Nimeombwa kuwa "Husband for hire"

Nimeombwa kuwa "Husband for hire"

Ukishafunga ndoa bomani si itabidi mpeane talaka, na mbeleni kabla ya kuoa na maishani mwako status yako itakuwa lazima mtu alie divorce. Ukitaka kwenda kuoa kanisani lazima utataja ya bomani etc

Sasa upo tayari kupitia yote haya na hata kujieleza kwa ndugu zako na za mke kama ukipata wa kumuoa.

Ila inaonekana unampenda huyu na ndio unataka kumsaidia, bila hivyo si unasema no tu. Na kama hawajai ishi mjini Dar hiyo itakuwa habari ingine.
 
Kuchana original siyo solution, nakala itabaki bomani, akiamua kukufix atakufix tu. Atasema wewe ni mumewe, vyeti vilipotea/kuibiwa n.k. ushahidi uko bomani. Akifungua kesi, mtu wa bomani atakuja kuthibitisha hiyo ndoa mahakamani, think before you leap

Umeona eeh! Kijana aelewe hilo. Ikitokea bahati mbaya (Mungu apishie mbali) kijana huyu akafariki, huyu mwanadada ana haki ya kudai mirathi, kwa sababu ni mwanandoa halali kabisa!
 
yataka moyo asee kuigiza maisha ni hatari mara nyingine
 
Hapana The Boss

Huyu rafiki angu nilimwonea huruma sana alivyopangiwa huko Tabora ndanindani.

Hatuna feelings kabisa.

The easy way kutoka huko ndo hyo suggestion.

Original certificate nitakaa nayo yeye nitampa copy, akishahamishiwa dar naichana na kila mtu anaendelea na maisha yake,

Vipi kuhusu nakala itakayobaki Bomani, utaichana nayo ? Kumbuka kuwa vyeti vinavyotolewa kanisani ni hivyo hivyo vya Bomani na jinsi sasa hivi nchi inapoelekea kwenye usajili wa watu kuna uwezekano mkubwa wa michezo kama hiyo kugundulika.
 
Mm..akili kumkichwa..sasa uyo dada hana mchumbake wafanye hiyo mishe..si ndo kushow love kwenye shida na raha..hana mchumba anafunga ndoa na wew usiye ata na mchumba pia..affu unasema ni mbaya..mm si ndo umepatwa rafiki yangu..akigoma hamtengani ndo tayari izo biashara zako naye ana mkono..na akija dar lazma mtakua karibu..we si ndo mwenyeji bhana..we achana na iyo habari..
 
Bulldog,,umsaidie mfunge ndoa arudishwe Dar kwa mume wake????!!Kwa nini hasimwambie huyo mumewake wakafunga hiyo ndoa?

Hali kadhalika hiki kipengele sijakielewa kabisa...mume yupo halafu Bulldog 'anakodiwa' au ni mchumba tu? Na mchumba anaogopa 'kuoa' kweli kwa sababu bado hajafanya maamuzi?
 
Na wewe baadaye ukitaka kuoa je huyo mwanamke akilita kipingamizi???
 
kwanza hakuna uhamisho wa namna hiyo siku hizi ....
 
hii story yakutunga haikaa vizuri,mtunzi kakae tena uje upya....ufunge nae ndoa aende kwa mumewe?????toa bangi hapa
 
mie sio mfanyakazi, ni mfanya biashara

Basi usithubutu kufanya hiyo kitu..trust me it'll wont work na ndoa feki utakuwa ushaiingia...kumbuka hata ukichana nyaraka za ndoa bado kutakuwa na nakala bomani
 
ndugu yangu unajitia kitanzi mwenyewe, kuna vitu vya ku-act lakini hilo sikuungi mkono madhara yake baadae ni makubwa,watu siku hizi hawaaminiki vigeugeu.
 
Hapana The Boss

Huyu rafiki angu nilimwonea huruma sana alivyopangiwa huko Tabora ndanindani.

Hatuna feelings kabisa.

The easy way kutoka huko ndo hyo suggestion.

Original certificate nitakaa nayo yeye nitampa copy, akishahamishiwa dar naichana na kila mtu anaendelea na maisha yake,
Kumbukumbu zitaendelea kuonesha kwamba huyo ni mke wako wa ndoa. mimi nitakuwa wa kwanza kupinga ndoa nyingine kufungwa kati ya huyo mwanamke na mume wake.
 
habari zenu wakuu.

Nina rafiki angu (sio mpenzi, just a friend) mwalimu amepangiwa mkoani halafu porini sana.

Leo kaniomba twende tukafunge ndoa za bomani ili apate cheti akaombe transfer arudishwe dar (kwa mume wake).

Akishahamishiwa dar ndoa yetu inavunjika kila mtu na maisha yake.

Naombeni msaada wa kunieleza ndoa za bomani zinakuwaje.

Shukrani kwa msaada.
nsha funga ndoa na binamu yangu mwalimu kama huyo na ameamishiwa mjini..ila ndo kinyama cha hamu
 
kuna movie inaitwa fake fiancé kaitafute utajifunza kitu naamini.

another thing nyie ni marafiki tena seems very responsible for each other, kama u r both single ukifanya hivyo jua hiyo ndiyo ndoa yenu for goods, unless una wife to be wako dont try this at hooooooooome!:israel:
 
Habari zenu wakuu.

Nina rafiki angu (sio mpenzi, just a friend) mwalimu amepangiwa mkoani halafu porini sana.

Leo kaniomba twende tukafunge ndoa za bomani ili apate cheti akaombe transfer arudishwe Dar (kwa mume wake).

Akishahamishiwa Dar ndoa yetu inavunjika kila mtu na maisha yake.

Naombeni msaada wa kunieleza ndoa za bomani zinakuwaje.

Shukrani kwa msaada.
Mbona unanichanganya mkuu? Hapo alipo anaishi na nani? Nifafanulie mkuu huyu mume wake maana yake nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom