Nimetapeliwa Sinza

Nimetapeliwa Sinza

Mkuu pole sana, naungana na waliosema utafute vijana wa kazi. Niliwahi kupanga nyumba baada ya kulipa kodi nikaombwa nisubiri ujenzi (wiring) ukamilike, kumbe kijana alokuwa analinda hiyo nyumba katengeneza copy ya funguo. Siku moja nimesafiri, kukacha asubuhi ndani kutupu, wamekomba kila kitu. Kuna jamaa 3 X-vibaka, kazi yao ni kutrace wahalifu na mali zilizoibiwa, gharama yao ni 1/4 ya mali itakayopatikana. Baada ya siku 4, Saa 8 usiku walimleta dogo akiwa hafai, akaeleza wapi vitu vilipelekwa. Tulikuta almost nusu vimeshapigwa bei.
Aliyewahi kuibiwa anajua machungu haya, narudia POLE SANA mkuu HEKAYA.
 
Last edited by a moderator:
Milion sita? Ina maana laki 5 kwa mwezi? Na ulikopa ili upange kifamilia? Au kibiashara? Sinza kwa Remmy? Kweli tunatofautiana sana!
 
HEKAYA ZA ABUNUASI?? Mimi naomba kutoa pole huku nikipita kimyakimya, maana nimeponea chupu chupu kuporwa simu na kukabwa na wahuni mchana kweupeee maeneo ya mtoni mtongani. halafu begi lilisheheni kila kitu muhimu kwangu. yaani nikikukuta unamtetea mwizi au tapeli nakuua hapo hapo!

Asante na pole kwa yaliyokukuta
 
Mkuu pole sana, naungana na waliosema utafute vijana wa kazi. Niliwahi kupanga nyumba baada ya kulipa kodi nikaombwa nisubiri ujenzi (wiring) ukamilike, kumbe kijana alokuwa analinda hiyo nyumba katengeneza copy ya funguo. Siku moja nimesafiri, kukacha asubuhi ndani kutupu, wamekomba kila kitu. Kuna jamaa 3 X-vibaka, kazi yao ni kutrace wahalifu na mali zilizoibiwa, gharama yao ni 1/4 ya mali itakayopatikana. Baada ya siku 4, Saa 8 usiku walimleta dogo akiwa hafai, akaeleza wapi vitu vilipelekwa. Tulikuta almost nusu vimeshapigwa bei.
Aliyewahi kuibiwa anajua machungu haya, narudia POLE SANA mkuu HEKAYA.

Asante mkuu kwa ushauri, nitakapo wakamata, nitawapiga picha na kuleta picha zao hapa jamvini
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nenda kwa mganga umtoe mtu roho milion 6 nyingi sn.
 
hujawahi hata kusifiwa na wadawa wa kitaa hivi? au hata wamama (ila usimuamini mama yako. watu wanasemaga my cute boy ama gelo ila nikiangalia natamani kupiga yowe)

Sijijui mkuu, halafu mimi huwa sina muda wa kujiangalia kwenye kioo
 
Hiyo ID yako inanifanya nishindwe kuchangia hii mada maana kutoa 6ml kwa mtu mkononi tu tena ni nje ya eneo husika napata shida kuelewa.
 
Pole sana mkuu, ilikuwaje ukalipa pesa bila kukabidhiwa funguo. Nafikiri huu ni wakati wa kuwakataa Mdalali wasiotambulika Kisheria.

Kwa kweli madalali mimi siwapendi tu hata awe dalali wa nini. Hakuna cha kutambulika kisheria, madalali ni watu waongo, waliojaa utapeli na kiswahili kingi. Tena ndo wanafanya vitu mjini kupanda sana bei mfano vyumba vya kupanga na viwanja vya kujenga, bila kuzingatia kipato cha mtu wa chini. Madalali wangepigwa marufuku
 
Hiyo ID yako inanifanya nishindwe kuchangia hii mada maana kutoa 6ml kwa mtu mkononi tu tena ni nje ya eneo husika napata shida kuelewa.

