Kontena zaidi ya 2 ya Jezi feki zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. Bilioni 2 zakamatwa

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626

Kontena zaidi ya mbili zenye jezi feki za Simba, Yanga na Taifa Stars zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni mbili zimekamatwa kwenye ghala moja lililopo eneo la Chang’ombe Jijini Dar es salaam huku Mtu aliyeziingiza nchini pamoja na Mmiliki wa ghala lililokutwa na jezi wakitokomea na hadi sasa Mmiliki wa jezi hizo feki hajafahamika.

Maafisa wa Idara mbalimbali za Serikali wameonekana wakifanya tathmini ya mzigo huo ili kujua makadirio ya thamani yake halisi na hasara iliyopatikana pamoja na viwango na ubora wake, huku Mmiliki akishindwa kufika eneo hilo wala kubainika hadi kufikia asubuhi hii.

Licha ya uwepo wa Maafisa wa Serikali, wengine waliokuwa katika eneo hilo hadi usiku wa manane ni pamoja na Viongozi wa Simba na Yanga pamoja na Wawakilishi kutoka GSM na Sandaland ambao walionekana kufuatilia kwa ukaribu kila kilichoendelea.

Viongozi wa Taasisi za Serikali hawakuwa tayari kuongea huku wakiahidi kutoa taarifa leo hii lakini Mwakilishi wa Kampuni ya GSM amesema kuwa uwepo wa jezi feki hizo unakwamisha jezi original kuuzwa na amewataka Mashabiki kununua jezi halisi kwenye maduka yaliyotangazwa kwakuwa kunua jezi feki kunaua mpira wa Tanzania na kuwatia hasara wanaowekeza pesa zao kutengeneza na kusambaza jezi original

Ayo TV
 
Kontena zaidi ya mbili zenye jezi feki za Simba, Yanga na Taifa Stars zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni mbili zimekamatwa kwenye ghala moja lililopo eneo la Chang’ombe Jijini Dar es salaam huku Mtu aliyeziingiza nchini pamoja na Mmiliki wa ghala lililokutwa na jezi wakitokomea na hadi sasa Mmiliki wa jezi hizo feki hajafahamika.
Ni mtandao mpana wanajuana kwa vilemba vyao hao na usishangae ni igizo hilo
 
Kontena zaidi ya mbili zenye jezi feki za Simba, Yanga na Taifa Stars zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni mbili zimekamatwa kwenye ghala moja lililopo eneo la Chang’ombe Jijini Dar es salaam huku Mtu aliyeziingiza nchini

Ayo TV
Hivi iyo ni kesi ya jinai au ya madai? hiyo si infringement of a copyright? kama ni jinai, huyo mwenye ghala ana kosa? nadhani wazitaifishe tu na kugawia simba na yanga waziuze na wapate pesa hiyo ndio itakuwa hasara nzuri kwa hao matapeli.
 
Mwenye ghala lazima ajulikane, kitendo cha kuingiza jezi inaonyesha jinsi gani bandarini na tra kulivyooza.
Utaratibu wa jezi ilitakiwe ziuzwe kwenye maduka maalumu yenye kutoa risiti za efd lakini unapouza jezi mpaka unatandaza chini lazima wauzaji wa jezi feki wapitishie humohumo.
 

Kontena zaidi ya mbili zenye jezi feki za Simba, Yanga na Taifa Stars zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni mbili zimekamatwa kwenye ghala moja lililopo eneo la Chang’ombe Jijini Dar es salaam huku Mtu aliyeziingiza nchini pamoja na Mmiliki wa ghala lililokutwa na jezi wakitokomea na hadi sasa Mmiliki wa jezi hizo feki hajafahamika.

Maafisa wa Idara mbalimbali za Serikali wameonekana wakifanya tathmini ya mzigo huo ili kujua makadirio ya thamani yake halisi na hasara iliyopatikana pamoja na viwango na ubora wake, huku Mmiliki akishindwa kufika eneo hilo wala kubainika hadi kufikia asubuhi hii.

Licha ya uwepo wa Maafisa wa Serikali, wengine waliokuwa katika eneo hilo hadi usiku wa manane ni pamoja na Viongozi wa Simba na Yanga pamoja na Wawakilishi kutoka GSM na Sandaland ambao walionekana kufuatilia kwa ukaribu kila kilichoendelea.

Viongozi wa Taasisi za Serikali hawakuwa tayari kuongea huku wakiahidi kutoa taarifa leo hii lakini Mwakilishi wa Kampuni ya GSM amesema kuwa uwepo wa jezi feki hizo unakwamisha jezi original kuuzwa na amewataka Mashabiki kununua jezi halisi kwenye maduka yaliyotangazwa kwakuwa kunua jezi feki kunaua mpira wa Tanzania na kuwatia hasara wanaowekeza pesa zao kutengeneza na kusambaza jezi original

Ayo TV
Nchi hii ilivyo ya ajabu watasema mmiliki wa mzigo hajulikani.
 
Utakuta ni dili la mfanyabiashara na kigogo
Ila mfanyabiashara naona alitaka kumzidi akili boss
Nawaza tu maana kuna watu wanatakatisha hela kwa njia nyingi
Hapo wamechomana kwa sharti la kutosemana ni nani mwenye mali
Acha niendelee na ndoto yangu
 
Hizi ndio jezi wanazovaa mashabiki OyaOya. Mdomoni porojo nyingi, ukimwambia changia timu anakwepa kununua jezi Original anaenda kuchukua hizi za buku tatu.

Halafu baadae utamkuta kwenye kijiwe cha draft anapiga kelele "tunataka viongozi wamsajili Shalulile".. Nigga?!!!! Kwa uchumi gani?!! Wakati wewe kama shabiki ndio unakua mstari wa mbele kuididimiza klabu yako. SHABIKI MAANDAZI.
 
Back
Top Bottom