Nimeshangaa kukuta Benki ni kweupe

Nimeshangaa kukuta Benki ni kweupe

Hakiya nani jamani nyie, leo mwenzenu nilishikwa na butwaa kukuta ndani ya Bank hakuna ile misululu wa watu niliyoizoea kuikuta siku zote niendapo bank.

Nilikwenda kulipia ada za watoto wangu kwenye bank mbili tofauti zilizopo jijini Dar mitaa ya New Bagamoyo Rd. Nilikwenda kwenye matawi ya Bank maarufu na makongwe hapa nchini zilizoko mbembezoni mwa barabara ya New Bagamoyo Road.

Nilichokikuta mule ndani sikutaka kuyaamini macho yangu baada ya kukuta hakuna wetaja wanaohudumiwa.

Nilipotoka ofisini nilikwishajiandaa na foleni ndefu za benki zile. Baada ya kuona hamna watu Nilisimama kwanza karibu na kile kitufe nilichozoea kubonyeza ili kupata coupon ya kuhudumiwa, nilidhani kuwa labda kuna tangazo linalokataza watu wasiingie ndani ya benk kwa wakati ule ambalo mimi sikuliona huko nje, hivyo nilitaka kutoka nje nikaangalie kama kuna tangazo kama hilo, lakini mhudumu alidakia karibu.

Tawi lile lina tellers (counter) 7 lakini ilikuwa imefunguliwa teller moja tu. Mhudumu akaniita na kuniuliza nikusaidie nini nikamwambia naomba form ya kutuma ada ya shule, akanambia hakuna kujaza form njoo tu moja kwa moja nikuhudumie, we taja tu account number ya shule.

Wakati ananihudumia nikamuuliza kulikoni leo kuko hivi, akasema hali ni mbaya hivi sasa, tunasubiri tu labla mwisho wa mwezi ndo watu wanakuwa wengi kidogo, hatujui na sisi hatima yetu itakuwaje.

Nilipomalizana na bank ile nikaenda bank ile nyingine kutuma ada kwa mtoto mwingine, loo huko pia hali nikaikuta mbaya zaidi, sikukuta kabisa mhudumu kwenye madirisha (tellers) ya kuhudumia wateja, wahudumu walikuwa wanafanya kazi nyingine.

Nikajiuliza maswali mengi mwenyewe kama vile
1. Ni kweli watanzania wengi walikuwa mission town?
2. Ni kweli uchumi wetu utakuwa?
3. Ni kweli mishahara ya watumishi inawafikisha mwisho wa mwezi? na kama haiwafikishi hizo siku zitakazobaki watafanyaje?
4. Nini kifanyike ili watu wengi waende kupata huduma za kibenki kama zamani?
Lakini mkuu siku hizi huduma nyingi za kifedha zimerahisishwa sana hasa kupitia mitandao ya kijamii, hata hayo mabenki pia wamelink account za watu kupitia Mpesa, Tigopesa, Airtel money n.k na hata kulipia bill za huduma mbalimbali huna haja ya kwenda benki tena. Mashirika makubwa wanatumia miamala kwa Cheque na malipo ya online... Huduma nyingi zinakuwepo mwisho wa mwezi kwa sababu ya mishahara ya wafanyakazi na kwa jinsi teknolojia inavyokuwa si ajabu miaka michache baadae hata mishahara itakuwa inatumwa kwenye simu za mikononi.
 
mkuu usivunjike moyo maana kila mtu saa hizi anafanya kazi ili apate hela ya kula tu. Mkuu kwenye kula ndio kitu cha mwisho kitakacho kosa hela ya matumizi so dont be dissapointed.
TraNsaction nyingi ni kwa mitandao huna haja ya kwenda benki ndio maana misururu hakuna
 
Utafiti gani huu? umekwenda benki moja!! tena kwa siku moja!! halafu unaanzia kujiuliza maswali yasiyo na kichwa wala miguu.
Cross section study (snap shot) ni mojawapo ya mbinu za utafiti kama wewe hujui, sample size yangu ilikuwa ndogo lakini ni random. Hata hivyo studies za watafiti wengine kutoka matawi mengine nchini zinaunga mkono matokeo ya utafiti wangu pia. hii inamaanisha kuwa sikuwa peke yangu aliyelishangaa hili. atm, online, mpesa simbanking zilikuwepo tangu miaka 10+ nyuma, why now.
 
Hawa wanasiasa si wakuwaamini kila walisemalo. Kwa sasa wimbo wao ni maisha magumu. Kwangu mimi maisha yamekuwa rahisi tukianzia na nyumba za kupanga zimepungua bei siyo kama mwaka jana, vyakula bei iko chini sana, nyanya ndio usiseme, viwanja, vifaa vya ujenzi kama cement bei inaendelea kupungua. Huduma za afya na elimu kwa sisi walalahoi zinaboreshwa, Service charge kwenye umeme hatulipi tena. Mtaani kwangu tumeletewa maji ya bomba na imepunguza gharama ya maji ya kununua kutoka elfu sitini kwa mwezi na sasa nalipia elfu kumi tu kwa mwezi. Nyinyi wanasiasa mnaotafuta umaarufu hayo maisha magumu ni kwa akina nani? Ni bora maisha yawe magumu kwa wachache(mafisadi) na yawe nafuu kwa watu wengi(walalahoi). Gharama za mahitaji muhimu ya watu wengi kama yako chini mimi sioni tatizo.
bei ya vyakula kuwa chini unajua maana yake? hii ina maana kuwa wakulima ambao ndio wengi wamepata hasara kubwa isiyomithilika. unapofurahia nyanya imeshuka ni sawa na kusema mkulima ameshuka kimaisha, ndicho hiki unachofirahia? k......z wa uchumi ww
 
Utaitwa mchochezi shauri yako
uchochezi ni msamiati mpya tutauzoea nao pia na kuuona wa kawaida. usiogope kutoa fikra zako kwa kuogopa kuitwa mchochezi. unaekuonya usikombe mboga anakutaka ushibe.
 
Wewe hujiulizi kwanini "mmawia" kakosa bando la kukomenti humu??????? Namba inasomeka
 
Online banking mkuu
Sikumbuki last time nilienda branch sababu kila kitu nafanya online
Jitahidi kubadilika uende na teknolojia Ya kisasa

Hivi na large cash huwa inakuwa deposit online???? Mleta mada ana kikubwa sana cha watu kujifunza ili kujua tunapoelekea. Hii nadhani wanaijua watu waliopo ndani ya bank industry tu. Ukweli hali ni mbaya.
 
Hakiya nani jamani nyie, leo mwenzenu nilishikwa na butwaa kukuta ndani ya Bank hakuna ile misululu wa watu niliyoizoea kuikuta siku zote niendapo bank.

Nilikwenda kulipia ada za watoto wangu kwenye bank mbili tofauti zilizopo jijini Dar mitaa ya New Bagamoyo Rd. Nilikwenda kwenye matawi ya Bank maarufu na makongwe hapa nchini zilizoko mbembezoni mwa barabara ya New Bagamoyo Road.

Nilichokikuta mule ndani sikutaka kuyaamini macho yangu baada ya kukuta hakuna wetaja wanaohudumiwa.

Nilipotoka ofisini nilikwishajiandaa na foleni ndefu za benki zile. Baada ya kuona hamna watu Nilisimama kwanza karibu na kile kitufe nilichozoea kubonyeza ili kupata coupon ya kuhudumiwa, nilidhani kuwa labda kuna tangazo linalokataza watu wasiingie ndani ya benk kwa wakati ule ambalo mimi sikuliona huko nje, hivyo nilitaka kutoka nje nikaangalie kama kuna tangazo kama hilo, lakini mhudumu alidakia karibu.

Tawi lile lina tellers (counter) 7 lakini ilikuwa imefunguliwa teller moja tu. Mhudumu akaniita na kuniuliza nikusaidie nini nikamwambia naomba form ya kutuma ada ya shule, akanambia hakuna kujaza form njoo tu moja kwa moja nikuhudumie, we taja tu account number ya shule.

Wakati ananihudumia nikamuuliza kulikoni leo kuko hivi, akasema hali ni mbaya hivi sasa, tunasubiri tu labla mwisho wa mwezi ndo watu wanakuwa wengi kidogo, hatujui na sisi hatima yetu itakuwaje.

Nilipomalizana na bank ile nikaenda bank ile nyingine kutuma ada kwa mtoto mwingine, loo huko pia hali nikaikuta mbaya zaidi, sikukuta kabisa mhudumu kwenye madirisha (tellers) ya kuhudumia wateja, wahudumu walikuwa wanafanya kazi nyingine.

Nikajiuliza maswali mengi mwenyewe kama vile
1. Ni kweli watanzania wengi walikuwa mission town?
2. Ni kweli uchumi wetu utakuwa?
3. Ni kweli mishahara ya watumishi inawafikisha mwisho wa mwezi? na kama haiwafikishi hizo siku zitakazobaki watafanyaje?
4. Nini kifanyike ili watu wengi waende kupata huduma za kibenki kama zamani?
Hilo swali namba 2 linatuhusu wengi sana..
Tunaishi kama mashetani now days
 
acheni kupeana moyo kwa mambo ya kipuuzi,mnapinga kwa ujinga tu,hebu niwaulize hayo mambo ya kutumia mitandao tameanza mwezi huu?au mwaka huu?maisha yamekua magumu kama sio kwako basi kwetu.
Hao wafia chama huwaambia lolote kila siku wao wanawaza jinsi gani ya kushinda uchaguzi tu na hawawazi maendeleo
 
Kuna miamala mingine lazima ufike bank, fikiria unataka kuweka fedha bank, huwezi kuweka online, utakwenda tu bank halafu ukitaka kuzitumia ndipo online banking inapofanya kazi.
Lakini pia bado zipo taasisi ambazo ili kujiridhisha kuwa umelipia huduma fulani, lazima uwapelekee pay slip, huna namna, lazima utakwenda bank.
Ni kweli teknolojia imeturahisishia sana katika ishu nzima ya utumiaji wa fedha zetu mara tuziwekapo bank
Kukosekana kwa watu bank, ni ishara kuwa watu hawana pesa za kupeleka huko, kinachopatikana kinaliwa, senti ya kuweka akiba haipo.
Kuweka pesa benki sio lazima uende benki husika, kuna wakala wa benki kama wa NMB, CRDB etc waliojaa mitaani kwetu unaweza kuweka na kutoa pesa.
 
" NATAKA WALIOISHI KAMA MALAIKA WAISHI KAMA MASHETANI " Na wala siyo walioishi kama shetani waishi kama malaika , Hapa kazi tu !
Ss bora walioishi km makaika bado hali yao ht km mbaya sio sawa na walioishi km mashetani ndo hali mby zaidi
 
Back
Top Bottom