Unajua mkuu obwato umefikiria sana kwani hata mimi pia hiyo ID inanifanya nifikirie pengine hata hiki anachotueleza ni kama hadithi za Abunuwasi tu na si kweli. Kwani ktk hali ya kawaida kuikabidhi mil. 6 kirahisirahisi tu bila documents na mashahidi wa kueleweka haiingii akilini
 
Nimeguswa na nimejikuta hasira zimenikaba. Yani pesa ilivyo ngumu hivyo Washenzi wanachukua kwa urahisi na kihuni tu. Kaka, kopa tena laki 2 uhonge hao polisi. Ndo mfumo wa nchi yetu hivyo si ajabu kujipanga kutoa rushwa!! Uwe unawakatia hapo pesa kidogo kidogo mpaka wamkamte huyo mpuuzi. Pole sana kamanda
 
Nimeandika uzi huu ili watu wajifunze na waelewe kuwa kuna utapeli wa namna hiyo. Na kwa kuwa humu jamvini kuna watu tofauti naweza kupata mawazo nini cha kufanya

Bwana hekaya nakushauri kakomae na police watakusaidia muende ktk ile nyumba yule jamaa mpaka mumtie mikononi. Kinyume na hivyo hutopata haki yako
 
Unajua mkuu obwato umefikiria sana kwani hata mimi pia hiyo ID inanifanya nifikirie pengine hata hiki anachotueleza ni kama hadithi za Abunuwasi tu na si kweli. Kwani ktk hali ya kawaida kuikabidhi mil. 6 kirahisirahisi tu bila documents na mashahidi wa kueleweka haiingii akilini

Mkuu MODFIELD! ID isikusumbe soma vizuri hiyo post chukua hii kama changamoto!Nitakapo wapata hawa watu nitakuja tena kwenu na nitawapiga picha
 
Kwenye sheria za mikataba ya kuuziana ardhi/nyumba kuna principle moja inasema "caveat emptor" aka "let the buyer be aware".

Sheria hii inatokana na kwamba wakati muuzaji huwa anakuwa na habari kuhusiana na ardhi/nyumba anayotaka kuiuza, mara nyingi mnunuaji anakuwa hana habari za kutosha kuhusiana ardhi/nyumba anayotaka kuinunua.

Kwa hiyo, muuzaji anaweza kuficha baadhi ya habari muhimu kuhusiana na anachouza. Hapo mnunuaji lazima afahamu hizo habari. lazima awe makini kwa kujidhihirisha mwenyewe mmiliki halali wa hiyo nyumba.

Ukiwa kama mnunuaji ulitakiwa ujue kwanza mmilikaji halali wa hiyo ardhi/nyumba. Kwa maelezo yako, inaonyesha kuwa hukufanya checks kujua kama kweli "muuzaji" alikuwa mmiliki halali wa hiyo nyumba.

Yaani mtu hawezi kukupigia simu na kukuambia kuwa "njoo kwa Remi kuna nyumba" na wewe ukaenda, then baada ya kuiona nyumba ukaenda moja kwa moja "makongo kwa Mwenye nyumba" na kumlipa bila hata kuhakikisha kuwa kweli yeye ni mmiliki halali wa hiyo nyumba.

How come unampa mtu pesa zote hizo bila hata kumtaka adhibitishe kwanza kuwa anamiliki hiyo nyumba kisheria? Even the richest person on earth hatafanya hivyo.

Pole kwa yaliyokukuta lakini as a buyer, you should have been aware. I hope wewe na wengine watajifunza ili in future msiingizwe tena mkenge kiulaini hivyo. Hata hivyo, this is not one of those things you should have learned in a hard way.
 
Mkuu pole sana usijali pesa yako utaipata tú punguza jazba relax.....jasho la mtu halipotei ivi Ivi kabla ya kuendelea Iyo Ml6 ulotoa ni kodi ya mda gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom