Bexb
JF-Expert Member
- Oct 24, 2016
- 658
- 1,394
Ninaamini kabisa kuwa utapeli upo lakini kuna namna huwa watu tunaweza kuchukua tahadhari na kupunguza visa vya kutapeliwa.
KWA VIWANJA VILIVYOPIMWA:
🔥Baada ya kuwa umeoneshwa kiwanja husika na mmekubaliana bei, hakikisha kuwa unampa wakili kazi ya kusimamia mauzo hayo maana ni lazma atafanya search katika mamlaka husika kujua mmiliki halali ama kama kuna attachment yoyote juu ya kiwanja husika
🔥 Hakikisha unajua marital status ya muuza kiwanja, kama atakwambia wameachana hakikisha anakuonesha hati ya talaka ama ya kutengana iliyotolewa na MAHAKAMA na sio vinginevyo.
🔥 Endapo ametengana kienyeji na mwenza wake hakikisha huyo mwenza anajaza fomu maalumu (spousal consent) ya kuridhia mauzo ya kiwanja husika yaani hata kama wamenuniana hakikisha mwenza amejaza hiyo form yeye mwenyewe.
🔥 Kama kutakua na wasiwasi wowote wa vipimo vya kiwanja husika vile vya kwenye nyaraka na uhalisia hakikisha mnaitumia mamlaka ya ardhi eneo husika kisha kuwakutanisha na majirani wako ili kuweka sawa suala hilo.
KWA VIWANJA/MAENEO AMBAYO HAYAJAPIMWA:
🔥Hakikisha kuwa unawapata watu wote wa pande zote ambazo eneo hilo mnapakana na wakuoneshe na mkubaliane wote mipaka halisi ya eneo unalotaka kununua na hawa ndio watakua mashuhuda wa mjataba wako.
🔥Hakikisha mauziano hayo yanasimamiwa na wakili ambaye atakuongiza katika kufanya search na taratibu sahihi.
🔥Hakikisha mwenza wa anayekuuzia eneo husika anajaza form maalumu ya kuridhia mauzo hayo na kama wameachana hakikisha unapata nyaraka ya mahakama kuthibitisha hili.
KWA MAENEO YA UKOO/FAMILIA/URITHI.
Hapa ndio kuna kivumbi na wanunuzi hupoteza sana pesa hapa.
Kuna wakati ambapo mzazi/mmiliki wa eneo akifariki basi familia haifungui mirathi mahakamani bali hukaa kikao na kuamua kutoaiuza ardhi lakini wakagawanya vyumba ama hisa katika nyumba husika mfano, huweza kugawana vyumba hivyo kila mmoja akawa na mpangaji wake ama wakaipangisha kisha kila kodi ikitolewa basi wanagawana.
Sasa endapo unataka kununua ardhi ya mazingira ya namna hii unatakiwa kuwa makini sanaaa na endapo nyumba ni ya familia hakikisha kuwa wale wanafamilia woooote yaani namaanisha WOTE sio wengi hapana, nasema WANAFAMILIA WOTE wahaohusika na ardhi ama nyumba husika ndipo muweze kuendelea na mauzo. Hii ni kwa sababu endapo ikatokea mmoja ama sehemu ya wanahisa wa hiyo ardhi ya familia hakuridhia basi utakua umepigwaaa(rejea kilichomkuta S. H. Amon hapo Kariakoo)
Iwapo nyumba inamilikiwa na Ukoo yaani vizazi hata viwili ama vitatu yaani nyumba alikua anamiliki babu yangu ambaye alikua na watoto nane na wote hao walikua na familia, wakafariki 4 na watoto wa babu wakazaa tukatokea sisi na baadhi yetu tumeshafariki lakini tumeacha watoto wetu ambao wana haki kupitia baba na babu zao aisee mimi NINAKUSHAURU USINUNUE ARDHI HIYO hakikisha kabla ya kununua au kulipia hata sh mia unawasiliana na wakili wako.
Kiukweli wakuu ukitapeliwa kwenye kiwanja kilichopimwa ni lazma wewe mnunuzi kuna mahali ulizembea kwenye utaratibu mzima wa manunuzi maana kwa upande wa hivi viwanja vilivyopimwa utaratibu upo wazi sana.
Nilichogundua ni kuwa wengi wana mazoea na kukalili taratibu za kizamani zisizotambuliwa kisheria yaani mtu anaona kutoa 2M kwa wakili asimamie mchakato mzima wa mauziano ya 50M anamuamini dalali ambaye atalipwa 10% na mtedaji/mwenyekiti halafu anatoa hela😂😂😂😂😂😂
HAKIKISHENI MNAFUATA MIONGOZO YA WANASHERIA KUPUNGUZA KUTAPELIWA
KWA VIWANJA VILIVYOPIMWA:
🔥Baada ya kuwa umeoneshwa kiwanja husika na mmekubaliana bei, hakikisha kuwa unampa wakili kazi ya kusimamia mauzo hayo maana ni lazma atafanya search katika mamlaka husika kujua mmiliki halali ama kama kuna attachment yoyote juu ya kiwanja husika
🔥 Hakikisha unajua marital status ya muuza kiwanja, kama atakwambia wameachana hakikisha anakuonesha hati ya talaka ama ya kutengana iliyotolewa na MAHAKAMA na sio vinginevyo.
🔥 Endapo ametengana kienyeji na mwenza wake hakikisha huyo mwenza anajaza fomu maalumu (spousal consent) ya kuridhia mauzo ya kiwanja husika yaani hata kama wamenuniana hakikisha mwenza amejaza hiyo form yeye mwenyewe.
🔥 Kama kutakua na wasiwasi wowote wa vipimo vya kiwanja husika vile vya kwenye nyaraka na uhalisia hakikisha mnaitumia mamlaka ya ardhi eneo husika kisha kuwakutanisha na majirani wako ili kuweka sawa suala hilo.
KWA VIWANJA/MAENEO AMBAYO HAYAJAPIMWA:
🔥Hakikisha kuwa unawapata watu wote wa pande zote ambazo eneo hilo mnapakana na wakuoneshe na mkubaliane wote mipaka halisi ya eneo unalotaka kununua na hawa ndio watakua mashuhuda wa mjataba wako.
🔥Hakikisha mauziano hayo yanasimamiwa na wakili ambaye atakuongiza katika kufanya search na taratibu sahihi.
🔥Hakikisha mwenza wa anayekuuzia eneo husika anajaza form maalumu ya kuridhia mauzo hayo na kama wameachana hakikisha unapata nyaraka ya mahakama kuthibitisha hili.
KWA MAENEO YA UKOO/FAMILIA/URITHI.
Hapa ndio kuna kivumbi na wanunuzi hupoteza sana pesa hapa.
Kuna wakati ambapo mzazi/mmiliki wa eneo akifariki basi familia haifungui mirathi mahakamani bali hukaa kikao na kuamua kutoaiuza ardhi lakini wakagawanya vyumba ama hisa katika nyumba husika mfano, huweza kugawana vyumba hivyo kila mmoja akawa na mpangaji wake ama wakaipangisha kisha kila kodi ikitolewa basi wanagawana.
Sasa endapo unataka kununua ardhi ya mazingira ya namna hii unatakiwa kuwa makini sanaaa na endapo nyumba ni ya familia hakikisha kuwa wale wanafamilia woooote yaani namaanisha WOTE sio wengi hapana, nasema WANAFAMILIA WOTE wahaohusika na ardhi ama nyumba husika ndipo muweze kuendelea na mauzo. Hii ni kwa sababu endapo ikatokea mmoja ama sehemu ya wanahisa wa hiyo ardhi ya familia hakuridhia basi utakua umepigwaaa(rejea kilichomkuta S. H. Amon hapo Kariakoo)
Iwapo nyumba inamilikiwa na Ukoo yaani vizazi hata viwili ama vitatu yaani nyumba alikua anamiliki babu yangu ambaye alikua na watoto nane na wote hao walikua na familia, wakafariki 4 na watoto wa babu wakazaa tukatokea sisi na baadhi yetu tumeshafariki lakini tumeacha watoto wetu ambao wana haki kupitia baba na babu zao aisee mimi NINAKUSHAURU USINUNUE ARDHI HIYO hakikisha kabla ya kununua au kulipia hata sh mia unawasiliana na wakili wako.
Kiukweli wakuu ukitapeliwa kwenye kiwanja kilichopimwa ni lazma wewe mnunuzi kuna mahali ulizembea kwenye utaratibu mzima wa manunuzi maana kwa upande wa hivi viwanja vilivyopimwa utaratibu upo wazi sana.
Nilichogundua ni kuwa wengi wana mazoea na kukalili taratibu za kizamani zisizotambuliwa kisheria yaani mtu anaona kutoa 2M kwa wakili asimamie mchakato mzima wa mauziano ya 50M anamuamini dalali ambaye atalipwa 10% na mtedaji/mwenyekiti halafu anatoa hela😂😂😂😂😂😂
HAKIKISHENI MNAFUATA MIONGOZO YA WANASHERIA KUPUNGUZA KUTAPELIWA