwenye tukio la kujiunga JKT. Na kwa kuwa ni tukio naomba uwe unatupia mapicha ya huko jinsi tukio hilo litakavyokuwa kwa hizo wik tatu.

Usisahau kumchukua na nduguyo Emily Ngaponda nae akusaidie kupiga hizo picha
 
Ulikua mwili tu kichwani hakuna kitu (kama kopo tupu na mfuniko wake)...nenda kafundishwe nidhamu na jinsi ya kuishi na watu! Tunategemea mabadiliko. Nape, Lusinde vp?
 
Wana JF, salam!

Nategemea kushiriki mafunzo ya JKT yatakayoshirikisha wabunge vijana. Nafanya hivyo kwa ajili ya NCHI YANGU, VIJANA WENZANGU NA CHAMA CHANGU.

Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.

Ila ndg yangu ulikuwa na tuhuma nyingi kuhusu wake za watu, sijui kama zilikuwa za kweli au la, nafikri JKT itakusaidia kwa namna moja ua nyingine kujenga msingi mipya ya kuishi na wenzako.
 
Mwigulu Nchemba, tunakutakia kila la heri, nadhani ukirudi kutoka huko Hautapoteza muda wako kuitukana CHADEMA na viongozi wake. Mafunzo ya Jeshi yanachangamsha akili hautabaki kama ulivyokuwa mwanzo...Mungu akusaidie kabisa

Asante kwa taarifa....
Jeshini kuna kitu kinaitwa daily order na hii inakufanya usitumie akili kwani kila kitu kinakuwa kimepangwa.Huna nafasi ya kutumia akili yako na ndio maana Mwanajeshi anatii amri.
La muhimu katika era hii ya HIV/AIDS watu ni lazima wawe extra careful la sivyo kitakuwa kiwanda cha kuzalishia wagonjwa,matron wawe matron kweli!!!!
 
umepimwa wale jamaa wa hiv kwa vipimo vya kweli isiwe feki ukapotelea huko
 
Mkuu, ni bora uende kwa manufaa ya nchi,na sio 'KUONGEZA CV' yako. ALL THE BEST Kuruta mwigulu
 
Wiki tatu hiyo ni camping tu, hakuna mafunzo ya kijeshi, kimaadili na kizalendo yataweza kuleta tija kwa muda huo. Ninachoona kwa kina Mwigulu Nchemba ni kutafuta ujiko wa kisiasa kwamba wamebatizwa kizalendo na sasa ni watu wapya
 
Wana JF, salam!

Nategemea kushiriki mafunzo ya JKT yatakayoshirikisha wabunge vijana. Nafanya hivyo kwa ajili ya NCHI YANGU, VIJANA WENZANGU NA CHAMA CHANGU.

Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.
Haya kaka kila la heri, labda ukirudi huko utakuwa umejifunza uzalendo sio "KUVAA SCAFU YA BENDERA YA TANZANIA"
 
Barua imeonesha muda wa kuanza tu ila najua sio mwaka mmoja ni kipindi kisichopungua wiki tatu wala si zaidi ya miezi mitatu

tanzania kwa usanii ! we JKT gani ya wiki tatu ? kila kitu fasta fasta . CCM mbona mna visa ? mnao madokta fasta fasta . maprofesta fasta sasa na mtakuwa na mkamada fasta , maana kwa kupenda vyeo si hajabu utarudi ukiitwa kanali au brigedia Nchemba si ndo zenu hizo ? kama mie jesi nimepiga kwata miezi sita na uservis miezi sita wee hiyo JKT gani unakwenda hata mgambo haiwi vile.
 
Ngoja nikupe kisa kimoja ambacho KOPLO hawezi kusamehe KURUTA. (hii ni ya makutupola JKT)

Mimi Koplo Lukanga nikikusamehe wewe Kuruta wa Danger-coy itabidi kwanza afande x( Mkuu wa kombania) aitishe kikao cha dharura kwa nini nimekusamehe.

Hapo itashindikana, itabidi kesi iende kwa mkuu wa kikosi kwamba mimi Koplo nimekusamehe na kikao kitashindwa kuamua kwa hiyo kesi hiyo itaenda moja kwa moja kwa mkuu wa JKT dar es salaam.

Huko nako kesi hiyo takuwa ngumu sana, ibadili afande (mkuu wa JKT) aitishe kikao cha dharura ili kujadili suala hili - itashindikana ndipo atachukua uamuzi wa kumwandikia Waziri wa ulinzi.

Waziri wa ulinzi naye ataitisha kikao cha makamanda pamoja na katibu mkuu wa wizara, hapo pia itashindikana na sasa suala hili litaenda bungeni kama hoja binafsi ya serikali toka kwa waziri wa ulinzi.

Bunge litajadili na itashindikana kupata uamuzi, kwa hiyo sasa kitakachofuata ni Rais wa nchi kuvunja Bunge na turudie uchaguzi Upya

-- YAANI YOTE HAYA KWA SABABU YAKO KURUTAA!!!! Haiwezekani kabisa
Chini -- chini -- chinii -- Juuu -- juuu pale utapiga pushapu kama 50 hivi ukisimama unaona blue blue...
baada ya DK mbili hivi unapewa msosi umalize fasta fasta... aisee lazima urudishe chenji na kukumbuka home.
 
Nafikiri JKT itakusaidia kuheshimu watu, kujiheshimu mwenyewe na kuheshimiwa.


Ukirudi bado na matusi yako kwa wazee kama Slaa then tutajua kuwa jeshi halikukusaidia bali ulikwenda kwa ajili ya CCM kama ulivyosema hapo juu na si nchi yako!!
 
Hapa kuna kitu Mwigulu si kawaida yako kabisa kutushirikisha mambo yako hapa JF. Ila utakuwa mjanja sana, haya kila la heri kiongozi tunashukuru umegundua kama ya maana yote yanapatikana JF
Are you serious? Mwigulu?
 
I smell a big rat!! Isije ikawa baadae ikaonekana ambaye hakupitia JKT akatukanwa kwa kukosa "kujifunza" uzalendo. Naiambatanisha hii na kupenda kuvaa pendera ya taifa shingoni!!

It's just another political gesture. Huenda ni kwenda kujifunza mazingira ya kuendesha siasa katika makambi ya jeshi!

I stand to be corrected, if I am wrong.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom