Nimepigwa na butwaa

Mkuu sasa kwa hali ya humu jf kweli bi mdashi et awe ana log in...
Imagine tuu
Hii hapana sitaki iwe hvo mkuu
Hutaki iwe hivyo au hupendi iwe hivyo, embu fafanua kidogo!

Wenzake wa 70+yrs old tupo humu na ninyi tukihangaika, kwani shida iko wapi?

Na ukianza tu ubaguzi wa umri mwisho wa siku utakuja kujinyanyapaa wewe mwenyewe na habari yako itaishia hapo.
 
simu ya mama,mke? au mama mzazi?
 
Mkuu huyu ni bi mkubwa ujue..
Hilo jambo hata wewe lingekushangaza mi ndo nilinunua hi simu alafu... Hii ya leo imenistukiza sana
Nakubali kaka ni bimkubwa.. ila humu kumbuka kuna nyuzi nyingi mno za elimu, biashara, kilimo, mapishi, siasa n.k sasa ye huenda alisachi kitu Google afu kwenye kufungua ile link ikamleta direct humu akaamua aichukue app kabisa ..

ni maoni tu we endelea kupigwa na butwaa ๐Ÿ˜‚
 
Huwenda mkuu ila daah hii imenifanya nishangae mpaka sasa...

Mi leo naskilizia jioni akilalamika kama nimefuta app zake hapo tajua kweli yupo humu..

Hapo ndo taanza kufatilia A to Z aiseee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