Dadii
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 749
- 1,180
naaam umeiva mkuu...hicho kipengele cha kuonea huruma baada ya kupata mtoto huwa kinawadhulu sana wanaume...wanahisi walifanya msaada...owa mtu unayempenda kisikusumbue wewe mwenyewe na huwa wanaogopa kutamka kwa wake zao maana kitazalisha vita ya 3 ya dunia.!!Nina maswali ya kukuuliza:
Umesema ulikutana nae ujingani? JIbu: bado ana mawazo ya wewe kuchepuka kwa sababu ya njia uliyompata
Umesema una miaka 4 pamoja, je miaka hiyo minne unaishi nae au ni miaka ambayo mmefahamiana ukijumlisha ya kukaa?
Je hii tabia ya kutokuwekea maji bafuni imeanzaje? Aliwahi kuwa anakuwekea maji?
Mkeo ni mfanyakazi au ni mama wa nyumbani?
Kabla ya kuanzisha mahusiano, amewahi kukudanganya?
Hii tabia kuchunguza simu yako imeanza baada ya kukaa nae au mkiwa uchumbani alikuwa akishika simu yako.
Mkeo umemuoa kwa mapenzi au umemuoa baada ya kuwa umezalisha, ukamuonea huruma ili mlee watoto?
Ukinijibu vizuri haya maswali, ukawa genuin, naweza kushauri kitu hapa. ikawa funzo kwa wanaume wengine wanaopitia changamoto kama yako.
Mwanamke atasema nipe talaka utaanza kumbwelesha...maana hujajiandaa naye kagundua kumbe hukuwa na mapenzi nae ni.mtoto tu kaleta ndoa.
Tathimini ni muhimu sana kabla ya ndoa.