Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Status
Not open for further replies.
Barua imeonesha muda wa kuanza tu ila najua sio mwaka mmoja ni kipindi kisichopungua wiki tatu wala si zaidi ya miezi mitatu

Kama kingekuwa chakula tungesema kimeipuliwa kabla hakijaiva na hakitalika, lakini nyie ni watu ni bora tu niseme tu kuwa "kwa style hiyo, hii inaweza kutuzalishia majambazi tu" mafunzo yenu hatakuwa na tija kwa taifa letu hivyo ni heri msiende.
 
Nina wasiwasi na hii intake ya jkt..hii iko kisiasa zaidi kuliko madhumuni halisi ya kuanzishwa kwa jkt ya mwl. Nyerere.

Nikiwa ni mmoja wapo wa vjiana tuliomalizia jkt ya mwl. Nyerere mwaka 1993, nilipelekwa jkt makutupola nilichokikuta hapo ni kizazaa. Moja wapo la dhumuni kubwa la jkt ni kuleta usawa kwa watanzania wote yaani mtoto wa mkulima,mfanyakazi,rais,waziri,na viongozi wote kwa ujumla kupata mafunzo na treatment sawa. Hapo makutupola tulikuwa na mtoto wa waziri mkuu msuya, wakati sisi watoto wa walalahoi tukila kwa kunyakuwa kwanza yeye alikuwa anakula sgt mess tena bila bugudha....walio kwenda makutu wataongezea. Hapo usawa uko wapi?

Wale waliokuwa ruvu kazi yao kubwa ilikuwa ni kufuga kuku na kulima bustani, jmosi na jpili ukitaka kwenda kula dar es salaam ilikuwa ruksa.....hapo napo je?

Kwa hawa wabunge wanao kwenda jkt ni kiini macho tu kwani watapata matunzo mazuri kuliko wengine na kambi watakazo kuwa wajeshi hawatachakachua vyakula.....

Makamanda wasasa wamejaa upendeleo na kujuana mno kuliko utendaji wa kazi wa kufuata taratibu na miiko ya kazi zilizopo....hivyo kurudisha jkt ni ufujaji wa fedha za walipa kodi tu. Uzalendo hauletwi na kwenda jkt bwana bali ni matendo ya wananchi wenyewe na viongozi wao... Hao waliokula fedha za epa, kagoda nk mbona wote wame kwenda jkt na wala hawana uzalendo? Usalama wa taifa na majeshi mbona wote wana mafunzo lakini ni madudu mtupu?

Tatizo ni kuendekeza u-ccm, mwenzetu nk bila kuweka utanzania mbele..umeona katibu maswi anamsifu bosi wa eura kwa kusaidia ngoma isitoboke wakati nchi ina kwenda gizani....hicho ndo tatizo


kila raheri na unafiki wenu wa kwenda jkt
 
Inasikitisha sana kuona bunge na serikali dhaifu limerudisha JKT bila kufanya tafakuli ya kina. Na sema hivyo kwa sababu tofauti na JKT ya mwl. Nyerere iliyojikita katika kufunza maadili,ukakamavu, nguvu kazi pamoja na uzalishaji, JKT ya awamu hii pamoja na nyakati kuwa tofauti - najua bado wata/wanatumia mbuni za mia a ya 80 kufundishia ambazo hazihakisi mabadiliko ya Karen hii; ya digitali na mitandao, na ya sayansi na technologia. Lakini udhaifu si huo tu, Bali hofu kubwa na pengine ndo iliyowasukuma wabunge kuirejesha na wao kushabikia na kutangaza nia na kujiunga na mafunzo haya nikutaka kupata UHALALI WA KISIASA; ni wazalendo na kwamba wamelitumikia jeshi kwa kipindi hicho. Tujiulize ni ujuzi gani unaweza kuupata katika mafunzo ya wiki tatu?; kwamba kuna mantiki gani mtu mwenye digrii ya uzamivu kwenda kujifunza nguvu kazi pamoja na uzalishaji? Skills ambazo naamini amefundishwa katika digrii ya kwanza NA pili.

Kwahiyo si kweli kwamba Bwana Nchemba anaenda kwa lengo la kujifunza Bali anakwenda kupitia JKT iliapate UHALALI WA KISIASA.

Tue macho na matapeli WA kisiasa
 
Kila la kheri kk! Natumai utarudi na ukakamavu zaidi na kutumikia vema wananchi wako.
 
Abba.wasiwasi wako wa kuanzishwa kwa tena kwa kutumia mbinu za zamani za ujima umekua kweli.hakuna pesa za kutosha,miundo mbinu ni mibovu,mazingira ni duni na kusababisha maradhi ya mlipuko,tiba za kubabaisha.mafunzo ni ya mateso na visasi zaidi na kusababisha vifo kwa vijana.bunge lililopitisha sheria hiyo kandamizi halina habari na maafa yanayotokea jkt.hili ni tatizo kubwa.
 
najua huwezi kuwa mzungu kwa kuoga , mafunzo ya wiki tatu ? ila yatakusaidia kiasi yamkini ukirudi utakuwa umepata pata adabu ya kuishi na wapinzani kwa hoja sio maneno yasiyo na tija
 
Abba.wasiwasi wako wa kuanzishwa kwa tena kwa kutumia mbinu za zamani za ujima umekua kweli.hakuna pesa za kutosha,miundo mbinu ni mibovu,mazingira ni duni na kusababisha maradhi ya mlipuko,tiba za kubabaisha.mafunzo ni ya mateso na visasi zaidi na kusababisha vifo kwa vijana.bunge lililopitisha sheria hiyo kandamizi halina habari na maafa yanayotokea jkt.hili ni tatizo kubwa.

Tatizo ni wewe uliyekuwa na upunguani na akili za visasi. Ushasikia kuna nchi ambayo haipeleki vijana wake mafunzoni. Miaka yote JKT ipo na inatoa vijana imara. Hiyo hoja yako haina mashiko yoyote. Huwezi kwenda au kumpeleka kijana huko basi mtafutie kazi rahisi ya kukuna nazi au akajiunge na david cameron. Chizi kabisa wewe hata siku moja usichezee issue inayohusu usalama wa nchi. Jaribu nenda Goma au south sudan ndio utajua nini umuhim wa kuwa na vijana wakakamavu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom