Nimeokota peni ya ajabu

Nimeokota peni ya ajabu

Dah... Hilo ni jini subiani.... Huwezi kuishi zaidi ya siku 3.... Kaitupe baharini haraka sana. .

Cc: Prof. mshana jr
 
Kuna mtu anataka kutapeliwa humu ivi kuna anayejua bei ya diamond kwa kiasi cha wingi wa huo ujazo ulioko kny hiyo peni,
 
Almasi kwenye peni!
Sababu ipi hasa?
Sababu ni kuificha na kuwapumbaza wezi na matapeli. Nilishashuhudia sana michezo ya dealers. Wengine hutengenezea tochi au kibiriti cha gas.
 
Picha limeanza nasubiria part two harufu ya utapeli inanukia apa. Abiria chunga mzigo wako
 
hizo peni au key holders, maduka ya dhahabu huwa wanawapa wateja wao kama zawadi, lakini wateja wengi hawapendi kwenda nazo kwao kwa ajili ya ushirikina, hivyo huvitupa au kuwapa watu wengine njiani.
sio vizuri kuchukua zawadi kutoka kwa sonara kama umenunua kitu kwake!
 
Kwa usawa huu kweli zali la almasi au burungutu kiana tu
 
Jana katika matembezi yangu ya kutafuta AJIRA mitaa ya Indira Ghandi kule mnazi mmoja, nikapita sehemu moja inaitwa GoldePlaza, ndipo nikaokota peni iliyoandikwa "QUEEN'S GEM & JEWELLERY DAR ES SALAAM" hii peni ni nzito kiasi na ni ya kioo, nilibaki nayo na kurudi nayo hadi home Tabata.

Sasa jana usiku nilipatwa na mshangao baada ya kuona kile kioo kilichopo kwenye peni kutoa mwanga wa ajabu baada ya kuiweka juu ya meza, ilibidi niitoe na kuiweka kwenye bag, leo asubuhi nimeitoa na kuikagua vizuri na hadi sasa nimefikia hatua ya kuivunja na ndani nimekuta vijiwe vinang'aa sana ni kama almasi."sijui sina sifa za madini ya almasi ni zipi"

Kwa yoyote mwenye msaada katika hili anisaidie maana inaweza ikawa ndio nimetusua kwa style hii.

1469262387252-jpg.369687
Soma hapa Queens Jewellery habari zao hao huwa wanatengeneza vito vya madin kama almasi ,dhahabu nk
 
Na hakika kabisa kuanzia sasa basi maisha yako yako hatarini.

Hii Kampuni ya wenye kalamu yao nahakika wameshaanza kukusaka.


Tahadhali, Kaa nayo angalau mwaka hivi ukatike na Usijibu PM Yoyote ya humu ndani.
Hapoana mkuu hizo pen ni za promo kutoka kwa hao majamaa ni masonara wapo hapa dar kariakoo mtaa wa indra kwenye jengo la golden plaza pitia Queens Jewellery so hizo pen ni kama bango lao la matamgazo tu na si vinginevyo.na humo ndani ni aina ya madini yenye mng'ao kama almasi na sio almasi na hayana thaman yeyote.
 
Sababu ni kuificha na kuwapumbaza wezi na matapeli. Nilishashuhudia sana michezo ya dealers. Wengine hutengenezea tochi au kibiriti cha gas.

Umesoma maelezo yake? Umeangalia picha??

Kalamu ilikua na maandishi ya kuashiria madini! Madini yaliwekwa kwenye kioo yakionekana kwa nje!

Punguani gani ataficha kwa hivyo?
 
Huyu jamaa yupo wapi!!! Njoo ufunge uzi wako utupe na mgao kabisa... PM's hazifai
 
Hizi nadhani zitakuwa pen za kupewa... Baada ya kununua kitu cha thamani kama pete kwenye duka yao... Ila fanya utafiti zaid...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom