Ngoja nikupe kisa kimoja ambacho KOPLO hawezi kusamehe KURUTA. (hii ni ya makutupola JKT)
Mimi Koplo Lukanga nikikusamehe wewe Kuruta wa Danger-coy itabidi kwanza afande x( Mkuu wa kombania) aitishe kikao cha dharura kwa nini nimekusamehe.
Hapo itashindikana, itabidi kesi iende kwa mkuu wa kikosi kwamba mimi Koplo nimekusamehe na kikao kitashindwa kuamua kwa hiyo kesi hiyo itaenda moja kwa moja kwa mkuu wa JKT dar es salaam.
Huko nako kesi hiyo takuwa ngumu sana, ibadili afande (mkuu wa JKT) aitishe kikao cha dharura ili kujadili suala hili - itashindikana ndipo atachukua uamuzi wa kumwandikia Waziri wa ulinzi.
Waziri wa ulinzi naye ataitisha kikao cha makamanda pamoja na katibu mkuu wa wizara, hapo pia itashindikana na sasa suala hili litaenda bungeni kama hoja binafsi ya serikali toka kwa waziri wa ulinzi.
Bunge litajadili na itashindikana kupata uamuzi, kwa hiyo sasa kitakachofuata ni Rais wa nchi kuvunja Bunge na turudie uchaguzi Upya
-- YAANI YOTE HAYA KWA SABABU YAKO KURUTAA!!!! Haiwezekani kabisa
Chini -- chini -- chinii -- Juuu -- juuu pale utapiga pushapu kama 50 hivi ukisimama unaona blue blue...
baada ya DK mbili hivi unapewa msosi umalize fasta fasta... aisee lazima urudishe chenji na kukumbuka home.